Sadaka Wakati Wa Kuweka Wakfu Maskani Ya Bwana
17:1 Kut 40:9, 10, 17; 30:26; 2Nya 7:9; 1Fal 8:64Mose alipomaliza kuisimamisha Maskani, aliitia mafuta na kuiweka wakfu pamoja na samani zake zote. Pia alitia madhabahu mafuta na kuiweka wakfu, pamoja na vyombo vyake vyote. 27:2 Hes 1:5-16, 19; Kut 35:27; 1Nya 29:6-8; Ezr 2:68-69; Neh 7:70-72Ndipo viongozi wa Israeli, wale wakuu wa jamaa waliokuwa viongozi wa kabila wasimamizi wa wale waliohesabiwa, wakatoa sadaka. 37:3 Mwa 45:19; 1Sam 6:7-14; 1Nya 13:6-7Walizileta kama matoleo yao mbele za Bwana: magari sita ya kukokotwa yaliyofunikwa, pamoja na maksai kumi na wawili; yaani maksai mmoja kutoka kwa kila kiongozi, na gari moja la kukokotwa kutoka kwa kila viongozi wawili. Haya waliyaleta mbele ya Maskani.
4Bwana akamwambia Mose, 5“Vikubali vitu hivi kutoka kwao, ili viweze kutumika katika kazi kwenye Hema la Kukutania. Wapatie Walawi kama kazi ya kila mtu itakavyohitaji.”
6Hivyo Mose akachukua yale magari ya kukokotwa pamoja na maksai, na kuwapa Walawi. 77:7 Hes 4:24-28Aliwapa Wagershoni magari mawili ya kukokotwa na maksai wanne, kama walivyohitaji kwa kazi yao, 87:8 Hes 4:31-33na pia aliwapa Wamerari magari manne ya kukokotwa na maksai wanane, kama kazi yao ilivyohitaji. Wote walikuwa chini ya maelekezo ya Ithamari mwana wa kuhani, Aroni. 97:9 Hes 4:4, 15; 1Nya 23:26; 2Sam 6:13Lakini Mose hakuwapa Wakohathi chochote kati ya hivyo, kwa sababu walitakiwa kubeba vitu vitakatifu mabegani mwao, vile walikuwa wanawajibika.
107:10 Hes 7:1; Kut 29:36; 2Nya 7:9; Kum 20:5; Ezr 6:16Wakati madhabahu yalitiwa mafuta, viongozi walileta sadaka zao kwa ajili ya kule kuwekwa wakfu kwake na kuziweka mbele ya madhabahu. 117:11 1Kor 14:33Kwa maana Bwana alikuwa amemwambia Mose, “Kila siku kiongozi mmoja ataleta sadaka yake ili kuwekwa wakfu madhabahu.”
127:12 Hes 1:7Yule ambaye alileta sadaka yake siku ya kwanza alikuwa Nashoni, mwana wa Aminadabu, wa kabila la Yuda.
137:13 Kut 27:3; 30:13; Law 27:3-7; 2:1; Hes 6:15; 15:14; Ezr 8:25; Yer 52:19Sadaka yake ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli 130,7:13 Shekeli 130 za fedha ni sawa na kilo 1.5. na bakuli moja la fedha la kunyunyizia lenye uzito wa shekeli sabini,7:13 Shekeli 70 za fedha ni sawa gramu 800. vyote kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, vikiwa vimejazwa unga laini uliochanganywa na mafuta kama sadaka ya nafaka; 147:14 1Fal 7:50; 2Fal 25:14; 2Nya 4:22; 24:14; Kut 25:6; 30:34; Eze 18:16; Mal 1:11; Ufu 5:8sinia moja la dhahabu lenye uzito wa shekeli kumi,7:14 Shekeli 10 za dhahabu ni sawa na gramu 110. likiwa limejazwa uvumba; 157:15 Kut 24:5; 29:3; Hes 28:11; Law 1:3fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja na mwana-kondoo dume mmoja wa mwaka mmoja, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa; 167:16 Law 4:3mbuzi dume mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi; 177:17 Law 3:1; Hes 1:77:17 Lk 3:32maksai wawili, kondoo dume watano, mbuzi dume watano na wana-kondoo dume watano wa mwaka mmoja, ili vitolewe dhabihu kama sadaka ya amani. Hii ndiyo ilikuwa sadaka ya Nashoni mwana wa Aminadabu.
