Hesabu 24 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Hesabu 24:1-25

124:1 Hes 23:20, 23, 28Basi Balaamu alipoona imempendeza Bwana kubariki Israeli, hakuendelea tena kutafuta uchawi kama nyakati nyingine, bali aligeuza uso wake kuelekea nyikani. 224:2 Hes 11:25; 1Sam 19:20; 2Nya 15:1; Mt 7:21-22; 1Kor 12:8-10Balaamu alipotazama nje na kuona Israeli amepiga kambi kabila kwa kabila, Roho wa Mungu akawa juu yake, 324:3 Hes 23:7naye akatoa ujumbe wake:

“Ujumbe wa Balaamu mwana wa Beori,

ujumbe wake yeye ambaye jicho lake linaona vizuri;

424:4 Hes 22:9; Mwa 15:1; 1Sam 19:24; Eze 1:28; Dan 8:18; 10:15; 2Kor 12:2ujumbe wake yeye ambaye husikia maneno ya Mungu,

ambaye huona maono kutoka kwa Mwenyezi,24:4 Mwenyezi hapa ina maana ya Shaddai kwa Kiebrania (pia 24:16).

ambaye huanguka kifudifudi, na ambaye macho yake yamefunguka:

524:5 Yer 4:20; 30:18; Mal 2:12“Tazama jinsi yalivyo mazuri mahema yako, ee Yakobo,

maskani yako, ee Israeli!

624:6 Mwa 2:10; Za 1:3; 45:8; 104:16; Wim 4:14; Ay 29:19; Eze 31:5“Kama mabonde, yanaenea,

kama bustani kando ya mto,

kama miti ya udi iliyopandwa na Bwana,

kama mierezi kando ya maji.

724:7 Kut 17:8-16; Kum 28:1; 2Sam 5:12; 1Nya 14:2; Za 89:27; 145:11-13Maji yatatiririka kutoka ndoo zake;

mbegu yake itakuwa na maji tele.

“Mfalme wake atakuwa mkuu kuliko Mfalme Agagi;

ufalme wake utatukuka.

824:8 Kut 15:6; Yer 50:17; 2Sam 18:14; Za 45:5“Mungu alimleta kutoka Misri;

yeye ana nguvu kama nyati.

Anayararua mataifa yaliyo adui zake,

na kuvunja mifupa yao vipande vipande;

huwachoma kwa mishale yake.

924:9 Kut 23:23; Hes 23:24; Mwa 12:2, 3; 27:29; Za 122:6Hujikunyata na kuvizia kama simba,

kama simba jike; nani anayethubutu kumwamsha?

“Abarikiwe kila akubarikiye,

na alaaniwe kila akulaaniye!”

1024:10 Kut 4:14; Ay 27:23; 34:37; Mao 2:15; Eze 21:14; 22:13; 25:6; Hes 22:6; 23:7-11, 18-24; Kum 23:5Ndipo hasira ya Balaki ikawaka dhidi ya Balaamu. Akapiga mikono yake pamoja, akamwambia Balaamu, “Nilikuita uje kuwalaani adui zangu, lakini umewabariki mara hizi tatu. 1124:11 Hes 22:17Sasa ondoka upesi uende nyumbani! Mimi nilisema nitakuzawadia vizuri sana, lakini Bwana amekuzuia usizawadiwe.”

1224:12 Hes 22:18Balaamu akamwambia Balaki, “Je, hukumbuki jinsi nilivyowaambia wajumbe uliowatuma kwangu? Niliwaambia hivi, 1324:13 Hes 22:18, 20‘Hata ikiwa Balaki angenipa jumba lake la kifalme likiwa limejazwa fedha na dhahabu, nisingeweza kufanya kitu chochote kwa matakwa yangu, kikiwa kizuri au kibaya, kwenda kinyume na agizo la Bwana, nami imenipasa kusema tu kile Bwana atakachosema’? 1424:14 Mwa 49:1; Hes 31:8; Mik 6:5Sasa ninarudi kwa watu wangu. Lakini njoo, nikuonye kuhusu kile watu hawa watakachowatenda watu wako siku zijazo.”

Ujumbe Wa Nne Wa Balaamu

15Kisha Balaamu akatoa ujumbe wake:

“Ujumbe wa Balaamu mwana wa Beori,

ujumbe wake yeye ambaye jicho lake linaona vizuri;

1624:16 Hes 22:9; Mwa 14:18; Isa 14:14ujumbe wake yeye ambaye husikia maneno ya Mungu,

ambaye ana maarifa kutoka kwa Aliye Juu Sana,

huona maono kutoka Mwenyezi,

ambaye huanguka kifudifudi

na ambaye macho yake yamefunguka:

1724:17 Ufu 1:7; Mt 2:2; Mwa 49:10; 19:37; Hes 21:29; Kum 23:6; Isa 15:1–16:14; Yer 48:45“Namwona yeye, lakini si sasa;

namtazama yeye, lakini si karibu.

