Hesabu 33 – NEN & TNCV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Hesabu 33:1-56

Vituo Katika Safari Ya Waisraeli

133:1 Kut 17:1; 40:36; Hes 1:1; Kut 4:16; 6:26Hivi ndivyo vituo katika safari ya Waisraeli walipotoka Misri kwa vikosi chini ya uongozi wa Mose na Aroni. 233:2 Kut 17:4Kwa agizo la Bwana, Mose aliweka kumbukumbu ya vituo katika safari yao. Hivi ndivyo vituo katika safari yao:

333:3 Hes 10:2; Mwa 47:11; Yos 5:10; Kut 14:8; 1:11; 12:37; 12:2; 13:4; Za 105:38; Isa 52:12; Kut 14:8Waisraeli walisafiri kutoka Ramesesi katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa kwanza, siku iliyofuata Pasaka. Walitembea kwa ujasiri wazi mbele ya Wamisri wote, 433:4 Kut 4:23; 2Nya 24:24; Yer 15:3; Eze 14:21; Kut 12:12; Isa 19:1; Sef 2:11; Ufu 12:8waliokuwa wakizika wazaliwa wao wa kwanza wote, ambao Bwana alikuwa amewaua katikati yao, kwa kuwa Bwana alikuwa ameleta hukumu juu ya miungu yao.

533:5 Kut 12:37Waisraeli waliondoka Ramesesi na kupiga kambi huko Sukothi.

633:6 Kut 13:20; Mwa 33:17; Yos 13:27; Za 60:6Wakaondoka Sukothi na kupiga kambi huko Ethamu, pembeni mwa jangwa.

733:7 Kut 13:17, 18; 14:2, 9Wakaondoka Ethamu, wakageuka wakarudi Pi-Hahirothi, hadi mashariki ya Baal-Sefoni, wakapiga kambi yao karibu na Migdoli.

833:8 Kut 14:2; 14:22; 15:23Wakaondoka Pi-Hahirothi wakapita katikati ya bahari mpaka jangwani, na baada ya kusafiri kwa siku tatu katika Jangwa la Ethamu, walipiga kambi huko Mara.

933:9 Kut 15:27Wakaondoka Mara wakaenda Elimu, mahali ambapo palikuwa na chemchemi kumi na mbili na mitende sabini, huko wakapiga kambi.

1033:10 Kut 16:1Wakaondoka Elimu na kupiga kambi kando ya Bahari ya Shamu.

1133:11 Kut 16:1; 17:1Wakaondoka kando ya Bahari ya Shamu na kupiga kambi katika Jangwa la Sini.

12Wakaondoka katika Jangwa la Sini, wakapiga kambi huko Dofka.

13Wakaondoka Dofka, wakapiga kambi huko Alushi.

1433:14 Kut 15:22; 17:2Wakaondoka Alushi, wakapiga kambi Refidimu, mahali ambapo hapakuwa na maji kwa ajili ya watu kunywa.

1533:15 Kut 17:1; 19:1Wakaondoka Refidimu na kupiga kambi katika Jangwa la Sinai.

1633:16 Hes 11:34Wakaondoka katika Jangwa la Sinai na kupiga kambi huko Kibroth-Hataava.

1733:17 Hes 11; 35; Kum 9:22Wakaondoka Kibroth-Hataava na kupiga kambi huko Haserothi.

1833:18 Hes 12:16; Kum 1:1Wakaondoka Haserothi na kupiga kambi huko Rithma.

19Wakaondoka Rithma na kupiga kambi huko Rimon-Peresi.

2033:20 Yos 10:29; 12:15; 15:42; 21:13; 2Fal 8:22; 19:8; 23:31; 1Nya 6:57; 2Nya 21:10; Isa 37:8; Yer 52:1Wakaondoka Rimon-Peresi na kupiga kambi huko Libna.

21Wakaondoka Libna na kupiga kambi huko Risa.

22Wakaondoka Risa na kupiga kambi huko Kehelatha.

23Wakaondoka Kehelatha na kupiga kambi kwenye mlima Sheferi.

24Wakaondoka kwenye mlima Sheferi na kupiga kambi huko Harada.

25Wakaondoka Harada na kupiga kambi huko Makelothi.

26Wakaondoka Makelothi na kupiga kambi huko Tahathi.

27Wakaondoka Tahathi na kupiga kambi huko Tera.

28Wakaondoka Tera na kupiga kambi huko Mithka.

29Wakaondoka Mithka na kupiga kambi huko Hashmona.

