Hesabu 8 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Hesabu 8:1-26

Kuwekwa Kwa Taa

1Bwana akamwambia Mose, 28:2 Kut 25:37; Law 24:2-4; Za 119:105; Isa 8:20; Mt 5:14“Sema na Aroni umwambie, ‘Wakati utakapoziweka zile taa saba, zinatakiwa kuangaza eneo lililo mbele ya kinara cha taa.’ ”

3Aroni akafanya hivyo; akaziweka zile taa ili zielekee mbele kwenye kinara cha taa, kama vile Bwana alivyomwamuru Mose. 48:4 Kut 25:9, 36Hivi ndivyo kinara cha taa kilivyotengenezwa: Kilitengenezwa kwa dhahabu iliyofuliwa, kuanzia kwenye kitako chake hadi kwenye maua yake. Kinara cha taa kilitengenezwa sawasawa kabisa na kielelezo ambacho Bwana alikuwa amemwonyesha Mose.

Kutengwa Kwa Walawi Kwa Ajili Ya Bwana

5Bwana akamwambia Mose: 68:6 Law 22:2; Isa 52:11; Za 26:6; Ebr 7:26; 10:22“Watwae Walawi kutoka miongoni mwa Waisraeli wengine na uwatakase kwa kawaida ya ibada. 78:7 Hes 19:9, 17; 31:23; Law 14:8, 9; Hes 6:9; Kum 21:21; Mwa 35:2Ili kuwatakasa fanya hivi: Nyunyizia maji ya utakaso juu yao; kisha uwaambie wanyoe nywele kwenye mwili mzima, wafue nguo zao na hivyo wajitakase wenyewe. 88:8 Law 2:1; 4:3; Hes 15:8-10Waambie wamchukue fahali mchanga pamoja na sadaka yake ya nafaka ya unga laini uliochanganywa na mafuta; kisha utamchukua fahali mchanga wa pili kwa ajili ya sadaka ya dhambi. 98:9 Kut 40:12; Law 8:3Walete Walawi mbele ya Hema la Kukutania na ukusanye jumuiya yote ya Waisraeli. 108:10 Law 3:2; Mdo 6:6Utawaleta Walawi mbele za Bwana, na Waisraeli wataweka mikono yao juu ya Walawi. 118:11 Kut 29:24; Law 7:30Aroni atawaweka Walawi mbele za Bwana kama sadaka ya kuinua kutoka kwa Waisraeli, ili kwamba wawe tayari kuifanya kazi ya Bwana.

128:12 Kut 29:10, 36; Law 4:3; Hes 6:11“Baada ya Walawi kuweka mikono yao juu ya vichwa vya hao mafahali wawili, tumia mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi kwa Bwana, na mwingine kuwa sadaka ya kuteketezwa, ili kufanya upatanisho kwa ajili ya Walawi. 138:13 Kut 29:24Waambie hao Walawi wasimame mbele ya Aroni na wanawe, kisha wawatoe kama sadaka ya kuinuliwa kwa Bwana. 148:14 Hes 3:12; 3:45; 16:9; Mal 3:17Kwa njia hii utakuwa umewatenga Walawi kutoka kwa Waisraeli wengine, nao Walawi watakuwa wangu.

158:15 Kut 29:24; 40:2“Utakapokuwa umekwisha kuwatakasa Walawi na kuwatoa kama sadaka ya kuinuliwa, watakuja kufanya kazi yao katika Hema la Kukutania. 168:16 Hes 1:20; 3:12Wao ndio Waisraeli ambao watatolewa kabisa kwangu. Nimewatwaa kama mali yangu mwenyewe badala ya mzaliwa wa kwanza, mzaliwa wa kwanza wa kiume kutoka kwa kila mwanamke wa Kiisraeli. 178:17 Kut 4:23; 22:29; 13:2; Lk 2:23Kila mzaliwa wa kwanza wa kiume katika Israeli, awe wa mwanadamu au mnyama, ni wangu. Wakati nilipowaua wazaliwa wote wa kwanza huko Misri, niliwatenga kwa ajili yangu mwenyewe. 188:18 Hes 3:12Nami nimewatwaa Walawi badala ya wazaliwa wote wa kwanza wa kiume katika Israeli. 198:19 Hes 3:7-9; 1:53; 16:46; 18:2-6Kati ya Waisraeli wote, nimempa Aroni na wanawe Walawi kama zawadi ili wafanye kazi katika Hema la Kukutania kwa niaba ya Waisraeli, na kufanya upatanisho kwa ajili yao ili pasiwepo na pigo lolote litakalowapata Waisraeli wakati watakapokaribia mahali patakatifu.”

