Hesabu 26 – NEN & KLB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Hesabu 26:1-65

Kuhesabiwa Watu Mara Ya Pili

126:1 Hes 14:37; 25:8Baada ya hiyo tauni, Bwana akamwambia Mose na Eleazari mwana wa kuhani Aroni, 226:2 Kut 30:11-16; Hes 1:3; Kut 38:25“Hesabu jumuiya yote ya Kiisraeli kwa jamaa zao, wale wote wenye umri wa miaka ishirini na zaidi, ambao wanaweza kutumika katika jeshi la Israeli.” 326:3 Hes 33:48; Yos 13:22; Hes 22:1; Kum 4:46-49Hivyo Mose na kuhani Eleazari wakazungumza na watu kwenye nchi tambarare ya Moabu, ngʼambo ya Yordani kutokea Yeriko, wakasema, 426:4 Kut 6:14; 13:3“Hesabuni wanaume wenye umri wa miaka ishirini na zaidi, kama Bwana alivyomwagiza Mose.”

Hawa ndio Waisraeli waliotoka Misri:

526:5 Hes 1:20; Mwa 46:8, 9; 1Nya 5:3; Ufu 7:5Wazao wa Reubeni, mwana mzaliwa wa kwanza wa Israeli, walikuwa:

kutoka kwa Hanoki, ukoo wa Wahanoki;

kutoka kwa Palu, ukoo wa Wapalu;

626:6 1Nya 5:3; Mwa 46:9kutoka kwa Hesroni, ukoo wa Wahesroni;

kutoka kwa Karmi, ukoo wa Wakarmi.

7Hizi zilikuwa ndizo koo za Reubeni; wale waliohesabiwa walikuwa 43,730.

8Mwana wa Palu alikuwa Eliabu, 926:9 Hes 16:1; 1:16; 16:2; Isa 65:16; Kum 11:6; Hes 27:3; 16:1, 2nao wana wa Eliabu walikuwa Nemueli, Dathani na Abiramu. Hawa wawili Dathani na Abiramu ndio walikuwa maafisa wa jumuiya ambao walimwasi Mose na Aroni, na walikuwa miongoni mwa wafuasi wa Kora wakati walimwasi Bwana. 1026:10 Kut 15:12; Hes 16:35, 38; Kut 3:12; Ay 31:3; Za 145:20; Yer 29:22; 2Pet 2:6; Yud 7Ardhi ilifunua kinywa chake na kuwameza pamoja na Kora, ambaye wafuasi wake walikufa wakati moto ulipowateketeza wanaume 250. Nao walikuwa kama alama ya onyo. 1126:11 Kut 6:24; Hes 16:33; Kum 5:9; 24:16; 2Fal 14:6; 2Nya 25:4; Eze 18:20Pamoja na hayo, hao ukoo wa Kora hawakufa.

1226:12 Mwa 46:10; 1Nya 4:24; Kut 6:15Wazao wa Simeoni kwa koo zao walikuwa:

kutoka kwa Nemueli, ukoo wa Wanemueli;

kutoka kwa Yamini, ukoo wa Wayamini;

kutoka wa Yakini, ukoo wa Wayakini;

1326:13 Mwa 46:10kutoka kwa Zera, ukoo wa Wazera;

kutoka kwa Shauli, ukoo wa Washauli.

1426:14 Mwa 46:10; Hes 1:23Hizi ndizo koo za Simeoni; walikuwa 22,200.

1526:15 Mwa 46:16Wazao wa Gadi kwa koo zao walikuwa:

kutoka kwa Sifoni, ukoo wa Wasifoni;

kutoka kwa Hagi, ukoo wa Wahagi;

kutoka kwa Shuni, ukoo wa Washuni;

16kutoka kwa Ozni, ukoo wa Waozni;

kutoka kwa Eri, ukoo wa Waeri;

1726:17 Mwa 46:16kutoka kwa Arodi, ukoo wa Waarodi;

kutoka kwa Areli, ukoo wa Waareli.

1826:18 Mwa 30:11; Hes 1:25; Yos 13:24-28Hizi ndizo zilizokuwa koo za Gadi; wale waliohesabiwa walikuwa 40,500.