3033:30 Kum 10:6Wakaondoka Hashmona na kupiga kambi Moserothi.

3133:31 Kum 10:6Wakaondoka Moserothi na kupiga kambi huko Bene-Yakani.

3233:32 Mwa 36:27; Kum 10:6; 1Nya 1:42Wakaondoka Bene-Yakani na kupiga kambi huko Hor-Hagidgadi.

3333:33 Kum 10:7Wakaondoka Hor-Hagidgadi na kupiga kambi huko Yotbatha.

34Wakaondoka Yotbatha na kupiga kambi huko Abrona.

3533:35 Kum 2:8; 1Fal 9:26; 22:48Wakaondoka Abrona na kupiga kambi huko Esion-Geberi.

3633:36 Hes 13:21; 20:1; Kum 32:51; Yos 15:1Wakaondoka Esion-Geberi na kupiga kambi huko Kadeshi katika Jangwa la Sini.

3733:37 Hes 20:22; Mwa 36:16; Hes 20:16Wakaondoka Kadeshi na kupiga kambi kwenye Mlima Hori, mpakani mwa Edomu. 3833:38 Hes 27:13; Kut 16:35; Hes 20:25-28; Kum 10:6; 32:50Kwa amri ya Bwana, kuhani Aroni alipanda Mlima Hori, mahali alipofia katika siku ya kwanza ya mwezi wa tano, mwaka wa arobaini baada ya Waisraeli kutoka Misri. 39Aroni alikufa juu ya Mlima Hori akiwa na umri wa miaka 123.

4033:40 Mwa 10:18; Hes 21:1; Mwa 12:9; Amu 1:16Mfalme Mkanaani wa Aradi, ambaye aliishi huko Negebu ya Kanaani, akasikia kwamba Waisraeli wanakuja.

41Wakaondoka kwenye mlima Hori na kupiga kambi huko Salmona.

42Wakaondoka Salmona, wakapiga kambi huko Punoni.

4333:43 Hes 21:10Wakaondoka Punoni, wakapiga kambi huko Obothi.

4433:44 Hes 21:11Wakaondoka Obothi, wakapiga kambi huko Iye-Abarimu, mipakani mwa Moabu.

4533:45 Hes 32:34Wakaondoka Iye-Abarimu, wakapiga kambi huko Dibon-Gadi.

4633:46 Yer 48:22; Eze 6:14Wakaondoka Dibon-Gadi na kupiga kambi huko Almon-Diblathaimu.

4733:47 Hes 27:12; 32:3; Kum 32:49Wakaondoka Almon-Diblathaimu na kupiga kambi katika milima ya Abarimu, karibu na Nebo.

4833:48 Hes 27:12; 26:3; Mwa 13:10; Hes 22:1; Yos 12:9Wakaondoka kwenye milima ya Abarimu na kupiga kambi kwenye tambarare ya Moabu, kando ya Yordani ngʼambo ya Yeriko. 4933:49 Yos 12:3; 13:20; Eze 25:9; Hes 21:16Huko kwenye tambarare za Moabu walipiga kambi kandokando ya Mto Yordani, kuanzia Beth-Yeshimothi mpaka Abel-Shitimu.

5033:50 Hes 33:48; 34:2Katika tambarare za Moabu kando ya Yordani kuvukia Yeriko, Bwana akamwambia Mose, 5133:51 Kum 7:1; 9:1; Yos 3:17“Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Mtakapovuka Mto Yordani kuingia Kanaani, 5233:52 Law 26:1; Za 106:34-36; Kut 23:24; 34:12-17; Kum 7:2-5, 25, 26; Yos 11:12; 23:7; Amu 2:2wafukuzeni wakazi wote wa nchi iliyo mbele yenu. Haribuni sanamu zao zote za kuchongwa, na sanamu zilizotengenezwa kwa kuyeyusha chuma, na kupabomoa mahali pao pa ibada. 5333:53 Kum 11:31; 17:14; Yos 1:11; 21:43; Za 24:1; Ay 14:11; Dan 4:35Mtaimiliki nchi hiyo na kukaa huko, kwa kuwa nimewapeni ninyi kuimiliki. 5433:54 Law 16:8; Hes 36:2; 26:54; 35:8; Yos 18:10Mtaigawanya nchi hiyo kwa kupiga kura, kufuatana na koo zenu. Kwa kundi kubwa zaidi toa urithi mkubwa zaidi, na kwa kundi dogo zaidi urithi mdogo zaidi. Chochote kinachowaangukia kwa kura kitakuwa chao. Mtaigawanya nchi kufuatana na makabila ya babu zenu.

