Hesabu 26 – NEN & NTLR

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Hesabu 26:1-65

Kuhesabiwa Watu Mara Ya Pili

126:1 Hes 14:37; 25:8Baada ya hiyo tauni, Bwana akamwambia Mose na Eleazari mwana wa kuhani Aroni, 226:2 Kut 30:11-16; Hes 1:3; Kut 38:25“Hesabu jumuiya yote ya Kiisraeli kwa jamaa zao, wale wote wenye umri wa miaka ishirini na zaidi, ambao wanaweza kutumika katika jeshi la Israeli.” 326:3 Hes 33:48; Yos 13:22; Hes 22:1; Kum 4:46-49Hivyo Mose na kuhani Eleazari wakazungumza na watu kwenye nchi tambarare ya Moabu, ngʼambo ya Yordani kutokea Yeriko, wakasema, 426:4 Kut 6:14; 13:3“Hesabuni wanaume wenye umri wa miaka ishirini na zaidi, kama Bwana alivyomwagiza Mose.”

Hawa ndio Waisraeli waliotoka Misri:

526:5 Hes 1:20; Mwa 46:8, 9; 1Nya 5:3; Ufu 7:5Wazao wa Reubeni, mwana mzaliwa wa kwanza wa Israeli, walikuwa:

kutoka kwa Hanoki, ukoo wa Wahanoki;

kutoka kwa Palu, ukoo wa Wapalu;

626:6 1Nya 5:3; Mwa 46:9kutoka kwa Hesroni, ukoo wa Wahesroni;

kutoka kwa Karmi, ukoo wa Wakarmi.

7Hizi zilikuwa ndizo koo za Reubeni; wale waliohesabiwa walikuwa 43,730.

8Mwana wa Palu alikuwa Eliabu, 926:9 Hes 16:1; 1:16; 16:2; Isa 65:16; Kum 11:6; Hes 27:3; 16:1, 2nao wana wa Eliabu walikuwa Nemueli, Dathani na Abiramu. Hawa wawili Dathani na Abiramu ndio walikuwa maafisa wa jumuiya ambao walimwasi Mose na Aroni, na walikuwa miongoni mwa wafuasi wa Kora wakati walimwasi Bwana. 1026:10 Kut 15:12; Hes 16:35, 38; Kut 3:12; Ay 31:3; Za 145:20; Yer 29:22; 2Pet 2:6; Yud 7Ardhi ilifunua kinywa chake na kuwameza pamoja na Kora, ambaye wafuasi wake walikufa wakati moto ulipowateketeza wanaume 250. Nao walikuwa kama alama ya onyo. 1126:11 Kut 6:24; Hes 16:33; Kum 5:9; 24:16; 2Fal 14:6; 2Nya 25:4; Eze 18:20Pamoja na hayo, hao ukoo wa Kora hawakufa.

1226:12 Mwa 46:10; 1Nya 4:24; Kut 6:15Wazao wa Simeoni kwa koo zao walikuwa:

kutoka kwa Nemueli, ukoo wa Wanemueli;

kutoka kwa Yamini, ukoo wa Wayamini;

kutoka wa Yakini, ukoo wa Wayakini;

1326:13 Mwa 46:10kutoka kwa Zera, ukoo wa Wazera;

kutoka kwa Shauli, ukoo wa Washauli.

1426:14 Mwa 46:10; Hes 1:23Hizi ndizo koo za Simeoni; walikuwa 22,200.

1526:15 Mwa 46:16Wazao wa Gadi kwa koo zao walikuwa:

kutoka kwa Sifoni, ukoo wa Wasifoni;

kutoka kwa Hagi, ukoo wa Wahagi;

kutoka kwa Shuni, ukoo wa Washuni;

16kutoka kwa Ozni, ukoo wa Waozni;

kutoka kwa Eri, ukoo wa Waeri;

1726:17 Mwa 46:16kutoka kwa Arodi, ukoo wa Waarodi;

kutoka kwa Areli, ukoo wa Waareli.

