Hesabu 28 – NEN & KLB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Hesabu 28:1-31

Sadaka Za Kila Siku

(Kutoka 29:38-46)

1Bwana akamwambia Mose, 228:2 Law 23:1-44; 3:11; 1:9; Mal 1:7-12“Wape Waisraeli agizo hili na uwaambie: ‘Hakikisheni kwamba mnaniletea mimi kwa wakati uliowekwa chakula kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa kwa moto, kama harufu nzuri ya kupendeza.’ 328:3 Kut 12:3; 29:38; Amo 4:4; Kut 29:38Waambie: ‘Hii ni sadaka ya kuteketezwa kwa moto mnayomtolea Bwana: wana-kondoo wawili wa mwaka mmoja wasio na dosari, kama sadaka ya kawaida ya kuteketezwa kila siku. 428:4 Kut 29:39; 12:6Andaa mwana-kondoo mmoja asubuhi na mwingine jioni, 528:5 Hes 29:6; Law 6:20; 2:1; Kut 16:36; 29:38-42; Hes 15:4kila mmoja atolewe pamoja na sadaka ya nafaka sehemu ya kumi ya efa28:5 Sehemu ya kumi ya efa ni sawa na kilo moja. ya unga laini uliochanganywa pamoja na robo ya hini28:5 Robo ya hini ni sawa na lita moja. ya mafuta ya zeituni. 628:6 Law 1:3; Kut 19:3; Law 1:9Hii ni sadaka ya kawaida ya kuteketezwa iliyoanzishwa katika Mlima Sinai kama harufu nzuri ya kupendeza, sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto. 728:7 Hes 6:15; Law 10:9; 3:7; Hes 3:28; Kut 29:42; 30:9; Law 23:13; Hes 15:5-10; Isa 57:1Sadaka ya kinywaji itakayotolewa pamoja na kila mwana-kondoo ni robo ya hini ya kinywaji kilichochachuka. Mimina sadaka ya kinywaji kwa Bwana mahali patakatifu. 828:8 Kut 29:39; Law 23:7; 1:9Andaa yule mwana-kondoo wa pili jioni, pamoja na sadaka ya nafaka na sadaka ya kinywaji kama ulivyofanya kwa ile sadaka nyingine ya asubuhi. Hii ni sadaka iliyotolewa kwa kuteketezwa kwa moto, harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.

Sadaka Za Sabato

928:9 Kut 20:10; Mt 12:5; Law 23:13; Eze 46:4; 40:4“ ‘Siku ya Sabato, utatoa sadaka ya wana-kondoo wawili wa mwaka mmoja wasiokuwa na dosari pamoja na sadaka yake ya kinywaji na sadaka ya nafaka yenye uzito wa sehemu mbili za kumi za efa28:9 Sehemu mbili za kumi za efa ni sawa na kilo 2. za unga laini uliochanganywa na mafuta. 1028:10 Law 23:38; 1Sam 20:5; 1Nya 23:31; Neh 10:33; Isa 1:13-14; Eze 45:17; Hos 2:11; Kol 2:16Hii ni sadaka ya kuteketezwa itakayotolewa kwa ajili ya kila Sabato, pamoja na sadaka ya kawaida ya kuteketezwa na sadaka yake ya kinywaji.

Sadaka Za Kila Mwezi

1128:11 Hes 10:10; 7:15; Law 5:15; 1:3“ ‘Siku ya kwanza ya kila mwezi, mtamletea Bwana sadaka ya kuteketezwa ya fahali wawili wachanga, kondoo dume mmoja na wana-kondoo saba wa mwaka mmoja, wote wasiokuwa na dosari. 1228:12 Hes 15:6; 29:3; 15:9Pamoja na kila fahali, kutakuwa na sadaka ya nafaka ya unga laini sehemu tatu za kumi za efa,28:12 Sehemu tatu za kumi za efa ni sawa na kilo 3. uliochanganywa na mafuta, pamoja na kondoo dume mmoja, sadaka ya nafaka ya unga laini uliochanganywa na mafuta; 1328:13 Law 6:14; Hes 15:3; Law 1:9pamoja na kila mwana-kondoo, sadaka ya nafaka yenye uzito wa sehemu ya kumi ya efa ya unga laini uliochanganywa na mafuta. Hii ni kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, harufu nzuri, sadaka ya kuteketezwa iliyotolewa kwa moto kwa Bwana. 1428:14 Hes 15:11; 2Nya 2:4; Eze 3:5Pamoja na kila fahali kutakuwa na sadaka ya kinywaji nusu ya hini28:14 Nusu ya hini ni sawa na lita 2. ya divai; pamoja na kila kondoo dume, theluthi moja ya hini,28:14 Theluthi moja ya hini ni sawa na lita 1.2. na pamoja na kila mwana-kondoo robo hini. Hii ni sadaka ya kuteketezwa ya kila mwezi itakayotolewa kila mwandamo wa mwezi kwa mwaka. 1528:15 Hes 4:3; 29:16Zaidi ya sadaka ya kawaida ya kuteketezwa pamoja na sadaka yake ya kinywaji, mbuzi mmoja dume atatolewa kwa Bwana kama sadaka ya dhambi.