187:18 Hes 1:8Siku ya pili yake Nethaneli mwana wa Suari, kiongozi wa kabila la Isakari, alileta sadaka yake.
19Sadaka aliyoleta ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli 130, na bakuli moja la fedha la kunyunyizia lenye uzito wa shekeli sabini, vyote kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, vikiwa vimejazwa unga laini uliochanganywa na mafuta kama sadaka ya nafaka; 20sinia moja la dhahabu lenye uzito wa shekeli kumi, likiwa limejazwa uvumba; 217:21 Mwa 8:20; Za 20:1-3; 50:19; Efe 5:2; Ebr 9:13fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja na mwana-kondoo dume mmoja wa mwaka mmoja, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa; 22mbuzi dume mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi; 237:23 1Fal 8:63; Law 7:11-13; Mit 7:14; Kol 1:20maksai wawili, kondoo dume watano, mbuzi dume watano na wana-kondoo dume watano wa mwaka mmoja, ili vitolewe dhabihu kama sadaka ya amani. Hii ndiyo ilikuwa sadaka ya Nethaneli mwana wa Suari.
247:24 Hes 1:9Siku ya tatu Eliabu mwana wa Heloni, kiongozi wa kabila la Zabuloni, alileta sadaka yake.
257:25 Isa 53:7; Mdo 8:32; Ufu 5:6-11; 13:8Sadaka aliyoleta ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli 130, na bakuli moja la fedha la kunyunyizia lenye uzito wa shekeli sabini, vyote kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, vikiwa vimejazwa unga laini uliochanganywa na mafuta kama sadaka ya nafaka; 26sinia moja la dhahabu lenye uzito wa shekeli kumi, likiwa limejazwa uvumba; 27fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja na mwana-kondoo dume mmoja wa mwaka mmoja, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa; 28mbuzi dume mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi; 29maksai wawili, kondoo dume watano, mbuzi dume watano na wana-kondoo dume watano wa mwaka mmoja, ili vitolewe dhabihu kama sadaka ya amani. Hii ndiyo ilikuwa sadaka ya Eliabu mwana wa Heloni.
307:30 Hes 1:5Siku ya nne Elisuri mwana wa Shedeuri, kiongozi wa kabila la Reubeni, alileta sadaka yake.
31Sadaka aliyoleta ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli 130, na bakuli moja la fedha la kunyunyizia lenye uzito wa shekeli sabini, vyote kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, vikiwa vimejazwa unga laini uliochanganywa na mafuta kama sadaka ya nafaka; 32sinia moja la dhahabu lenye uzito wa shekeli kumi, likiwa limejazwa uvumba; 33fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja na mwana-kondoo dume mmoja wa mwaka mmoja, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa; 34mbuzi dume mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi; 35maksai wawili, kondoo dume watano, mbuzi dume watano na wana-kondoo dume watano wa mwaka mmoja, ili vitolewe dhabihu kama sadaka ya amani. Hii ndiyo ilikuwa sadaka ya Elisuri mwana wa Shedeuri.
367:36 Hes 1:6Siku ya tano Shelumieli mwana wa Surishadai, kiongozi wa watu wa Simeoni, alileta sadaka yake.
37Sadaka aliyoleta ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli 130, na bakuli moja la fedha la kunyunyizia lenye uzito wa shekeli sabini, vyote kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, vikiwa vimejazwa unga laini uliochanganywa na mafuta kama sadaka ya nafaka; 38sinia moja la dhahabu lenye uzito wa shekeli kumi, likiwa limejazwa uvumba; 397:39 Kut 12:5; Ebr 9:28; 1Pet 3:18fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja na mwana-kondoo dume mmoja wa mwaka mmoja, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa; 40mbuzi dume mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi; 41maksai wawili, kondoo dume watano, mbuzi dume watano na wana-kondoo dume watano wa mwaka mmoja, ili vitolewe dhabihu kama sadaka ya amani. Hii ndiyo ilikuwa sadaka ya Shelumieli mwana wa Surishadai.
427:42 Hes 1:14Siku ya sita Eliasafu mwana wa Deueli, kiongozi wa watu wa Gadi, alileta sadaka yake.
