Hosea 7 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Hosea 7:1-16

17:1 Eze 24:13; Hos 4:2; 6:4; Kut 22:2; Sef 2:7; Za 126:1kila mara nilipotaka kumponya Israeli,

dhambi za Efraimu zinafichuliwa

na maovu ya Samaria yanafunuliwa.

Wanafanya udanganyifu,

wevi huvunja nyumba,

maharamia hunyangʼanya barabarani,

27:2 Yer 14:10; 44:21; Mit 5:22; Yer 2:19; 4:18; Hos 8:13; Ay 35:15lakini hawafahamu kwamba

ninakumbuka matendo yao yote mabaya.

Dhambi zao zimewameza,

ziko mbele zangu siku zote.

37:3 Rum 1:32; Yer 28:1-4; Mik 7:3; Hos 4:2; 10:13“Wanamfurahisha sana mfalme kwa maovu yao,

wakuu wao kwa uongo wao.

47:4 Yer 9:2Wote ni wazinzi,

wanawaka kama tanuru

ambayo moto wake mwokaji hana haja ya kuuchochea

kuanzia kukanda unga

hadi umekwisha kuumuka.

57:5 Isa 28:1, 7; Za 1:1Katika sikukuu ya mfalme wetu

wakuu wanawaka kwa mvinyo,

naye anawaunga mkono wenye mizaha.

67:6 Za 21:9Mioyo yao ni kama tanuru,

wanamwendea kwa hila.

Hasira yao inafoka moshi usiku kucha,

wakati wa asubuhi inalipuka

kama miali ya moto.

77:7 Za 14:4; Sef 1:6; Isa 9:13; Hos 13:10Wote ni moto kama tanuru;

wanawaangamiza watawala wao.

Wafalme wake wote wanaanguka,

wala hakuna yeyote kati yao aniitaye mimi.

87:8 Za 106:35; Hos 5:13; 7:11“Efraimu anajichanganya na mataifa;

Efraimu ni mkate ambao haukuiva.

97:9 Isa 1:7; Hos 8:7Wageni wananyonya nguvu zake,

lakini hafahamu hilo.

Nywele zake zina mvi hapa na pale,

lakini hana habari.

107:10 Hos 5:5; Isa 9:13Kiburi cha Israeli kinashuhudia dhidi yake,

lakini pamoja na haya yote

harudi kwa Bwana Mungu wake

wala kumtafuta.

117:11 Mwa 8:8; Hos 9:3; 11:11; Mao 5:6; Yer 2:18“Efraimu ni kama hua,

hudanganywa kwa urahisi na hana akili:

mara anaita Misri,

mara anageukia Ashuru.

127:12 Eze 12:13; 32:3; Law 26:14Wakati watakapokwenda,

nitatupa wavu wangu juu yao;

nitawavuta chini waanguke

kama ndege wa angani.

Nitakaposikia wakikusanyika pamoja,

nitawanasa.

137:13 Hos 9:12, 17; Yer 14:10; 51:9; Eze 34:4-6; Mt 23:37; Za 116:11Ole wao, kwa sababu

wamepotoka kutoka kwangu!

Maangamizi ni yao

kwa sababu wameniasi!

Ninatamani kuwakomboa,

lakini wanasema uongo dhidi yangu.

147:14 Ay 35:9; Yer 3:10; Hos 4:10; 13:16; Za 78:34-37; Amo 2:8Hawanililii mimi kutoka mioyoni mwao,

bali wanaomboleza vitandani mwao.

Hukusanyika pamoja kwa ajili ya nafaka na divai mpya,

lakini hugeukia mbali nami.

157:15 Za 2:1; 140:2; Nah 1:9; Hos 11:3Niliwafundisha na kuwatia nguvu,

lakini wanapanga mabaya dhidi yangu.

167:16 Za 78:57; Eze 23:32; Hos 9:3; 11:5; Mal 3:14Hawamgeukii Yeye Aliye Juu Sana,

wako kama upinde wenye kasoro.

Viongozi wao wataanguka kwa upanga

kwa sababu ya maneno yao ya jeuri.

Kwa ajili ya hili watadhihakiwa

katika nchi ya Misri.

King James Version

Hosea 7:1-16

1When I would have healed Israel, then the iniquity of Ephraim was discovered, and the wickedness of Samaria: for they commit falsehood; and the thief cometh in, and the troop of robbers spoileth without.7.1 wickedness: Heb. evils7.1 spoileth: Heb. strippeth 2And they consider not in their hearts that I remember all their wickedness: now their own doings have beset them about; they are before my face.7.2 consider…: Heb. say not to 3They make the king glad with their wickedness, and the princes with their lies. 4They are all adulterers, as an oven heated by the baker, who ceaseth from raising after he hath kneaded the dough, until it be leavened.7.4 who…: or, the raiser will cease7.4 raising: or, waking 5In the day of our king the princes have made him sick with bottles of wine; he stretched out his hand with scorners.7.5 bottles…: or, heat through wine 6For they have made ready their heart like an oven, whiles they lie in wait: their baker sleepeth all the night; in the morning it burneth as a flaming fire.7.6 made…: or, applied 7They are all hot as an oven, and have devoured their judges; all their kings are fallen: there is none among them that calleth unto me.

8Ephraim, he hath mixed himself among the people; Ephraim is a cake not turned. 9Strangers have devoured his strength, and he knoweth it not: yea, gray hairs are here and there upon him, yet he knoweth not.7.9 here…: Heb. sprinkled 10And the pride of Israel testifieth to his face: and they do not return to the LORD their God, nor seek him for all this.

11¶ Ephraim also is like a silly dove without heart: they call to Egypt, they go to Assyria. 12When they shall go, I will spread my net upon them; I will bring them down as the fowls of the heaven; I will chastise them, as their congregation hath heard. 13Woe unto them! for they have fled from me: destruction unto them! because they have transgressed against me: though I have redeemed them, yet they have spoken lies against me.7.13 destruction: Heb. spoil 14And they have not cried unto me with their heart, when they howled upon their beds: they assemble themselves for corn and wine, and they rebel against me. 15Though I have bound and strengthened their arms, yet do they imagine mischief against me.7.15 have…: or, chastened 16They return, but not to the most High: they are like a deceitful bow: their princes shall fall by the sword for the rage of their tongue: this shall be their derision in the land of Egypt.