Hesabu 8 – NEN & NIV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Hesabu 8:1-26

Kuwekwa Kwa Taa

1Bwana akamwambia Mose, 28:2 Kut 25:37; Law 24:2-4; Za 119:105; Isa 8:20; Mt 5:14“Sema na Aroni umwambie, ‘Wakati utakapoziweka zile taa saba, zinatakiwa kuangaza eneo lililo mbele ya kinara cha taa.’ ”

3Aroni akafanya hivyo; akaziweka zile taa ili zielekee mbele kwenye kinara cha taa, kama vile Bwana alivyomwamuru Mose. 48:4 Kut 25:9, 36Hivi ndivyo kinara cha taa kilivyotengenezwa: Kilitengenezwa kwa dhahabu iliyofuliwa, kuanzia kwenye kitako chake hadi kwenye maua yake. Kinara cha taa kilitengenezwa sawasawa kabisa na kielelezo ambacho Bwana alikuwa amemwonyesha Mose.

Kutengwa Kwa Walawi Kwa Ajili Ya Bwana

5Bwana akamwambia Mose: 68:6 Law 22:2; Isa 52:11; Za 26:6; Ebr 7:26; 10:22“Watwae Walawi kutoka miongoni mwa Waisraeli wengine na uwatakase kwa kawaida ya ibada. 78:7 Hes 19:9, 17; 31:23; Law 14:8, 9; Hes 6:9; Kum 21:21; Mwa 35:2Ili kuwatakasa fanya hivi: Nyunyizia maji ya utakaso juu yao; kisha uwaambie wanyoe nywele kwenye mwili mzima, wafue nguo zao na hivyo wajitakase wenyewe. 88:8 Law 2:1; 4:3; Hes 15:8-10Waambie wamchukue fahali mchanga pamoja na sadaka yake ya nafaka ya unga laini uliochanganywa na mafuta; kisha utamchukua fahali mchanga wa pili kwa ajili ya sadaka ya dhambi. 98:9 Kut 40:12; Law 8:3Walete Walawi mbele ya Hema la Kukutania na ukusanye jumuiya yote ya Waisraeli. 108:10 Law 3:2; Mdo 6:6Utawaleta Walawi mbele za Bwana, na Waisraeli wataweka mikono yao juu ya Walawi. 118:11 Kut 29:24; Law 7:30Aroni atawaweka Walawi mbele za Bwana kama sadaka ya kuinua kutoka kwa Waisraeli, ili kwamba wawe tayari kuifanya kazi ya Bwana.

128:12 Kut 29:10, 36; Law 4:3; Hes 6:11“Baada ya Walawi kuweka mikono yao juu ya vichwa vya hao mafahali wawili, tumia mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi kwa Bwana, na mwingine kuwa sadaka ya kuteketezwa, ili kufanya upatanisho kwa ajili ya Walawi. 138:13 Kut 29:24Waambie hao Walawi wasimame mbele ya Aroni na wanawe, kisha wawatoe kama sadaka ya kuinuliwa kwa Bwana. 148:14 Hes 3:12; 3:45; 16:9; Mal 3:17Kwa njia hii utakuwa umewatenga Walawi kutoka kwa Waisraeli wengine, nao Walawi watakuwa wangu.

158:15 Kut 29:24; 40:2“Utakapokuwa umekwisha kuwatakasa Walawi na kuwatoa kama sadaka ya kuinuliwa, watakuja kufanya kazi yao katika Hema la Kukutania. 168:16 Hes 1:20; 3:12Wao ndio Waisraeli ambao watatolewa kabisa kwangu. Nimewatwaa kama mali yangu mwenyewe badala ya mzaliwa wa kwanza, mzaliwa wa kwanza wa kiume kutoka kwa kila mwanamke wa Kiisraeli. 178:17 Kut 4:23; 22:29; 13:2; Lk 2:23Kila mzaliwa wa kwanza wa kiume katika Israeli, awe wa mwanadamu au mnyama, ni wangu. Wakati nilipowaua wazaliwa wote wa kwanza huko Misri, niliwatenga kwa ajili yangu mwenyewe. 188:18 Hes 3:12Nami nimewatwaa Walawi badala ya wazaliwa wote wa kwanza wa kiume katika Israeli. 198:19 Hes 3:7-9; 1:53; 16:46; 18:2-6Kati ya Waisraeli wote, nimempa Aroni na wanawe Walawi kama zawadi ili wafanye kazi katika Hema la Kukutania kwa niaba ya Waisraeli, na kufanya upatanisho kwa ajili yao ili pasiwepo na pigo lolote litakalowapata Waisraeli wakati watakapokaribia mahali patakatifu.”

