Hesabu 4 – NEN & NIV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Hesabu 4:1-49

Wakohathi

1Bwana akawaambia Mose na Aroni, 24:2 Kut 30:12“Wahesabu Wakohathi walio sehemu ya Walawi kwa koo zao na jamaa zao. 34:3 Hes 1:46; 8:25; 1Nya 23:3, 24-27; Mwa 41:46; Ezr 3:8; Lk 3:23Wahesabu wanaume wote wenye umri wa miaka thelathini hadi hamsini wanaokuja kutumika katika kazi ya Hema la Kukutania.

44:4 Hes 3:28; 7:9“Hii ndiyo kazi ya Wakohathi katika Hema la Kukutania: Watatunza vitu vilivyo vitakatifu sana. 54:5 Kut 25:10, 16; 26:31-33; 1Nya 23:26; Law 16:2; 2Nya 3:14; Mt 27:51Wakati kambi inapohamishwa, Aroni na wanawe wataingia ndani na kushusha lile pazia la kuzuilia na kufunika nalo Sanduku la Ushuhuda. 64:6 Kut 25:5, 13-15; 1Fal 8:7; 2Nya 5:8Kisha watafunika juu yake na ngozi za pomboo,4:6 Pomboo hapa ina maana ya mnyama mwenye ngozi laini aishiye kwenye milima yenye misitu, au pengine nguva au sili. na kutandaza juu yake kitambaa cha rangi ya buluu iliyokolea na kuingiza mipiko mahali pake.

74:7 Law 24:6; Kut 25:30; 39:36; Yer 52:19“Juu ya meza ya mikate ya Wonyesho watatandaza kitambaa cha buluu na waweke sahani juu yake, masinia, bakuli na magudulia kwa ajili ya sadaka za kinywaji; mkate ule ambao upo hapa daima utabaki juu yake. 84:8 Kut 26:26-28Juu ya hivyo vitu watatandaza kitambaa chekundu na kufunika kwa ngozi za pomboo na kuweka mipiko yake mahali pake.

94:9 Kut 25:38“Watachukua kitambaa cha buluu na kufunika kinara cha taa kilicho kwa ajili ya nuru, pamoja na taa zake, mikasi yake, sinia zake, magudulia yake yote yaliyotumika kuwekea mafuta. 10Kisha watakisokotea pamoja na vifaa vyake vyote katika ngozi za pomboo na kukiweka kwenye jukwaa lake.

114:11 Kut 30:1-4“Juu ya madhabahu ya dhahabu watatandaza kitambaa cha buluu na kukifunika kwa ngozi za pomboo na kuweka mipiko yake mahali pake.

124:12 Hes 3:31“Watavichukua vyombo vyote vinavyotumika kuhudumia mahali patakatifu, watavisokotea kwenye kitambaa cha buluu na kufunika kwa ngozi za pomboo, na kuviweka juu ya miti ya kuchukulia.

134:13 Law 1:16; Kut 27:1-8; Hes 3:31“Wataondoa majivu kutoka madhabahu ya shaba na kutandaza kitambaa cha zambarau juu yake. 144:14 Kut 31:9; 27:3, 6; 1Nya 28:17; 2Nya 4:8, 11-16; Hes 7:84; Yer 52:6Kisha wataweka vyombo vyote juu yake vinavyotumika kwa kuhudumia madhabahuni pamoja na vyombo vya kutolea moto, nyuma, miiko na mabakuli ya kunyunyizia. Juu yake watatandaza ngozi za pomboo ya kufunika, na kuweka mipiko mahali pake.

154:15 Hes 3:27; 7:9; Kut 28:43; Hes 1:51; 2Sam 6:6, 7; Kum 31:9; 2Sam 6:6-7, 13; 1Nya 28:12-13“Baada ya Aroni na wanawe kumaliza kazi ya kufunika samani takatifu na vyombo vyake vyote, watu watakapokuwa tayari kungʼoa kambi, Wakohathi watakuja kufanya kazi ya kubeba. Lakini wasije wakagusa vitu vitakatifu la sivyo watakufa. Wakohathi ndio watakaobeba vile vitu vilivyomo katika Hema la Kukutania.

164:16 Law 6:14-23; 10:6; Hes 3:32; Kut 25:6; 29:41“Eleazari mwana wa Aroni, kuhani, ndiye atakayesimamia mafuta kwa ajili ya taa, uvumba wenye harufu nzuri, sadaka za kila siku za nafaka na mafuta ya upako. Ndiye atakayekuwa msimamizi wa maskani yote ya Bwana na kila kitu kilichomo ndani mwake pamoja na samani takatifu na vyombo vyake.”

17Bwana akawaambia Mose na Aroni, 18“Hakikisheni kwamba koo za kabila la Wakohathi hawatengwi kutoka Walawi. 194:19 Hes 3:32Ili wapate kuishi wala wasife wanapokaribia vitu vitakatifu sana, uwafanyie hivi: Aroni na wanawe watakwenda mahali patakatifu na kumgawia kila mtu kazi yake, na kwamba ni nini atakachochukua. 204:20 Kut 19:21; 1Sam 6:19Lakini Wakohathi hawaruhusiwi kuingia ndani ili kuangalia vitu vitakatifu, hata kwa kitambo kidogo, la sivyo watakufa.”

