Hesabu 3 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Hesabu 3:1-51

Walawi

13:1 Kut 6:27; 19:11Hii ni hesabu ya jamaa ya Aroni na Mose kwa wakati ambao Bwana alizungumza na Mose katika Mlima Sinai.

23:2 Hes 1:20; 26:30; Kut 6:23; 1Nya 6:3Majina ya wana wa Aroni yalikuwa: Nadabu mzaliwa wa kwanza na Abihu, Eleazari na Ithamari. 33:3 Kut 28:41; 29:30Hayo yalikuwa majina ya wana wa Aroni, makuhani wapakwa mafuta, waliokuwa wamesimikwa kuhudumu kama makuhani. 43:4 Law 10:1-6, 12; Hes 4:28; 1Nya 24:1; Hes 26:61; Kum 4:24; Isa 66:15; 2The 1:8; Ebr 12:29Hata hivyo Nadabu na Abihu walikufa mbele za Bwana walipotoa sadaka kwa moto usioruhusiwa mbele zake katika Jangwa la Sinai. Hawakuwa na wana; kwa hiyo Eleazari na Ithamari walihudumu peke yao kama makuhani wakati wote wa maisha ya Aroni baba yao.

5Bwana akamwambia Mose, 63:6 Kum 10:8; 31:9; 1Nya 15:2; Hes 8:6-22; 18:1-7; 2Nya 29:11“Walete watu wa kabila la Lawi mbele ya Aroni kuhani ili wamsaidie. 73:7 Hes 1:53; 8:19; Law 8:35Watafanya huduma kwa ajili yake na kwa jumuiya yote katika Hema la Kukutania kwa kufanya kazi za Maskani. 8Watatunza samani zote za Hema la Kukutania, wakitimiza wajibu wa kuhudumia Waisraeli kwa kufanya kazi ya Maskani. 93:9 Hes 8:19; 18:6Wakabidhi Walawi kwa Aroni na wanawe; hao ndio Waisraeli ambao wanakabidhiwa kwake kabisa. 103:10 Kut 30:7; 29:9; Hes 1:51; 18:7; Mdo 6:3-4; Rum 12:7; 1Sam 6:19; Hes 16:40; 18:7Waweke Aroni na wanawe kuhudumu kama makuhani; mtu mwingine yeyote atakayesogea mahali patakatifu ni lazima auawe.”

11Bwana akamwambia Mose, 123:12 Neh 13:12; Mal 2:4; Hes 8:14, 16-18; 16:9; Kut 13:2“Nimewatwaa Walawi kutoka miongoni mwa Waisraeli badala ya mzaliwa wa kwanza wa kiume wa kila mwanamke wa Mwisraeli. Walawi ni wangu, 133:13 Kut 13:12; Law 11:44kwa kuwa wazaliwa wote wa kwanza ni wangu. Nilipowaua wazaliwa wa kwanza huko Misri, nilimtenga kila mzaliwa wa kwanza katika Israeli awe wangu, akiwa mwanadamu au mnyama. Watakuwa wangu. Mimi ndimi Bwana.”

14Bwana akamwambia Mose katika Jangwa la Sinai, 153:15 Hes 1:19; 18:16; 26:62“Wahesabu Walawi kwa jamaa zao na koo zao. Mhesabu kila mwanaume mwenye umri wa mwezi mmoja au zaidi.” 16Kwa hiyo Mose akawahesabu, kama alivyoamriwa na neno la Bwana.

173:17 Mwa 29:34; 46:11; Hes 1:47; 1Nya 15:4; 23:6; 2Nya 29:12; Yos 21:4-6Haya yalikuwa majina ya wana wa Lawi:

Gershoni, Kohathi na Merari.

183:18 Kut 6:16-17Haya ndiyo yaliyokuwa majina ya koo za Wagershoni:

Libni na Shimei.

193:19 Kut 6:18Koo za Wakohathi zilikuwa ni:

Amramu, Ishari, Hebroni na Uzieli.

203:20 Mwa 46:11; Kut 6:19Koo za Wamerari zilikuwa ni:

Mahli na Mushi.

Hizi ndizo zilizokuwa koo za Walawi, kufuatana na jamaa zao.

