Hesabu 6 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Hesabu 6:1-27

Mnadhiri

1Bwana akamwambia Mose, 26:2 Hes 6:5, 6; Mwa 28:20; Mdo 21:23; Amu 13:5; 16:17“Sema na Waisraeli na uwaambie: ‘Ikiwa mwanaume au mwanamke anataka kuweka nadhiri maalum, nadhiri ya kutengwa kwa ajili ya Bwana kama Mnadhiri, 36:3 Law 10:9; 25:5; Lk 1:15; Rut 2:14; Za 69:21; Mit 10:26ni lazima ajitenge na mvinyo na kinywaji kingine chochote chenye chachu, na kamwe asinywe siki itokanayo na mvinyo au itokanayo na kinywaji kingine chenye chachu. Kamwe asinywe maji ya zabibu wala kula zabibu mbichi au kavu. 4Kwa muda wote atakaokuwa Mnadhiri, kamwe hatakula chochote kitokanacho na mzabibu, sio mbegu wala maganda.

56:5 Za 52:2; 57:4; 59:7; Isa 7:20; Eze 5:1; 1Sam 1:11; Mao 4:7“ ‘Kwa muda wote wa nadhiri yake ya kujitenga kwa ajili ya Bwana, wembe hautapita kichwani mwake. Ni lazima awe mtakatifu mpaka kipindi cha kujitenga kwake kwa ajili ya Bwana kiishe; ni lazima aache nywele za kichwa chake zirefuke. 66:6 Law 21:1-3; Hes 19:11-22; Law 19:28; Yer 16:5-6; Eze 24:18; Mt 8:21Kwa kipindi chochote cha kujitenga kwa ajili ya Bwana hatakaribia maiti. 76:7 Hes 9:6Hata kama baba yake mwenyewe au mama au kaka au dada akifa, hatajinajisi mwenyewe kwa taratibu za ibada kwa ajili yao, kwa sababu ishara ya kujiweka wakfu kwake kwa Mungu ipo katika kichwa chake. 8Kwa kipindi chote cha kujitenga kwake yeye ni wakfu kwa Bwana.

96:9 Law 14:9; Hes 6:18“ ‘Kama mtu yeyote akifa ghafula karibu naye, atakuwa ametiwa unajisi nywele zake alizoziweka wakfu, hivyo ni lazima anyoe nywele zake siku ya utakaso wake, yaani siku ya saba. 106:10 Law 14:10-11; 5:7; 14:22Kisha siku ya nane ni lazima alete hua wawili au makinda mawili ya njiwa kwa kuhani katika mlango wa Hema la Kukutania. 116:11 Kut 29:36; 30:10; Mwa 8:20Kuhani atatoa mmoja kama sadaka ya dhambi, na mwingine kama sadaka ya kuteketezwa ili kufanya upatanisho kwa ajili yake kwa sababu ametenda dhambi kwa kuwepo mbele ya maiti. Siku iyo hiyo atakiweka wakfu kichwa chake. 126:12 Law 12:6; 5:15Ni lazima ajitoe kabisa kwa Bwana kwa kipindi cha kujitenga kwake, na ni lazima atoe mwana-kondoo wa mwaka mmoja kama sadaka ya hatia. Siku zilizopita hazitahesabiwa kwa sababu alijitia unajisi katika siku zake za kujitenga.

136:13 Mdo 21:26; Law 14:11“ ‘Basi hii ndiyo sheria kwa ajili ya Mnadhiri baada ya kipindi chake cha kujitenga kupita. Ataletwa kwenye ingilio la Hema la Kukutania. 146:14 Kut 12:5; Law 4:3; 14:10; 5:15; 3:1Hapo atatoa sadaka zake kwa Bwana: yaani, mwana-kondoo wa mwaka mmoja asiye na waa kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, kondoo mke wa mwaka mmoja asiye na waa kwa ajili ya sadaka ya dhambi, kondoo dume asiye na waa kwa ajili ya sadaka ya amani, 156:15 Law 2:1; 6:14; Mwa 35:14; Kut 29:2; Hes 15:1-7; Yn 6:50-53; Isa 62:9; 1Kor 10:31; 11:26pamoja na sadaka zake za nafaka na za vinywaji, na kikapu cha mikate isiyotiwa chachu, yaani maandazi yaliyotengenezwa kwa unga laini uliochanganywa na mafuta, na mikate myembamba iliyopakwa mafuta.

16“ ‘Kuhani atavileta vitu hivyo mbele za Bwana na kufanya sadaka ya dhambi na sadaka ya kuteketezwa. 176:17 Kut 29:41; Law 23:13Ataleta pia kikapu cha mikate isiyotiwa chachu, na atatoa dhabihu kondoo dume kama sadaka ya amani kwa Bwana, pamoja na sadaka yake ya nafaka na sadaka ya kinywaji.

186:18 Mdo 21:24; Lk 17:10; Rum 6:6; Gal 5:24; Efe 4:23; Kol 3:9“ ‘Kisha kwenye ingilio la Hema la Kukutania, Mnadhiri ni lazima anyoe nywele zake ambazo alikuwa ameziweka wakfu. Atazichukua hizo nywele na kuziweka ndani ya moto ulio chini ya dhabihu ya sadaka ya amani.

