Hesabu 31 – NEN & CST

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Hesabu 31:1-54

Kulipiza Kisasi Juu Ya Wamidiani

1Bwana akamwambia Mose, 231:2 Mwa 25:2; Hes 20:26; 25:17; Kum 32:35, 43; Mwa 15:15“Uwalipize kisasi Wamidiani kwa ajili ya Waisraeli. Halafu baada ya hayo, utakufa.”

331:3 Amu 11:36; 1Sam 24:12; 2Sam 4:8; 22:48; Za 94:1; 149:7; Isa 34:8; Yer 11:20; 46:10; Eze 25:17; Kum 32:35; Yer 50:28; Za 94:1; Rum 12:19; Ebr 10:30Kwa hiyo Mose akawaambia watu, “Waandaeni baadhi ya wanaume wenu waende vitani kupigana na Wamidiani ili wawalipize kisasi cha Bwana. 4Peleka wanaume 1,000 vitani kutoka kila kabila la Israeli.” 5Kwa hiyo waliandaliwa wanaume 12,000 kwa vita, wanaume 1,000 kutoka kila kabila, walitolewa kutoka koo za Israeli. 631:6 Kut 6:25; Hes 14:44; 10:2; 10:9Mose aliwatuma vitani, watu 1,000 kutoka kila kabila, pamoja na Finehasi mwana wa kuhani Eleazari, ambaye alichukua vyombo vya mahali patakatifu na tarumbeta za kuashiria.

731:7 Hes 25:16; Kum 20:13; Amu 21:11; 1Fal 11:15; 1Sam 27:9; 1Fal 11:15-16; Kum 20:13; Amu 21:11; 6:2, 33; 6:1Walipigana dhidi ya Wamidiani, kama Bwana alivyomwagiza Mose, nao waliua kila mwanaume. 831:8 Yos 13:21; Hes 25:15; 22:5; 24:14; Yos 13:22; Za 9:12; Yud 11; Ufu 2:14; 19:20Miongoni mwa watu waliouawa walikuwepo wafalme watano wa Midiani, nao ni Evi, Rekemu, Suri, Huri na Reba. Vilevile walimuua Balaamu mwana wa Beori kwa upanga. 931:9 Mwa 34:29Waisraeli waliwateka wanawake wa Kimidiani pamoja na watoto wao na walichukua makundi ya ngʼombe, kondoo na mali zao kama nyara. 1031:10 Yos 6:24; 8:28; 11:11; Amu 18:27; Mwa 25:16; 1Nya 6:54; Za 69:25; Eze 25:4Walichoma moto miji yote ambayo Wamidiani walikuwa wanaishi, pamoja na kambi zao zote. 1131:11 Kum 20:14; 2Nya 28:8Walichukua nyara zote na mateka, pamoja na watu na wanyama, 1231:12 Mwa 49:27; Kut 15:9; Hes 27:2nao waliwaleta wafungwa mateka na nyara kwa Mose na kwa kuhani Eleazari, nao Waisraeli walikusanyika kwenye kambi zao katika tambarare za nchi ya Moabu, kando ya Yordani ngʼambo ya Yeriko.

13Mose, kuhani Eleazari na viongozi wote wa jumuiya wakatoka kuwalaki nje ya kambi. 1431:14 Kut 18:21; Kum 1:15; 2Sam 18:1Mose aliwakasirikia maafisa wa jeshi, yaani hao wakuu wa jeshi wa maelfu na wakuu wa jeshi wa mamia, ambao walirudi kutoka vitani.

1531:15 Kum 2:34; 20:13; Yos 6:21; 8:25; 1Sam 15:3; Yos 10:40; 11:14Mose akawauliza, “Je, mmewaacha wanawake wote hai?” 1631:16 Hes 22:5; 24:14; 2Pet 2:15; Hes 23:25; 25:1-9; 14:37; Yos 22:17; Za 106:28-29; Hos 9:10; Mik 6:5; Ufu 2:14“Wanawake hao ndio waliofuata ushauri wa Balaamu, nao ndio waliowasababisha Waisraeli wamwasi Bwana kwa kile kilichotokea kule Peori, na kwa hiyo pigo liliwapata watu wa Bwana. 1731:17 Kum 7:2; 20:16; Amu 21:11Sasa waue wavulana wote. Pia muue kila mwanamke ambaye alikwisha fanya tendo la ndoa, 18lakini mwacheni hai kwa ajili yenu kila msichana ambaye kamwe hajawahi kuzini na mwanaume.

