Hosea 13 – NEN & CARS

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Hosea 13:1-16

Hasira Ya Bwana Dhidi Ya Israeli

113:1 Mit 18:12; Amu 8:1; 12:1; Hos 11:2Wakati Efraimu alipozungumza, watu walitetemeka,

alikuwa ametukuzwa katika Israeli.

Lakini alikuwa na hatia ya kumwabudu Baali

naye akafa.

213:2 Isa 46:6; Yer 10:4; 44:8; Isa 44:17-20; Hos 8:4; 1Fal 19:18Sasa wanatenda dhambi zaidi na zaidi;

wanajitengenezea sanamu

kutokana na fedha yao,

vinyago vilivyotengenezwa kwa uhodari,

vyote kazi ya fundi stadi.

Inasemekana kuhusu hawa watu,

“Hutoa dhabihu za binadamu

na kubusu sanamu za ndama.”

313:3 Hos 6:4; Ay 13:25; Dan 2:35; Za 68:213:3 Isa 17:13Kwa hiyo watakuwa kama ukungu wa asubuhi,

kama umande wa alfajiri utowekao,

kama makapi yapeperushwayo

kutoka sakafu ya kupuria nafaka,

kama moshi utorokao kupitia dirishani.

413:4 Yer 2:6; Isa 43:10; 45:21-22; Hos 2:20; 12:9; Kut 20:3; Za 18:46“Bali mimi ndimi Bwana Mungu wenu,

niliyewaleta ninyi toka Misri.

Msimkubali Mungu mwingine ila mimi,

hakuna Mwokozi isipokuwa mimi.

513:5 Kum 1:19; 2:7; 32:10; 8:15; 32:10Niliwatunza huko jangwani,

katika nchi yenye joto liunguzalo.

613:6 Mit 30:7-9; Yer 7:5; Eze 28:5; Kum 32:18; Isa 17:10; Hos 2:13; 4:7Nilipowalisha, walishiba,

waliposhiba, wakajivuna,

kisha wakanisahau mimi.

713:7 Ay 10:16; Yer 4:7; Mao 3:10Kwa hiyo nitakuja juu yao kama simba,

kama chui nitawavizia kando ya njia.

813:8 2Sam 17:8; Za 17:12; 50:22; Mao 3:10; Hos 2:12Kama dubu aliyenyangʼanywa watoto wake,

nitawashambulia na kurarua vifua vyenu.

Kama simba nitawala;

mnyama pori atawararua vipande vipande.

913:9 Yer 2:17-19; Kum 33:29“Ee Israeli, umeangamizwa,

kwa sababu wewe u kinyume nami,

kinyume na msaidizi wako.

1013:10 2Fal 17:4; 1Sam 8:6; Hos 7:7; 8:4Yuko wapi mfalme wako,

ili apate kukuokoa?

Wako wapi watawala wako katika miji yako yote

ambao ulisema kuwahusu,

‘Nipe mfalme na wakuu’?

1113:11 Yos 24:20; 1Sam 13:14; Hes 11:20; 1Fal 14:10; Hos 10:7Hivyo katika hasira yangu nilikupa mfalme

na katika ghadhabu yangu nilimwondoa.

1213:12 Kum 32:34; Ay 14:7Kosa la Efraimu limehifadhiwa,

dhambi zake zimewekwa katika kumbukumbu.

1313:13 Isa 13:8; Mik 4:9-10; Isa 66:9; 2Fal 19:3Utungu kama wa mwanamke anayejifungua mtoto humjia,

lakini yeye ni mtoto asiyekuwa na hekima;

wakati utakapowadia hatatoka

katika tumbo la mama yake.

1413:14 1The 4:14-17; Za 16:10; 49:15; Eze 37:12-13; 1Kor 15:54-55; Ufu 21:4“Nitawakomboa watu hawa kutoka nguvu za kaburi,

nitawakomboa kutoka mautini.

Yako wapi, ee mauti, mateso yako?

Uko wapi, ee kuzimu, uharibifu wako?

“Sitakuwa na huruma,

1513:15 Ay 1:19; Eze 19:12; Yer 20:5; 51:36; Hos 4:19hata ingawa Efraimu atastawi

miongoni mwa ndugu zake.

Upepo wa mashariki kutoka kwa Bwana utakuja,

ukivuma kutoka jangwani,

chemchemi yake haitatoa maji

na kisima chake kitakauka.

Ghala lake litatekwa

hazina zake zote.

1613:16 2Fal 8:12; 15:16; 17:5; Hos 7:14; 10:2, 14; Isa 13:16; Amo 1:13Watu wa Samaria ni lazima wabebe hatia yao,

kwa sababu wameasi dhidi ya Mungu wao.

Wataanguka kwa upanga;

watoto wao wadogo watatupwa kwa nguvu ardhini,

wanawake wao walio na mimba watatumbuliwa.”

Священное Писание

Осия 13:1-15

Гнев Вечного против Исраила

1Когда Ефраим говорил, люди дрожали.

Он был возвышен в Исраиле,

но стал повинен в поклонении Баалу и погиб.

2Теперь они грешат всё больше и больше:

они делают для себя идолов из своего серебра,

мастерски отлитые истуканы;

всё это – изделия ремесленников.

Они говорят людям:

«Приносите жертвы

и целуйте идолов-тельцов».

3Поэтому они будут как утренний туман,

как роса, что вскоре исчезает,

словно мякина от зерна, сдуваемая ветром,

как дым, выходящий через дымоход.

4– Но Я – Вечный, ваш Бог,

Который вывел вас из Египта.

Вы не должны признавать другого Бога, кроме Меня,

и никакого спасителя, кроме Меня.

5Я заботился о вас в пустыне,

в обжигающей зноем земле.

6Когда Я кормил вас13:6 Или: «Когда у вас были пастбища»., вы насыщались,

а насытившись, становились гордыми;

поэтому вы забыли обо Мне.

7Итак, Я настигну вас, как лев,

как барс в ожидании, притаюсь у дороги.

8Как медведица, лишённая своих медвежат,

Я нападу на вас и раздеру вам грудь.

Как львица, Я буду поедать вас,

и, как дикое животное, буду раздирать вас на части.

9Я уничтожу тебя, Исраил,

потому что ты против Меня,

против своего Помощника.

10Где теперь твой царь?

Пусть он спасёт тебя во всех твоих городах!

Где твои судьи, о которых ты просил:

«Дай нам царя и вождей»?

11В Своём негодовании Я дал тебе царя,

и в гневе Своём Я забрал его.

12Беззаконие Ефраима завязано в узел,

грехи его хранятся.

13Его настигнут муки, как у женщины при родах,

но он – неразумное дитя;

ему пришло время родиться,

а он упирается, желая остаться в утробе.

14Я избавлю их от власти мира мёртвых,

Я искуплю их от смерти.

О смерть! Где твоё бедствие?

О мир мёртвых! Где твоё разрушение?

Я не пожалею об этом.

15Хотя Ефраим13:15 Букв.: «он». процветает среди своих братьев,

придёт восточный ветер от Вечного,

задует из пустыни,

и иссохнет родник его,

иссякнет источник его;

унесёт все его драгоценности

из сокровищницы.