20Mose, Aroni na jumuiya yote ya Waisraeli wakawafanyia Walawi kama Bwana alivyomwamuru Mose. 218:21 Mwa 35:2; Rum 15:16Walawi wakajitakasa wenyewe na wakafua nguo zao. Kisha Aroni akawasogeza mbele za Bwana kuwa sadaka ya kuinuliwa, na kufanya upatanisho kwa ajili yao ili kuwatakasa. 228:22 2Nya 30:15Baada ya hayo, Walawi walikuja kufanya kazi yao katika Hema la Kukutania chini ya usimamizi wa Aroni na wanawe. Waliwafanyia Walawi kama vile Bwana alivyomwamuru Mose.

23Bwana akamwambia Mose, 248:24 1Nya 23:3; Kut 38:21; Hes 4:3“Hili linawahusu Walawi: Wanaume wenye umri wa miaka ishirini na mitano au zaidi watakuja kushiriki katika kazi kwenye Hema la Kukutania, 258:25 1Nya 23:28-31; Eze 44:8-11lakini watakapofika umri wa miaka hamsini, ni lazima waache kazi zao za kawaida wala wasiendelee. 26Wanaweza kuwasaidia ndugu zao kufanya wajibu wao katika Hema la Kukutania, lakini wao wenyewe kamwe hawatafanya hiyo kazi. Basi, hivi ndivyo utakavyogawa wajibu kwa Walawi.”

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

民数记 8:1-26

安置七盏灯

1耶和华对摩西说: 2“你告诉亚伦,安放灯的时候,七盏灯都要照向灯台的前面。” 3亚伦就照耶和华对摩西的吩咐把灯放好,使灯照向前方。 4整座灯台,从灯座到上面的花苞,都是照耶和华对摩西的吩咐用金子锤制而成的。

为利未人行洁净与奉献礼

5耶和华对摩西说: 6“你要把利未人从其他以色列人中分别出来,洁净他们。 7要用以下的方法洁净他们,把洁净水洒在他们身上,叫他们用剃刀剃净全身,洗净衣服,这样他们就洁净了。 8然后叫他们带来一头公牛犊及作素祭的调了油的细面粉,你要另献一头公牛犊作赎罪祭。 9你要招聚以色列全体会众,将利未人带到会幕前, 10带到耶和华面前,会众要按手在他们身上。 11亚伦要把他们献给耶和华,作为以色列人献的摇祭,使他们可以事奉耶和华。 12利未人要按手在那两头公牛的头上,然后你要把一头作为赎罪祭,一头作为燔祭献给耶和华,好为利未人赎罪。 13你要让利未人站在亚伦父子们面前,把他们当作摇祭献给耶和华。 14这样,你就把利未人从其他以色列人中分别出来,使他们归给我。 15利未人被洁净、当作摇祭献上以后,就可以进会幕司职, 16因为在以色列人中,他们完全属于我,我拣选他们归我所有,以代替以色列人所有的长子。 17以色列人所有的长子和头生的牲畜都属于我。我击杀埃及人所有的长子和头生的牲畜那天,已把以色列人所有的长子和头生的牲畜都分别出来,使之圣洁,归给我。 18我现在已拣选利未人代替以色列人所有的长子, 19把他们交给亚伦父子们,替以色列人在会幕中司职,为以色列人赎罪,免得以色列人因接近圣所而遭祸。”

20摩西亚伦以色列全体会众就按照耶和华对摩西的吩咐把利未人献上。 21利未人自洁、洗净衣服后,亚伦把他们当作摇祭献给耶和华,又为他们赎罪,使他们洁净。 22之后,利未人便进入会幕,在亚伦父子们的监督下司职。以色列人照耶和华对摩西的吩咐奉献了利未人。

23耶和华对摩西说: 24“二十五岁以上的利未人都要到会幕司职, 25五十岁时退休。 26退休之后,他们可以协助本族弟兄看守会幕,不用再司职。你要这样给他们分派工作。”