1931:19 Hes 5:2; 9:6, 10; 19:11, 12, 16; Law 21:1“Ninyi nyote ambao mmeua mtu yeyote au kumgusa mtu yeyote ambaye ameuawa, lazima mkae nje ya kambi kwa muda wa siku saba. Katika siku ya tatu na ya saba lazima mjitakase wenyewe pamoja na wafungwa wenu. 2031:20 Hes 19:19; Law 11:32Takaseni kila vazi pamoja na kila kitu kilichotengenezwa kwa ngozi, kwa singa za mbuzi au kwa mti.”

21Kisha kuhani Eleazari aliwaambia askari waliokuwa wamekwenda vitani, “Haya ndiyo matakwa ya sheria ambayo Bwana alimpa Mose: 2231:22 Yos 6:19; 22:8Dhahabu, fedha, shaba, chuma, bati, risasi, 2331:23 1Kor 3:13; Hes 8:7; 19:9, 17na kitu kingine chochote ambacho kinaweza kuhimili moto lazima mkipitishe kwenye moto, kisha kitakuwa safi. Lakini ni lazima pia kitakaswe kwa maji ya utakaso. Kitu chochote kisichoweza kuhimili moto lazima kipitishwe kwenye yale maji ya utakaso. 2431:24 Law 11:25; 14:8; Hes 19:10, 22; Za 51:2; Efe 5:26; Ebr 9:9-10Katika siku ya saba fueni nguo zenu, nanyi mtakuwa safi. Kisha mtaweza kuingia kambini.”

Kugawanya Mateka

25Bwana akamwambia Mose, 2631:26 Hes 1:4; 1:19“Wewe na kuhani Eleazari pamoja na viongozi wa jamaa ya jumuiya mtahesabu watu wote na wanyama ambao walitekwa. 2731:27 Yos 22:8; 1Sam 25:13; 30:24; Za 68:12Gawanyeni hizo nyara kati ya askari ambao walishiriki katika vita na kwa jumuiya. 2831:28 Hes 18:21; 2Sam 8:11; 1Nya 8:11; 26:27; Isa 18:7; 23:18; Mt 22:21Kutoka fungu la wale waliokwenda kupigana vitani, tenga kama ushuru kwa ajili ya Bwana kitu kimoja kati ya kila mia tano, ikiwa ni wanadamu, ngʼombe, punda, kondoo au mbuzi. 29Chukua ushuru huu kutoka fungu lao, umpe kuhani Eleazari kama sehemu ya Bwana. 3031:30 Hes 3:7; 16:3Kutoka fungu la Waisraeli, chukua kitu kimoja kati ya kila hamsini, ikiwa ni wanadamu, ngʼombe, punda, kondoo, mbuzi au wanyama wengine. Hivyo uwape Walawi, ambao wanawajibika kutunza Maskani ya Bwana.” 31Kwa hiyo Mose na kuhani Eleazari wakafanya kama Bwana alivyomwagiza Mose.

32Nyara zilizobaki kutoka mateka ambayo askari walichukua ni kondoo 675,000, 33ngʼombe 72,000, 34punda 61,000, 35na wanawake 32,000 ambao hawakumjua mume kwa kufanya tendo la ndoa.

36Nusu ya fungu la wale waliokwenda kupigana vitani lilikuwa:

Kondoo 337,500 3731:37 Law 25:23; Kum 10:14; Za 50:12; Mk 12:17; Lk 20:25; 1Kor 10:26ambayo ushuru kwa ajili ya Bwana ilikuwa kondoo 675;

38ngʼombe 36,000 ambao ushuru kwa ajili ya Bwana ulikuwa ngʼombe 72;

39punda 30,500 ambao ushuru kwa ajili ya Bwana ulikuwa punda 61;

40Watu 16,000 ambao ushuru kwa ajili ya Bwana ulikuwa watu 32.

4131:41 Hes 5:9; 18:8, 19Mose alimpa kuhani Eleazari ushuru kama sehemu ya Bwana, kama Bwana alivyomwagiza Mose.

42Ile nusu iliyokuwa ya Waisraeli, ambayo Mose aliitenga kutoka kwa ile ya watu waliokwenda vitani, 43nusu iliyokuwa ya jumuiya, ilikuwa kondoo 337,500, 44ngʼombe 36,000, 45punda 30,500, 46na wanadamu 16,000. 47Kutoka hiyo nusu iliyokuwa ya Waisraeli, Mose alichagua moja kati ya kila hamsini ya wanadamu na wanyama, kama Bwana alivyomwagiza, naye aliwapa Walawi, ambao waliwajibika kutunza Maskani ya Bwana.