213:21 Mwa 46:11; Kut 6:17Kulikuwa na koo za Walibni na Washimei kwa Gershoni; hizi ndizo zilizokuwa koo za Wagershoni. 22Idadi ya waume wote waliokuwa na mwezi mmoja au zaidi waliohesabiwa walikuwa 7,500. 233:23 Hes 2:18Ukoo wa Wagershoni walitakiwa kuweka kambi zao upande wa magharibi, nyuma ya Maskani. 24Kiongozi wa jamaa za Wagershoni alikuwa Eliasafu mwana wa Laeli. 253:25 Kut 25:9; 26:14, 36; 40:2; Hes 7:1; 4:25; 1Nya 9:14-33; Ezr 8:28-30Katika Hema la Kukutania, Wagershoni walikuwa na wajibu wa kutunza Maskani na hema, vifuniko vyake, pazia katika mlango wa kuingilia ndani ya Hema la Kukutania, 263:26 Kut 27:9; 35:18; Hes 4:26mapazia ya ua, pazia katika ingilio la ua unaozunguka Maskani na madhabahu, pamoja na kamba, na kila kinachohusika kwa matumizi yake.

273:27 Mwa 46:11; Kut 6:18; 1Nya 26:23; Hes 4:15, 37Kwa Kohathi kulikuwepo koo za Waamramu, Waishari, Wahebroni na Wauzieli; hizi ndizo zilizokuwa koo za Wakohathi. 283:28 Hes 4:4, 15; Kut 25:8; 30:13; 2Nya 30:19; Za 15:1; 20:2; Eze 44:27Hesabu ya waume wote wenye mwezi mmoja au zaidi ilikuwa watu 8,600. Wakohathi waliwajibika kutunza mahali patakatifu. 293:29 Hes 1:53Koo za Wakohathi zilitakiwa kuweka kambi zao upande wa kusini wa Maskani. 303:30 Kut 6:22Kiongozi wa jamaa za koo za Wakohathi alikuwa Elisafani mwana wa Uzieli. 313:31 Kut 25:10-22, 23, 31; 26:33; Kum 10:1-8; 2Nya 5:2; Yer 3:16; 1Nya 28:15; Yer 52:19; Hes 1:50; 4:5, 15; 18:3Waliwajibika kutunza Sanduku la Agano, meza, kinara cha taa, madhabahu, na vile vyombo vya mahali patakatifu vinavyotumika kuhudumu, pazia, na kila kitu kinachohusika na matumizi yake. 323:32 Kut 6:23; Hes 4:19; 18:3; 20:25-28; 2Fal 25:18Kiongozi mkuu wa Walawi alikuwa Eleazari mwana wa kuhani, Aroni. Aliwekwa juu ya wale waliowajibika kutunza mahali patakatifu.

333:33 Kut 6:19; Mwa 46:11Kwa Merari kulikuwa na koo za Wamahli na Wamushi; hizi zilikuwa koo za Merari. 34Hesabu ya waume wote wenye umri wa mwaka mmoja au zaidi waliohesabiwa walikuwa 6,200. 353:35 Hes 1:53; 2:25Kiongozi wa jamaa za koo za Wamerari alikuwa Surieli mwana wa Abihaili; hawa walitakiwa kuweka kambi zao upande wa kaskazini mwa Maskani. 363:36 Hes 4:32; Kut 26:15-25; 35:20-29; 36:36; Hes 18:3Wamerari waliwekwa kutunza miimo ya Maskani, mataruma yake, nguzo, vitako na vifaa vyake vyote na kila kitu kilichohusika na matumizi yake, 373:37 Kut 27:10-19na pia nguzo za ua unaozunguka pamoja na vitako vyake, vigingi vya hema na kamba zake.

383:38 Hes 2:3; 18:5; 1:51; 1Nya 9:27; 23:32Mose, na Aroni na wanawe walitakiwa kuweka kambi zao mashariki mwa Maskani, kuelekea mawio ya jua, mbele ya Hema la Kukutania. Wao walihusika na utunzaji wa mahali patakatifu kwa niaba ya Waisraeli. Mtu mwingine yeyote aliyepasogelea mahali patakatifu angeuawa.

