Hesabu 29 – NEN & NUB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Hesabu 29:1-40

Sikukuu Ya Tarumbeta

(Walawi 23:23-25)

129:1 Hes 28:18“ ‘Katika siku ya kwanza ya mwezi wa saba mtakuwa na kusanyiko takatifu na msifanye kazi ya kawaida. Ni siku kwa ajili yenu ya kupiga tarumbeta. 229:2 Hes 28:2; Law 1:9; Hes 28:11; Law 1:3; Hes 28:3Mtatayarisha sadaka ya kuteketezwa kama harufu nzuri impendezayo Bwana ya fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja, na wana-kondoo saba wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari. 329:3 Hes 28:12Pamoja na fahali, andaeni sadaka ya nafaka sehemu ya kumi tatu za efa za unga laini uliochanganywa na mafuta; kwa kondoo dume, andaa unga sehemu ya kumi mbili za efa; 429:4 Hes 28:13na pamoja na wana-kondoo saba kila mmoja aandaliwe na sehemu ya kumi ya efa ya unga. 529:5 Hes 28:15Ongeza beberu mmoja kama sadaka ya dhambi kufanya upatanisho kwa ajili yenu. 629:6 Hes 28:11; 28:3; 28:5; 28:7; Law 1:9; Hes 28:2; Dan 12:11; Law 6:9; Hes 15:11, 12Hivi ni nyongeza ya sadaka za kuteketezwa kila mwezi na kila siku pamoja na sadaka zake za nafaka na sadaka za vinywaji kama ilivyoainishwa. Ni sadaka zinazotolewa kwa Bwana kwa moto, harufu inayopendeza.

Siku Ya Upatanisho

(Walawi 23:26-32)

729:7 Mdo 27:9; Kut 31:15; Law 16:29; Ezr 8:21; Za 35:13; Isa 58:5; Lk 13:3-4; 1Kor 9:27; Yak 4:9“ ‘Kwenye siku ya kumi ya mwezi huu wa saba mtakuwa na kusanyiko takatifu. Mtajikana wenyewe na msifanye kazi. 829:8 Law 22:20; Hes 28:19; 29:8; Kum 15:21; 17:1Toeni sadaka ya kuteketezwa ya fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja, na wana-kondoo saba wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari, kama harufu nzuri inayompendeza Bwana. 929:9 Hes 28:12Pamoja na fahali, andaeni sadaka ya nafaka sehemu ya kumi tatu za efa za unga laini uliochanganywa na mafuta; pamoja na kondoo dume, sehemu ya kumi mbili za efa za unga laini; 1029:10 Hes 28:13na kwa kila mmoja wa wana-kondoo saba andaa sehemu ya kumi ya unga laini kwa kila mmoja. 1129:11 Hes 28:12; Law 16:3Ongeza beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, katika nyongeza ya sadaka ya dhambi kwa ajili ya upatanisho, na sadaka ya kawaida ya kuteketezwa pamoja na sadaka yake ya nafaka, na sadaka zake za vinywaji.

Sikukuu Ya Vibanda

(Walawi 23:33-44)

1229:12 1Fal 8:2; 12:32; Law 23:24“ ‘Katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa saba, mtakuwa na kusanyiko takatifu, na hamtafanya kazi za kawaida. Adhimisheni sikukuu kwa Bwana kwa siku saba. 1329:13 Hes 28:2; 28:3; Ebr 10:1-18; Ezr 3:8; Dan 9:24Toeni sadaka ya kuteketezwa mafahali wachanga kumi na watatu, kondoo dume wawili, na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari, kama harufu nzuri inayompendeza Bwana. 1429:14 Hes 15:6Pamoja na hao mafahali kumi na watatu, kila mmoja aandaliwe na sadaka ya nafaka sehemu ya kumi tatu za efa za unga laini uliochanganywa na mafuta; kwa kondoo dume wawili, kila mmoja aandaliwe sehemu ya kumi mbili za efa za unga laini; 1529:15 Hes 28:13na kwa wana-kondoo kumi na wanne, kila mmoja aandaliwe sehemu ya kumi ya efa ya unga laini. 1629:16 Hes 28:15Ongeza beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, kwa nyongeza ya sadaka ya kawaida ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka, pamoja na sadaka ya vinywaji.

1729:17 Law 23:36; Hes 28:3“ ‘Katika siku ya pili andaeni mafahali wachanga kumi na wawili, kondoo dume wawili, na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari. 1829:18 Hes 28:7, 14; 15:4-12; Law 2:1Pamoja na mafahali, kondoo dume, na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka na sadaka za vinywaji, kulingana na idadi iliyoainishwa. 1929:19 Hes 28:15; 28:3Weka beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, kwa nyongeza ya kawaida ya sadaka ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka, pamoja na sadaka zao za vinywaji.

