Hosea 2 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Hosea 2:1-23

12:1 1Pet 2:10; Hos 2:5“Waambie ndugu zako, ‘Watu wangu,’ na pia waambie dada zako, ‘Wapendwa wangu.’

Israeli Aadhibiwa Na Kurudishwa

22:2 Isa 1:21; 50:1; Eze 16:25; 23:45; Hos 4:5“Mkemeeni mama yenu, mkemeeni,

kwa maana yeye si mke wangu,

nami si mume wake.

Aondoe sura ya uzinzi katika uso wake

na uzinzi kati ya matiti yake.

32:3 Eze 16:4, 37; 19:13; Isa 32:13-14Kama sivyo nitamvua nguo zake awe uchi

na kumwacha uchi kama siku ile aliyozaliwa.

Nitamfanya kama jangwa,

nitamgeuza awe nchi ya kiu,

nami nitamuua kwa kiu.

42:4 Eze 8:18; Hos 1:6; 5:7Sitaonyesha upendo wangu kwa watoto wake,

kwa sababu ni watoto wa uzinzi.

52:5 Yer 3:6; 44:17-18; Hos 1:2Mama yao amekosa uaminifu

na amewachukua mimba katika aibu.

Gomeri alisema, ‘Nitawaendea wapenzi wangu,

ambao hunipa chakula changu

na maji yangu,

sufu yangu na kitani yangu, mafuta yangu

na kinywaji changu.’

62:6 Ay 3:23; 19:8; Mao 3:9Kwa hiyo mimi Mungu nitaizuia njia yake

kwa vichaka vya miiba,

nitamjengea ukuta ili kwamba

asiweze kutoka.

72:7 Hos 5:13; Yer 3:1; Eze 16:8; Isa 54:5Gomeri atawafuatia wapenzi wake lakini hatawapata;

atawatafuta lakini hatawapata.

Kisha atasema,

‘Nitarudi kwa mume wangu kama kwanza,

kwa maana nilikuwa na hali njema zaidi

kuliko sasa.’

82:8 Eze 16:15-19; Hes 18:12; Kum 8:18; Hos 8:4Gomeri hajakubali kuwa mimi ndiye

niliyempa nafaka, divai mpya na mafuta,

niliyemwongezea fedha na dhahabu waliyoitumia

kwa kumtumikia Baali.

92:9 Hos 8:7; 9:2“Kwa hiyo nitachukua nafaka yangu wakati itakapokomaa

na divai yangu mpya wakati itakapokuwa tayari.

Nitamnyangʼanya sufu yangu na kitani yangu

iliyokusudiwa kufunika uchi wake.

102:10 Eze 16:37; 23:10; Yer 13:26Basi sasa nitaufunua ufisadi wake

mbele ya wapenzi wake;

hakuna yeyote atakayemtoa

mikononi mwangu.

112:11 Isa 1:14; 24:8; Amo 5:21; 8:10; Yer 7:34; 16:9; Hos 9:5Nitakomesha furaha na macheko yake yote:

sikukuu zake za mwaka,

sikukuu za Miandamo ya Mwezi,

siku zake za Sabato,

sikukuu zake zote zilizoamriwa.

122:12 Isa 5:6; 7:23; Yer 8:13; Hos 5:7; 13:8Nitaiharibu mizabibu yake na mitini yake,

ambayo alisema yalikuwa malipo yake

kutoka kwa wapenzi wake;

nitaifanya kuwa kichaka,

nao wanyama pori wataila.

132:13 Yer 7:9; Hos 4:13; 8:14; 11:2; 13:6; Eze 16:17; 23:40; Isa 65:7Nitamwadhibu kwa ajili ya siku

alizowafukizia uvumba Mabaali;

alipojipamba kwa pete

na kwa vito vya thamani,

na kuwaendea wapenzi wake,

lakini mimi alinisahau,”

asema Bwana.

142:14 Eze 19:14“Kwa hiyo sasa nitamshawishi;

nitamwongoza hadi jangwani

na kuzungumza naye kwa upole.

152:15 Yos 7:24-26; Kut 15:1-18; Eze 16:22; 28:26; Hos 12:9; 1Kor 13:13Huko nitamrudishia mashamba yake ya mizabibu,

nami nitalifanya Bonde la Akori2:15 Akori maana yake ni Taabu.

mlango wa matumaini.

Huko ataimba kama alivyofanya katika siku za ujana wake,

kama siku zile alizotoka Misri.

162:16 Isa 54:5“Katika siku ile,” asema Bwana,

“utaniita mimi ‘Mume wangu’;

hutaniita tena mimi ‘Bwana wangu.’

172:17 Kut 23:13; Za 16:4; Yer 23:7; Zek 13:2Nitaondoa majina ya Mabaali kutoka midomoni mwake,

wala hataomba tena kwa majina yao.

182:18 Ay 5:22-23; Za 49:6; Zek 9:10; Eze 34:25; Yer 23:6Katika siku ile nitafanya Agano kwa ajili yao

na wanyama wa kondeni, na ndege wa angani,

na viumbe vile vitambaavyo ardhini.