Nyota itatoka kwa Yakobo,

fimbo ya ufalme itainuka kutoka kwa Israeli.

Atawaponda Wamoabu vipaji vya nyuso

na mafuvu yote ya wana wa Shethi.

1824:18 2Sam 8:12; 1Nya 18:11; Za 60:8; Isa 11:14; Amo 9:12; Mwa 9:25; 14:6; Kum 1:44; Yos 12:7; 15:10; Amu 5:4; Oba 1:2Edomu itamilikiwa,

Seiri, adui wake, itamilikiwa,

lakini Israeli atakuwa na nguvu.

1924:19 Mwa 49:10; Mik 5:2Mtawala atakuja kutoka kwa Yakobo

na kuangamiza walionusurika katika mji.”

Ujumbe Wa Mwisho Wa Balaamu

2024:20 Mwa 14:7; Kut 17:14; Kum 25:19; 1Sam 15:20; 30:17-20; 2Sam 8:12; 1Nya 18:11Kisha Balaamu akawaona watu wa Amaleki, na kutoa ujumbe wake:

“Amaleki ilikuwa ya kwanza miongoni mwa mataifa,

lakini mwisho wake itaangamizwa milele.”

2124:21 Mwa 15:19; Za 37:27; Mit 1:33; Isa 32:18; Eze 34:27Kisha akawaona Wakeni, akatoa ujumbe wake:

“Makao yenu ni salama,

kiota chenu kiko kwenye mwamba.

2224:22 Mwa 10:22Hata hivyo ninyi Wakeni mtaangamizwa

Ashuru atakapowachukua mateka.”

23Ndipo akatoa ujumbe wake:

“Lo, ni nani atakayeweza kuishi wakati Mungu atakapofanya hili?

2424:24 Mwa 10:4, 21; Hes 22:5; Isa 23:1; Dan 11:30; Law 26:28; Kum 28:36; Mt 23:37Meli zitakuja kutoka pwani za Kitimu,

zitaitiisha Ashuru na Eberi,

lakini nao pia wataangamizwa.”

25Kisha Balaamu akainuka na kurudi nyumbani kwake, naye Balaki akashika njia yake.

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

民數記 24:1-25

巴蘭第三次預言

1巴蘭見耶和華樂意賜福給以色列人,就不再像先前兩次那樣去求兆頭,而是面向曠野, 2舉目四望,看見以色列人按支派紮營。上帝的靈降在他身上, 3他便吟詩預言說:

比珥之子巴蘭的預言,

是眼睛明亮者的話,

4他得聽上帝之言,

俯伏在地,

得見全能者的異象。

5雅各啊,

你的帳篷何等華美!

以色列啊,

你的居所何等佳美!

6像連綿的山谷,

河畔的園子;

又如耶和華栽種的沉香,

水邊的香柏樹。

7他們沐浴充沛的甘霖,

撒種於濕潤的沃土。

他們的君王高過亞甲

國度名震四方。

8上帝把他們帶出埃及

24·8 」有古卷作「他們」。的力量如野牛之角。

他們要吞滅敵國,

打碎敵人的骨頭,

用利箭射穿仇敵。

9他們蹲伏如雄獅,

躺臥如母獅,誰敢招惹?

祝福他們的人有福了!

咒詛他們的人有禍了!」

10巴勒聽了大怒,用力擊掌,對巴蘭說:「我請你來咒詛我的仇敵,你竟三次祝福他們。 11現在快回家去吧!我說過要給你重賞,但耶和華不讓你得到。」 12巴蘭說:「我不是對你派來的使臣說過嗎? 13就是你把滿屋的金銀都給我,我也不能違背耶和華的命令、憑自己的意思行事——無論好事壞事。我只能說耶和華讓我說的話。 14現在我要回本族去了。但我要告訴你日後以色列人會怎樣對待你的人民。」

巴蘭第四次預言

15巴蘭吟詩預言說:

比珥之子巴蘭的預言,

是眼睛明亮者的話,

16他得聽上帝之言,

明白至高者的旨意,

俯伏在地,

得見全能者的異象。

17我所見的尚未發生,

我目睹的關乎將來。

一顆星要從雅各家升起,

一位君王要從以色列興起。

他要打爛摩押的前額,

擊碎舍特人的頭顱。

18他必征服以東

佔領敵疆西珥

以色列必勇往直前。

19雅各的後裔必掌權,

消滅城中的餘民。」

巴蘭最後的預言

20巴蘭觀看亞瑪力人,並以詩歌預言說:

亞瑪力原是列國之首,

但他的結局卻是滅亡。」

21巴蘭又觀看基尼人,並以詩歌預言說:

「雖然你的居所堅固,

你的巢築在峭壁,

22但你必遭滅頂,

亞述擄去。」

23巴蘭又以詩歌預言說:

「唉!若非上帝許可,

誰能存活呢?

24船隻從基提駛來,

征服亞述希伯

但他也要滅亡。」

25說完,巴蘭動身返回家鄉,巴勒也回去了。