Hosea 2 – NEN & NIV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Hosea 2:1-23

12:1 1Pet 2:10; Hos 2:5“Waambie ndugu zako, ‘Watu wangu,’ na pia waambie dada zako, ‘Wapendwa wangu.’

Israeli Aadhibiwa Na Kurudishwa

22:2 Isa 1:21; 50:1; Eze 16:25; 23:45; Hos 4:5“Mkemeeni mama yenu, mkemeeni,

kwa maana yeye si mke wangu,

nami si mume wake.

Aondoe sura ya uzinzi katika uso wake

na uzinzi kati ya matiti yake.

32:3 Eze 16:4, 37; 19:13; Isa 32:13-14Kama sivyo nitamvua nguo zake awe uchi

na kumwacha uchi kama siku ile aliyozaliwa.

Nitamfanya kama jangwa,

nitamgeuza awe nchi ya kiu,

nami nitamuua kwa kiu.

42:4 Eze 8:18; Hos 1:6; 5:7Sitaonyesha upendo wangu kwa watoto wake,

kwa sababu ni watoto wa uzinzi.

52:5 Yer 3:6; 44:17-18; Hos 1:2Mama yao amekosa uaminifu

na amewachukua mimba katika aibu.

Gomeri alisema, ‘Nitawaendea wapenzi wangu,

ambao hunipa chakula changu

na maji yangu,

sufu yangu na kitani yangu, mafuta yangu

na kinywaji changu.’

62:6 Ay 3:23; 19:8; Mao 3:9Kwa hiyo mimi Mungu nitaizuia njia yake

kwa vichaka vya miiba,

nitamjengea ukuta ili kwamba

asiweze kutoka.

72:7 Hos 5:13; Yer 3:1; Eze 16:8; Isa 54:5Gomeri atawafuatia wapenzi wake lakini hatawapata;

atawatafuta lakini hatawapata.

Kisha atasema,

‘Nitarudi kwa mume wangu kama kwanza,

kwa maana nilikuwa na hali njema zaidi

kuliko sasa.’

82:8 Eze 16:15-19; Hes 18:12; Kum 8:18; Hos 8:4Gomeri hajakubali kuwa mimi ndiye

niliyempa nafaka, divai mpya na mafuta,

niliyemwongezea fedha na dhahabu waliyoitumia

kwa kumtumikia Baali.

92:9 Hos 8:7; 9:2“Kwa hiyo nitachukua nafaka yangu wakati itakapokomaa

na divai yangu mpya wakati itakapokuwa tayari.

Nitamnyangʼanya sufu yangu na kitani yangu

iliyokusudiwa kufunika uchi wake.

102:10 Eze 16:37; 23:10; Yer 13:26Basi sasa nitaufunua ufisadi wake

mbele ya wapenzi wake;

hakuna yeyote atakayemtoa

mikononi mwangu.

112:11 Isa 1:14; 24:8; Amo 5:21; 8:10; Yer 7:34; 16:9; Hos 9:5Nitakomesha furaha na macheko yake yote:

sikukuu zake za mwaka,

sikukuu za Miandamo ya Mwezi,

siku zake za Sabato,

sikukuu zake zote zilizoamriwa.

122:12 Isa 5:6; 7:23; Yer 8:13; Hos 5:7; 13:8Nitaiharibu mizabibu yake na mitini yake,

ambayo alisema yalikuwa malipo yake

kutoka kwa wapenzi wake;

nitaifanya kuwa kichaka,

nao wanyama pori wataila.

132:13 Yer 7:9; Hos 4:13; 8:14; 11:2; 13:6; Eze 16:17; 23:40; Isa 65:7Nitamwadhibu kwa ajili ya siku

alizowafukizia uvumba Mabaali;

alipojipamba kwa pete

na kwa vito vya thamani,

na kuwaendea wapenzi wake,

lakini mimi alinisahau,”

asema Bwana.

142:14 Eze 19:14“Kwa hiyo sasa nitamshawishi;

nitamwongoza hadi jangwani

na kuzungumza naye kwa upole.

152:15 Yos 7:24-26; Kut 15:1-18; Eze 16:22; 28:26; Hos 12:9; 1Kor 13:13Huko nitamrudishia mashamba yake ya mizabibu,

nami nitalifanya Bonde la Akori2:15 Akori maana yake ni Taabu.

mlango wa matumaini.

Huko ataimba kama alivyofanya katika siku za ujana wake,

kama siku zile alizotoka Misri.

162:16 Isa 54:5“Katika siku ile,” asema Bwana,

“utaniita mimi ‘Mume wangu’;

hutaniita tena mimi ‘Bwana wangu.’

172:17 Kut 23:13; Za 16:4; Yer 23:7; Zek 13:2Nitaondoa majina ya Mabaali kutoka midomoni mwake,

wala hataomba tena kwa majina yao.

