Hosea 7 – NEN & NIV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Hosea 7:1-16

17:1 Eze 24:13; Hos 4:2; 6:4; Kut 22:2; Sef 2:7; Za 126:1kila mara nilipotaka kumponya Israeli,

dhambi za Efraimu zinafichuliwa

na maovu ya Samaria yanafunuliwa.

Wanafanya udanganyifu,

wevi huvunja nyumba,

maharamia hunyangʼanya barabarani,

27:2 Yer 14:10; 44:21; Mit 5:22; Yer 2:19; 4:18; Hos 8:13; Ay 35:15lakini hawafahamu kwamba

ninakumbuka matendo yao yote mabaya.

Dhambi zao zimewameza,

ziko mbele zangu siku zote.

37:3 Rum 1:32; Yer 28:1-4; Mik 7:3; Hos 4:2; 10:13“Wanamfurahisha sana mfalme kwa maovu yao,

wakuu wao kwa uongo wao.

47:4 Yer 9:2Wote ni wazinzi,

wanawaka kama tanuru

ambayo moto wake mwokaji hana haja ya kuuchochea

kuanzia kukanda unga

hadi umekwisha kuumuka.

57:5 Isa 28:1, 7; Za 1:1Katika sikukuu ya mfalme wetu

wakuu wanawaka kwa mvinyo,

naye anawaunga mkono wenye mizaha.

67:6 Za 21:9Mioyo yao ni kama tanuru,

wanamwendea kwa hila.

Hasira yao inafoka moshi usiku kucha,

wakati wa asubuhi inalipuka

kama miali ya moto.

77:7 Za 14:4; Sef 1:6; Isa 9:13; Hos 13:10Wote ni moto kama tanuru;

wanawaangamiza watawala wao.

Wafalme wake wote wanaanguka,

wala hakuna yeyote kati yao aniitaye mimi.

87:8 Za 106:35; Hos 5:13; 7:11“Efraimu anajichanganya na mataifa;

Efraimu ni mkate ambao haukuiva.

97:9 Isa 1:7; Hos 8:7Wageni wananyonya nguvu zake,

lakini hafahamu hilo.

Nywele zake zina mvi hapa na pale,

lakini hana habari.

107:10 Hos 5:5; Isa 9:13Kiburi cha Israeli kinashuhudia dhidi yake,

lakini pamoja na haya yote

harudi kwa Bwana Mungu wake

wala kumtafuta.

117:11 Mwa 8:8; Hos 9:3; 11:11; Mao 5:6; Yer 2:18“Efraimu ni kama hua,

hudanganywa kwa urahisi na hana akili:

mara anaita Misri,

mara anageukia Ashuru.

127:12 Eze 12:13; 32:3; Law 26:14Wakati watakapokwenda,

nitatupa wavu wangu juu yao;

nitawavuta chini waanguke

kama ndege wa angani.

Nitakaposikia wakikusanyika pamoja,

nitawanasa.

137:13 Hos 9:12, 17; Yer 14:10; 51:9; Eze 34:4-6; Mt 23:37; Za 116:11Ole wao, kwa sababu

wamepotoka kutoka kwangu!

Maangamizi ni yao

kwa sababu wameniasi!

Ninatamani kuwakomboa,

lakini wanasema uongo dhidi yangu.

147:14 Ay 35:9; Yer 3:10; Hos 4:10; 13:16; Za 78:34-37; Amo 2:8Hawanililii mimi kutoka mioyoni mwao,

bali wanaomboleza vitandani mwao.

Hukusanyika pamoja kwa ajili ya nafaka na divai mpya,

lakini hugeukia mbali nami.

157:15 Za 2:1; 140:2; Nah 1:9; Hos 11:3Niliwafundisha na kuwatia nguvu,

lakini wanapanga mabaya dhidi yangu.

167:16 Za 78:57; Eze 23:32; Hos 9:3; 11:5; Mal 3:14Hawamgeukii Yeye Aliye Juu Sana,

wako kama upinde wenye kasoro.

Viongozi wao wataanguka kwa upanga

kwa sababu ya maneno yao ya jeuri.

Kwa ajili ya hili watadhihakiwa

katika nchi ya Misri.

New International Version

Hosea 7:1-16

1whenever I would heal Israel,

the sins of Ephraim are exposed

and the crimes of Samaria revealed.

They practice deceit,

thieves break into houses,

bandits rob in the streets;

2but they do not realize

that I remember all their evil deeds.

Their sins engulf them;

they are always before me.

3“They delight the king with their wickedness,

the princes with their lies.

4They are all adulterers,

burning like an oven

whose fire the baker need not stir

from the kneading of the dough till it rises.

5On the day of the festival of our king

the princes become inflamed with wine,

and he joins hands with the mockers.

6Their hearts are like an oven;

they approach him with intrigue.

Their passion smolders all night;

in the morning it blazes like a flaming fire.

7All of them are hot as an oven;

they devour their rulers.

All their kings fall,

and none of them calls on me.

8“Ephraim mixes with the nations;

Ephraim is a flat loaf not turned over.

9Foreigners sap his strength,

but he does not realize it.

His hair is sprinkled with gray,

but he does not notice.

10Israel’s arrogance testifies against him,

but despite all this

he does not return to the Lord his God

or search for him.

11“Ephraim is like a dove,

easily deceived and senseless—

now calling to Egypt,

now turning to Assyria.

12When they go, I will throw my net over them;

I will pull them down like the birds in the sky.

When I hear them flocking together,

I will catch them.

13Woe to them,

because they have strayed from me!

Destruction to them,

because they have rebelled against me!

I long to redeem them

but they speak about me falsely.

14They do not cry out to me from their hearts

but wail on their beds.

They slash themselves,7:14 Some Hebrew manuscripts and Septuagint; most Hebrew manuscripts They gather together appealing to their gods

for grain and new wine,

but they turn away from me.

15I trained them and strengthened their arms,

but they plot evil against me.

16They do not turn to the Most High;

they are like a faulty bow.

Their leaders will fall by the sword

because of their insolent words.

For this they will be ridiculed

in the land of Egypt.