393:39 Hes 26:62Jumla ya hesabu ya Walawi waliohesabiwa na Mose na Aroni kwa amri ya Bwana, kufuatana na koo, pamoja na kila mume mwenye umri wa mwezi mmoja au zaidi, walikuwa 22,000.

40Bwana akamwambia Mose, “Wahesabu wazaliwa wa kwanza wa kiume wote wa Waisraeli wenye umri wa mwezi mmoja au zaidi na uorodheshe majina yao. 413:41 Law 11:44Nitwalie Walawi badala ya wazaliwa wa kwanza wa Waisraeli, nayo mifugo ya Walawi badala ya wazaliwa wa mifugo ya Waisraeli. Mimi ndimi Bwana.”

42Hivyo Mose akawahesabu wazaliwa wa kwanza wote wa Waisraeli, kama Bwana alivyomwamuru. 43Jumla ya hesabu ya wazaliwa wa kwanza waume wenye umri wa mwezi mmoja au zaidi, walioorodheshwa kwa majina, walikuwa 22,273.

44Bwana akamwambia Mose, 453:45 Hes 3:12; 1Sam 1:28“Watwae Walawi badala ya wazaliwa wa kwanza wote wa Israeli, nayo mifugo ya Walawi badala ya mifugo yao. Walawi watakuwa wangu. Mimi ndimi Bwana. 463:46 Kut 13:13; Hes 18:15Ili kukomboa wazao wa kwanza 273 wa Waisraeli ambao wamezidi hesabu ya Walawi, 473:47 Law 27:6, 25; Kut 30:13; Hes 18:16; Eze 45:12kusanya shekeli tano3:47 Shekeli tano ni sawa na gramu 55. kwa kila mmoja, kufuatana na shekeli ya mahali patakatifu, ambayo ina uzito wa gera ishirini.3:47 Gera 20 ni sawa na gramu 11. 48Mpe Aroni na wanawe hizo fedha kwa ajili ya ukombozi wa idadi ya Waisraeli waliozidi.”

493:49 1Tim 2:6; Tit 2:14; Gal 4:4-5; 1Pet 1:18; Ebr 9:12Kwa hiyo Mose akakusanya fedha za ukombozi kutoka kwa wale ambao hesabu yao ilizidi wale waliokombolewa na Walawi. 503:50 1Sam 12:3-4; Mdo 20:33Kutokana na wazaliwa wa kwanza wa Waisraeli alikusanya fedha yenye uzito wa shekeli 1,3653:50 Shekeli 1,365 ni sawa na kilo 15.5. kufuatana na shekeli ya mahali patakatifu. 51Mose akampa Aroni na wanawe ile fedha ya ukombozi, kama alivyoamriwa na neno la Bwana.

New International Reader’s Version

Numbers 3:1-51

The Levites

1Here is the story of the family line of Aaron and Moses. It belongs to the time when the Lord spoke to Moses at Mount Sinai.

2Aaron’s oldest son was Nadab. Aaron’s other sons were Abihu, Eleazar and Ithamar. 3Those were the names of Aaron’s sons. They were the anointed priests. They were given authority to serve the Lord as priests. 4But Nadab and Abihu made an offering to the Lord by using fire that wasn’t allowed. So they died in front of him. That happened in the Desert of Sinai. They didn’t have any sons. Only Eleazar and Ithamar served as priests while their father Aaron was living.

5The Lord spoke to Moses. He said, 6“Bring the men of the tribe of Levi to Aaron the priest. They will help him. 7They must work at the tent of meeting for Aaron and for the whole community. They must do what needs to be done at the holy tent. 8They must take care of everything connected with the tent of meeting. When they do, they are acting for all the Israelites. 9Give the Levites to Aaron and his sons. They are the men of Israel who must be given completely to him. 10Appoint Aaron and his sons to serve as priests. Anyone else who approaches the sacred tent must be put to death.”

11The Lord also said to Moses, 12“I have taken the Levites from among the Israelites. I have taken them in place of the son born first to each woman in Israel. The Levites belong to me. 13That’s because every male born first to a mother is mine. In Egypt I struck down all the males born first. I did it when I set apart for myself every male born first to a mother in Israel. That is true for men and animals alike. They belong to me. I am the Lord.”