Wagershoni

21Bwana akamwambia Mose, 22“Wahesabu pia Wagershoni kwa jamaa zao na koo zao. 234:23 Hes 4:3; 1Nya 23:3; 24:27Wahesabu wanaume wote wenye umri wa miaka thelathini hadi hamsini ambao huja kutumika katika Hema la Kukutania.

24“Hii ndiyo huduma ya koo za Wagershoni wakati wanapofanya kazi na kubeba mizigo. 254:25 Kut 26:14; 27:10-18; Hes 3:25Watabeba mapazia ya maskani. Hema la Kukutania, kifuniko chake na kifuniko cha nje cha ngozi za pomboo, mapazia ya maingilio ya Hema la Kukutania, 264:26 Kut 27:9, 16; Hes 3:26mapazia ya ua unaozunguka Maskani na madhabahu, pazia la maingilio, kamba na vifaa vyote vinavyotumika katika huduma yake. Wagershoni watafanya yote yatakiwayo kufanyika na vitu hivi. 27Utumishi wao wote ukiwa ni kuchukua au wa kufanya kazi nyingine, utafanyika chini ya maelekezo ya Aroni na wanawe. Mtawapangia kama wajibu wao yote watakayoyafanya. 284:28 Hes 7:7; Kut 6:23Hii ndiyo huduma ya koo za Wagershoni katika Hema la Kukutania. Wajibu wao utakuwa chini ya maelekezo ya Ithamari mwana wa kuhani Aroni.

Wamerari

294:29 Kut 30:12; Mwa 46:11“Wahesabu Wamerari kwa koo zao na jamaa zao. 30Wahesabu wanaume wote kuanzia umri wa miaka thelathini hadi hamsini ambao watakuja kutumika katika Hema la Kukutania. 314:31 Hes 3:36; Kut 26:15; 27:9-19Huu ndio wajibu wao wanapofanya huduma katika Hema la Kukutania: kubeba miimo ya Maskani, mataruma yake, nguzo na vitako, 324:32 Hes 3:37; Kut 25:9; 1Nya 9:29; Ezr 8:24-30nguzo za ua unaozunguka pamoja na vitako vyake, vigingi vya hema, kamba, vifaa vyake vyote na kila kitu kinachohusiana na matumizi yake. Kila mtu mpangie vitu maalum vya kubeba. 334:33 Kut 28:21Huu ndio utumishi wa koo za Merari kama watakavyofanya kazi katika Hema la Kukutania, chini ya maelekezo ya Ithamari mwana wa kuhani, Aroni.”

Kuhesabiwa Kwa Koo Za Walawi

344:34 Hes 4:35-40; 1Kor 12:8-12; Kum 33:25Mose, Aroni na viongozi wa jumuiya wakawahesabu Wakohathi kwa koo zao na jamaa zao. 35Wanaume wote kuanzia umri wa miaka thelathini hadi hamsini ambao walikuja kutumika katika Hema la Kukutania, 36waliohesabiwa kwa koo zao, walikuwa 2,750. 374:37 Hes 3:27Hii ilikuwa ndiyo jumla ya wote wale wa koo za Wakohathi ambao walitumika katika Hema la Kukutania. Mose na Aroni waliwahesabu kufuatana na amri ya Bwana kupitia kwa Mose.

384:38 Mwa 46:11Wagershoni walihesabiwa kwa koo zao na jamaa zao. 39Watu wote kuanzia umri wa miaka thelathini hadi hamsini ambao walikuja kutumika katika Hema la Kukutania, 40waliohesabiwa kwa koo zao na jamaa zao, walikuwa 2,630. 41Hii ilikuwa ndiyo jumla ya wale wa koo za Gershoni ambao walitumika katika Hema la Kukutania. Mose na Aroni waliwahesabu kufuatana na amri ya Bwana.

42Wamerari walihesabiwa kwa koo zao na jamaa zao. 43Wanaume wote kuanzia umri wa miaka thelathini hadi miaka hamsini ambao walikuja kutumika katika Hema la Kukutania, 44waliohesabiwa kwa koo zao, walikuwa 3,200. 45Hii ilikuwa ndiyo jumla ya wale wa koo za Wamerari. Mose na Aroni waliwahesabu kufuatia amri ya Bwana kupitia kwa Mose.

46Hivyo Mose, Aroni na viongozi wa Israeli waliwahesabu Walawi wote kwa koo zao na jamaa zao. 474:47 Rum 12:6-8Wanaume wote wenye umri kuanzia miaka thelathini hadi hamsini waliokuja kufanya kazi ya kuhudumu na kubeba Hema la Kukutania 484:48 Hes 3:39walikuwa watu 8,580. 494:49 Hes 1:47; Rum 12:6-8Kwa amri ya Bwana kupitia Mose, kila mmoja aligawiwa kazi yake na kuambiwa kitu cha kubeba.

Hivyo ndivyo walivyohesabiwa kama Bwana alivyomwamuru Mose.