Upinde, upanga na vita,

nitaondolea mbali katika nchi,

ili kwamba wote waweze kukaa salama.

192:19 Isa 1:27; 62:4; 54:8; 2Kor 11:2Nitakuposa uwe wangu milele;

nitakuposa kwa uadilifu na haki,

kwa upendo na huruma.

202:20 Yer 31:34; Hos 4:1; 6:6; 13:4; Eze 16:8Nitakuposa kwa uaminifu,

nawe utamkubali Bwana.

212:21 Zek 8:12; Mal 3:10-11; Isa 55:10“Katika siku ile nitajibu,”

asema Bwana,

“nitajibu kwa anga,

nazo anga zitajibu kwa nchi;

222:22 Yer 31:12; Yoe 2:19; Hos 14:7; Eze 36:29-30nayo nchi itajibu kwa nafaka,

divai mpya na mafuta,

navyo vitajibu kwa Yezreeli.

232:23 Yer 29:12; 31:27; Isa 19:25; Hos 1:10; Rum 9:25; Zek 13:9; 1Pet 2:10Nitampanda katika nchi kwa ajili yangu mwenyewe;

nami nitaonyesha pendo langu kwake

yule ambaye nilimwita, ‘Si mpenzi wangu.2:23 Kiebrania ni Lo-Ruhama.

Nitawaambia wale walioitwa, ‘Sio watu wangu,’2:23 Kiebrania ni Lo-Ami.

‘Ninyi ni watu wangu’;

nao watasema, ‘Wewe ndiwe Mungu wangu.’ ”

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

何西阿書 2:1-23

1「你們要稱你們的弟兄為阿米2·1 阿米」意思是「我的子民」。,要稱你們的姊妹為路哈瑪2·1 路哈瑪」意思是「得蒙憐憫」。

對不貞之婦的控訴

2「你們去跟你們的母親理論吧!

因為她不再是我的妻子,

我也不再是她的丈夫。

叫她別再出賣色相,

別再露出乳間的淫態。

3不然,我要剝光她的衣服,

使她像初生之時一樣赤身露體;

我要使她像沙漠,如旱地,

乾渴而死。

4我也不憐憫她的兒女,

因為他們都是娼妓所生的兒女。

5他們的母親淫亂放蕩,厚顏無恥,

她說,『我要跟隨我的情人,

他們給我食物和水、羊毛和麻布、油和酒。』

6因此,我要用荊棘圍堵她,

築牆阻斷她的去路。

7她要追隨情人,卻追不上;

尋找情人,卻找不到。

於是,她說,『我倒不如回到丈夫身邊,

我從前的光景比現在還好。』

8她不知道是我給她五穀、新酒和油,

又賜給她大量金銀——

她卻用這些供奉巴力

9因此,到了收割和釀酒的季節,

我要收走我的五穀和新酒,

奪回我給她遮體的羊毛和麻布。

10我要當著她情人的面剝光她的衣服,

顯出她的淫態,

無人能從我手中把她救出去。

11我要終止她一切的歡慶,

終止她的年節、朔日2·11 朔日」即每月初一。、安息日及其他節期。

12她說她的葡萄樹和無花果樹是情人給她的報酬,

我要摧毀它們,

使它們變為荒林,

被野獸吞吃。

13我要懲罰她,

因為她在節日向巴力燒香。

那時她戴耳環佩首飾,

追逐她的情人,把我忘記。

這是耶和華說的。

對不貞之婦的愛

14「然而,我要挽回她,

領她到曠野,

柔聲安慰她。

15我要把葡萄園賜給她,

使災禍之谷2·15 災禍之谷」希伯來文是「亞割谷」,「亞割」意思是「災禍」。參見約書亞記第七章。成為希望之門。

她要在那裡快樂地歌唱,

如在妙齡時的日子,

如從埃及出來之時。」

16耶和華說:

「那時,你要稱我為丈夫,

不再稱我為主人2·16 此處的「主人」希伯來文是「巴力」。「巴力」意思是「主人或丈夫」,也是迦南人神明的名字。

17我要從你口中除掉巴力的名字,

再也不讓你提起。

18那時,我要跟田間的走獸、空中的飛鳥及地上的爬蟲立約,

使牠們不再傷害你。

我要在你境內毀滅戰弓和刀劍,止息戰事,

使你安居樂業。

19我要聘你永遠做我的妻,

以仁義、正直、慈愛、憐憫聘你。

20我要以信實聘你為妻,

這樣你必認識耶和華。」

21耶和華說:

「那時,我要應允,

我要應允天的祈求,

天要應允地的祈求,

22地要應允五穀、新酒和油的祈求,

五穀、新酒和油要應允耶斯列的祈求。

23我要把你栽種在這片土地上,歸我所有。

我要憐憫那不蒙憐憫的人,

對那不是我子民的人說,『你是我的子民。』

他們也要對我說,『你是我的上帝。』」