Hesabu 8 – NEN & CARS

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Hesabu 8:1-26

Kuwekwa Kwa Taa

1Bwana akamwambia Mose, 28:2 Kut 25:37; Law 24:2-4; Za 119:105; Isa 8:20; Mt 5:14“Sema na Aroni umwambie, ‘Wakati utakapoziweka zile taa saba, zinatakiwa kuangaza eneo lililo mbele ya kinara cha taa.’ ”

3Aroni akafanya hivyo; akaziweka zile taa ili zielekee mbele kwenye kinara cha taa, kama vile Bwana alivyomwamuru Mose. 48:4 Kut 25:9, 36Hivi ndivyo kinara cha taa kilivyotengenezwa: Kilitengenezwa kwa dhahabu iliyofuliwa, kuanzia kwenye kitako chake hadi kwenye maua yake. Kinara cha taa kilitengenezwa sawasawa kabisa na kielelezo ambacho Bwana alikuwa amemwonyesha Mose.

Kutengwa Kwa Walawi Kwa Ajili Ya Bwana

5Bwana akamwambia Mose: 68:6 Law 22:2; Isa 52:11; Za 26:6; Ebr 7:26; 10:22“Watwae Walawi kutoka miongoni mwa Waisraeli wengine na uwatakase kwa kawaida ya ibada. 78:7 Hes 19:9, 17; 31:23; Law 14:8, 9; Hes 6:9; Kum 21:21; Mwa 35:2Ili kuwatakasa fanya hivi: Nyunyizia maji ya utakaso juu yao; kisha uwaambie wanyoe nywele kwenye mwili mzima, wafue nguo zao na hivyo wajitakase wenyewe. 88:8 Law 2:1; 4:3; Hes 15:8-10Waambie wamchukue fahali mchanga pamoja na sadaka yake ya nafaka ya unga laini uliochanganywa na mafuta; kisha utamchukua fahali mchanga wa pili kwa ajili ya sadaka ya dhambi. 98:9 Kut 40:12; Law 8:3Walete Walawi mbele ya Hema la Kukutania na ukusanye jumuiya yote ya Waisraeli. 108:10 Law 3:2; Mdo 6:6Utawaleta Walawi mbele za Bwana, na Waisraeli wataweka mikono yao juu ya Walawi. 118:11 Kut 29:24; Law 7:30Aroni atawaweka Walawi mbele za Bwana kama sadaka ya kuinua kutoka kwa Waisraeli, ili kwamba wawe tayari kuifanya kazi ya Bwana.

128:12 Kut 29:10, 36; Law 4:3; Hes 6:11“Baada ya Walawi kuweka mikono yao juu ya vichwa vya hao mafahali wawili, tumia mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi kwa Bwana, na mwingine kuwa sadaka ya kuteketezwa, ili kufanya upatanisho kwa ajili ya Walawi. 138:13 Kut 29:24Waambie hao Walawi wasimame mbele ya Aroni na wanawe, kisha wawatoe kama sadaka ya kuinuliwa kwa Bwana. 148:14 Hes 3:12; 3:45; 16:9; Mal 3:17Kwa njia hii utakuwa umewatenga Walawi kutoka kwa Waisraeli wengine, nao Walawi watakuwa wangu.

158:15 Kut 29:24; 40:2“Utakapokuwa umekwisha kuwatakasa Walawi na kuwatoa kama sadaka ya kuinuliwa, watakuja kufanya kazi yao katika Hema la Kukutania. 168:16 Hes 1:20; 3:12Wao ndio Waisraeli ambao watatolewa kabisa kwangu. Nimewatwaa kama mali yangu mwenyewe badala ya mzaliwa wa kwanza, mzaliwa wa kwanza wa kiume kutoka kwa kila mwanamke wa Kiisraeli. 178:17 Kut 4:23; 22:29; 13:2; Lk 2:23Kila mzaliwa wa kwanza wa kiume katika Israeli, awe wa mwanadamu au mnyama, ni wangu. Wakati nilipowaua wazaliwa wote wa kwanza huko Misri, niliwatenga kwa ajili yangu mwenyewe. 188:18 Hes 3:12Nami nimewatwaa Walawi badala ya wazaliwa wote wa kwanza wa kiume katika Israeli. 198:19 Hes 3:7-9; 1:53; 16:46; 18:2-6Kati ya Waisraeli wote, nimempa Aroni na wanawe Walawi kama zawadi ili wafanye kazi katika Hema la Kukutania kwa niaba ya Waisraeli, na kufanya upatanisho kwa ajili yao ili pasiwepo na pigo lolote litakalowapata Waisraeli wakati watakapokaribia mahali patakatifu.”