1826:18 Mwa 30:11; Hes 1:25; Yos 13:24-28Hizi ndizo zilizokuwa koo za Gadi; wale waliohesabiwa walikuwa 40,500.

1926:19 Mwa 38:3; 38:4; 38:7; 46:12; 1Nya 2:3Eri na Onani walikuwa wana wa Yuda, lakini walifia huko Kanaani.

2026:20 Mwa 38:5; 38:29; Yos 7:17Wazao wa Yuda kwa koo zao walikuwa:

kutoka kwa Shela, ukoo wa Washela;

kutoka kwa Peresi, ukoo wa Waperesi;

kutoka kwa Zera, ukoo wa Wazera.

2126:21 Mwa 38:29; Rut 4:19; 1Fal 2:9Wazao wa Peresi walikuwa:

kutoka kwa Hesroni, ukoo wa Wahesroni;

kutoka kwa Hamuli, ukoo wa Wahamuli.

2226:22 Hes 1:27Hizi ndizo zilizokuwa koo za Yuda; wale waliohesabiwa walikuwa 76,500.

2326:23 Mwa 46:13; 49:14Wazao wa Isakari kwa koo zao walikuwa:

kutoka kwa Tola, ukoo wa Watola;

kutoka kwa Puva, ukoo wa Wapuva;

2426:24 Mwa 46:13kutoka kwa Yashubu, ukoo wa Wayashubu;

kutoka kwa Shimroni, ukoo wa Washimroni.

2526:25 Mwa 30:18Hizi ndizo zilizokuwa koo za Isakari; wale waliohesabiwa walikuwa 64,300.

2626:26 Hes 1:30; Mwa 46:14; 49:13Wazao wa Zabuloni kwa koo zao walikuwa:

kutoka kwa Seredi, ukoo wa Waseredi;

kutoka kwa Eloni, ukoo wa Waeloni;

kutoka kwa Yaleeli, ukoo wa Wayaleeli.

2726:27 Mwa 30:20Hizi ndizo zilizokuwa koo za Zabuloni, wale waliohesabiwa walikuwa 60,500.

2826:28 Hes 1:32; 36:1; Mwa 41:52; 46:20; 48:3Wazao wa Yosefu kwa koo zao kutoka kwa Manase na kwa Efraimu walikuwa:

2926:29 Hes 1:34; Mwa 50:23; Amu 11:1; Hes 32:39Wazao wa Manase:

kutoka kwa Makiri, ukoo wa Wamakiri (Makiri alikuwa baba wa Gileadi);

kutoka kwa Gileadi, ukoo wa Wagileadi.

3026:30 Hes 27:1; 36:1; 1Nya 7:14; Yos 17:2; Amu 6:11; 8:2Hawa ndio waliokuwa wazao wa Gileadi:

kutoka kwa Iezeri, ukoo wa Waiezeri;

kutoka kwa Heleki, ukoo wa Waheleki;

31kutoka kwa Asirieli, ukoo wa Waasirieli;

kutoka kwa Shekemu, ukoo wa Washekemu;

32kutoka kwa Shemida, ukoo wa Washemida;

kutoka kwa Heferi, ukoo wa Waheferi.

3326:33 Hes 27:1; 36:2; Yos 17:3; 1Nya 7:15; Hes 27:3; 36:11(Selofehadi mwana wa Heferi hakuzaa wana, bali alikuwa na watoto wa kike tu, ambao majina yao yalikuwa Mahla, Noa, Hogla, Milka na Tirsa.)

3426:34 Hes 1:35Hizi ndizo zilizokuwa koo za Manase; wale waliohesabiwa walikuwa 52,700.

3526:35 Hes 1:32; 1Nya 7:20Hawa walikuwa wazao wa Efraimu kwa koo zao:

kutoka kwa Shuthela, ukoo wa Washuthela;

kutoka kwa Bekeri, ukoo wa Wabekeri;

kutoka kwa Tahani, ukoo wa Watahani;

36Hawa ndio walikuwa wazao wa Shuthela:

kutoka kwa Erani, ukoo wa Waerani.

