Hosea 13 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Hosea 13:1-16

Hasira Ya Bwana Dhidi Ya Israeli

113:1 Mit 18:12; Amu 8:1; 12:1; Hos 11:2Wakati Efraimu alipozungumza, watu walitetemeka,

alikuwa ametukuzwa katika Israeli.

Lakini alikuwa na hatia ya kumwabudu Baali

naye akafa.

213:2 Isa 46:6; Yer 10:4; 44:8; Isa 44:17-20; Hos 8:4; 1Fal 19:18Sasa wanatenda dhambi zaidi na zaidi;

wanajitengenezea sanamu

kutokana na fedha yao,

vinyago vilivyotengenezwa kwa uhodari,

vyote kazi ya fundi stadi.

Inasemekana kuhusu hawa watu,

“Hutoa dhabihu za binadamu

na kubusu sanamu za ndama.”

313:3 Hos 6:4; Ay 13:25; Dan 2:35; Za 68:213:3 Isa 17:13Kwa hiyo watakuwa kama ukungu wa asubuhi,

kama umande wa alfajiri utowekao,

kama makapi yapeperushwayo

kutoka sakafu ya kupuria nafaka,

kama moshi utorokao kupitia dirishani.

413:4 Yer 2:6; Isa 43:10; 45:21-22; Hos 2:20; 12:9; Kut 20:3; Za 18:46“Bali mimi ndimi Bwana Mungu wenu,

niliyewaleta ninyi toka Misri.

Msimkubali Mungu mwingine ila mimi,

hakuna Mwokozi isipokuwa mimi.

513:5 Kum 1:19; 2:7; 32:10; 8:15; 32:10Niliwatunza huko jangwani,

katika nchi yenye joto liunguzalo.

613:6 Mit 30:7-9; Yer 7:5; Eze 28:5; Kum 32:18; Isa 17:10; Hos 2:13; 4:7Nilipowalisha, walishiba,

waliposhiba, wakajivuna,

kisha wakanisahau mimi.

713:7 Ay 10:16; Yer 4:7; Mao 3:10Kwa hiyo nitakuja juu yao kama simba,

kama chui nitawavizia kando ya njia.

813:8 2Sam 17:8; Za 17:12; 50:22; Mao 3:10; Hos 2:12Kama dubu aliyenyangʼanywa watoto wake,

nitawashambulia na kurarua vifua vyenu.

Kama simba nitawala;

mnyama pori atawararua vipande vipande.

913:9 Yer 2:17-19; Kum 33:29“Ee Israeli, umeangamizwa,

kwa sababu wewe u kinyume nami,

kinyume na msaidizi wako.

1013:10 2Fal 17:4; 1Sam 8:6; Hos 7:7; 8:4Yuko wapi mfalme wako,

ili apate kukuokoa?

Wako wapi watawala wako katika miji yako yote

ambao ulisema kuwahusu,

‘Nipe mfalme na wakuu’?

1113:11 Yos 24:20; 1Sam 13:14; Hes 11:20; 1Fal 14:10; Hos 10:7Hivyo katika hasira yangu nilikupa mfalme

na katika ghadhabu yangu nilimwondoa.

1213:12 Kum 32:34; Ay 14:7Kosa la Efraimu limehifadhiwa,

dhambi zake zimewekwa katika kumbukumbu.

1313:13 Isa 13:8; Mik 4:9-10; Isa 66:9; 2Fal 19:3Utungu kama wa mwanamke anayejifungua mtoto humjia,

lakini yeye ni mtoto asiyekuwa na hekima;

wakati utakapowadia hatatoka

katika tumbo la mama yake.

1413:14 1The 4:14-17; Za 16:10; 49:15; Eze 37:12-13; 1Kor 15:54-55; Ufu 21:4“Nitawakomboa watu hawa kutoka nguvu za kaburi,

nitawakomboa kutoka mautini.

Yako wapi, ee mauti, mateso yako?

Uko wapi, ee kuzimu, uharibifu wako?

“Sitakuwa na huruma,

1513:15 Ay 1:19; Eze 19:12; Yer 20:5; 51:36; Hos 4:19hata ingawa Efraimu atastawi

miongoni mwa ndugu zake.

Upepo wa mashariki kutoka kwa Bwana utakuja,

ukivuma kutoka jangwani,

chemchemi yake haitatoa maji

na kisima chake kitakauka.

Ghala lake litatekwa

hazina zake zote.

1613:16 2Fal 8:12; 15:16; 17:5; Hos 7:14; 10:2, 14; Isa 13:16; Amo 1:13Watu wa Samaria ni lazima wabebe hatia yao,

kwa sababu wameasi dhidi ya Mungu wao.

Wataanguka kwa upanga;

watoto wao wadogo watatupwa kwa nguvu ardhini,

wanawake wao walio na mimba watatumbuliwa.”

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

何西阿書 13:1-16

對以色列的最後審判

1以法蓮支派在以色列地位崇高,

他們一開口,人都恐懼顫抖。

但他們卻祭拜巴力,自招滅亡。

2如今他們作惡日甚,

憑藉自己的聰明用銀子鑄造神像,

但這不過是匠人之作。

人們議論他們說:

「那些獻祭的人竟親吻牛犢偶像!」

3他們像晨霧,如轉瞬即逝的朝露,

像麥場上飛旋而去的糠秕,

又像窗口冒出的輕煙。

4耶和華說:

「自從你們離開埃及以來,

我就是你們的上帝耶和華。

除我以外,你們不可有別的神明;

在我以外,你們也沒有別的救主。

5我曾在乾旱的曠野照顧你們,

6但你們吃得飽足以後,

就心高氣傲,忘記了我。

7因此,我要像獅子攻擊你們,

如豹子潛伏在路旁;

8我要像一頭失了幼崽的母熊衝向你們,

撕裂你們的胸膛;

我要像母獅吞噬你們,

像兇猛的野獸撕碎你們。

9以色列啊,你要滅亡了,

因為你抵擋我,抵擋你的幫助者。

10你曾求我為你設立君王和首領,

現在拯救你的君王在哪裡呢?

在各城管理你的首領在哪裡呢?

11我在憤怒中賜給你君王,

也在憤怒中廢黜他們。

12以法蓮的過犯已被記錄在冊,

他的罪惡已被儲存入庫。

13臨產的陣痛要臨到他,

但他是毫無智慧的孩子,

分娩之時卻不離開母腹。

14我要把他們從陰間的權勢下贖回嗎?

我要救他們脫離死亡嗎?

死亡啊,你去降災給他們吧!

陰間啊,你去毀滅他們吧!

我不會再憐憫他們。

15儘管以法蓮在眾弟兄中最強盛,

但炙熱的東風——耶和華的風要從沙漠颳來,

使清泉枯竭,水井乾涸。

他儲藏的一切珍寶都要被擄去。

16撒瑪利亞人背叛了他們的上帝,

要擔當自己的罪過。

他們將喪身刀下,

他們的孩子要被摔死,

孕婦要被剖腹。」