Isaya 11 – NEN & NAV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Isaya 11:1-16

Tawi Kutoka Kwa Yese

111:1 Zek 6:12; Isa 9:7; Mdo 13:23; Ay 14:7; 2Fal 19:26-30; Isa 27:9; Ufu 5:5Chipukizi litatokea kutoka shina la Yese,

kutoka mizizi yake Tawi litazaa tunda.

211:2 Mt 3:16; Yoe 2:28; Yn 16:13; Kut 28:3; Kol 2:3; Amo 3:10; Isa 32:15; 48:16Roho wa Bwana atakaa juu yake,

Roho wa hekima na wa ufahamu,

Roho wa shauri na wa uweza,

Roho wa maarifa na wa kumcha Bwana

311:3 Isa 33:6; Yn 7:24; 2:25naye atafurahia kumcha Bwana.

Hatahukumu kwa yale ayaonayo kwa macho yake,

wala kuamua kwa yale ayasikiayo kwa masikio yake,

411:4 Ufu 19:11; Za 72:2-4; Zek 14:12; 2The 2:8; Za 18:8; Isa 14:30; Ufu 19:11; Ay 5:16bali kwa uadilifu atahukumu wahitaji,

kwa haki ataamua wanyenyekevu wa dunia.

Ataipiga dunia kwa fimbo ya kinywa chake,

kwa pumzi ya midomo yake atawaua waovu.

511:5 Isa 25:1; Efe 4:16; Kut 12:11; 1Fal 18:46Haki itakuwa mkanda wake

na uaminifu utakuwa mshipi kiunoni mwake.

611:6 Hos 2:18; Isa 65:25Mbwa mwitu ataishi pamoja na mwana-kondoo,

naye chui atalala pamoja na mbuzi,

ndama, mwana simba na ngʼombe wa mwaka mmoja watakaa pamoja,

naye mtoto mdogo atawaongoza.

711:7 Ay 40:15Ngʼombe na dubu watalisha pamoja,

watoto wao watalala pamoja,

na simba atakula majani makavu kama maksai.

811:8 Isa 65:20; 14:29; 30:6; 59:5Mtoto mchanga atacheza karibu na shimo la nyoka,

naye mtoto mdogo ataweka mkono wake

kwenye kiota cha fira.

911:9 Hab 2:14; Hes 25:12; Za 98:2-3; Ay 5:23; 1Sam 17:46; Isa 19:21; 52:10Hawatadhuru wala kuharibu

juu ya mlima wangu mtakatifu wote,

kwa kuwa dunia itajawa na kumjua Bwana

kama maji yajazavyo bahari.

1011:10 Yn 12:32; Rum 15:10-12; Mdo 11:18; Za 116:7; Isa 60:5, 10; 32:17-18; Yer 6:16Katika siku hiyo, Shina la Yese atasimama kama bendera kwa ajili ya mataifa. Mataifa yatakusanyika kwake, na mahali pake pa kupumzikia patakuwa utukufu. 1111:11 Mwa 10:22; Zek 10:10; Mik 7:12; Isa 66:19; 10:20; 19:24; Kum 30:4; Hos 11:11Katika siku hiyo Bwana atanyoosha mkono wake mara ya pili kurudisha mabaki ya watu wake waliosalia kutoka Ashuru, Misri, Pathrosi,11:11 Pathrosi ina maana Misri ya Juu. Kushi, Elamu, Babeli, Hamathi na kutoka visiwa vya baharini.

1211:12 Yn 7:35; Sef 3:10; Eze 28:25; Za 20:5; Isa 14:2; 43:5; Yer 16:15; 31:10Atainua bendera kwa mataifa

na kuwakusanya Waisraeli walioko uhamishoni;

atawakusanya watu wa Yuda waliotawanyika

kutoka pembe nne za dunia.

1311:13 2Nya 28:6; Hos 1:11; Gal 3:28; Yer 3:18; Eze 16:22; 37:16-17, 22Wivu wa Efraimu utatoweka,

na adui wa Yuda watakatiliwa mbali;

Efraimu hatamwonea Yuda wivu,

wala Yuda hatakuwa na uadui na Efraimu.

1411:14 Yoe 3:19; Sef 2:8-11; Yer 48:40; 2Nya 26:6; Amu 6:3; 11:14-18; Isa 25:3; Hes 24:18Watawashukia katika miteremko ya Wafilisti

hadi upande wa magharibi,

kwa pamoja watawateka watu nyara

hadi upande wa mashariki.

Watawapiga Edomu na Moabu,

na Waamoni watatawaliwa nao.

1511:15 Isa 19:16; 30:32; 7:20; Ufu 16:12; Kut 14:22, 29; Kum 11:10; Yer 50:38; Mwa 41:16Bwana atakausha

ghuba ya bahari ya Misri;

kwa upepo mkavu ataupeleka mkono wake

juu ya Mto Frati.

Ataugawanya katika vijito saba

ili watu waweze kuuvuka wakiwa wamevaa viatu.

1611:16 Kut 14:26-31; Yer 50:5; Isa 19:23; 35:8; 51:10; 62:10; Mwa 45:7Itakuwepo njia kuu kwa mabaki ya watu wake

wale waliosalia kutoka Ashuru,

kama ilivyokuwa kwa Israeli

walipopanda kutoka Misri.