3726:37 Hes 1:33; Kum 33:13-17Hizi ndizo zilizokuwa koo za Efraimu; wale waliohesabiwa walikuwa 32,500.

Hawa ndio waliokuwa wazao wa Yosefu kwa koo zao.

3826:38 Mwa 46:21; Hes 1:36; 1Nya 8:40Wazao wa Benyamini kwa koo zao walikuwa:

kutoka kwa Bela, ukoo wa Wabela;

kutoka kwa Ashbeli, ukoo wa Waashbeli;

kutoka kwa Ahiramu, ukoo wa Waahiramu;

3926:39 Mwa 46:21; 1Nya 7:12kutoka kwa Shufamu, ukoo wa Washufamu;

kutoka kwa Hufamu, ukoo wa Wahufamu.

4026:40 Mwa 46:21; 1Nya 8:3Wazao wa Bela kutoka kwa Ardi na Naamani walikuwa:

kutoka kwa Ardi, ukoo wa Waardi;

kutoka kwa Naamani, ukoo wa Wanaamani.

4126:41 Hes 1:37Hizi ndizo zilizokuwa koo za Benyamini; wale waliohesabiwa walikuwa 45,600.

4226:42 Hes 1:38, 39; Amu 18:19; Mwa 46:23; 49:16; Kum 33:22Hawa ndio waliokuwa wazao wa Dani kwa koo zao:

kutoka kwa Shuhamu, ukoo wa Washuhamu.

Hizi ndizo zilizokuwa koo za Dani: 43Wote walikuwa koo za Washuhamu; wale waliohesabiwa walikuwa 64,400.

4426:44 Hes 1:40; 26:47; 1:41Wazao wa Asheri kwa koo zao walikuwa:

kutoka kwa Imna, ukoo wa Waimna;

kutoka kwa Ishvi, ukoo wa Waishvi;

kutoka kwa Beria, ukoo wa Waberia;

45kutoka kwa wazao wa Beria:

kutoka kwa Heberi, ukoo wa Waheberi;

kutoka kwa Malkieli, ukoo wa Wamalkieli.

46(Asheri alikuwa na binti aliyeitwa Sera.)

47Hizi ndizo zilizokuwa koo za Asheri; wale waliohesabiwa walikuwa 53,400.

4826:48 Mwa 30:8; 46:24; 1Nya 7:13Wazao wa Naftali kwa koo zao walikuwa:

kutoka kwa Yaseeli, ukoo wa Wayaseeli;

kutoka kwa Guni, ukoo wa Waguni;

4926:49 1Nya 7:13kutoka kwa Yeseri, ukoo wa Wayeseri;

kutoka kwa Shilemu, ukoo wa Washilemu.

5026:50 Hes 1:42, 43Hizi ndizo zilizokuwa koo za Naftali; wale waliohesabiwa walikuwa 45,400.

5126:51 Kut 12:37; Hes 1:46; 2:32Jumla ya hesabu ya wanaume wa Israeli ilikuwa 601,730.

52Bwana akamwambia Mose, 5326:53 Yos 11:23; 14:1; Eze 45:8“Watagawiwa nchi kama urithi kwa kulingana na hesabu ya majina. 5426:54 Hes 33:54; 35:8Kundi kubwa zaidi lipe urithi mkubwa zaidi, na kundi dogo zaidi lipewe urithi mdogo zaidi; kila kundi litapokea urithi wake kulingana na hesabu ya wale walioorodheshwa. 5526:55 Hes 34:13; Yos 11:23; 14:2Hakikisha kuwa nchi inagawanywa kwa kura. Kile kitakachorithiwa na kila kikundi kitakuwa kwa kulingana na majina ya kabila la babu yao. 56Kila urithi utagawanywa kwa kura miongoni mwa makundi makubwa na madogo.”