Pasaka

(Walawi 23:5-14)

1628:16 Kut 12:11; 2Nya 30:13; 35:1; Kut 12:6; Law 23:5; Lk 22:7“ ‘Katika siku ya kumi na nne ya mwezi wa kwanza, itafanyika Pasaka ya Bwana. 1728:17 Kut 12:19; 12:15Katika siku ya kumi na tano ya mwezi huo itakuwa sikukuu; kwa siku saba mtakula mikate isiyotiwa chachu. 1828:18 Kut 12:16; Law 23:7Katika siku ya kwanza mtakuwa na kusanyiko takatifu, msifanye kazi za kawaida. 1928:19 Law 1:9; 22:20; Hes 29:8; Kum 15:21Leteni mbele za Bwana sadaka ya kuteketezwa, sadaka ya kuteketezwa ya mafahali wawili wachanga, kondoo dume mmoja na wana-kondoo dume saba wenye umri wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari. 2028:20 Law 14:10Pamoja na kila fahali, andaa sadaka ya nafaka sehemu tatu za kumi za efa za unga laini uliochanganywa na mafuta; pamoja na kondoo dume, andaa sehemu mbili za kumi za efa; 21pia pamoja na kila mmoja wa wale wana-kondoo saba, andaa sehemu ya kumi ya efa. 2228:22 Law 4:2; 8:3; Hes 15:28; Law 16:18; Rum 8:3; Gal 4:4; Ebr 9:12; 10:1Pia mtoe beberu mmoja kama sadaka ya dhambi ambaye atafanya upatanisho kwa ajili yenu. 23Andaa hizi licha ya zile sadaka za kawaida za kuteketezwa za kila asubuhi. 2428:24 Law 1:9; 2Kor 2:15; Efe 5:2Kwa njia hii andaa chakula cha sadaka ya kuteketezwa kila siku, kwa siku saba kama harufu nzuri impendezayo Bwana. Hii itaandaliwa licha ya ile sadaka ya kawaida ya kuteketezwa ya kila siku pamoja na sadaka yake ya kinywaji. 2528:25 Kut 12:16; 13:6; Law 23:8Siku ya saba mwe na kusanyiko takatifu na msifanye kazi zenu za kawaida.

Sikukuu Ya Majuma

(Walawi 23:15-22)

2628:26 Kut 34:2; 23:16; Law 23:10; Kum 16:10; Mit 3:9; Mdo 2:1“ ‘Siku ya malimbuko, mnapomletea Bwana sadaka ya nafaka mpya wakati wa Sikukuu ya Majuma, mwe na kusanyiko takatifu na msifanye kazi zenu za kawaida. 2728:27 Law 23:18-19Mlete sadaka ya kuteketezwa ya mafahali wawili wachanga, kondoo dume mmoja, na pia wana-kondoo saba wenye umri wa mwaka mmoja, kama harufu nzuri ya kumpendeza Bwana. 28Pamoja na kila fahali itatolewa sadaka ya nafaka ya unga laini sehemu tatu za kumi za efa uliochanganywa na mafuta; pamoja na kondoo dume, andaa sehemu mbili za kumi za efa za unga laini; 29na sehemu ya kumi ya efa ya unga laini kwa kila mmoja wa wana-kondoo saba. 30Ongeza beberu mmoja kwa kufanya upatanisho kwa ajili yenu. 31Andaa hizi sadaka pamoja na sadaka zake za vinywaji, kuwa nyongeza ya sadaka za kawaida za kuteketezwa, pamoja na sadaka yake ya nafaka. Hakikisha kuwa wanyama hao hawana dosari.

Korean Living Bible

민수기 28:1-31

매일 드릴 제물

1여호와께서는 이스라엘 백성에게 이렇게 전하라고 모세에게 말씀하

2셨다. “너희가 제단에 태워 바치는 예물은 나의 양식이며 나를 기쁘게 하는 향기이다. 그러므로 너희는 그것을 정해진 시기에 바치도록 하여라.

3너희가 불로 태워 화제로 바칠 제물은 다음과 같다: 일 년 된 흠 없는 숫양 두 마리를 매일 번제로 바쳐라.