20“ ‘Katika siku ya tatu andaeni mafahali wachanga kumi na wawili, kondoo dume wawili, na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari. 21Pamoja na mafahali, kondoo dume, na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka na sadaka za vinywaji, kulingana na idadi iliyoainishwa. 22Weka beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, kwa nyongeza ya kawaida ya sadaka ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka, pamoja na sadaka zao za vinywaji.

23“ ‘Katika siku ya nne andaeni mafahali wachanga kumi na wawili, kondoo dume wawili, na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari. 24Pamoja na mafahali, kondoo dume, na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka na sadaka za vinywaji, kulingana na idadi iliyoainishwa. 25Weka beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, kwa nyongeza ya kawaida ya sadaka ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka, pamoja na sadaka zao za vinywaji.

2629:26 Yn 1:29; Ebr 7:26; Ufu 5:6-14“ ‘Katika siku ya tano andaeni mafahali tisa, kondoo dume wawili na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari. 27Pamoja na mafahali, kondoo dume na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka na sadaka za kinywaji kulingana na idadi iliyoainishwa. 28Ongeza beberu mmoja kama sadaka ya dhambi katika nyongeza ya sadaka ya kawaida ya kuteketezwa na sadaka yake ya nafaka pamoja na sadaka ya kinywaji.

29“ ‘Katika siku ya sita andaeni mafahali wachanga kumi na wawili, kondoo dume wawili, na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari. 30Pamoja na mafahali, kondoo dume, na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka na sadaka za vinywaji, kulingana na idadi iliyoainishwa. 31Weka beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, kwa nyongeza ya kawaida ya sadaka ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka, pamoja na sadaka zao za vinywaji.

32“ ‘Katika siku ya saba andaeni mafahali wachanga kumi na wawili, kondoo dume wawili, na wana-kondoo kumi na wanne wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari. 33Pamoja na mafahali, kondoo dume, na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka na sadaka za vinywaji, kulingana na idadi iliyoainishwa. 34Weka beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, kwa nyongeza ya kawaida ya sadaka ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka, pamoja na sadaka zao za vinywaji.

3529:35 Law 23:36; Za 47:5-6; Isa 11:10; Ufu 7:9-17; 11:15“ ‘Katika siku ya nane mtakuwa na kusanyiko, na msifanye kazi ya kawaida. 36Toeni sadaka ya kuteketezwa kama harufu nzuri inayompendeza Bwana, sadaka ya kuteketezwa ya fahali mmoja, kondoo dume mmoja, na wana-kondoo dume saba wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari. 37Pamoja na fahali, kondoo dume na wana-kondoo, andaeni sadaka zao za nafaka, na sadaka za vinywaji, kulingana na idadi iliyoainishwa. 38Ongeza beberu mmoja kama sadaka ya dhambi, katika nyongeza ya sadaka ya kawaida ya kuteketezwa, na sadaka yake ya nafaka pamoja na sadaka ya kinywaji.

3929:39 Hes 36:2; 7:16; 23:2; 1:3; 1Nya 23:31; 2Nya 31:3; Law 3:1“ ‘Zaidi ya kile unachoweka nadhiri na sadaka zenu za hiari, andaeni hizi kwa ajili ya Bwana kwenye sikukuu zenu zilizoamriwa: sadaka zenu za kuteketezwa, sadaka za nafaka, sadaka za vinywaji, pamoja na sadaka zenu za amani.’ ”

4029:40 Kut 24:3; Kum 5:27-31; Yn 7:19; Mdo 7:37-38; 7:38Mose akawaambia Waisraeli yale yote Bwana alimwagiza.

Swedish Contemporary Bible

4 Moseboken 29:1-39

Offer under nyårshögtiden

(3 Mos 23:23-25)

1Den första dagen i sjunde månaden29:1 Nyårsdagen. Se 3 Mos 23:24 med fotnot. ska ni hålla en helig sammankomst och ingen får utföra något arbete. Låt hornen ljuda den dagen. 2Bär fram ett brännoffer, en välbehaglig lukt för Herren, som består av en ung tjur, en bagge och sju årsgamla lamm av hankön, alla felfria. 3Ett matoffer på nio liter fint mjöl blandat med olja ska offras tillsammans med tjuren, sex liter tillsammans med baggen 4och tre liter till vart och ett av de sju lammen. 5Till detta ska ni offra en bock som syndoffer för att få försoning. 6Dessa ska offras förutom nymånadsbrännoffret med dess matoffer och också utöver det dagliga brännoffret med dess tillhörande matoffer och dryckesoffer som det är bestämt, som en välbehaglig lukt för Herren.