437:43 Law 2:5; 14:10Sadaka aliyoleta ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli 130, na bakuli moja la fedha la kunyunyizia lenye uzito wa shekeli sabini, vyote kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, vikiwa vimejazwa unga laini uliochanganywa na mafuta kama sadaka ya nafaka; 44sinia moja la dhahabu lenye uzito wa shekeli kumi, likiwa limejazwa uvumba; 457:45 Za 40:6; 51:16; Isa 53:4; Yer 7:22; Amo 5:22fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja na mwana-kondoo dume mmoja wa mwaka mmoja, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa; 46mbuzi dume mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi; 47maksai wawili, kondoo dume watano, mbuzi dume watano na wana-kondoo dume watano wa mwaka mmoja, ili vitolewe dhabihu kama sadaka ya amani. Hii ndiyo ilikuwa sadaka ya Eliasafu mwana wa Deueli.
487:48 Hes 1:10; 2:18; 1Nya 7:26Siku ya saba Elishama mwana wa Amihudi, kiongozi wa watu wa Efraimu, alileta sadaka yake.
49Sadaka aliyoleta ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli 130, na bakuli moja la fedha la kunyunyizia lenye uzito wa shekeli sabini, vyote kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, vikiwa vimejazwa unga laini uliochanganywa na mafuta kama sadaka ya nafaka; 507:50 Kum 33:10; Za 66:15; Lk 1:10sinia moja la dhahabu lenye uzito wa shekeli kumi, likiwa limejazwa uvumba; 517:51 Mik 6:6-8fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja na mwana-kondoo dume mmoja wa mwaka mmoja, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa; 52mbuzi dume mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi; 53maksai wawili, kondoo dume watano, mbuzi dume watano na wana-kondoo dume watano wa mwaka mmoja, ili vitolewe dhabihu kama sadaka ya amani. Hii ndiyo ilikuwa sadaka ya Elishama mwana wa Amihudi.
547:54 Hes 1:10Siku ya nane Gamalieli mwana wa Pedasuri, kiongozi wa watu wa Manase, alileta sadaka yake.
55Sadaka aliyoleta ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli 130, na bakuli moja la fedha la kunyunyizia lenye uzito wa shekeli sabini, vyote kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, vikiwa vimejazwa unga laini uliochanganywa na mafuta kama sadaka ya nafaka; 567:56 Kut 30:7sinia moja la dhahabu lenye uzito wa shekeli kumi, likiwa limejazwa uvumba; 577:57 Kut 12:5; Mdo 8:32; 1Pet 1:19fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja na mwana-kondoo dume mmoja wa mwaka mmoja, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa; 58mbuzi dume mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi; 59maksai wawili, kondoo dume watano, mbuzi dume watano na wana-kondoo dume watano wa mwaka mmoja, ili vitolewe dhabihu kama sadaka ya amani. Hii ndiyo ilikuwa sadaka ya Gamalieli mwana wa Pedasuri.
607:60 Hes 1:11Siku ya tisa Abidani mwana wa Gideoni, kiongozi wa watu wa Benyamini, alileta sadaka yake.
61Sadaka aliyoleta ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli 130, na bakuli moja la fedha la kunyunyizia lenye uzito wa shekeli sabini, vyote kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, vikiwa vimejazwa unga laini uliochanganywa na mafuta kama sadaka ya nafaka; 627:62 Isa 66:20; Dan 9:27; Rum 15:16; Ebr 13:15; Ufu 8:3-4sinia moja la dhahabu lenye uzito wa shekeli kumi, likiwa limejazwa uvumba; 637:63 Za 40:6; Isa 53:4; 2Kor 5:21fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja na mwana-kondoo dume mmoja wa mwaka mmoja, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa; 64mbuzi dume mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi; 657:65 Mit 7:14; Eze 45:17; Kol 1:20maksai wawili, kondoo dume watano, mbuzi dume watano na wana-kondoo dume watano wa mwaka mmoja, ili vitolewe dhabihu kama sadaka ya amani. Hii ndiyo ilikuwa sadaka ya Abidani mwana wa Gideoni.
667:66 Hes 1:12; 2:25Siku ya kumi Ahiezeri mwana wa Amishadai, kiongozi wa watu wa Dani, alileta sadaka yake.