1926:19 Mwa 38:3; 38:4; 38:7; 46:12; 1Nya 2:3Eri na Onani walikuwa wana wa Yuda, lakini walifia huko Kanaani.

2026:20 Mwa 38:5; 38:29; Yos 7:17Wazao wa Yuda kwa koo zao walikuwa:

kutoka kwa Shela, ukoo wa Washela;

kutoka kwa Peresi, ukoo wa Waperesi;

kutoka kwa Zera, ukoo wa Wazera.

2126:21 Mwa 38:29; Rut 4:19; 1Fal 2:9Wazao wa Peresi walikuwa:

kutoka kwa Hesroni, ukoo wa Wahesroni;

kutoka kwa Hamuli, ukoo wa Wahamuli.

2226:22 Hes 1:27Hizi ndizo zilizokuwa koo za Yuda; wale waliohesabiwa walikuwa 76,500.

2326:23 Mwa 46:13; 49:14Wazao wa Isakari kwa koo zao walikuwa:

kutoka kwa Tola, ukoo wa Watola;

kutoka kwa Puva, ukoo wa Wapuva;

2426:24 Mwa 46:13kutoka kwa Yashubu, ukoo wa Wayashubu;

kutoka kwa Shimroni, ukoo wa Washimroni.

2526:25 Mwa 30:18Hizi ndizo zilizokuwa koo za Isakari; wale waliohesabiwa walikuwa 64,300.

2626:26 Hes 1:30; Mwa 46:14; 49:13Wazao wa Zabuloni kwa koo zao walikuwa:

kutoka kwa Seredi, ukoo wa Waseredi;

kutoka kwa Eloni, ukoo wa Waeloni;

kutoka kwa Yaleeli, ukoo wa Wayaleeli.

2726:27 Mwa 30:20Hizi ndizo zilizokuwa koo za Zabuloni, wale waliohesabiwa walikuwa 60,500.

2826:28 Hes 1:32; 36:1; Mwa 41:52; 46:20; 48:3Wazao wa Yosefu kwa koo zao kutoka kwa Manase na kwa Efraimu walikuwa:

2926:29 Hes 1:34; Mwa 50:23; Amu 11:1; Hes 32:39Wazao wa Manase:

kutoka kwa Makiri, ukoo wa Wamakiri (Makiri alikuwa baba wa Gileadi);

kutoka kwa Gileadi, ukoo wa Wagileadi.

3026:30 Hes 27:1; 36:1; 1Nya 7:14; Yos 17:2; Amu 6:11; 8:2Hawa ndio waliokuwa wazao wa Gileadi:

kutoka kwa Iezeri, ukoo wa Waiezeri;

kutoka kwa Heleki, ukoo wa Waheleki;

31kutoka kwa Asirieli, ukoo wa Waasirieli;

kutoka kwa Shekemu, ukoo wa Washekemu;

32kutoka kwa Shemida, ukoo wa Washemida;

kutoka kwa Heferi, ukoo wa Waheferi.

3326:33 Hes 27:1; 36:2; Yos 17:3; 1Nya 7:15; Hes 27:3; 36:11(Selofehadi mwana wa Heferi hakuzaa wana, bali alikuwa na watoto wa kike tu, ambao majina yao yalikuwa Mahla, Noa, Hogla, Milka na Tirsa.)

3426:34 Hes 1:35Hizi ndizo zilizokuwa koo za Manase; wale waliohesabiwa walikuwa 52,700.

3526:35 Hes 1:32; 1Nya 7:20Hawa walikuwa wazao wa Efraimu kwa koo zao:

kutoka kwa Shuthela, ukoo wa Washuthela;

kutoka kwa Bekeri, ukoo wa Wabekeri;

kutoka kwa Tahani, ukoo wa Watahani;

36Hawa ndio walikuwa wazao wa Shuthela:

kutoka kwa Erani, ukoo wa Waerani.

3726:37 Hes 1:33; Kum 33:13-17Hizi ndizo zilizokuwa koo za Efraimu; wale waliohesabiwa walikuwa 32,500.

