Hesabu 28 – NEN & JCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Hesabu 28:1-31

Sadaka Za Kila Siku

(Kutoka 29:38-46)

1Bwana akamwambia Mose, 228:2 Law 23:1-44; 3:11; 1:9; Mal 1:7-12“Wape Waisraeli agizo hili na uwaambie: ‘Hakikisheni kwamba mnaniletea mimi kwa wakati uliowekwa chakula kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa kwa moto, kama harufu nzuri ya kupendeza.’ 328:3 Kut 12:3; 29:38; Amo 4:4; Kut 29:38Waambie: ‘Hii ni sadaka ya kuteketezwa kwa moto mnayomtolea Bwana: wana-kondoo wawili wa mwaka mmoja wasio na dosari, kama sadaka ya kawaida ya kuteketezwa kila siku. 428:4 Kut 29:39; 12:6Andaa mwana-kondoo mmoja asubuhi na mwingine jioni, 528:5 Hes 29:6; Law 6:20; 2:1; Kut 16:36; 29:38-42; Hes 15:4kila mmoja atolewe pamoja na sadaka ya nafaka sehemu ya kumi ya efa28:5 Sehemu ya kumi ya efa ni sawa na kilo moja. ya unga laini uliochanganywa pamoja na robo ya hini28:5 Robo ya hini ni sawa na lita moja. ya mafuta ya zeituni. 628:6 Law 1:3; Kut 19:3; Law 1:9Hii ni sadaka ya kawaida ya kuteketezwa iliyoanzishwa katika Mlima Sinai kama harufu nzuri ya kupendeza, sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto. 728:7 Hes 6:15; Law 10:9; 3:7; Hes 3:28; Kut 29:42; 30:9; Law 23:13; Hes 15:5-10; Isa 57:1Sadaka ya kinywaji itakayotolewa pamoja na kila mwana-kondoo ni robo ya hini ya kinywaji kilichochachuka. Mimina sadaka ya kinywaji kwa Bwana mahali patakatifu. 828:8 Kut 29:39; Law 23:7; 1:9Andaa yule mwana-kondoo wa pili jioni, pamoja na sadaka ya nafaka na sadaka ya kinywaji kama ulivyofanya kwa ile sadaka nyingine ya asubuhi. Hii ni sadaka iliyotolewa kwa kuteketezwa kwa moto, harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.

Sadaka Za Sabato

928:9 Kut 20:10; Mt 12:5; Law 23:13; Eze 46:4; 40:4“ ‘Siku ya Sabato, utatoa sadaka ya wana-kondoo wawili wa mwaka mmoja wasiokuwa na dosari pamoja na sadaka yake ya kinywaji na sadaka ya nafaka yenye uzito wa sehemu mbili za kumi za efa28:9 Sehemu mbili za kumi za efa ni sawa na kilo 2. za unga laini uliochanganywa na mafuta. 1028:10 Law 23:38; 1Sam 20:5; 1Nya 23:31; Neh 10:33; Isa 1:13-14; Eze 45:17; Hos 2:11; Kol 2:16Hii ni sadaka ya kuteketezwa itakayotolewa kwa ajili ya kila Sabato, pamoja na sadaka ya kawaida ya kuteketezwa na sadaka yake ya kinywaji.

Sadaka Za Kila Mwezi

1128:11 Hes 10:10; 7:15; Law 5:15; 1:3“ ‘Siku ya kwanza ya kila mwezi, mtamletea Bwana sadaka ya kuteketezwa ya fahali wawili wachanga, kondoo dume mmoja na wana-kondoo saba wa mwaka mmoja, wote wasiokuwa na dosari. 1228:12 Hes 15:6; 29:3; 15:9Pamoja na kila fahali, kutakuwa na sadaka ya nafaka ya unga laini sehemu tatu za kumi za efa,28:12 Sehemu tatu za kumi za efa ni sawa na kilo 3. uliochanganywa na mafuta, pamoja na kondoo dume mmoja, sadaka ya nafaka ya unga laini uliochanganywa na mafuta; 1328:13 Law 6:14; Hes 15:3; Law 1:9pamoja na kila mwana-kondoo, sadaka ya nafaka yenye uzito wa sehemu ya kumi ya efa ya unga laini uliochanganywa na mafuta. Hii ni kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa, harufu nzuri, sadaka ya kuteketezwa iliyotolewa kwa moto kwa Bwana. 1428:14 Hes 15:11; 2Nya 2:4; Eze 3:5Pamoja na kila fahali kutakuwa na sadaka ya kinywaji nusu ya hini28:14 Nusu ya hini ni sawa na lita 2. ya divai; pamoja na kila kondoo dume, theluthi moja ya hini,28:14 Theluthi moja ya hini ni sawa na lita 1.2. na pamoja na kila mwana-kondoo robo hini. Hii ni sadaka ya kuteketezwa ya kila mwezi itakayotolewa kila mwandamo wa mwezi kwa mwaka. 1528:15 Hes 4:3; 29:16Zaidi ya sadaka ya kawaida ya kuteketezwa pamoja na sadaka yake ya kinywaji, mbuzi mmoja dume atatolewa kwa Bwana kama sadaka ya dhambi.