Offer på försoningsdagen

(3 Mos 23:26-32)

7På tionde dagen i samma månad, den sjunde, ska en helig sammankomst hållas. Då ska ni ödmjuka er och inget arbete av något slag får då utföras. 8Då ska ni offra ett brännoffer till Herren, en behaglig lukt för honom, och det ska bestå av en ung tjur, en bagge och sju årsgamla lamm av hankön, alla felfria. 9Matoffret ska vara nio liter fint mjöl blandat med olja att offras tillsammans med tjuren, sex liter till baggen 10och tre liter till vart och ett av de sju lammen. 11Ni ska också offra en bock som syndoffer. Detta ska offras förutom försoningsdagens syndoffer och utöver det dagliga brännoffret med dess tillhörande matoffer och dryckesoffer.

Offer under lövhyddefesten

(3 Mos 23:33-43; 5 Mos 16:13-17)

12På femtonde dagen i sjunde månaden ska en helig sammankomst hållas och då får inget arbete utföras. Det är en sju dagar lång högtid inför Herren. 13Som brännoffer, ett eldoffer, en välbehaglig lukt inför Herren, ska ni offra tretton unga tjurar, två baggar och fjorton årsgamla lamm av hankön, alla felfria. 14Som tillhörande matoffer ska ni ge nio liter fint mjöl blandat med olja för var och en av de tretton tjurarna, sex liter för var och en av de två baggarna 15och tre liter för vart och ett av de fjorton lammen. 16Ni ska också bära fram en bock som syndoffer förutom det dagliga brännoffret med dess tillhörande matoffer och dryckesoffer.

17På den andra dagen ska ni offra tolv unga tjurar, två baggar och fjorton årsgamla lamm av hankön, alla felfria, 18tillsammans med de vanliga matoffren och dryckesoffren, efter antalet tjurar, baggar och lamm som det är föreskrivet. 19Ni ska också offra en bock som syndoffer utöver det dagliga brännoffret med dess tillhörande matoffer och dryckesoffer.

20På den tredje dagen i högtiden ska ni offra elva unga tjurar, två baggar, fjorton årsgamla lamm av hankön, alla felfria 21och de vanliga offren och dryckesoffren tillsammans med tjurarna, baggarna och lammen enligt givna föreskrifter och deras antal. 22Ni ska också offra en bock som syndoffer utöver det dagliga brännoffret med dess tillhörande matoffer och dryckesoffer.

23På den fjärde dagen ska ni offra tio unga tjurar, två baggar och fjorton årsgamla lamm av hankön, alla felfria 24och med tillhörande matoffer och dryckesoffer tillsammans med tjurarna, baggarna och lammen enligt givna föreskrifter och efter deras antal. 25Offra också en bock som syndoffer utöver det dagliga brännoffret med dess matoffer och dryckesoffer.

26På den femte dagen ska ni offra nio unga tjurar, två baggar och fjorton årsgamla lamm av hankön, alla felfria, 27tillsammans med de vanliga matoffren och dryckesoffren för tjurarna, baggarna och lammen enligt givna föreskrifter och efter deras antal. 28Offra också en bock som syndoffer utöver det dagliga brännoffret med dess tillhörande matoffer och dryckesoffer.

29På den sjätte dagen ska ni offra åtta unga tjurar, två baggar och fjorton årsgamla lamm av hankön, alla felfria 30tillsammans med de för tjurarna, baggarna och lammen föreskrivna matoffren och dryckesoffren efter djurens antal. 31Offra också en bock som syndoffer utöver det dagliga brännoffret med dess tillhörande mat- och dryckesoffer.

32På den sjunde dagen av högtiden ska ni offra sju unga tjurar, två baggar och fjorton årsgamla lamm av hankön, alla felfria, 33tillsammans med de för tjurarna, baggarna och lammen föreskrivna matoffren och dryckesoffren efter djurens antal. 34Offra också en bock som syndoffer utöver det dagliga brännoffret med dess tillhörande mat- och dryckesoffer.

35På den åttonde dagen ska ni samlas till högtid och ingen får arbeta den dagen. 36Bär fram ett brännoffer, ett eldoffer, en välbehaglig lukt inför Herren, som består av en ung tjur, en bagge och sju årsgamla lamm av hankön, alla felfria, 37tillsammans med de för tjuren, baggen och lammen föreskrivna mat- och dryckesoffren efter deras antal. 38Offra också en bock som syndoffer förutom det dagliga brännoffret med dess mat- och dryckesoffer. 39Dessa ska ni offra åt Herren vid era årliga högtider utöver de offer ni ger på grund av löften eller som frivilliga offer, brännoffer, matoffer, dryckesoffer eller gemenskapsoffer.’ ”