Hawa ndio waliokuwa wazao wa Yosefu kwa koo zao.

3826:38 Mwa 46:21; Hes 1:36; 1Nya 8:40Wazao wa Benyamini kwa koo zao walikuwa:

kutoka kwa Bela, ukoo wa Wabela;

kutoka kwa Ashbeli, ukoo wa Waashbeli;

kutoka kwa Ahiramu, ukoo wa Waahiramu;

3926:39 Mwa 46:21; 1Nya 7:12kutoka kwa Shufamu, ukoo wa Washufamu;

kutoka kwa Hufamu, ukoo wa Wahufamu.

4026:40 Mwa 46:21; 1Nya 8:3Wazao wa Bela kutoka kwa Ardi na Naamani walikuwa:

kutoka kwa Ardi, ukoo wa Waardi;

kutoka kwa Naamani, ukoo wa Wanaamani.

4126:41 Hes 1:37Hizi ndizo zilizokuwa koo za Benyamini; wale waliohesabiwa walikuwa 45,600.

4226:42 Hes 1:38, 39; Amu 18:19; Mwa 46:23; 49:16; Kum 33:22Hawa ndio waliokuwa wazao wa Dani kwa koo zao:

kutoka kwa Shuhamu, ukoo wa Washuhamu.

Hizi ndizo zilizokuwa koo za Dani: 43Wote walikuwa koo za Washuhamu; wale waliohesabiwa walikuwa 64,400.

4426:44 Hes 1:40; 26:47; 1:41Wazao wa Asheri kwa koo zao walikuwa:

kutoka kwa Imna, ukoo wa Waimna;

kutoka kwa Ishvi, ukoo wa Waishvi;

kutoka kwa Beria, ukoo wa Waberia;

45kutoka kwa wazao wa Beria:

kutoka kwa Heberi, ukoo wa Waheberi;

kutoka kwa Malkieli, ukoo wa Wamalkieli.

46(Asheri alikuwa na binti aliyeitwa Sera.)

47Hizi ndizo zilizokuwa koo za Asheri; wale waliohesabiwa walikuwa 53,400.

4826:48 Mwa 30:8; 46:24; 1Nya 7:13Wazao wa Naftali kwa koo zao walikuwa:

kutoka kwa Yaseeli, ukoo wa Wayaseeli;

kutoka kwa Guni, ukoo wa Waguni;

4926:49 1Nya 7:13kutoka kwa Yeseri, ukoo wa Wayeseri;

kutoka kwa Shilemu, ukoo wa Washilemu.

5026:50 Hes 1:42, 43Hizi ndizo zilizokuwa koo za Naftali; wale waliohesabiwa walikuwa 45,400.

5126:51 Kut 12:37; Hes 1:46; 2:32Jumla ya hesabu ya wanaume wa Israeli ilikuwa 601,730.

52Bwana akamwambia Mose, 5326:53 Yos 11:23; 14:1; Eze 45:8“Watagawiwa nchi kama urithi kwa kulingana na hesabu ya majina. 5426:54 Hes 33:54; 35:8Kundi kubwa zaidi lipe urithi mkubwa zaidi, na kundi dogo zaidi lipewe urithi mdogo zaidi; kila kundi litapokea urithi wake kulingana na hesabu ya wale walioorodheshwa. 5526:55 Hes 34:13; Yos 11:23; 14:2Hakikisha kuwa nchi inagawanywa kwa kura. Kile kitakachorithiwa na kila kikundi kitakuwa kwa kulingana na majina ya kabila la babu yao. 56Kila urithi utagawanywa kwa kura miongoni mwa makundi makubwa na madogo.”

5726:57 Mwa 46:11; Kut 6:16; 1Nya 6:16Hawa walikuwa Walawi ambao walihesabiwa kwa koo zao:

kutoka kwa Gershoni, ukoo wa Wagershoni;

kutoka kwa Kohathi, ukoo wa Wakohathi;

kutoka kwa Merari, ukoo wa Wamerari.

5826:58 Kut 6:20Hizi pia zilikuwa koo za Walawi:

ukoo wa Walibni;

ukoo wa Wahebroni;

ukoo wa Wamahli;

ukoo wa Wamushi;

ukoo wa wana wa Kora.