Ketab El Hayat

إشعياء 11:1-16

برعم من جذع يسَّى

1وَيُفْرِخُ بُرْعُمٌ مِنْ جِذْعِ يَسَّى، وَيَنْبُتُ غُصْنٌ مِنْ جُذُورِهِ، 2وَيَسْتَقِرُّ عَلَيْهِ رُوحُ الرَّبِّ، رُوحُ الْحِكْمَةِ وَالْفِطْنَةِ، رُوحُ الْمَشُورَةِ وَالْقُوَّةِ، رُوحُ مَعْرِفَةِ الرَّبِّ وَمَخَافَتِهِ. 3وَتَكُونُ مَسَرَّتُهُ فِي تَقْوى الرَّبِّ، وَلا يَقْضِي بِحَسَبِ مَا تَشْهَدُ عَيْنَاهُ، وَلا يَحْكُمُ بِمُقْتَضَى مَا تَسْمَعُ أُذُنَاهُ، 4إِنَّمَا يَقْضِي بِعَدْلٍ لِلْمَسَاكِينِ، وَيَحَكُمُ بِالإِنْصَافِ لِبَائِسِي الأَرْضِ، وَيُعَاقِبُ الأَرْضَ بِقَضِيبِ فَمِهِ، وَيُمِيتُ الْمُنَافِقَ بِنَفْخَةِ شَفَتَيْهِ، 5لأَنَّهُ سَيَرْتَدِي الْبِرَّ وَيَتَمَنْطَقُ بِالأَمَانَةِ.

6فَيَسْكُنُ الذِّئْبُ مَعَ الْحَمَلِ، وَيَرْبِضُ النِّمْرُ إِلَى جِوَارِ الْجَدْيِ، وَيَتَآلَفُ الْعِجْلُ وَالأَسَدُ وَكُلُّ حَيَوَانٍ مَعْلُوفٍ مَعاً، وَيَسُوقُهَا جَمِيعاً صَبِيٌّ صَغِيرٌ. 7تَرْعَى الْبَقَرَةُ وَالدُّبُّ مَعاً، وَيَرْبِضُ أَوْلادُهُمَا مُتجَاوِرِينَ، وَيَأْكُلُ الأَسَدُ التِّبْنَ كَالثَّوْرِ، 8وَيَلْعَبُ الرَّضِيعُ فِي (أَمَانٍ) عِنْدَ جُحْرِ الصِّلِّ، وَيَمُدُّ الفَطِيمُ يَدَهُ إِلَى وَكْرِ الأَفْعَى (فَلا يُصِيبُهُ سُوءٌ). 9لَا يُؤْذُونَ وَلا يُسِيئُونَ فِي كُلِّ جَبَلِ قُدْسِي، لأَنَّ الأَرْضَ تَمْتَلِئُ مِنْ مَعْرِفَةِ الرَّبِّ كَمَا تَغْمُرُ الْمِيَاهُ الْبَحْرَ. 10فِي ذَلِكَ الْيَوْمِ يَنْتَصِبُ أَصْلُ يَسَّى رَايَةً لِلأُمَمِ، وَإِلَيْهِ تَسْعَى جَمِيعُ الشُّعُوبِ، وَيَكُونُ مَسْكَنُهُ مَجِيداً.

11فَيَعُودُ الرَّبُّ لِيَمُدَّ يَدَهُ ثَانِيَةً لِيَسْتَرِدَّ الْبَقِيَّةَ الْبَاقِيَةَ مِنْ شَعْبِهِ، مِنْ أَشُورَ وَمِصْرَ وَفَتْرُوسَ وَكُوشَ وَعِيلامَ وَشِنْعَارَ وَحَمَاةَ، وَمِنْ جَزَائِرِ الْبَحْرِ، 12وَيَنْصُبُ رَايَةً لِلأُمَمِ وَيَجْمَعُ مَنْفِيِّي إِسْرَائِيلَ وَمُشَتَّتِي يَهُوذَا مِنْ أَرْبَعَةِ أَطْرَافِ الأَرْضِ، 13فَيَتَلاشَى حَسَدُ أَفْرَايِمَ، وَتَزُولُ عَدَاوَةُ يَهُوذَا، فَلا أَفْرَايِمَ يَحْسُدُ يَهُوذَا، وَلا يَهُوذَا يُعَادِي أَفْرَايِمَ، 14وَيَنْقَضَّانِ عَلَى أَكْتَافِ الْفِلِسْطِينِيِّينَ غَرْباً وَيَغْزُوَانِ أَبْنَاءَ الْمَشْرِقِ مَعاً، وَيَسْتَوْلِيَانِ عَلَى بِلادِ أَدُومَ وَمُوآبَ، وَيَخْضَعُ لَهُمْ بَنُو عَمُّونَ. 15وَيُجَفِّفُ الرَّبُّ تَمَاماً لِسَانَ بَحْرِ مِصْرَ، وَيَهُزُّ يَدَهُ عَلَى النَّهْرِ فَتَهُبُّ رِيحٌ عَاِصفَةٌ تَقْسِمُ مَاءَهُ إِلَى سَبْعِ مَمَرَّاتٍ تَعْبُرُ فِيهَا الْجُيُوشُ. 16وَيَمُدُّ الرَّبُّ طَرِيقاً مِنْ أَشُّورَ لِيَعُودَ مِنْهُ مَنْ بَقِيَ هُنَاكَ مِنْ بَنِي إِسْرَائِيلَ، كَمَا أَعَادَ الرَّبُّ جَمِيعَ إِسْرَائِيلَ مِنْ مِصْرَ.