Hesabu 9 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Hesabu 9:1-23

Pasaka Huko Sinai

19:1 Hes 1:1; Kut 40:2Bwana akasema na Mose katika Jangwa la Sinai katika mwezi wa kwanza wa mwaka wa pili baada ya Waisraeli kutoka Misri. Akasema, 29:2 Kut 12:11; Hes 28:16; Ebr 10:1“Waamuru Waisraeli waadhimishe Pasaka katika wakati ulioamriwa. 39:3 Kut 12:2-11, 43-49; Law 23:5-8; Kum 16:1-8Adhimisheni wakati ulioamriwa, yaani wakati wa kuzama jua siku ya kumi na nne ya mwezi huu, kufuatana na desturi zake zote na masharti yake.”

49:4 Kut 12:11Hivyo Mose akawaambia Waisraeli waiadhimishe Pasaka, 59:5 Kut 12:6; Yos 5:10nao wakafanya hivyo kwenye Jangwa la Sinai wakati wa kuzama jua siku ya kumi na nne ya mwezi wa kwanza. Waisraeli wakafanya kila kitu kama vile Bwana alivyomwamuru Mose.

69:6 Law 5:3; 13:3; 21:11; Kut 18:15; Hes 27:2; Yn 18:28; Hes 6:6-7Lakini baadhi yao hawakuweza kuadhimisha Pasaka siku ile kwa sababu walikuwa najisi kwa taratibu za kiibada kwa ajili ya kugusa maiti. Kwa hiyo wakamwendea Mose na Aroni siku ile ile, 7wakamwambia Mose, “Tumekuwa najisi kwa sababu tumegusa maiti, lakini kwa nini tuzuiliwe kumtolea Bwana sadaka yake pamoja na Waisraeli wengine katika wakati ulioamriwa?”

89:8 Kut 18:15; Law 24:12; Hes 15:34; 27:5, 21; Za 85:8; Yn 7:17; Efe 1:9, 18; Ebr 3:5-6Mose akawajibu, “Ngojeni mpaka nitafute kile Bwana anachoagiza kuwahusu ninyi.”

9Ndipo Bwana akamwambia Mose, 109:10 2Nya 30:2“Waambie Waisraeli: ‘Wakati mmoja wenu au wazao wenu wanapokuwa najisi kwa sababu ya maiti au wakiwa safarini, hata hivyo wanaweza kuadhimisha Pasaka ya Bwana. 119:11 Kut 12:6-8; 2Nya 30:2, 15Wataiadhimisha wakati wa kuzama jua siku ya kumi na nne ya mwezi wa pili. Watamla mwana-kondoo, pamoja na mkate usiotiwa chachu, na mboga chungu. 129:12 Kut 12:8, 10, 43, 46; Yn 19:36Wasibakize chochote hadi asubuhi wala wasivunje mifupa ya mwana-kondoo. Wakati wanapoadhimisha Pasaka, hawana budi kufuata masharti yote. 139:13 Mwa 17:14; Kut 12:15; Law 17:4; Ebr 12:25; Hes 5:31; Gal 3:10; Ebr 10:26Lakini kama mtu ni safi kwa taratibu za kiibada naye hayuko safarini, asipoadhimisha Pasaka, mtu huyo hana budi kukatiliwa mbali na watu wake kwa sababu hakutoa sadaka ya Bwana kwa wakati ulioamriwa. Mtu huyo atawajibika kubeba matokeo ya dhambi yake.

149:14 Kut 12:19, 43-49“ ‘Mgeni anayeishi miongoni mwenu ambaye anataka kuadhimisha Pasaka ya Bwana, lazima afanye hivyo kwa kufuata desturi na masharti. Lazima masharti yawe sawasawa kwa mgeni na mzawa.’ ”

Wingu La Moto Juu Ya Maskani

(Kutoka 40:34-38)

159:15 Kut 38:21; 26:30; 33:16; 13:21; 40:34Katika siku hiyo ambayo Maskani, Hema la Ushuhuda, iliposimamishwa, wingu liliifunika. Kuanzia jioni mpaka asubuhi wingu lililokuwa juu ya Maskani lilionekana kama moto. 169:16 Kut 40:38; Kum 1:33; Neh 9:12Hivyo ndivyo lilivyoendelea kuwa; wingu liliifunika wakati wa mchana, na usiku lilionekana kama moto. 179:17 Kut 40:36-38; 1Kor 10:1; Za 78:14; Isa 49:10; Yn 10:4; Hes 9:21; Kut 13:21, 22Wakati wowote wingu lilipoinuka kutoka juu ya Hema, nao Waisraeli waliondoka; mahali popote wingu liliposimama, Waisraeli walipiga kambi. 189:18 Kut 40:37Kwa amri ya Bwana Waisraeli waliondoka, na kwa amri yake walipiga kambi. Kwa muda wote wingu liliposimama juu ya Maskani, Waisraeli walibaki wamepiga kambi.