182:18 Ay 5:22-23; Za 49:6; Zek 9:10; Eze 34:25; Yer 23:6Katika siku ile nitafanya Agano kwa ajili yao

na wanyama wa kondeni, na ndege wa angani,

na viumbe vile vitambaavyo ardhini.

Upinde, upanga na vita,

nitaondolea mbali katika nchi,

ili kwamba wote waweze kukaa salama.

192:19 Isa 1:27; 62:4; 54:8; 2Kor 11:2Nitakuposa uwe wangu milele;

nitakuposa kwa uadilifu na haki,

kwa upendo na huruma.

202:20 Yer 31:34; Hos 4:1; 6:6; 13:4; Eze 16:8Nitakuposa kwa uaminifu,

nawe utamkubali Bwana.

212:21 Zek 8:12; Mal 3:10-11; Isa 55:10“Katika siku ile nitajibu,”

asema Bwana,

“nitajibu kwa anga,

nazo anga zitajibu kwa nchi;

222:22 Yer 31:12; Yoe 2:19; Hos 14:7; Eze 36:29-30nayo nchi itajibu kwa nafaka,

divai mpya na mafuta,

navyo vitajibu kwa Yezreeli.

232:23 Yer 29:12; 31:27; Isa 19:25; Hos 1:10; Rum 9:25; Zek 13:9; 1Pet 2:10Nitampanda katika nchi kwa ajili yangu mwenyewe;

nami nitaonyesha pendo langu kwake

yule ambaye nilimwita, ‘Si mpenzi wangu.2:23 Kiebrania ni Lo-Ruhama.

Nitawaambia wale walioitwa, ‘Sio watu wangu,’2:23 Kiebrania ni Lo-Ami.

‘Ninyi ni watu wangu’;

nao watasema, ‘Wewe ndiwe Mungu wangu.’ ”

New International Version

Hosea 2:1-23

In Hebrew texts 2:1-23 is numbered 2:3-25. 1“Say of your brothers, ‘My people,’ and of your sisters, ‘My loved one.’

Israel Punished and Restored

2“Rebuke your mother, rebuke her,

for she is not my wife,

and I am not her husband.

Let her remove the adulterous look from her face

and the unfaithfulness from between her breasts.

3Otherwise I will strip her naked

and make her as bare as on the day she was born;

I will make her like a desert,

turn her into a parched land,

and slay her with thirst.

4I will not show my love to her children,

because they are the children of adultery.

5Their mother has been unfaithful

and has conceived them in disgrace.

She said, ‘I will go after my lovers,

who give me my food and my water,

my wool and my linen, my olive oil and my drink.’

6Therefore I will block her path with thornbushes;

I will wall her in so that she cannot find her way.

7She will chase after her lovers but not catch them;

she will look for them but not find them.

Then she will say,

‘I will go back to my husband as at first,

for then I was better off than now.’

8She has not acknowledged that I was the one

who gave her the grain, the new wine and oil,

who lavished on her the silver and gold—

which they used for Baal.

9“Therefore I will take away my grain when it ripens,

and my new wine when it is ready.

I will take back my wool and my linen,

intended to cover her naked body.

10So now I will expose her lewdness

before the eyes of her lovers;

no one will take her out of my hands.

11I will stop all her celebrations:

her yearly festivals, her New Moons,

her Sabbath days—all her appointed festivals.

12I will ruin her vines and her fig trees,

which she said were her pay from her lovers;

I will make them a thicket,

and wild animals will devour them.

13I will punish her for the days

she burned incense to the Baals;

she decked herself with rings and jewelry,

and went after her lovers,

but me she forgot,”

declares the Lord.

14“Therefore I am now going to allure her;

I will lead her into the wilderness

and speak tenderly to her.

15There I will give her back her vineyards,

and will make the Valley of Achor2:15 Achor means trouble. a door of hope.

There she will respond2:15 Or sing as in the days of her youth,

as in the day she came up out of Egypt.

16“In that day,” declares the Lord,

“you will call me ‘my husband’;

you will no longer call me ‘my master.2:16 Hebrew baal

17I will remove the names of the Baals from her lips;

no longer will their names be invoked.

18In that day I will make a covenant for them

with the beasts of the field, the birds in the sky

and the creatures that move along the ground.

Bow and sword and battle

I will abolish from the land,

so that all may lie down in safety.

19I will betroth you to me forever;

I will betroth you in2:19 Or with; also in verse 20 righteousness and justice,

in2:19 Or with love and compassion.

20I will betroth you in faithfulness,

and you will acknowledge the Lord.

21“In that day I will respond,”

declares the Lord

“I will respond to the skies,

and they will respond to the earth;

22and the earth will respond to the grain,

the new wine and the olive oil,

and they will respond to Jezreel.2:22 Jezreel means God plants.

23I will plant her for myself in the land;

I will show my love to the one I called ‘Not my loved one.2:23 Hebrew Lo-Ruhamah (see 1:6)

I will say to those called ‘Not my people,2:23 Hebrew Lo-Ammi (see 1:9)’ ‘You are my people’;

and they will say, ‘You are my God.’ ”