5726:57 Mwa 46:11; Kut 6:16; 1Nya 6:16Hawa walikuwa Walawi ambao walihesabiwa kwa koo zao:

kutoka kwa Gershoni, ukoo wa Wagershoni;

kutoka kwa Kohathi, ukoo wa Wakohathi;

kutoka kwa Merari, ukoo wa Wamerari.

5826:58 Kut 6:20Hizi pia zilikuwa koo za Walawi:

ukoo wa Walibni;

ukoo wa Wahebroni;

ukoo wa Wamahli;

ukoo wa Wamushi;

ukoo wa wana wa Kora.

(Kohathi alikuwa baba aliyemzaa Amramu; 5926:59 Kut 2:1; 6:20; 2:4; 15:20jina la mke wa Amramu ni Yokebedi, naye pia alikuwa mzao wa Lawi, ambaye alizaliwa kwa Walawi nchini Misri. Alimzalia Amramu: Aroni, Mose na dada yao Miriamu. 6026:60 Kut 6:23Aroni alikuwa baba yake Nadabu na Abihu, Eleazari na Ithamari. 6126:61 Law 10:1-2; Hes 3:4; 1Nya 24; 2Lakini Nadabu na Abihu walikufa wakati walitoa sadaka mbele za Bwana kwa moto usioruhusiwa.)

6226:62 Hes 3:39; 1:47; 18:23; 2:33; 18:20-24; 35:2-8; Kum 14:27-29Wanaume wote wa Walawi wa umri wa mwezi mmoja na zaidi walikuwa 23,000. Wao hawakuhesabiwa pamoja na Waisraeli wengine kwa sababu hawakupokea urithi miongoni mwao.

6326:63 Hes 1:19; 22:1Hawa ndio walioorodheshwa na Mose na kuhani Eleazari wakati waliwahesabu Waisraeli kwenye nchi tambarare ya Moabu, kando ya Yordani ngʼambo ya Yeriko. 6426:64 Hes 14:29; 1:44; 1:1; Kum 2:14, 15Hakuna hata mmoja wao aliyekuwa miongoni mwa wale waliohesabiwa na Mose na kuhani Aroni wakati waliwahesabu Waisraeli katika Jangwa la Sinai. 6526:65 Hes 14:18; 1Kor 10:5; Hes 13:6; 11:28; Za 90:3-8; Rum 11:22; Kum 32:49-50; Yos 14:10; Hes 14:18, 30; Ebr 3:17, 18; Yud 5Kwa maana Bwana alikuwa amewaambia hao Waisraeli hakika wangekufa huko jangwani, wala hakuna mmoja wao aliyeachwa, isipokuwa Kalebu mwana wa Yefune na Yoshua mwana wa Nuni.

Nouă Traducere În Limba Română

Numeri 26:1-65

Al doilea recensământ al lui Israel

1După această urgie, Domnul le‑a vorbit lui Moise și preotului Elazar, fiul lui Aaron, zicând: 2„Faceți numărătoarea întregii comunități a fiilor lui Israel, potrivit caselor părinților lor, a fiecăruia din Israel, de la douăzeci de ani în sus, care este în stare să iasă la război.“

3Moise și preotul Elazar au vorbit poporului în câmpiile Moabului, lângă Iordan, în fața Ierihonului, zicând: 4„Faceți numărătoarea tuturor celor care au peste douăzeci de ani, așa cum Domnul le‑a poruncit lui Moise și fiilor lui Israel care au ieșit din țara Egiptului.“

5Ruben a fost întâiul născut al lui Israel. Fiii lui Ruben au fost:

prin Hanoh, clanul hanohiților;

prin Palu, clanul paluiților;

6prin Hețron, clanul hețroniților;

prin Carmi, clanul carmiților.

7Acestea alcătuiau clanurile rubeniților; au fost numărați patruzeci și trei de mii șapte sute treizeci de bărbați.

