Hosea 4 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Hosea 4:1-19

Shtaka Dhidi Ya Israeli

14:1 Mit 10:21; 24:2; Mik 6:2; Isa 1:3; Ay 10:2; Yer 2:9; 7:28; 51:5; Hos 2:20Sikieni neno la Bwana, enyi Waisraeli,

kwa sababu Bwana analo shtaka

dhidi yenu ninyi mnaoishi katika nchi:

“Hakuna uaminifu, hakuna upendo,

hakuna kumjua Mungu katika nchi.

24:2 Isa 59:3; Hos 5:2; 6:2; 7:1; 11:12; Eze 22:2-9; 1Fal 21:16Kuna kulaani tu, uongo na uuaji,

wizi na uzinzi,

bila kuwa na mipaka,

nao umwagaji damu mmoja

baada ya mwingine.

34:3 Yer 4:25, 28; 9:10; Amo 8:8; Isa 15:6; 33:9; Sef 1:3Kwa sababu hii nchi huomboleza,

wote waishio ndani mwake wanadhoofika,

wanyama wa kondeni, ndege wa angani

na samaki wa baharini wanakufa.

44:4 Kum 17:12; Eze 3:26“Lakini mtu awaye yote na asilete shtaka,

mtu yeyote na asimlaumu mwenzake,

kwa maana watu wako ni kama wale

waletao mashtaka dhidi ya kuhani.

54:5 Eze 7:19; 14:7; Hos 2:2Unajikwaa usiku na mchana,

nao manabii hujikwaa pamoja nawe.

Kwa hiyo nitamwangamiza mama yako:

64:6 Mit 10:21; Hos 2:13; 8:1-12; Mal 2:7-8watu wangu wanaangamizwa

kwa kukosa maarifa,

“Kwa kuwa wewe umeyakataa maarifa,

mimi nami nitakukataa wewe

usiwe kuhani kwangu mimi;

kwa kuwa umeacha kuijali sheria ya Mungu wako

mimi nami sitawajali watoto wako.

74:7 Hab 2:16; Hos 9:11; 13:6Kadiri makuhani walivyoongezeka,

ndivyo walivyozidi kutenda dhambi dhidi yangu,

walibadilisha utukufu wao kwa kitu cha aibu.

84:8 Isa 56:11; Mik 3:11; Hos 14:1Hujilisha dhambi za watu wangu

na kupendezwa na uovu wao.

94:9 Isa 24:2; Yer 5:31; Hos 8:13; 10:10; 12:2Hata itakuwa: Kama walivyo watu,

ndivyo walivyo makuhani.

Nitawaadhibu wote wawili kwa ajili ya njia zao

na kuwalipa kwa matendo yao.

104:10 Mik 6:14; Isa 55:2; Hos 7:14; 9:17; Eze 22:9; Law 26:26“Watakula lakini hawatashiba;

watajiingiza katika ukahaba

lakini hawataongezeka,

kwa sababu wamemwacha Bwana

na kujiingiza wenyewe

114:11 Isa 28:7; Hos 5:4; Mit 20:1; Law 10:9; 1Sam 25:36katika ukahaba,

divai ya zamani na divai mpya,

ambavyo huondoa ufahamu

124:12 Yer 2:27; Ufu 17:2; Hab 2:19; Isa 44:20; Hes 15:39; Za 73:27wa watu wangu.

Hutaka shauri kutoka kwa sanamu ya mti

nao hujibiwa na fimbo ya mti.

Roho ya ukahaba imewapotosha,

hawana uaminifu kwa Mungu wao.

134:13 Isa 1:28; Hos 2:13; 10:9; Yer 2:20; Amo 7:17; Rum 1:28Wanatoa dhabihu juu ya vilele vya milima

na sadaka za kuteketezwa juu ya vilima,

chini ya mialoni, milibua na miela,

ambako kuna vivuli vizuri.

Kwa hiyo binti zenu wamegeukia ukahaba

na wake za wana wenu uzinzi.