196:19 Law 7:12-13“ ‘Baada ya Mnadhiri kunyoa hizo nywele zake za kujitenga kwake, kuhani atampa mikononi mwake bega la kondoo dume lililochemshwa, na pia andazi na mkate mwembamba kutoka kwenye kikapu, vyote vikiwa vimetengenezwa bila kuwekwa chachu. 206:20 Law 7:30; 27:9; 7:34; Mhu 9:7; Isa 35:10; Ufu 14:13Kisha kuhani ataviinua mbele za Bwana kama sadaka ya kuinua; ni vitakatifu na ni mali ya kuhani, pamoja na kile kidari kilichoinuliwa na lile paja lililotolewa. Baada ya hayo, Mnadhiri anaweza kunywa divai.

21“ ‘Hii ndiyo sheria ya Mnadhiri ambaye anaweka nadhiri kwa matoleo yake kwa Bwana kufuatana na kujitenga kwake, zaidi ya chochote kile anachoweza kupata. Ni lazima atimize nadhiri aliyoiweka kufuatana na sheria ya Mnadhiri.’ ”

Baraka Ya Kikuhani

22Bwana akamwambia Mose, 236:23 Kum 21:5; 1Nya 23:13“Mwambie Aroni na wanawe, ‘Hivi ndivyo mtakavyowabariki Waisraeli. Waambieni:

246:24 Mwa 28:3; Kum 28:3-6; Za 17:9; 28:9; 128:5; 1Sam 2:9“ ‘ “Bwana akubariki

na kukulinda;

256:25 Ay 29:24; Za 4:6; 25:16; 86:16; 31:16; 80:3; 119:29, 135; Mwa 43:29Bwana akuangazie nuru ya uso wake

na kukufadhili;

266:26 Za 4:6; 44:3; 4:8; 29:11; 37:11, 37; 127:2; Isa 14:7; Yer 33:6; Yn 14:27Bwana akugeuzie uso wake

na kukupa amani.” ’

276:27 Kum 28:10; 2Sam 7:23; Neh 9:10; Yer 25:29; Eze 36:23“Hivyo wataliweka Jina langu juu ya Waisraeli, nami nitawabariki.”

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

民數記 6:1-27

拿細耳人的條例

1耶和華對摩西說: 2「你把以下條例告訴以色列人。

「無論男女,如果許願做拿細耳人,把自己獻給耶和華, 3就要禁戒淡酒和烈酒、淡酒或烈酒做的醋、葡萄汁、葡萄和葡萄乾。 4在做拿細耳人期間,葡萄樹所結的,包括葡萄核和葡萄皮,都不可吃。 5在許願做拿細耳人期間,不可用剃刀剃頭,要任由頭髮生長,要保持聖潔,一直到獻給耶和華的日期滿了。 6在獻給耶和華期間,不可挨近死屍, 7即使父母或是兄弟姊妹死了,也不可挨近,以免沾染不潔,因為他頭上有將自己奉獻給上帝的記號。 8在做拿細耳人期間,他是奉獻給耶和華的人。 9如果有人在他身邊暴斃,使他的頭髮沾染不潔,他要等到第七天潔淨的日子剃掉頭髮。 10第八天,他要帶兩隻斑鳩或雛鴿到會幕門口交給祭司。 11祭司要獻一隻作贖罪祭,另一隻作燔祭,為他碰過死屍贖罪。他要在當日使頭聖潔, 12重新開始過奉獻給耶和華的日子,還要帶一隻一歲的公羊羔作贖過祭。他以前做拿細耳人的日子無效,因為他沾染了不潔之物。

13「獻給耶和華的日子期滿後,拿細耳人要遵行以下條例。他要被帶到會幕門口, 14在那裡獻給耶和華一隻毫無殘疾、一歲的公羊羔作燔祭,一隻毫無殘疾、一歲母羊羔作贖罪祭,一隻毫無殘疾的公綿羊作平安祭, 15一籃調油的無酵細麵餅和塗油的無酵薄餅,以及素祭和奠祭。 16祭司要把這些祭物帶到耶和華面前,為他獻上贖罪祭和燔祭, 17然後把公綿羊和無酵餅獻給耶和華作平安祭,再獻上素祭和奠祭。 18拿細耳人要在會幕門口剃掉作為奉獻記號的頭髮,把頭髮放在平安祭的火裡燒掉。 19拿細耳人剃頭以後,祭司要取出一條煮好的公綿羊前腿,再從籃中拿出一塊無酵餅和一塊無酵薄餅,放在拿細耳人手中。 20然後,祭司要把這些祭物作為搖祭在耶和華面前搖一搖。這些祭物與作搖祭的胸肉和作舉祭的腿肉一樣,都是歸給祭司的聖物。此後,拿細耳人便可以喝酒。

21「以上是許願獻供物給耶和華的拿細耳人當守的條例和當獻的祭物。但如果他額外許願獻上力所能及之物,就必須還所許的願。」

祭司的祝福

22耶和華對摩西說: 23「你告訴亞倫父子們要這樣為以色列人祝福, 24『願耶和華賜福給你,保護你; 25願耶和華笑顏垂顧你,施恩給你; 26願耶和華恩待你,賜你平安。』 27他們要奉我的名為以色列人祝福,我必賜福給他們。」