8Fiul lui Palu a fost Eliab. 9Fiii lui Eliab au fost: Nemuel, Datan și Abiram. Acest Datan și acest Abiram au fost cei chemați din comunitate, care s‑au răzvrătit împotriva lui Moise și împotriva lui Aaron, în comunitatea lui Korah, atunci când s‑au răzvrătit împotriva Domnului. 10Pământul și‑a deschis gura și i‑a înghițit împreună cu Korah, când focul a mistuit acea comunitate, în număr de două sute cincizeci de bărbați. Ei au slujit drept pildă pentru popor. 11Fiii lui Korah n‑au murit atunci.

12Urmașii lui Simeon, potrivit clanurilor lor, erau:

prin Nemuel, clanul nemueliților;

prin Iamin, clanul iaminiților;

prin Iachin, clanul iachiniților;

13prin Zerah, clanul zerahiților;

prin Saul, clanul sauliților.

14Acestea alcătuiau clanurile simeoniților; au fost numărați douăzeci și două de mii două sute de bărbați.

15Urmașii lui Gad, potrivit clanurilor lor, erau:

prin Țefon, clanul țefoniților;

prin Haghi, clanul haghiților;

prin Șuni, clanul șuniților;

16prin Ozni, clanul ozniților;

prin Eri, clanul eriților;

17prin Arodi, clanul arodiților;

prin Areli, clanul areliților.

18Acestea alcătuiau clanurile urmașilor lui Gad; au fost numărați patruzeci de mii cinci sute de bărbați.

19Fiii lui Iuda au fost Er și Onan; dar atât Er, cât și Onan au murit în Canaan.

20Fiii lui Iuda, potrivit clanurilor lor, erau:

prin Șela, clanul șelaniților;

prin Pereț, clanul perețiților;

prin Zerah, clanul zerahiților.

21Urmașii lui Pereț au fost:

prin Hețron, clanul hețroniților;

prin Hamul, clanul hamuliților.

22Acestea alcătuiau clanurile urmașilor lui Iuda; au fost numărați șaptezeci și șase de mii cinci sute de bărbați.

23Urmașii lui Isahar, potrivit clanurilor lor, erau:

prin Tola, clanul tolaiților;

prin Puia, clanul puiților;

24prin Iașub, clanul iașubiților;

prin Șimron, clanul șimroniților.

25Acestea alcătuiau clanurile urmașilor lui Isahar; au fost numărați șaizeci și patru de mii trei sute de bărbați.

26Urmașii lui Zabulon, potrivit clanurilor lor, erau:

prin Sered, clanul serediților;

prin Elon, clanul eloniților;

prin Iahleel, clanul iahleeliților.

27Acestea alcătuiau clanurile urmașilor lui Zabulon; au fost numărați șaizeci de mii cinci sute de bărbați.

28Urmașii lui Iosif, potrivit clanurilor lor, erau: Manase și Efraim.

29Urmașii lui Manase au fost:

prin Machir, clanul machiriților (Machir a fost tatăl lui Ghilad);

prin Ghilad, clanul ghiladiților.

30Urmașii lui Ghilad au fost:

prin Iezer, clanul iezeriților;

prin Helek, clanul helekiților;

31prin Asriel, clanul asrieliților;

prin Șechem, clanul șechemiților;

32prin Șemida, clanul șemidaiților;

prin Hefer, clanul heferiților.

33(Țelofhad, fiul lui Hefer, nu a avut fii; el a avut doar fiice, ale căror nume erau: Mahla, Noa, Hogla, Milca și Tirța.)

34Acestea alcătuiau clanurile urmașilor lui Manase; au fost numărați cincizeci și două de mii șapte sute de bărbați.

35Urmașii lui Efraim, potrivit clanurilor lor, au fost:

prin Șutelah, clanul șutelahiților;

prin Becher, clanul becheriților;

prin Tahan, clanul tahaniților.

36Urmașii lui Șutelah au fost:

prin Eran, clanul eraniților.

37Acestea alcătuiau clanurile urmașilor lui Efraim; au fost numărați treizeci și două de mii cinci sute de bărbați.

Aceștia au fost urmașii lui Iosif, potrivit clanurilor lor.

