Hosea 5 – NEN & NIV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Hosea 5:1-15

Hukumu Dhidi Ya Israeli

15:1 Hos 6:9; 9:8; Ay 10:12; Yer 5:26“Sikieni hili, enyi makuhani!

Kuweni wasikivu, enyi Waisraeli!

Sikieni, ee nyumba ya mfalme!

Hukumu hii ni dhidi yenu:

Mmekuwa mtego huko Mispa,

wavu uliotandwa juu ya Tabori.

25:2 Hos 4:2; 9:15Waasi wamezidisha sana mauaji.

Mimi nitawatiisha wote.

35:3 Eze 23:7; Za 90:8; Hos 1:2; 6:10; Amo 5:12Ninajua yote kuhusu Efraimu,

Israeli hukufichika kwangu.

Efraimu, sasa umegeukia ukahaba,

Israeli amenajisika.

45:4 Hos 4:6, 11; 7:10; Yer 4:22“Matendo yao hayawaachii

kurudi kwa Mungu wao.

Roho ya ukahaba imo ndani ya mioyo yao,

hawamkubali Bwana.

55:5 Isa 3:9; Yer 2:19; Hos 7:10Kiburi cha Israeli kinashuhudia dhidi yao;

Waisraeli, hata Efraimu,

wanajikwaa katika dhambi zao;

pia Yuda atajikwaa pamoja nao.

65:6 Mik 6:6-7; Mit 1:28; Mal 1:10; Eze 8:6; Isa 1:26Wakati wanapokwenda na makundi yao

ya kondoo na ngʼombe

kumtafuta Bwana,

hawatampata;

yeye amejiondoa kutoka kwao.

75:7 Isa 1:14; 24:16; Hos 2:4, 11-12; 6:7; Eze 12:28Wao si waaminifu kwa Bwana;

wamezaa watoto haramu.

Sasa sikukuu zao za Mwandamo wa Mwezi

zitawaangamiza wao

pamoja na mashamba yao.

85:8 Amu 19:12; Hos 4:15; 10:9; Isa 10:29; Yos 7:2; Hes 10:2; Yer 4:21“Pigeni tarumbeta huko Gibea,

baragumu huko Rama.

Paza kilio cha vita huko Beth-Aveni,5:8 Beth-Aveni maana yake Nyumba ya Ubatili (au Uovu), jina lingine la Betheli kwa dhihaka.

ongoza, ee Benyamini.

95:9 Isa 37:3; Hos 9:11-17; Isa 46:10; 7:16; Zek 1:6Efraimu ataachwa ukiwa

katika siku ya kuadhibiwa.

Miongoni mwa makabila ya Israeli

ninatangaza lile ambalo halina budi kutukia.

105:10 Kum 19:14; Eze 7:8Viongozi wa Yuda ni kama wale

wanaosogeza mawe ya mpaka.

Nitamwaga ghadhabu yangu juu yao

kama mafuriko ya maji.

115:11 Hos 9:16; Mik 6:16Efraimu ameonewa,

amekanyagwa katika hukumu

kwa kuwa amekusudia kufuatia sanamu.

125:12 Ay 13:28; Isa 51:8; Ay 18:16Mimi ni kama nondo kwa Efraimu,

na kama uozo kwa watu wa Yuda.

135:13 Hes 12:1; Eze 23:5; Mao 5:6; Hos 2:7; Yer 30:12; Isa 7:16; 3:7“Wakati Efraimu alipoona ugonjwa wake,

naye Yuda vidonda vyake,

ndipo Efraimu alipogeukia Ashuru,

na kuomba msaada kwa mfalme mkuu.

Lakini hawezi kukuponya,

wala hawezi kukuponya vidonda vyako.

145:14 Ay 10:16; Yer 4:7; Kum 32:39; Mik 5:8; Amo 3:4Kwa maana nitakuwa kama simba kwa Efraimu,

kama simba mkubwa kwa Yuda.

Nitawararua vipande vipande na kuondoka;

nitawachukua mbali,

na hakuna wa kuwaokoa.

155:15 Hes 21:7; Za 24:6; 50:15; Yer 2:27; Eze 20:43; Isa 18:4; 64:9Kisha nitarudi mahali pangu

mpaka watakapokubali kosa lao.

Nao watautafuta uso wangu;

katika taabu yao watanitafuta kwa bidii.”

New International Version

Hosea 5:1-15

Judgment Against Israel

1“Hear this, you priests!

Pay attention, you Israelites!

Listen, royal house!

This judgment is against you:

You have been a snare at Mizpah,

a net spread out on Tabor.

2The rebels are knee-deep in slaughter.

I will discipline all of them.

3I know all about Ephraim;

Israel is not hidden from me.

Ephraim, you have now turned to prostitution;

Israel is corrupt.

4“Their deeds do not permit them

to return to their God.

A spirit of prostitution is in their heart;

they do not acknowledge the Lord.

5Israel’s arrogance testifies against them;

the Israelites, even Ephraim, stumble in their sin;

Judah also stumbles with them.

6When they go with their flocks and herds

to seek the Lord,

they will not find him;

he has withdrawn himself from them.

7They are unfaithful to the Lord;

they give birth to illegitimate children.

When they celebrate their New Moon feasts,

he will devour5:7 Or Now their New Moon feasts / will devour them and their fields.

8“Sound the trumpet in Gibeah,

the horn in Ramah.

Raise the battle cry in Beth Aven5:8 Beth Aven means house of wickedness (a derogatory name for Bethel, which means house of God).;

lead on, Benjamin.

9Ephraim will be laid waste

on the day of reckoning.

Among the tribes of Israel

I proclaim what is certain.

10Judah’s leaders are like those

who move boundary stones.

I will pour out my wrath on them

like a flood of water.

11Ephraim is oppressed,

trampled in judgment,

intent on pursuing idols.5:11 The meaning of the Hebrew for this word is uncertain.

12I am like a moth to Ephraim,

like rot to the people of Judah.

13“When Ephraim saw his sickness,

and Judah his sores,

then Ephraim turned to Assyria,

and sent to the great king for help.

But he is not able to cure you,

not able to heal your sores.

14For I will be like a lion to Ephraim,

like a great lion to Judah.

I will tear them to pieces and go away;

I will carry them off, with no one to rescue them.

15Then I will return to my lair

until they have borne their guilt

and seek my face—

in their misery

they will earnestly seek me.”