4한 마리는 아침에, 한 마리는 저녁에 바쳐야 한다.

5그리고 어린 양 한 마리에 고운 밀가루 28:5 히 ‘에바 1/10’2.2리터와 감람기름 28:5 히 ‘힌 1/4’약 리터를 섞어 소제로 바쳐라.

6이것은 시내산에서 처음 시작된 것으로 매일 불로 태워 바치는 번제이며 나 여호와를 기쁘게 하는 향기이다.

7그리고 술로 바치는 전제로 어린 양 한 마리에 독주 약 리터를 거룩한 곳에서 나 여호와에게 부어 바쳐라.

8저녁에도 아침에 바칠 때와 마찬가지로 어린 양 한 마리에 소제와 전제를 함께 바쳐야 한다. 이것도 태워 바치는 화제이며 나 여호와를 기쁘게 하는 향기이다.”

안식일에 드릴 제물

9“안식일에는 일 년 된 흠 없는 숫양 두 마리와 고운 밀가루 28:9 히 ‘에바 2/10’4.4리터에 감람기름을 섞은 소제와 여기에 따르는 전제를 바쳐라.

10이것은 매일 바치는 번제와 전제 외에 안식일마다 바치는 번제이다.”

매월 초하루에 드릴 제물

11“매월 초하루에는 수송아지 두 마리와 숫양 한 마리와 일 년 된 흠 없는 숫양 일곱 마리를 나 여호와에게 번제로 바쳐라.

12곡식으로 드리는 소제로는 수송아지 한 마리마다 고운 밀가루 28:12 히 ‘에바 3/10’6.6리터에 기름을 섞어 바치고 숫양 한 마리에는 고운 밀가루 4.4리터에 기름을 섞어 바칠 것이며

13어린 양 한 마리에는 고운 밀가루 2.2리터를 기름에 섞어 불로 태워 바쳐라. 이것은 나 여호와에게 향기로운 번제이다.

14그리고 전제로 바치는 포도주는 수송아지 한 마리에 약 1.8리터, 숫양 한 마리에 약 1.2리터, 어린 양 한 마리에 약 리터씩 바쳐야 한다. 이것은 일 년 내내 매월 초하루에 불로 태워 바치는 번제이다.

15그리고 28:15 암시됨.매월 초하루에는 매일 바치는 번제와 그 전제 외에 숫염소 한 마리를 속죄제로 나 여호와에게 바쳐라.”

무교절에 드릴 제물

16“1월 14일은 나 여호와를 기념하는 유월절이며

1715일부터는 7일 동안의 명절이 시작된다. 이 기간 동안 너희는 누룩 넣지 않은 빵을 먹고

18이 명절 첫날에는 너희가 거룩한 모임을 가지고 아무 일도 하지 말아라.

19그리고 너희는 수송아지 두 마리와 숫양 한 마리와 일 년 된 숫양 일곱 마리를 다 흠 없는 것으로 나 여호와에게 번제로 바치고

20-21그 소제는 고운 밀가루에 기름을 섞어 서 바쳐야 하며 그 밀가루는 수송아지 한 마리에 6.6리터, 숫양 한 마리에 4.4리터, 어린 양 한 마리에 2.2리터씩 바쳐야 한다.

22그리고 너희 죄를 속하기 위해 숫염소 한 마리를 속죄제물로 바쳐라.

23이것은 매일 아침 드리는 번제 외에 바치는 것이다.

24너희는 이와 똑같은 방법으로 7일 동안 매일 이 제물들을 나 여호와에게 바쳐라. 이것은 나의 음식이며 나를 기쁘게 하는 향기로운 화제이다. 너희는 이것을 매일 바치는 번제와 전제 외에 바쳐야 한다.

25그리고 7일째 되는 날에도 거룩한 모임을 가지고 아무 일도 하지 말아라.”

칠칠절에 드릴 제물

26“너희는 처음 익은 곡식을 바치는 칠칠절에 거룩한 모임을 가지고 아무 일도 하지 말고

27수송아지 두 마리와 숫양 한 마리와 일 년 된 숫양 일곱 마리를 나 여호와에게 향기로운 번제로 바쳐라.

28여기에 따르는 소제는 고운 밀가루에 기름을 섞어서 바쳐야 하며 그 밀가루는 수송아지 한 마리에 6.6리터, 숫양 한 마리에 4.4리터,

29어린 양 한 마리에 2.2리터씩 바쳐야 한다.

30그리고 너희 죄를 속하기 위해 숫염소 한 마리도 바쳐라.

31너희는 매일 드리는 번제와 소제와 전제 외에 이 제물들을 흠이 없는 것으로 바쳐야 한다.”