20Mose, Aroni na jumuiya yote ya Waisraeli wakawafanyia Walawi kama Bwana alivyomwamuru Mose. 218:21 Mwa 35:2; Rum 15:16Walawi wakajitakasa wenyewe na wakafua nguo zao. Kisha Aroni akawasogeza mbele za Bwana kuwa sadaka ya kuinuliwa, na kufanya upatanisho kwa ajili yao ili kuwatakasa. 228:22 2Nya 30:15Baada ya hayo, Walawi walikuja kufanya kazi yao katika Hema la Kukutania chini ya usimamizi wa Aroni na wanawe. Waliwafanyia Walawi kama vile Bwana alivyomwamuru Mose.

23Bwana akamwambia Mose, 248:24 1Nya 23:3; Kut 38:21; Hes 4:3“Hili linawahusu Walawi: Wanaume wenye umri wa miaka ishirini na mitano au zaidi watakuja kushiriki katika kazi kwenye Hema la Kukutania, 258:25 1Nya 23:28-31; Eze 44:8-11lakini watakapofika umri wa miaka hamsini, ni lazima waache kazi zao za kawaida wala wasiendelee. 26Wanaweza kuwasaidia ndugu zao kufanya wajibu wao katika Hema la Kukutania, lakini wao wenyewe kamwe hawatafanya hiyo kazi. Basi, hivi ndivyo utakavyogawa wajibu kwa Walawi.”

New International Version

Numbers 8:1-26

Setting Up the Lamps

1The Lord said to Moses, 2“Speak to Aaron and say to him, ‘When you set up the lamps, see that all seven light up the area in front of the lampstand.’ ”

3Aaron did so; he set up the lamps so that they faced forward on the lampstand, just as the Lord commanded Moses. 4This is how the lampstand was made: It was made of hammered gold—from its base to its blossoms. The lampstand was made exactly like the pattern the Lord had shown Moses.

The Setting Apart of the Levites

5The Lord said to Moses: 6“Take the Levites from among all the Israelites and make them ceremonially clean. 7To purify them, do this: Sprinkle the water of cleansing on them; then have them shave their whole bodies and wash their clothes. And so they will purify themselves. 8Have them take a young bull with its grain offering of the finest flour mixed with olive oil; then you are to take a second young bull for a sin offering.8:8 Or purification offering; also in verse 12 9Bring the Levites to the front of the tent of meeting and assemble the whole Israelite community. 10You are to bring the Levites before the Lord, and the Israelites are to lay their hands on them. 11Aaron is to present the Levites before the Lord as a wave offering from the Israelites, so that they may be ready to do the work of the Lord.

12“Then the Levites are to lay their hands on the heads of the bulls, using one for a sin offering to the Lord and the other for a burnt offering, to make atonement for the Levites. 13Have the Levites stand in front of Aaron and his sons and then present them as a wave offering to the Lord. 14In this way you are to set the Levites apart from the other Israelites, and the Levites will be mine.

15“After you have purified the Levites and presented them as a wave offering, they are to come to do their work at the tent of meeting. 16They are the Israelites who are to be given wholly to me. I have taken them as my own in place of the firstborn, the first male offspring from every Israelite woman. 17Every firstborn male in Israel, whether human or animal, is mine. When I struck down all the firstborn in Egypt, I set them apart for myself. 18And I have taken the Levites in place of all the firstborn sons in Israel. 19From among all the Israelites, I have given the Levites as gifts to Aaron and his sons to do the work at the tent of meeting on behalf of the Israelites and to make atonement for them so that no plague will strike the Israelites when they go near the sanctuary.”

20Moses, Aaron and the whole Israelite community did with the Levites just as the Lord commanded Moses. 21The Levites purified themselves and washed their clothes. Then Aaron presented them as a wave offering before the Lord and made atonement for them to purify them. 22After that, the Levites came to do their work at the tent of meeting under the supervision of Aaron and his sons. They did with the Levites just as the Lord commanded Moses.

23The Lord said to Moses, 24“This applies to the Levites: Men twenty-five years old or more shall come to take part in the work at the tent of meeting, 25but at the age of fifty, they must retire from their regular service and work no longer. 26They may assist their brothers in performing their duties at the tent of meeting, but they themselves must not do the work. This, then, is how you are to assign the responsibilities of the Levites.”