677:67 Law 27:25; Hes 3:47; Kut 30:13Sadaka aliyoleta ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli 130, na bakuli moja la fedha la kunyunyizia lenye uzito wa shekeli sabini, vyote kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, vikiwa vimejazwa unga laini uliochanganywa na mafuta kama sadaka ya nafaka; 687:68 Hes 16:35; Za 141:2; Kut 30:7-9sinia moja la dhahabu lenye uzito wa shekeli kumi, likiwa limejazwa uvumba; 69fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja na mwana-kondoo dume mmoja wa mwaka mmoja, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa; 70mbuzi dume mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi; 71maksai wawili, kondoo dume watano, mbuzi dume watano na wana-kondoo dume watano wa mwaka mmoja, ili vitolewe dhabihu kama sadaka ya amani. Hii ndiyo ilikuwa sadaka ya Ahiezeri mwana wa Amishadai.
727:72 Hes 1:13Siku ya kumi na moja Pagieli mwana wa Okrani, kiongozi wa watu wa Asheri, alileta sadaka yake.
73Sadaka aliyoleta ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli 130, na bakuli moja la fedha la kunyunyizia lenye uzito wa shekeli sabini, vyote kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, vikiwa vimejazwa unga laini uliochanganywa na mafuta kama sadaka ya nafaka; 74sinia moja la dhahabu lenye uzito wa shekeli kumi, likiwa limejazwa uvumba; 75fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja na mwana-kondoo dume mmoja wa mwaka mmoja, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa; 76mbuzi dume mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi; 77maksai wawili, kondoo dume watano, mbuzi dume watano na wana-kondoo dume watano wa mwaka mmoja, ili vitolewe dhabihu kama sadaka ya amani. Hii ndiyo ilikuwa sadaka ya Pagieli mwana wa Okrani.
787:78 Hes 1:15; 2:29Siku ya kumi na mbili Ahira mwana wa Enani, kiongozi wa watu wa Naftali, alileta sadaka yake.
797:79 Ezr 1:9-10; Yer 52:19; Zek 14:20; Mt 14:8-11Sadaka aliyoleta ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli 130, na bakuli moja la fedha la kunyunyizia lenye uzito wa shekeli sabini, vyote kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, vikiwa vimejazwa unga laini uliochanganywa na mafuta kama sadaka ya nafaka; 80sinia moja la dhahabu lenye uzito wa shekeli kumi, likiwa limejazwa uvumba; 81fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja na mwana-kondoo dume mmoja wa mwaka mmoja, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa; 82mbuzi dume mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi; 83maksai wawili, kondoo dume watano, mbuzi dume watano na wana-kondoo dume watano wa mwaka mmoja, ili vitolewe dhabihu kama sadaka ya amani. Hii ndiyo ilikuwa sadaka ya Ahira mwana wa Enani.
847:84 Hes 4:14; Neh 7:70; Ebr 13:10; Amu 5:9; Yos 22:13-14; Hos 13:10; Mit 17:7Hizi ndizo zilikuwa sadaka za viongozi wa Israeli madhabahu yalipowekwa wakfu, wakati yalitiwa mafuta: sahani kumi na mbili za fedha, bakuli kumi na mbili za fedha za kunyunyizia, na masinia kumi na mawili ya dhahabu. 85Kila sahani ya fedha ilikuwa na uzito wa shekeli 130, na kila bakuli la fedha la kunyunyizia lilikuwa na uzito wa shekeli sabini. Masinia yote kumi na mawili yalikuwa na uzito wa shekeli 2,4007:85 Shekeli 2,400 za fedha ni sawa na kilo 28.kulingana na shekeli ya mahali patakatifu. 867:86 Kut 30:13Sahani kumi na mbili za dhahabu zilizojazwa uvumba zilikuwa na uzito wa shekeli kumi kila moja, kulingana na shekeli ya mahali patakatifu. Kwa jumla, sahani za dhahabu zilikuwa na uzito wa shekeli 120.7:86 Shekeli 120 za dhahabu ni sawa na kilo 1.4. 87Jumla ya wanyama waliotolewa kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa walikuwa fahali kumi na wawili wachanga, kondoo dume kumi na wawili na wana-kondoo dume kumi na wawili wa mwaka mmoja, pamoja na sadaka zao za nafaka. Mbuzi waume kumi na wawili walitolewa kwa ajili ya sadaka za dhambi. 887:88 Mwa 32:14Jumla ya wanyama kwa ajili ya dhabihu ya sadaka ya amani walikuwa maksai ishirini na wanne, kondoo dume sitini, mbuzi dume wa mwaka mmoja sitini na wana-kondoo dume wa mwaka mmoja sitini. Hizi ndizo zilikuwa sadaka zilizoletwa kwa ajili ya kuwekwa wakfu kwa madhabahu baada ya kutiwa mafuta.