48Kisha maafisa waliokuwa juu ya vikosi vya jeshi, wakuu wa jeshi wa maelfu na wakuu wa jeshi wa mamia, walimwendea Mose 4931:49 Hes 1:19; Yer 23:4; Kut 23:7; Law 26:7-9; Za 72:14; 116:15; 1Sam 30:19na kumwambia, “Watumishi wako wamehesabu askari walio chini ya amri yetu na hakuna hata mmoja aliyekosekana. 5031:50 Kut 30:16; Law 17:11; Mt 20:28; Rum 3:25Kwa hiyo tumeleta kama sadaka kwa Bwana vyombo vya dhahabu kila mmoja wetu alivyopata, yaani vikuku, bangili, pete za muhuri, vipuli na mikufu, ili kufanya upatanisho kwa ajili yetu mbele za Bwana.”

51Mose na kuhani Eleazari wakapokea kutoka kwao dhahabu, yaani vyombo vyote vilivyonakshiwa. 52Dhahabu yote kutoka kwa wakuu wa jeshi wa maelfu na wakuu wa jeshi wa mamia ambavyo Mose na kuhani Eleazari walimletea Bwana kama zawadi ilikuwa shekeli 16,75031:52 Shekeli 16,750 ni sawa na kilo 200. 5331:53 Mwa 34:29; Kum 20:14Kila askari alikuwa amejichukulia nyara zake binafsi. 5431:54 Kut 27:21; 40:2; 28:12; Hes 16:40; Kut 30:16; Yos 4:7; Zek 6:14; Lk 22:19; Mdo 1:4Mose na kuhani Eleazari walipokea dhahabu kutoka kwa wakuu wa jeshi wa maelfu na wakuu wa jeshi wa mamia, wakazileta katika Hema la Kukutania kama ukumbusho kwa Waisraeli mbele za Bwana.

Nueva Versión Internacional (Castilian)

Números 31:1-54

Guerra con Madián

1El Señor le dijo a Moisés: 2«Antes de partir de este mundo para reunirte con tus antepasados, en nombre de tu pueblo tienes que vengarte de los madianitas».

3Moisés se dirigió al pueblo y le dijo: «Preparad a algunos de vuestros hombres para la guerra contra Madián. Vamos a descargar sobre ellos la venganza del Señor. 4Que cada una de las tribus de Israel envíe mil hombres a la guerra».

5Los escuadrones de Israel proveyeron mil hombres por cada tribu, con lo que se reunieron doce mil hombres armados para la guerra. 6Moisés envió a la guerra a los mil hombres de cada tribu. Con ellos iba Finés, hijo del sacerdote Eleazar, quien tenía a su cargo los utensilios del santuario y las trompetas que darían la señal de ataque.

7Tal como el Señor le había ordenado a Moisés, los israelitas entraron en batalla y mataron a todos los madianitas. 8Pasaron a espada a Eví, Requen, Zur, Jur y Reba, que eran los cinco reyes de Madián, y también a Balán hijo de Beor. 9Capturaron a las mujeres y a los niños de los madianitas, y tomaron como botín de guerra todo su ganado, rebaños y bienes. 10A todas las ciudades y campamentos donde vivían los madianitas les prendieron fuego, 11y se apoderaron de gente y de animales. Todos los despojos y el botín 12se los llevaron a Moisés y al sacerdote Eleazar, y a toda la comunidad israelita. A los prisioneros, el botín y los despojos los llevaron hasta el campamento que estaba en las llanuras de Moab, cerca del Jordán, a la altura de Jericó.

13Moisés y el sacerdote Eleazar y todos los líderes de la comunidad salieron a recibirlos fuera del campamento. 14Moisés estaba furioso con los jefes de millares y de centenas de soldados que regresaban de la batalla. 15«¿Cómo es que dejasteis con vida a las mujeres? —les preguntó—. 16¡Si fueron ellas las que, aconsejadas por Balán, hicieron que los israelitas traicionaran al Señor en Baal Peor! Por eso murieron tantos del pueblo del Señor. 17Matad a todos los niños, y también a todas las mujeres que hayan tenido relaciones sexuales, 18pero quedaos con todas las muchachas que jamás las hayan tenido.