(Kohathi alikuwa baba aliyemzaa Amramu; 5926:59 Kut 2:1; 6:20; 2:4; 15:20jina la mke wa Amramu ni Yokebedi, naye pia alikuwa mzao wa Lawi, ambaye alizaliwa kwa Walawi nchini Misri. Alimzalia Amramu: Aroni, Mose na dada yao Miriamu. 6026:60 Kut 6:23Aroni alikuwa baba yake Nadabu na Abihu, Eleazari na Ithamari. 6126:61 Law 10:1-2; Hes 3:4; 1Nya 24; 2Lakini Nadabu na Abihu walikufa wakati walitoa sadaka mbele za Bwana kwa moto usioruhusiwa.)

6226:62 Hes 3:39; 1:47; 18:23; 2:33; 18:20-24; 35:2-8; Kum 14:27-29Wanaume wote wa Walawi wa umri wa mwezi mmoja na zaidi walikuwa 23,000. Wao hawakuhesabiwa pamoja na Waisraeli wengine kwa sababu hawakupokea urithi miongoni mwao.

6326:63 Hes 1:19; 22:1Hawa ndio walioorodheshwa na Mose na kuhani Eleazari wakati waliwahesabu Waisraeli kwenye nchi tambarare ya Moabu, kando ya Yordani ngʼambo ya Yeriko. 6426:64 Hes 14:29; 1:44; 1:1; Kum 2:14, 15Hakuna hata mmoja wao aliyekuwa miongoni mwa wale waliohesabiwa na Mose na kuhani Aroni wakati waliwahesabu Waisraeli katika Jangwa la Sinai. 6526:65 Hes 14:18; 1Kor 10:5; Hes 13:6; 11:28; Za 90:3-8; Rum 11:22; Kum 32:49-50; Yos 14:10; Hes 14:18, 30; Ebr 3:17, 18; Yud 5Kwa maana Bwana alikuwa amewaambia hao Waisraeli hakika wangekufa huko jangwani, wala hakuna mmoja wao aliyeachwa, isipokuwa Kalebu mwana wa Yefune na Yoshua mwana wa Nuni.

Korean Living Bible

민수기 26:1-65

이스라엘의 두 번째 인구 조사

1그 재앙이 그친 후에 여호와께서 모세와 아론의 아들 제사장 엘르아 살에게 이렇게 말씀하셨다.

2“모든 이스라엘 백성 가운데서 전쟁에 나가 싸울 수 있는 20세 이상의 사람이 몇 명이나 되는지 각 집안별로 조사하여라.”

3-4그래서 모세와 제사장 엘르아살은 여리 고 맞은편에 있는 요단 강변의 모압 평야에서 이스라엘 지도자들에게 지시하여 20세 이상의 남자들을 조사하게 하였는데 이집트에서 나온 사람들 가운데 20세 이상의 남자들은 다음과 같다:

5-7야곱의 장남 르우벤의 자손들인 하녹, 발루, 헤스론, 갈미의 집안에서 20세 이상의 남자가 43,730명이었다.

8그리고 발루의 아들은 엘리압이며

9엘리압의 아들은 느무엘과 다단과 아비람이었다. 이 다단과 아비람은 백성의 지도자로서 고라와 음모하여 모세와 아론을 반역하고 여호와를 거역한 자들인데

10이들은 땅이 입을 벌려 고라의 일당을 삼켰을 때 그들과 함께 죽음을 당했다. 그리고 그때 불이 고라의 추종자 250명을 태워 죽여 이스라엘 백성에게 경고가 되었으나

11고라의 아들들만은 죽지 않았다.

12-14시므온의 자손들인 느무엘, 야민, 야 긴, 세라, 사울 집안에서는 20세 이상의 남자가 22,200명,

15-18갓의 자손들인 스본, 학기, 수니, 오스니, 에리, 아로디, 아렐리 집안에서는 40,500명,

19-22유다의 자손들인 셀라, 베레스, 세라, 헤스론, 하물의 집안에서는 76,500명이었다. 유다의 두 아들인 엘과 오난은 가나안 땅에서 죽었다.