New International Version

Numbers 4:1-49

The Kohathites

1The Lord said to Moses and Aaron: 2“Take a census of the Kohathite branch of the Levites by their clans and families. 3Count all the men from thirty to fifty years of age who come to serve in the work at the tent of meeting.

4“This is the work of the Kohathites at the tent of meeting: the care of the most holy things. 5When the camp is to move, Aaron and his sons are to go in and take down the shielding curtain and put it over the ark of the covenant law. 6Then they are to cover the curtain with a durable leather,4:6 Possibly the hides of large aquatic mammals; also in verses 8, 10, 11, 12, 14 and 25 spread a cloth of solid blue over that and put the poles in place.

7“Over the table of the Presence they are to spread a blue cloth and put on it the plates, dishes and bowls, and the jars for drink offerings; the bread that is continually there is to remain on it. 8They are to spread a scarlet cloth over them, cover that with the durable leather and put the poles in place.

9“They are to take a blue cloth and cover the lampstand that is for light, together with its lamps, its wick trimmers and trays, and all its jars for the olive oil used to supply it. 10Then they are to wrap it and all its accessories in a covering of the durable leather and put it on a carrying frame.

11“Over the gold altar they are to spread a blue cloth and cover that with the durable leather and put the poles in place.

12“They are to take all the articles used for ministering in the sanctuary, wrap them in a blue cloth, cover that with the durable leather and put them on a carrying frame.

13“They are to remove the ashes from the bronze altar and spread a purple cloth over it. 14Then they are to place on it all the utensils used for ministering at the altar, including the firepans, meat forks, shovels and sprinkling bowls. Over it they are to spread a covering of the durable leather and put the poles in place.

15“After Aaron and his sons have finished covering the holy furnishings and all the holy articles, and when the camp is ready to move, only then are the Kohathites to come and do the carrying. But they must not touch the holy things or they will die. The Kohathites are to carry those things that are in the tent of meeting.

16“Eleazar son of Aaron, the priest, is to have charge of the oil for the light, the fragrant incense, the regular grain offering and the anointing oil. He is to be in charge of the entire tabernacle and everything in it, including its holy furnishings and articles.”

17The Lord said to Moses and Aaron, 18“See that the Kohathite tribal clans are not destroyed from among the Levites. 19So that they may live and not die when they come near the most holy things, do this for them: Aaron and his sons are to go into the sanctuary and assign to each man his work and what he is to carry. 20But the Kohathites must not go in to look at the holy things, even for a moment, or they will die.”

The Gershonites

21The Lord said to Moses, 22“Take a census also of the Gershonites by their families and clans. 23Count all the men from thirty to fifty years of age who come to serve in the work at the tent of meeting.

24“This is the service of the Gershonite clans in their carrying and their other work: 25They are to carry the curtains of the tabernacle, that is, the tent of meeting, its covering and its outer covering of durable leather, the curtains for the entrance to the tent of meeting, 26the curtains of the courtyard surrounding the tabernacle and altar, the curtain for the entrance to the courtyard, the ropes and all the equipment used in the service of the tent. The Gershonites are to do all that needs to be done with these things. 27All their service, whether carrying or doing other work, is to be done under the direction of Aaron and his sons. You shall assign to them as their responsibility all they are to carry. 28This is the service of the Gershonite clans at the tent of meeting. Their duties are to be under the direction of Ithamar son of Aaron, the priest.

The Merarites

29“Count the Merarites by their clans and families. 30Count all the men from thirty to fifty years of age who come to serve in the work at the tent of meeting. 31As part of all their service at the tent, they are to carry the frames of the tabernacle, its crossbars, posts and bases, 32as well as the posts of the surrounding courtyard with their bases, tent pegs, ropes, all their equipment and everything related to their use. Assign to each man the specific things he is to carry. 33This is the service of the Merarite clans as they work at the tent of meeting under the direction of Ithamar son of Aaron, the priest.”

The Numbering of the Levite Clans

34Moses, Aaron and the leaders of the community counted the Kohathites by their clans and families. 35All the men from thirty to fifty years of age who came to serve in the work at the tent of meeting, 36counted by clans, were 2,750. 37This was the total of all those in the Kohathite clans who served at the tent of meeting. Moses and Aaron counted them according to the Lord’s command through Moses.

38The Gershonites were counted by their clans and families. 39All the men from thirty to fifty years of age who came to serve in the work at the tent of meeting, 40counted by their clans and families, were 2,630. 41This was the total of those in the Gershonite clans who served at the tent of meeting. Moses and Aaron counted them according to the Lord’s command.

42The Merarites were counted by their clans and families. 43All the men from thirty to fifty years of age who came to serve in the work at the tent of meeting, 44counted by their clans, were 3,200. 45This was the total of those in the Merarite clans. Moses and Aaron counted them according to the Lord’s command through Moses.

46So Moses, Aaron and the leaders of Israel counted all the Levites by their clans and families. 47All the men from thirty to fifty years of age who came to do the work of serving and carrying the tent of meeting 48numbered 8,580. 49At the Lord’s command through Moses, each was assigned his work and told what to carry.

Thus they were counted, as the Lord commanded Moses.