5533:55 Yos 23:13; Amu 2:3; Za 106:36; Isa 55:13; Eze 2:6; 28:24; Mik 7:4; 2Kor 12:7; Kut 23:33; Mwa 17:8; Kum 1:7; Za 78:55; 105:11“ ‘Lakini kama hamkuwafukuza wenyeji wakaao katika nchi hiyo, wale mtakaowaruhusu wabaki watakuwa kama sindano kwenye macho yenu na miiba kwenu kila upande. Watawasumbua katika nchi mtakayoishi. 5633:56 Hes 14:28Kisha nitawatenda ninyi kile ambacho nimepanga kuwatenda wao.’ ”

Thai New Contemporary Bible

กันดารวิถี 33:1-56

เส้นทางการเดินทางของอิสราเอล

1ต่อไปนี้คือเส้นทางออกจากอียิปต์ของชาวอิสราเอล เป็นหมู่เหล่าภายใต้การนำของโมเสสกับอาโรน 2โมเสสบันทึกลำดับการเดินทางทุกระยะตามพระบัญชาขององค์พระผู้เป็นเจ้า

3ชนอิสราเอลออกจากเมืองราเมเสสในวันที่สิบห้าเดือนที่หนึ่ง วันรุ่งขึ้นหลังจากพิธีปัสกา พวกเขายกพลออกมาอย่างสง่าผ่าเผย ต่อหน้าต่อตาชาวอียิปต์ 4ซึ่งยุ่งอยู่กับการฝังศพบรรดาบุตรหัวปีที่ถูกองค์พระผู้เป็นเจ้าประหาร เนื่องด้วยองค์พระผู้เป็นเจ้าทรงลงโทษพระต่างๆ ของอียิปต์

5ชนอิสราเอลออกจากราเมเสสมาตั้งค่ายที่สุคคท

6จากสุคคทมาตั้งค่ายที่เอธามใกล้ถิ่นกันดาร

7จากเอธามวกกลับไปที่ปีหะหิโรท ไปยังแถบตะวันออกของบาอัลเซโฟน และตั้งค่ายใกล้ๆ มิกดล

8ออกจากปีหะหิโรท แล้วข้ามทะเลเข้าไปในถิ่นกันดาร และหลังจากเดินทางเป็นเวลาสามวันในถิ่นกันดาร เอธามก็มาตั้งค่ายที่มาราห์

9ออกจากมาราห์แล้วมาถึงเอลิม ที่ซึ่งมีธารน้ำพุสิบสองแห่ง และมีต้นอินทผลัมเจ็ดสิบต้น พวกเขาตั้งค่ายอยู่ที่นั่น