Pasaka

(Walawi 23:5-14)

1628:16 Kut 12:11; 2Nya 30:13; 35:1; Kut 12:6; Law 23:5; Lk 22:7“ ‘Katika siku ya kumi na nne ya mwezi wa kwanza, itafanyika Pasaka ya Bwana. 1728:17 Kut 12:19; 12:15Katika siku ya kumi na tano ya mwezi huo itakuwa sikukuu; kwa siku saba mtakula mikate isiyotiwa chachu. 1828:18 Kut 12:16; Law 23:7Katika siku ya kwanza mtakuwa na kusanyiko takatifu, msifanye kazi za kawaida. 1928:19 Law 1:9; 22:20; Hes 29:8; Kum 15:21Leteni mbele za Bwana sadaka ya kuteketezwa, sadaka ya kuteketezwa ya mafahali wawili wachanga, kondoo dume mmoja na wana-kondoo dume saba wenye umri wa mwaka mmoja, wote wasio na dosari. 2028:20 Law 14:10Pamoja na kila fahali, andaa sadaka ya nafaka sehemu tatu za kumi za efa za unga laini uliochanganywa na mafuta; pamoja na kondoo dume, andaa sehemu mbili za kumi za efa; 21pia pamoja na kila mmoja wa wale wana-kondoo saba, andaa sehemu ya kumi ya efa. 2228:22 Law 4:2; 8:3; Hes 15:28; Law 16:18; Rum 8:3; Gal 4:4; Ebr 9:12; 10:1Pia mtoe beberu mmoja kama sadaka ya dhambi ambaye atafanya upatanisho kwa ajili yenu. 23Andaa hizi licha ya zile sadaka za kawaida za kuteketezwa za kila asubuhi. 2428:24 Law 1:9; 2Kor 2:15; Efe 5:2Kwa njia hii andaa chakula cha sadaka ya kuteketezwa kila siku, kwa siku saba kama harufu nzuri impendezayo Bwana. Hii itaandaliwa licha ya ile sadaka ya kawaida ya kuteketezwa ya kila siku pamoja na sadaka yake ya kinywaji. 2528:25 Kut 12:16; 13:6; Law 23:8Siku ya saba mwe na kusanyiko takatifu na msifanye kazi zenu za kawaida.

Sikukuu Ya Majuma

(Walawi 23:15-22)

2628:26 Kut 34:2; 23:16; Law 23:10; Kum 16:10; Mit 3:9; Mdo 2:1“ ‘Siku ya malimbuko, mnapomletea Bwana sadaka ya nafaka mpya wakati wa Sikukuu ya Majuma, mwe na kusanyiko takatifu na msifanye kazi zenu za kawaida. 2728:27 Law 23:18-19Mlete sadaka ya kuteketezwa ya mafahali wawili wachanga, kondoo dume mmoja, na pia wana-kondoo saba wenye umri wa mwaka mmoja, kama harufu nzuri ya kumpendeza Bwana. 28Pamoja na kila fahali itatolewa sadaka ya nafaka ya unga laini sehemu tatu za kumi za efa uliochanganywa na mafuta; pamoja na kondoo dume, andaa sehemu mbili za kumi za efa za unga laini; 29na sehemu ya kumi ya efa ya unga laini kwa kila mmoja wa wana-kondoo saba. 30Ongeza beberu mmoja kwa kufanya upatanisho kwa ajili yenu. 31Andaa hizi sadaka pamoja na sadaka zake za vinywaji, kuwa nyongeza ya sadaka za kawaida za kuteketezwa, pamoja na sadaka yake ya nafaka. Hakikisha kuwa wanyama hao hawana dosari.