897:89 Kut 31:18; Hes 12:8; Ebr 4:167:89 Kut 25:22; 40:2; 29:42; 16:34; Za 80:1; 90:1; Hes 3:31Mose alipoingia kwenye Hema la Kukutania kuzungumza na Bwana, alisikia sauti ikisema naye kutoka kati ya wale makerubi wawili waliokuwa juu ya kile kiti cha rehema, juu ya Sanduku la Ushuhuda. Mose akazungumza naye.
Mise en place des institutions cultuelles
La mise en service du tabernacle et de l’autel
Offrandes pour la consécration du tabernacle
1Le jour où Moïse acheva de dresser le tabernacle, il versa de l’huile dessus pour le consacrer et fit de même pour ses accessoires ainsi que pour l’autel et tous ses accessoires. Il les oignit d’huile pour les consacrer7.1 Voir, pour les détails, Ex 40. Pour la consécration des prêtres, voir Lv 8.. 2Alors les chefs d’Israël, chefs de leurs groupes familiaux qui sont à la tête des tribus et qui avaient été chargés du recensement, 3apportèrent leur offrande devant l’Eternel : six chariots couverts7.3 Autre traduction : six tombereaux. et douze bœufs – soit un chariot pour deux chefs et un bœuf pour chacun d’eux ; ils les apportèrent devant le tabernacle.
4L’Eternel parla à Moïse en ces termes : 5Accepte ces présents de leur part ; ils seront destinés au service de la tente de la Rencontre. Tu les remettras aux lévites, à chacun selon les besoins de son service. 6Moïse prit les chariots et les bœufs et les donna aux lévites. 7Il donna deux chariots et quatre bœufs aux Guershonites selon les besoins de leur service. 8Il donna quatre chariots et huit bœufs aux Merarites, en raison du service qu’ils effectuaient sous la direction d’Itamar, le fils du prêtre Aaron. 9Il n’en donna pas aux Qehatites, car ils étaient responsables des objets sacrés et devaient les porter sur les épaules.
Offrandes pour la dédicace de l’autel
10Les chefs présentèrent leur offrande pour la dédicace de l’autel le jour où l’on en fit l’onction. Ils apportèrent leurs présents devant l’autel. 11Alors l’Eternel dit à Moïse : Que les chefs viennent à tour de rôle, un par jour, apporter leur offrande pour la dédicace de l’autel.
12Le premier jour, Nahshôn, fils d’Amminadab, vint présenter son offrande pour la tribu de Juda.
13Elle consistait en un plat d’argent pesant 1,5 kilogramme7.13 Dans tout ce chapitre, les poids sont donnés en sicles., un calice d’argent de 800 grammes, selon le poids utilisé au sanctuaire, tous deux remplis de fleur de farine pétrie à l’huile, pour l’offrande, 14et une coupe d’or de 110 grammes pleine d’encens. 15Il amena aussi un jeune taureau, un bélier et un agneau dans sa première année pour l’holocauste, 16un bouc comme sacrifice pour le péché 17et deux taureaux, cinq béliers, cinq boucs et cinq agneaux dans leur première année pour le sacrifice de communion. Telle fut l’offrande de Nahshôn, fils d’Amminadab.
18Le deuxième jour, Netanéel, fils de Tsouar, chef de la tribu d’Issacar, vint présenter son offrande.
19Elle consistait en un plat d’argent pesant 1,5 kilogramme, un calice d’argent de 800 grammes, selon le poids utilisé au sanctuaire, tous deux remplis de fleur de farine pétrie à l’huile, pour l’offrande, 20et une coupe d’or de 110 grammes pleine d’encens. 21Il amena aussi un jeune taureau, un bélier et un agneau dans sa première année pour l’holocauste, 22un bouc comme sacrifice pour le péché 23et deux taureaux, cinq béliers, cinq boucs et cinq agneaux dans leur première année pour le sacrifice de communion. Telle fut l’offrande de Netanéel, fils de Tsouar.
24Le troisième jour, Eliab, fils de Hélôn, chef de la tribu de Zabulon, vint présenter son offrande.