10จากเอลิม พวกเขามาตั้งค่ายพักริมทะเลแดง33:10 คือ ทะเลต้นกก

11และจากทะเลแดงมาตั้งค่ายที่ถิ่นกันดารสิน

12จากถิ่นกันดารสินมาตั้งค่ายที่โดฟคาห์

13จากโดฟคาห์มาตั้งค่ายที่อาลูช

14จากอาลูชมาตั้งค่ายที่เรฟีดิม ที่ซึ่งไม่มีน้ำให้ประชากรดื่ม

15จากเรฟีดิม พวกเขามายังถิ่นกันดารซีนาย

16จากถิ่นกันดารซีนายมาตั้งค่ายที่ขิบโรทหัทธาอาวาห์

17จากขิบโรทหัทธาอาวาห์มาตั้งค่ายที่ฮาเซโรท

18จากฮาเซโรทมาตั้งค่ายที่ริทมาห์

19จากริทมาห์มาตั้งค่ายที่ริมโมนเปเรศ

20จากริมโมนเปเรศมาตั้งค่ายที่ลิบนาห์

21จากลิบนาห์มาตั้งค่ายที่ริสสาห์

22จากริสสาห์มาตั้งค่ายที่เคเฮลาธาห์

23จากเคเฮลาธาห์มาตั้งค่ายที่ภูเขาเชเฟอร์

24จากภูเขาเชเฟอร์มาตั้งค่ายที่ฮาราดาห์

25จากฮาราดาห์มาตั้งค่ายที่มักเฮโลท

26จากมักเฮโลทมาตั้งค่ายที่ทาหัท

27จากทาหัทมาตั้งค่ายที่เทราห์

28จากเทราห์มาตั้งค่ายที่มิทคาห์

29จากมิทคาห์มาตั้งค่ายที่ฮัชโมนาห์

30จากฮัชโมนาห์มาตั้งค่ายที่โมเสโรท

31จากโมเสโรทมาตั้งค่ายที่เบเนยาอะคัน

32จากเบเนยาอะคันมาตั้งค่ายที่โฮร์ฮักกีดกาด

33จากโฮร์ฮักกีดกาดมาตั้งค่ายที่โยทบาธาห์

34จากโยทบาธาห์มาตั้งค่ายที่อับโรนาห์

35จากอับโรนาห์มาตั้งค่ายที่เอซีโอนเกเบอร์

36จากเอซีโอนเกเบอร์มาตั้งค่ายที่คาเดชในถิ่นกันดารศิน

37จากคาเดชมาตั้งค่ายที่ภูเขาโฮร์ ตรงชายแดนเอโดม 38ปุโรหิตอาโรนขึ้นไปบนภูเขาโฮร์ตามพระบัญชาขององค์พระผู้เป็นเจ้าและสิ้นชีวิตที่นั่น ในวันที่หนึ่งเดือนที่ห้าปีที่สี่สิบนับตั้งแต่ชนอิสราเอลออกมาจากอียิปต์ 39เมื่ออาโรนสิ้นชีวิตที่ภูเขาโฮร์นั้น เขามีอายุ 123 ปี

40กษัตริย์ชาวคานาอันแห่งอาราดผู้อาศัยอยู่ในเนเกบที่คานาอันได้ข่าวว่าชนอิสราเอลยกมา

41จากภูเขาโฮร์มาตั้งค่ายที่ศัลโมนาห์

42จากศัลโมนาห์มาตั้งค่ายที่ปูโนน

43จากปูโนนมาตั้งค่ายที่โอโบท

44จากโอโบทมาตั้งค่ายที่อิเยอาบาริมที่ชายแดนโมอับ

45จากไอยิม33:45 คือ อิเยอาบาริมมาตั้งค่ายที่ดีโบนกาด

46จากดีโบนกาดมาตั้งค่ายที่อัลโมนดิบลาธาอิม

47จากอัลโมนดิบลาธาอิมมาตั้งค่ายที่เทือกเขาอาบาริมใกล้เนโบ

48จากเทือกเขาอาบาริมมาตั้งค่ายในที่ราบโมอับริมแม่น้ำจอร์แดน ตรงข้ามเมืองเยรีโค 49ที่ซึ่งพวกเขาตั้งค่ายพักอยู่ริมแม่น้ำจอร์แดน จากเบธเยชิโมทจดอาแบลชิทธีม

50ในที่ราบโมอับริมแม่น้ำจอร์แดน ตรงข้ามเมืองเยรีโคนี้เององค์พระผู้เป็นเจ้าตรัสสั่งโมเสสว่า 51“จงแจ้งประชากรอิสราเอลว่า ‘เมื่อเจ้าทั้งหลายข้ามแม่น้ำจอร์แดนเข้าไปยังดินแดนคานาอัน 52จงขับไล่ชาวดินแดนนั้นออกไปให้หมด และทำลายล้างรูปเคารพทั้งปวงของพวกเขา ไม่ว่าหินสลัก รูปเคารพที่หล่อขึ้น และสถานบูชาบนที่สูงของพวกเขา 53จงเข้ายึดและตั้งถิ่นฐานที่นั่นเพราะเรายกดินแดนนี้ให้เจ้า 54จงทอดฉลากแบ่งสรรที่ดินกันตามตระกูล ที่ดินผืนใหญ่จะจับฉลากแบ่งกันในหมู่ตระกูลใหญ่ ส่วนที่เล็กลงมาจะจับฉลากแบ่งกันในหมู่ตระกูลเล็ก สิ่งที่เขาจับฉลากได้ก็จะเป็นของเขา จงแบ่งที่ดินไปตามเผ่าบรรพบุรุษของท่าน

55“ ‘แต่หากเจ้าทั้งหลายไม่ยอมขับไล่ประชากรที่อาศัยอยู่ที่นั่นออกไป คนที่เหลืออยู่จะเป็นหอกข้างแคร่และจะเป็นหนามยอกอกของเจ้า พวกเขาจะก่อปัญหาให้กับเจ้าในดินแดนที่เจ้าอาศัยอยู่ 56และเราจะทำกับเจ้าตามที่เราวางแผนไว้ว่าจะทำกับพวกเขา’ ”