38Urmașii lui Beniamin, potrivit clanurilor lor, erau:

prin Bela, clanul belaiților;

prin Așbel, clanul așbelaiților;

prin Ahiram, clanul ahiramiților;

39prin Șufam, clanul șufamiților;

prin Hufam, clanul hufamiților.

40Urmașii lui Bela, prin Ard și Naaman, au fost:

prin Ard, clanul ardiților;

prin Naaman, clanul naamaniților.

41Acestea alcătuiau clanurile urmașilor lui Beniamin; au fost numărați patruzeci și cinci de mii șase sute de bărbați.

42Fiii lui Dan, potrivit clanurilor lor, erau:

prin Șuham, clanul șuhamiților.

Acestea erau clanurile lui Dan, potrivit clanurilor lor. 43Toți cei din clanurile șuhamiților au fost în număr de șaizeci și patru de mii patru sute de bărbați.

44Urmașii lui Așer, potrivit clanurilor lor, erau:

prin Imna, clanul imniților;

prin Ișvi, clanul ișviților;

prin Beria, clanul beriților;

45iar prin urmașii lui Beria:

prin Heber, clanul heberiților;

prin Malchiel, clanul malchieliților.

46(Numele fiicei lui Așer era Serah.)

47Acestea alcătuiau clanurile urmașilor lui Așer; au fost numărați cincizeci și trei de mii patru sute de bărbați.

48Urmașii lui Neftali, potrivit clanurilor lor, erau:

prin Iahțeel, clanul iahțeeliților;

prin Guni, clanul guniților;

49prin Iețer, clanul iețeriților;

prin Șilem, clanul șilemiților.

50Acestea alcătuiau clanurile urmașilor lui Neftali; au fost numărați patruzeci și cinci de mii patru sute de bărbați.

51Numărul fiilor lui Israel era de șase sute unu mii șapte sute treizeci.

52Domnul i‑a vorbit lui Moise, zicând: 53„Țara să le fie împărțită acestora ca moștenire, după numărul numelor. 54Astfel, celor care sunt mai mulți să le dai o moștenire mai mare, iar celor ce sunt mai puțini să le dai o moștenire mai mică. Fiecăruia să i se dea moștenirea, ținându‑se cont de numărul lor. 55Însă țara să fie împărțită prin sorți. O vor moșteni potrivit numelor semințiilor părinților lor. 56Moștenirea fiecăruia va fi împărțită între cei mulți și cei puțini, potrivit cu decizia sorților.“

57Iată leviții care au fost numărați potrivit clanurilor lor:

prin Gherșon, clanul gherșoniților;

prin Chehat, clanul chehatiților;

prin Merari, clanul merariților.

58Alte clanuri ale lui Levi:

clanul libniților,

clanul hebroniților,

clanul mahliților,

clanul mușiților,

clanul korahiților.

(Chehat a fost tatăl lui Amram. 59Soția lui Amram se numea Iochebed, o urmașă a lui Levi, născută în Egipt. Ea i‑a născut lui Amram pe Aaron, pe Moise și pe sora lor, Miriam. 60Lui Aaron i s‑au născut: Nadab și Abihu, Elazar și Itamar. 61Dar Nadab și Abihu au murit când au adus foc străin înaintea Domnului.)

62Toți bărbații leviți care au fost numărați de la vârsta de o lună în sus erau în număr de douăzeci și trei de mii. Ei nu au fost incluși în numărătoarea fiilor lui Israel, deoarece lor nu li s‑a dat moștenire printre fiii lui Israel.

63Aceștia sunt cei care au fost numărați de Moise și de preotul Elazar. Ei i‑au numărat pe fiii lui Israel în câmpiile Moabului, lângă Iordan, în fața Ierihonului. 64Niciunul dintre aceștia nu luaseră parte la numărătoarea fiilor lui Israel, făcută de Moise și de preotul Aaron în pustia Sinai. 65Căci Domnul le spusese: „Vor muri cu siguranță în pustie.“ Și niciunul dintre ei n‑a mai rămas, în afară de Caleb, fiul lui Iefune, și Iosua, fiul lui Nun.