144:14 Mwa 38:21; Hos 9:10; Mit 10:21“Sitawaadhibu binti zenu wakati

wanapogeukia ukahaba,

wala wake za wana wenu

wanapofanya uzinzi,

kwa sababu wanaume wenyewe huandamana na malaya

na kutambikia pamoja na makahaba

wa mahali pa kuabudia miungu:

watu wasiokuwa na ufahamu

wataangamia!

154:15 Hos 9:15; 12:11; Amo 4:4; Yos 7:2“Ingawa umefanya uzinzi, ee Israeli,

Yuda naye asije akawa na hatia.

“Usiende Gilgali,

usipande kwenda Beth-Aveni4:15 Beth-Aveni maana yake Nyumba ya Ubatili (au Uovu), jina lingine la Betheli kwa dhihaka.

Wala usiape,

‘Hakika kama Bwana aishivyo!’

164:16 Isa 5:17; 7:25; Kut 32:9; Yer 31:18Waisraeli ni wakaidi,

kama mtamba wa ngʼombe ambaye ni mkaidi.

Ni jinsi gani basi Bwana anaweza kuwachunga

kama wana-kondoo

katika shamba la majani?

174:17 Mt 15:14Efraimu amejiunga na sanamu,

ondokana naye!

184:18 Mik 3:11; 7:3Hata wakati wamemaliza vileo vyao

wanaendelea na ukahaba wao,

watawala wao hupenda sana

njia za aibu.

194:19 Hos 12:11; 13:15; Isa 1:29Kisulisuli kitawafagilia mbali

na dhabihu zao zitawaletea aibu.

King James Version

Hosea 4:1-19

1Hear the word of the LORD, ye children of Israel: for the LORD hath a controversy with the inhabitants of the land, because there is no truth, nor mercy, nor knowledge of God in the land. 2By swearing, and lying, and killing, and stealing, and committing adultery, they break out, and blood toucheth blood.4.2 blood: Heb. bloods 3Therefore shall the land mourn, and every one that dwelleth therein shall languish, with the beasts of the field, and with the fowls of heaven; yea, the fishes of the sea also shall be taken away. 4Yet let no man strive, nor reprove another: for thy people are as they that strive with the priest. 5Therefore shalt thou fall in the day, and the prophet also shall fall with thee in the night, and I will destroy thy mother.4.5 destroy: Heb. cut off

6¶ My people are destroyed for lack of knowledge: because thou hast rejected knowledge, I will also reject thee, that thou shalt be no priest to me: seeing thou hast forgotten the law of thy God, I will also forget thy children.4.6 destroyed: Heb. cut off 7As they were increased, so they sinned against me: therefore will I change their glory into shame. 8They eat up the sin of my people, and they set their heart on their iniquity.4.8 set…: Heb. lift up their soul to 9And there shall be, like people, like priest: and I will punish them for their ways, and reward them their doings.4.9 punish: Heb. visit upon4.9 reward: Heb. cause to return 10For they shall eat, and not have enough: they shall commit whoredom, and shall not increase: because they have left off to take heed to the LORD. 11Whoredom and wine and new wine take away the heart.

12¶ My people ask counsel at their stocks, and their staff declareth unto them: for the spirit of whoredoms hath caused them to err, and they have gone a whoring from under their God. 13They sacrifice upon the tops of the mountains, and burn incense upon the hills, under oaks and poplars and elms, because the shadow thereof is good: therefore your daughters shall commit whoredom, and your spouses shall commit adultery. 14I will not punish your daughters when they commit whoredom, nor your spouses when they commit adultery: for themselves are separated with whores, and they sacrifice with harlots: therefore the people that doth not understand shall fall.4.14 I will not: or, Shall I not4.14 fall: or, be punished

15¶ Though thou, Israel, play the harlot, yet let not Judah offend; and come not ye unto Gilgal, neither go ye up to Beth-aven, nor swear, The LORD liveth. 16For Israel slideth back as a backsliding heifer: now the LORD will feed them as a lamb in a large place. 17Ephraim is joined to idols: let him alone. 18Their drink is sour: they have committed whoredom continually: her rulers with shame do love, Give ye.4.18 sour: Heb. gone4.18 rulers: Heb. shields 19The wind hath bound her up in her wings, and they shall be ashamed because of their sacrifices.