25Elle consistait en un plat d’argent pesant 1,5 kilogramme, un calice d’argent de 800 grammes, selon le poids utilisé au sanctuaire, tous deux remplis de fleur de farine pétrie à l’huile, pour l’offrande, 26et une coupe d’or de 110 grammes pleine d’encens. 27Il amena aussi un jeune taureau, un bélier et un agneau dans sa première année pour l’holocauste, 28un bouc comme sacrifice pour le péché 29et deux taureaux, cinq béliers, cinq boucs et cinq agneaux dans leur première année pour le sacrifice de communion. Telle fut l’offrande de Eliab, fils de Hélôn.
30Le quatrième jour, Elitsour, fils de Shedéour, chef de la tribu de Ruben, vint présenter son offrande.
31Elle consistait en un plat d’argent pesant 1,5 kilogramme, un calice d’argent de 800 grammes, selon le poids utilisé au sanctuaire, tous deux remplis de fleur de farine pétrie à l’huile, pour l’offrande, 32et une coupe d’or de 110 grammes pleine d’encens. 33Il amena aussi un jeune taureau, un bélier et un agneau dans sa première année pour l’holocauste, 34un bouc comme sacrifice pour le péché 35et deux taureaux, cinq béliers, cinq boucs et cinq agneaux dans leur première année pour le sacrifice de communion. Telle fut l’offrande de Elitsour, fils de Shedéour.
36Le cinquième jour, Sheloumiel, fils de Tsourishaddaï, chef de la tribu de Siméon, vint présenter son offrande.
37Elle consistait en un plat d’argent pesant 1,5 kilogramme, un calice d’argent de 800 grammes, selon le poids utilisé au sanctuaire, tous deux remplis de fleur de farine pétrie à l’huile, pour l’offrande, 38et une coupe d’or de 110 grammes pleine d’encens. 39Il amena aussi un jeune taureau, un bélier et un agneau dans sa première année pour l’holocauste, 40un bouc comme sacrifice pour le péché 41et deux taureaux, cinq béliers, cinq boucs et cinq agneaux dans leur première année pour le sacrifice de communion. Telle fut l’offrande de Sheloumiel, fils de Tsourishaddaï.
42Le sixième jour, Eliasaph, fils de Déouel, chef de la tribu de Gad, vint présenter son offrande.
43Elle consistait en un plat d’argent pesant 1,5 kilogramme, un calice d’argent de 800 grammes, selon le poids utilisé au sanctuaire, tous deux remplis de fleur de farine pétrie à l’huile, pour l’offrande, 44et une coupe d’or de 110 grammes pleine d’encens. 45Il amena aussi un jeune taureau, un bélier et un agneau dans sa première année pour l’holocauste, 46un bouc comme sacrifice pour le péché 47et deux taureaux, cinq béliers, cinq boucs et cinq agneaux dans leur première année pour le sacrifice de communion. Telle fut l’offrande d’Eliasaph, fils de Déouel.
48Le septième jour, Elishama, fils d’Ammihoud, chef de la tribu d’Ephraïm, vint présenter son offrande.
49Elle consistait en un plat d’argent pesant 1,5 kilogramme, un calice d’argent de 800 grammes, selon le poids utilisé au sanctuaire, tous deux remplis de fleur de farine pétrie à l’huile, pour l’offrande, 50et une coupe d’or de 110 grammes pleine d’encens. 51Il amena aussi un jeune taureau, un bélier et un agneau dans sa première année pour l’holocauste, 52un bouc comme sacrifice pour le péché 53et deux taureaux, cinq béliers, cinq boucs et cinq agneaux dans leur première année pour le sacrifice de communion. Telle fut l’offrande d’Elishama, fils d’Ammihoud.
54Le huitième jour, Gamliel, fils de Pédahtsour, chef de la tribu de Manassé, vint présenter son offrande.
55Elle consistait en un plat d’argent pesant 1,5 kilogramme, un calice d’argent de 800 grammes, selon le poids utilisé au sanctuaire, tous deux remplis de fleur de farine pétrie à l’huile, pour l’offrande, 56et une coupe d’or de 110 grammes pleine d’encens. 57Il amena aussi un jeune taureau, un bélier et un agneau dans sa première année pour l’holocauste, 58un bouc comme sacrifice pour le péché 59et deux taureaux, cinq béliers, cinq boucs et cinq agneaux dans leur première année pour le sacrifice de communion. Telle fut l’offrande de Gamliel, fils de Pédahtsour.