Purificación de combatientes y de prisioneros

19»Todos los que hayáis matado a alguien, o hayáis tocado un cadáver, deberéis quedaros fuera del campamento durante siete días. Al tercer día, y al séptimo, os purificaréis vosotros y vuestros prisioneros. 20También deberéis purificar toda la ropa, y todo artículo de cuero, de pelo de cabra, o de madera».

21El sacerdote Eleazar les dijo a los soldados que habían ido a la guerra: «Esto es lo que manda la ley que el Señor le entregó a Moisés: 22Oro, plata, bronce, hierro, estaño, plomo 23y todo lo que resista el fuego deberá ser pasado por el fuego para purificarse, pero también deberá limpiarse con las aguas de la purificación. Todo lo que no resista el fuego deberá pasar por las aguas de la purificación. 24Al séptimo día, lavaréis vosotros vuestros vestidos y quedaréis purificados. Entonces podréis reintegraros al campamento».

Reparto del botín

25El Señor le dijo a Moisés: 26«Tú y el sacerdote Eleazar y los jefes de las familias patriarcales haréis un recuento de toda la gente y de todos los animales capturados. 27Dividiréis el botín entre los soldados que fueron a la guerra y el resto de la comunidad. 28A los que fueron a la guerra les exigirás del botín una contribución para el Señor. Tanto de la gente como de los asnos, vacas u ovejas, apartarás uno de cada quinientos. 29Los tomarás de la parte que les tocó a los soldados, y se los darás al sacerdote Eleazar como contribución al Señor. 30De la parte que les toca a los israelitas, apartarás de la gente uno de cada cincuenta, lo mismo que de los asnos, vacas, ovejas u otros animales, y se los darás a los levitas, pues ellos son los responsables del cuidado de mi santuario».

31Moisés y el sacerdote Eleazar hicieron tal como el Señor le ordenó a Moisés.

32Sin tener en cuenta los despojos que tomaron los soldados, el botín fue de seiscientas setenta y cinco mil ovejas, 33setenta y dos mil cabezas de ganado, 34sesenta y un mil asnos 35y treinta y dos mil mujeres que jamás habían tenido relaciones sexuales.

36A los que fueron a la guerra les tocó lo siguiente:

Trescientas treinta y siete mil quinientas ovejas, 37de las cuales se entregaron seiscientas setenta y cinco como contribución al Señor.

38Treinta y seis mil vacas, de las cuales se entregaron setenta y dos como contribución al Señor.

39Treinta mil quinientos asnos, de los cuales se entregaron sesenta y uno como contribución al Señor.

40Dieciséis mil mujeres, de las cuales se entregaron treinta y dos como contribución al Señor.

41La parte que le correspondía al Señor, se la entregó Moisés al sacerdote Eleazar, tal como el Señor se lo había ordenado.

42Del botín que trajeron los soldados, Moisés tomó la mitad que les correspondía a los israelitas, 43de modo que a la comunidad le tocaron trescientas treinta y siete mil quinientas ovejas, 44treinta y seis mil vacas, 45treinta mil quinientos asnos 46y dieciséis mil mujeres. 47De la parte que les tocó a los israelitas, Moisés tomó una de cada cincuenta personas, y uno de cada cincuenta animales, tal como el Señor se lo había ordenado, y todos ellos se los entregó a los levitas, que eran los responsables del cuidado del santuario del Señor.

La ofrenda de los capitanes

48Entonces los oficiales que estaban a cargo de la tropa, es decir, los jefes de millares y de centenas de soldados, se acercaron a Moisés 49y le dijeron: «Tus siervos han pasado revista, y no falta ninguno de los soldados que estaban bajo nuestras órdenes. 50Por eso hemos traído, como ofrenda al Señor, los artículos de oro que cada uno de nosotros encontró: brazaletes, cadenas, sortijas, pendientes y collares. Todo esto lo traemos para hacer propiciación por nosotros ante el Señor».

51Moisés y el sacerdote Eleazar recibieron todos los artículos de oro. 52Todo el oro que los jefes de mil y de cien soldados presentaron como contribución al Señor pesó ciento noventa kilos.31:52 ciento noventa kilos. Lit. dieciséis mil setecientos cincuenta siclos. 53Cada soldado había tomado botín para sí mismo. 54Moisés y el sacerdote Eleazar recibieron el oro de manos de los jefes, y lo llevaron a la Tienda de reunión para que el Señor tuviera presentes a los israelitas.