199:19 Law 8:35; Kut 40:37Wakati wingu lilipobaki juu ya Maskani kwa muda mrefu, Waisraeli walitii amri ya Bwana nao hawakuondoka. 209:20 Za 48:14; Mit 3:5-6Wakati mwingine wingu lilikuwa juu ya Maskani kwa siku chache tu; kwa amri ya Bwana wangelipiga kambi na kisha kwa amri yake wangeliondoka. 219:21 Mt 28:20Wakati mwingine wingu lilikuwepo kuanzia jioni mpaka asubuhi tu, na lilipoinuka asubuhi, nao waliondoka. Ikiwa ni mchana au usiku, wakati wowote wingu lilipoinuka, waliondoka. 22Ikiwa wingu lilikaa juu ya Maskani kwa siku mbili au mwezi au mwaka, Waisraeli wangebaki wamepiga kambi na hawakuondoka; lakini lilipoinuka, wangeondoka.

239:23 Za 73:24; 107:7; Isa 63:14Kwa amri ya Bwana walipiga kambi, na kwa amri ya Bwana waliondoka. Walitii amri ya Bwana, kufuatana na agizo lake kupitia Mose.

New International Reader’s Version

Numbers 9:1-23

Israel Celebrates the Passover Feast

1The Lord spoke to Moses in the Desert of Sinai. It was the first month of the second year after the people came out of Egypt. He said, 2“Tell the Israelites to celebrate the Passover Feast. Have them do it at the appointed time. 3Celebrate it when the sun goes down on the 14th day of this month. Obey all its rules and laws.”

4So Moses told the Israelites to celebrate the Passover Feast. 5They did it in the Desert of Sinai. They celebrated it when the sun went down on the 14th day of the first month. The Israelites did everything just as the Lord had commanded Moses.

6But some of them couldn’t celebrate the Passover Feast on that day. That’s because they weren’t “clean.” They had gone near a dead body. So they came to Moses and Aaron that same day. 7They said to Moses, “We went near a dead body. So we aren’t ‘clean.’ But why should we be kept from bringing the Lord’s offering at the appointed time? Why shouldn’t we bring it along with the other Israelites?”

8Moses answered them, “Wait until I find out what the Lord wants you to do.”

9Then the Lord spoke to Moses. He said, 10“Tell the Israelites, ‘Suppose any of you or your children are “unclean” because they have gone near a dead body. Or suppose they are away on a journey. They must still celebrate the Lord’s Passover. 11They must celebrate it on the 14th day of the second month. They must do so when the sun goes down. They must eat the lamb together with bread made without yeast. They must eat it with bitter plants. 12They must not leave any of it until morning. They must not break any of its bones. When they celebrate the Passover Feast, they must follow all the rules. 13But suppose someone is “clean” and not on a journey. And they fail to celebrate the Passover Feast. Then they must be separated from the community of Israel. They did not bring the Lord’s offering at the appointed time. They will be punished for their sin.

14“ ‘What if there is an outsider living among you? And what if they want to celebrate the Lord’s Passover? Then they must obey its rules and laws. You must have the same laws for outsiders as you do for the Israelites.’ ”

The Cloud Covers the Holy Tent

15The holy tent was set up. It was the tent where the tablets of the covenant law were kept. On the day it was set up, the cloud covered it. From evening until morning the cloud above the tent looked like fire. 16That’s what continued to happen. The cloud covered the tent. At night the cloud looked like fire. 17When the cloud lifted from its place above the tent, the Israelites started out. Where the cloud settled, the Israelites camped. 18When the Lord gave the command, the Israelites started out. And when he gave the command, they camped. As long as the cloud stayed above the holy tent, they remained in camp. 19Sometimes the cloud remained above the tent for a long time. Then the Israelites obeyed the Lord’s order. They didn’t start out. 20Sometimes the cloud was above the tent for only a few days. When the Lord would give the command, they would camp. And when he would give the command, they would start out. 21Sometimes the cloud stayed only from evening until morning. When it lifted in the morning, they started out. It didn’t matter whether it was day or night. When the cloud lifted, the people started out. 22It didn’t matter whether the cloud stayed above the holy tent for two days or a month or a year. The Israelites would remain in camp. They wouldn’t start out. But when the cloud lifted, they would start out. 23When the Lord gave the command, they camped. And when he gave the command, they started out. They obeyed the Lord’s order. They obeyed him, just as he had commanded them through Moses.