Hosea 1 – NEN & NIV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Hosea 1:1-11

11:1 Mik 1:1; Isa 1:1; 2Fal 13:13; 14:12; 1Nya 3:12-13; Yer 1:2; 2Fal 14:21Neno la Bwana lililomjia Hosea mwana wa Beeri wakati wa utawala wa Uzia, Yothamu, Ahazi na Hezekia, wafalme wa Yuda, na wakati wa utawala wa Yeroboamu mwana wa Yehoashi, mfalme wa Israeli.

Mke Wa Hosea Na Watoto

21:2 Amu 2:17; Yer 3:14; Hos 2:5; 3:1; Yer 3:1; Kum 31:16Wakati Bwana alipoanza kuzungumza kupitia Hosea, Bwana alimwambia, “Nenda ukajitwalie mwanamke wa uzinzi na watoto wa uzinzi, kwa sababu nchi ina hatia ya uzinzi wa kupindukia kwa kumwacha Bwana.” 31:3 Hos 1:6Kwa hiyo alimwoa Gomeri binti Diblaimu, naye akachukua mimba na kumzalia Hosea mwana.

41:4 1Sam 29:1; 1Fal 18:45; 2Fal 10:1-14; Hos 2:22Kisha Bwana akamwambia Hosea, “Mwite Yezreeli,1:4 Yezreeli maana yake Mungu hupanda. kwa kuwa kitambo kidogo nitaiadhibu nyumba ya Yehu kwa ajili ya mauaji ya kule Yezreeli, nami nitaukomesha ufalme wa Israeli. 51:5 Yos 15:56; 1Sam 29:1; 2Fal 15:29Katika siku ile nitavunja upinde wa Israeli katika Bonde la Yezreeli.”

61:6 Hos 2:4, 23; 1:6Gomeri akachukua tena mimba akamzaa binti. Kisha Bwana akamwambia Hosea, “Mwite Lo-Ruhama,1:6 Lo-Ruhama maana yake Sio mpenzi wangu. kwa maana sitaonyesha tena upendo kwa nyumba ya Israeli, kwamba nisije kabisa nikawasamehe. 71:7 Za 44:6; Zek 2:6Hata hivyo nitaonyesha upendo kwa nyumba ya Yuda, nami nitawaokoa si kwa upinde, upanga au vita, wala kwa farasi na wapanda farasi, bali kwa njia ya Bwana Mungu wao.”

8Baada ya Gomeri kumwachisha Lo-Ruhama kunyonya, Gomeri alipata mwana mwingine. 91:9 Eze 11:19-20; 1Pet 2:10Kisha Bwana akasema, “Mwite Lo-Ami1:9 Lo-Ami maana yake Sio watu wangu. kwa maana ninyi si watu wangu, nami si Mungu wenu.

101:10 Mwa 22:17; Yer 33:22; Rum 9:26; Hos 2:23; Hes 23:10; Yos 3:10“Hata hivyo Waisraeli watakuwa kama mchanga kando ya bahari, ambao hauwezi kupimika wala kuhesabiwa. Mahali pale walipoambiwa, ‘Ninyi si watu wangu,’ wao wataitwa ‘wana wa Mungu aliye hai.’ 111:11 Isa 11:12-13; Yer 23:5-8; 30:9; Eze 37:15-28Watu wa Yuda na watu wa Israeli wataunganishwa tena, nao watamchagua kiongozi mmoja nao watakwea watoke katika nchi, kwa kuwa siku ya Yezreeli itakuwa kuu sana.

New International Version

Hosea 1:1-11

1The word of the Lord that came to Hosea son of Beeri during the reigns of Uzziah, Jotham, Ahaz and Hezekiah, kings of Judah, and during the reign of Jeroboam son of Jehoash1:1 Hebrew Joash, a variant of Jehoash king of Israel:

Hosea’s Wife and Children

2When the Lord began to speak through Hosea, the Lord said to him, “Go, marry a promiscuous woman and have children with her, for like an adulterous wife this land is guilty of unfaithfulness to the Lord.” 3So he married Gomer daughter of Diblaim, and she conceived and bore him a son.

4Then the Lord said to Hosea, “Call him Jezreel, because I will soon punish the house of Jehu for the massacre at Jezreel, and I will put an end to the kingdom of Israel. 5In that day I will break Israel’s bow in the Valley of Jezreel.”

6Gomer conceived again and gave birth to a daughter. Then the Lord said to Hosea, “Call her Lo-Ruhamah (which means “not loved”), for I will no longer show love to Israel, that I should at all forgive them. 7Yet I will show love to Judah; and I will save them—not by bow, sword or battle, or by horses and horsemen, but I, the Lord their God, will save them.”

8After she had weaned Lo-Ruhamah, Gomer had another son. 9Then the Lord said, “Call him Lo-Ammi (which means “not my people”), for you are not my people, and I am not your God.1:9 Or your I am

10“Yet the Israelites will be like the sand on the seashore, which cannot be measured or counted. In the place where it was said to them, ‘You are not my people,’ they will be called ‘children of the living God.’ 11The people of Judah and the people of Israel will come together; they will appoint one leader and will come up out of the land, for great will be the day of Jezreel.1:11 In Hebrew texts 1:10,11 is numbered 2:1,2.