Japanese Contemporary Bible

民数記 28:1-31

28

ささげ物の規定

1-2主はまた、モーセに告げて言いました。「人々にこう伝えなさい。祭壇で焼いてささげるいけにえは、わたしの食物だから、毎日きちんと、わたしが教えたとおりにささげなさい。わたしはその香りによるささげ物を喜ぶ。

3火で焼くいけにえには、傷のない一歳の雄の子羊を使う。毎日二頭ずつ、焼き尽くすいけにえをささげる。 4朝に一頭、夕方に一頭。 5それといっしょに、細かくひいた粉二・三リットルに〇・九リットルの油を混ぜ合わせたものを、穀物の供え物としてささげる。 6シナイ山で定めたとおりである。良い香りのする、火で焼くささげ物として、毎日ささげなければならない。 7そのほかに、子羊一頭につき〇・九リットルの強いぶどう酒を、飲み物の供え物としてささげ、聖所のわたしの前で注ぐ。 8夕方には、もう一頭を、穀物の供え物、飲み物の供え物といっしょにささげる。それもまた、良い香りのする、火で焼くささげ物である。

9-10安息日には、いつものささげ物のほかに、傷のない一歳の雄羊を二頭ささげる。上等の小麦粉四・六リットルに油を混ぜた穀物の供え物と、ふだんと同じ飲み物の供え物を、いっしょにささげなさい。

11さらに、毎月一日には、焼き尽くすいけにえをささげる。傷のない若い雄牛二頭、雄羊一頭、一歳の雄の子羊七頭である。 12雄牛一頭につき、細かくひいた粉六・九リットルに油を混ぜた、穀物の供え物をささげる。雄羊には、これも細かくひいた粉四・六リットルに油を混ぜたもの、 13子羊なら、同じような粉二・三リットルに油を混ぜたものをささげる。これは、わたしの受け入れる、火で焼くいけにえである。 14このほかに、それぞれのいけにえに飲み物の供え物をつける。雄牛一頭につきぶどう酒一・九リットル、雄羊には一・一リットル、子羊には〇・九リットル。以上が、月ごとにささげる焼き尽くすいけにえの決まりである。 15毎月一日にはまた、罪が赦されるためのいけにえとして、雄やぎを一頭ささげる。毎日ささげるいけにえや飲み物の供え物のほかに、これをささげなさい。

16毎年第一の月の十四日に過越の祭りを祝いなさい〔これは、イスラエル人がエジプトを脱出する時、エジプト人の長男を殺すために来た神の使いが、イスラエル人の長男は見逃したことに感謝し、記念する祭り〕。 17翌日から一週間は、盛大な祭りを祝う。この間は、パン種の入ったパンは食べられない。 18最初の日には、全国民が仕事を休み、わたしの前で聖なる集会を開く。 19その時、傷のない若い雄牛二頭、雄羊一頭、一歳の雄の子羊七頭を、焼き尽くすいけにえとしてささげなさい。 20-21それに穀物の供え物として上等の粉に油を混ぜたものを、雄牛一頭につき六・九リットル、雄羊には四・六リットル、子羊には二・三リットルずつささげる。 22また、罪を赦してもらうために、雄やぎ一頭を、罪が赦されるためのいけにえとしてささげなさい。 23毎日するささげ物のほかに、以上のささげ物をしなければならない。

24祭りの期間中、毎日、同じいけにえをささげる。わたしはそのいけにえを受け入れる。 25そして七日目にはまた、すべての民が仕事を休み、聖なる集会を開くのだ。

26七週の祭り〔のちのペンテコステの祭り〕とも言われる刈り入れの祭りの日には、収穫を祝う神聖な集会を開きなさい。その日には、どんな仕事も休み、穀物の供え物として初物をささげる。 27また、何よりも私の心にかなう焼き尽くすいけにえをささげなさい。若い雄牛二頭、雄羊一頭、一歳の雄の子羊七頭である。 28-29それに、油を混ぜた上等の粉を穀物の供え物として、雄牛一頭につき六・九リットル、雄羊には四・六リットル、子羊には二・三リットルずつつける。 30また、罪が赦されるために、雄やぎを一頭ささげる。 31この特別ないけにえは、いつもの焼き尽くすいけにえ、穀物の供え物、飲み物の供え物のほかにささげる。いけにえにする動物は、必ず傷のないものでなければならない。