23-25그리고 잇사갈의 자손들인 돌라, 부아, 야숩, 시므론 집안에서는 64,300명,

26-27스불론의 자손들인 세렛, 엘론, 얄르엘 집안에서는 60,500명이었다.

28요셉의 아들들은 므낫세와 에브라임이며

29므낫세의 자손들은 마길과 길르앗 집안 사람들이었다.

30-32그리고 길르앗 집안에서 이에셀, 헬렉, 아스리엘, 세겜, 스미다, 헤벨 가족이 생겼으며

33헤벨의 아들 슬로브핫에게는 아들이 없고 딸만 있었는데 그들의 이름은 말라, 노아, 호글라, 밀가, 디르사였다.

34이들은 다 므낫세의 자손들이며 이들 집안 가운데서 20세 이상의 남자는 모두 52,700명이었다.

35에브라임의 자손들은 수델라, 베겔, 다한 집안 사람들이었으며

36수델라 집안에서 에란 가족이 생겼다.

37이들은 다 에브라임 자손들이며 이들 집안 가운데서 20세 이상의 남자는 모두 32,500명이었다.

38-39베냐민 자손들은 벨라, 아스벨, 아히 람, 스부밤, 후밤 집안 사람들이었으며

40벨라 집안에서 아릇과 나아만 가족이 생겼다.

41이들은 베냐민의 자손들이며 이들 집안에서 20세 이상의 남자는 45,600명이었다.

42-43그리고 단의 자손인 수함 집안에서는 20세 이상의 남자가 64,400명이었다.

44아셀의 자손들은 임나, 이스위, 브리아 집안 사람들이며

45브리아 집안에서 헤벨과 말기엘 가족이 생겼다.

46또 아셀에게는 세라라는 딸이 있었다.

47이들은 아셀의 자손들이며 이들 집안에서 20세 이상의 남자는 53,400명이었다.

48-50그리고 납달리 자손들인 야셀, 구니, 예셀, 실렘 집안에서는 20세 이상의 남자가 45,400명이었다.

51이상은 이스라엘 백성 가운데 20세 이상의 남자들이며 그 전체 인원은 601,730명이었다.

52여호와께서 모세에게 말씀하셨다.

53“너는 그들의 인원수에 비례하여 땅을 나누어 주어라.

54인원수가 많은 지파에게는 많은 땅을 주고 인원수가 적은 지파에게는 땅을 적게 주어라.

55그러나 각 지파의 조상 이름을 따라서

56인원수가 많은 지파들은 넓은 땅을 차지할 지파들끼리 제비를 뽑고 인원수가 적은 지파들은 적은 땅을 차지할 지파들끼리 제비를 뽑게 하라.”

57레위 지파는 게르손, 고핫, 므라리 집안 사람들로 구성되었으며

58그들의 자손들은 립니, 헤브론, 마흘리, 무시, 고라 가족이었다. 그리고 고핫은 아므람을 낳았고

59아므람의 아내는 이집트에서 태어난 레위의 딸 요게벳이었으며 아므람과 요게벳 사이에서 아론과 모세와 그들의 누이 미리암이 태어났다.

60그리고 아론에게는 나답, 아비후, 엘르아살, 이다말 네 아들이 있었으며

61나답과 아비후는 여호와께서 명령하시지 않은 다른 불로 분향하다가 죽었다.

62이들 레위 사람들은 분배받을 땅이 없었기 때문에 별도로 인구 조사를 받았는데 그들 가운데 개월 이상의 남자는 모두 23,000명이었다.

63이상은 모세와 제사장 엘르아살이 여리고 맞은편에 있는 요단 강변의 모압 평야에서 실시한 인구 조사였다.

64그러나 여기에는 모세와 제사장 아론이 시나이 광야에서 인구 조사를 실시할 당시의 사람들은 하나도 포함되지 않았다.

65여호와께서는 그들이 광야에서 다 죽을 것이라고 말씀하셨으므로 여분네의 아들 갈렙과 눈의 아들 여호수아 외에는 한 사람도 살아 남은 자가 없었다.