14The Lord spoke to Moses in the Desert of Sinai. He said, 15“Count the Levites by their family groups. Count every male a month old or more.” 16So Moses counted them. He did just as the word of the Lord had commanded him.

17The sons of Levi were

Gershon, Kohath and Merari.

18The major families from Gershon were

Libni and Shimei.

19The major families from Kohath were

Amram, Izhar, Hebron and Uzziel.

20The major families from Merari were

Mahli and Mushi.

These were the major families of the Levites.

21The families of Libni and Shimei belonged to the family of Gershon.

22All the males a month old or more were counted. There were 7,500 of them.

23The families of Gershon had to camp on the west side. They had to camp behind the holy tent.

24The leader of the families of Gershon was Eliasaph, the son of Lael.

25Here are the duties of the families of Gershon at the tent of meeting. They were responsible for taking care of the holy tent and its coverings. They took care of the curtain at the entrance to the tent of meeting. 26They took care of the curtains of the courtyard. And they took care of the curtain at the entrance to the courtyard. The courtyard was all around the holy tent and altar. The families of Gershon also took care of the ropes. In fact, they had to take care of everything connected with the use of all those things.

27The families of Amram, Izhar, Hebron and Uzziel belonged to the family of Kohath.

28All the males a month old or more were counted. There were 8,600 of them.

The families of Kohath were responsible for taking care of the sacred tent.

29They had to camp on the south side of the holy tent.

30The leader of the families of Kohath was Elizaphan, the son of Uzziel.

31They were responsible for taking care of the ark of the covenant law. They took care of the table for the holy bread. They took care of the lampstand and the two altars. They took care of the things used for serving in the sacred tent. They also took care of the inner curtain. In fact, they had to take care of everything connected with the use of all those things.

32The chief leader of the Levites was Eleazar. He was the son of Aaron the priest. Eleazar was appointed over those responsible for taking care of the sacred tent.

33The families of Mahli and Mushi belonged to the family of Merari.

34All the males a month old or more were counted. There were 6,200 of them.

35The leader of the families of Merari was Zuriel, the son of Abihail.

The families of Merari had to camp on the north side of the holy tent.

36They were responsible for taking care of the frames of the tent. They took care of its crossbars, posts and bases. They took care of all its supplies. In fact, they had to take care of everything connected with the use of all those things. 37They also took care of the posts of the courtyard around the holy tent. And they took care of the bases, tent stakes and ropes.

38Moses, Aaron and Aaron’s sons had to camp to the east of the holy tent. They had to camp toward the sunrise in front of the tent of meeting.

They were responsible for taking care of the sacred tent. They had to do it for the Israelites.

Anyone else who approached the tent would be put to death.

39The total number of the Levite males was 22,000. They were counted family by family. Every male a month old or more was counted. Moses and Aaron counted them, just as the Lord had commanded.

40The Lord said to Moses, “Count all the Israelite males born first in their families. Count all those a month old or more. Make a list of their names. 41Take the Levites for me in their place. And take the livestock of the Levites in place of all the male animals in Israel born first to their mothers. I am the Lord.”

42So Moses counted all the oldest sons in Israel. He did just as the Lord had commanded him. 43There were 22,273 of those sons a month old or more. They were listed by name.

44The Lord also said to Moses, 45“Take the Levites in place of all the males born first in Israel. Also take the livestock of the Levites in place of the livestock of Israel. The Levites belong to me. I am the Lord. 46But there are 273 more males born first in Israel than there are male Levites. 47Collect two ounces of silver for each of them. Weigh it out according to the standard weights used in the sacred tent. 48Give the silver to Aaron and his sons. It will buy the freedom of the additional sons in Israel.”

49So Moses collected the silver from the additional sons in Israel to buy their freedom. The Levites took the place of all the others. 50Moses collected 35 pounds of silver. It was weighed out according to the weights used in the sacred tent. Moses collected it from the oldest sons in Israel. 51He gave the silver to Aaron and his sons. He did just as the Lord had commanded him.