60Le neuvième jour, Abidân, fils de Guideoni, chef de la tribu de Benjamin, vint présenter son offrande.
61Elle consistait en un plat d’argent pesant 1,5 kilogramme, un calice d’argent de 800 grammes, selon le poids utilisé au sanctuaire, tous deux remplis de fleur de farine pétrie à l’huile, pour l’offrande, 62et une coupe d’or de 110 grammes pleine d’encens. 63Il amena aussi un jeune taureau, un bélier et un agneau dans sa première année pour l’holocauste, 64un bouc comme sacrifice pour le péché 65et deux taureaux, cinq béliers, cinq boucs et cinq agneaux dans leur première année pour le sacrifice de communion. Telle fut l’offrande d’Abidân, fils de Guideoni.
66Le dixième jour, Ahiézer, fils d’Ammishaddaï, chef de la tribu de Dan, vint présenter son offrande.
67Elle consistait en un plat d’argent pesant 1,5 kilogramme, un calice d’argent de 800 grammes, selon le poids utilisé au sanctuaire, tous deux remplis de fleur de farine pétrie à l’huile, pour l’offrande, 68et une coupe d’or de 110 grammes pleine d’encens. 69Il amena aussi un jeune taureau, un bélier et un agneau dans sa première année pour l’holocauste, 70un bouc comme sacrifice pour le péché 71et deux taureaux, cinq béliers, cinq boucs et cinq agneaux dans leur première année pour le sacrifice de communion. Telle fut l’offrande d’Ahiézer, fils d’Ammishaddaï.
72Le onzième jour, Paguiel, fils d’Okrân, chef de la tribu d’Aser, vint présenter son offrande.
73Elle consistait en un plat d’argent pesant 1,5 kilogramme, un calice d’argent de 800 grammes, selon le poids utilisé au sanctuaire, tous deux remplis de fleur de farine pétrie à l’huile, pour l’offrande, 74et une coupe d’or de 110 grammes pleine d’encens. 75Il amena aussi un jeune taureau, un bélier et un agneau dans sa première année pour l’holocauste, 76un bouc comme sacrifice pour le péché 77et deux taureaux, cinq béliers, cinq boucs et cinq agneaux dans leur première année pour le sacrifice de communion. Telle fut l’offrande de Paguiel, fils d’Okrân.
78Le douzième jour, Ahira, fils d’Enân, chef de la tribu de Nephtali, vint présenter son offrande.
79Elle consistait en un plat d’argent pesant 1,5 kilogramme, un calice d’argent de 800 grammes, selon le poids utilisé au sanctuaire, tous deux remplis de fleur de farine pétrie à l’huile, pour l’offrande, 80et une coupe d’or de 110 grammes pleine d’encens. 81Il amena aussi un jeune taureau, un bélier et un agneau dans sa première année pour l’holocauste, 82un bouc comme sacrifice pour le péché 83et deux taureaux, cinq béliers, cinq boucs et cinq agneaux dans leur première année pour le sacrifice de communion. Telle fut l’offrande d’Ahira, fils d’Enân.
84En tout, pour la dédicace de l’autel le jour où l’on en fit l’onction, les chefs d’Israël offrirent donc douze plats d’argent, douze calices d’argent et douze coupes d’or. 85Chaque plat pesait 1,5 kilogramme et chaque calice 800 grammes, ils offrirent donc en tout 27,5 kilogrammes d’argent selon l’unité de poids du sanctuaire. 86Chaque coupe pesait 110 grammes, ils offrirent donc en tout 1 300 grammes d’or. 87Pour les holocaustes, ils apportèrent douze taureaux, douze béliers et douze agneaux dans leur première année avec les offrandes qui les accompagnent et douze boucs pour le sacrifice pour le péché. 88Pour le sacrifice de communion, ils offrirent vingt-quatre taureaux, soixante béliers, soixante boucs et soixante agneaux d’un an. Tels furent les présents offerts pour la dédicace de l’autel, après son onction.
L’Eternel et Moïse
89Lorsque Moïse entrait dans la tente de la Rencontre pour parler avec l’Eternel, il entendait la voix qui lui parlait d’au-dessus du propitiatoire placé sur le coffre de l’acte de l’alliance entre les deux chérubins. Et il lui parlait.