20Mose, Aroni na jumuiya yote ya Waisraeli wakawafanyia Walawi kama Bwana alivyomwamuru Mose. 218:21 Mwa 35:2; Rum 15:16Walawi wakajitakasa wenyewe na wakafua nguo zao. Kisha Aroni akawasogeza mbele za Bwana kuwa sadaka ya kuinuliwa, na kufanya upatanisho kwa ajili yao ili kuwatakasa. 228:22 2Nya 30:15Baada ya hayo, Walawi walikuja kufanya kazi yao katika Hema la Kukutania chini ya usimamizi wa Aroni na wanawe. Waliwafanyia Walawi kama vile Bwana alivyomwamuru Mose.

23Bwana akamwambia Mose, 248:24 1Nya 23:3; Kut 38:21; Hes 4:3“Hili linawahusu Walawi: Wanaume wenye umri wa miaka ishirini na mitano au zaidi watakuja kushiriki katika kazi kwenye Hema la Kukutania, 258:25 1Nya 23:28-31; Eze 44:8-11lakini watakapofika umri wa miaka hamsini, ni lazima waache kazi zao za kawaida wala wasiendelee. 26Wanaweza kuwasaidia ndugu zao kufanya wajibu wao katika Hema la Kukutania, lakini wao wenyewe kamwe hawatafanya hiyo kazi. Basi, hivi ndivyo utakavyogawa wajibu kwa Walawi.”

Священное Писание

Числа 8:1-26

Расположение лампад

1Вечный сказал Мусе:

2– Говори с Харуном, скажи ему: «Когда ты будешь устанавливать семь лампад на светильнике, то установи их так, чтобы они освещали пространство спереди».

3Харун так и сделал. Он установил лампады так, чтобы они светили перед светильником, как повелел Мусе Вечный. 4Вот как был сделан светильник: его сделали из кованого золота – от основания до цветков. Светильник был сделан по тому образцу, который показал Мусе Вечный.

Очищение и посвящение левитов

5Вечный сказал Мусе:

6– Отдели левитов от остальных исраильтян и очисти их. 7Чтобы очистить их, сделай так: окропи их водой очищения, и пусть они обреют всё тело и выстирают одежду. Так они очистятся. 8Пусть они возьмут молодого быка с положенным хлебным приношением из лучшей муки, смешанной с маслом, а ты возьми второго молодого быка для жертвы за грех. 9Приведи левитов к шатру встречи и собери всё общество Исраила. 10Поставь левитов перед Вечным, и пусть исраильтяне возложат на них руки. 11Пусть Харун посвятит левитов Вечному как приношение от исраильского народа, чтобы они могли служить Вечному.

12Когда левиты возложат руки на головы быков, принеси одного быка в жертву Вечному за грех, а другого – во всесожжение, чтобы очистить левитов. 13Поставь левитов перед Харуном и его сыновьями и посвяти их Вечному как приношение. 14Так ты отделишь левитов от остальных исраильтян, и левиты станут Моими.

15Когда ты очистишь левитов и посвятишь их как приношение, пусть они войдут, чтобы служить при шатре встречи. 16Они – те исраильтяне, которых нужно полностью отдать Мне. Я беру их Себе вместо первенцев мужского пола от любой исраильтянки. 17Все первенцы мужского пола в Исраиле – человек или животное – принадлежат Мне. Я отделил их Себе, умертвив всех первенцев в Египте. 18Я взял левитов вместо всех первородных сыновей Исраила. 19Я предназначил левитов в дар от исраильтян Харуну и его сыновьям, чтобы они служили за исраильтян при шатре встречи и совершали для них очищение, чтобы никакая напасть не поразила исраильтян, если они приблизятся к святилищу.

20Муса, Харун и всё общество Исраила поступили с левитами точно так, как повелел Мусе Вечный. 21Левиты очистились и выстирали одежду. Харун посвятил их Вечному как приношение и совершил для них очищение, чтобы сделать их чистыми. 22После этого левиты вошли, чтобы служить при шатре встречи под началом Харуна и его сыновей. Они поступили с левитами точно так, как повелел Мусе Вечный.

23Вечный сказал Мусе:

24– Это касается левитов: пусть мужчины двадцати пяти лет и старше принимаются за свои обязанности по службе при шатре встречи, 25но в пятьдесят лет пусть удаляются от постоянного служения и больше не служат. 26Они могут помогать своим братьям исполнять их обязанности при шатре встречи, но сами пусть не служат. Так ты обозначишь левитам их обязанности.