Hesabu 20 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Hesabu 20:1-29

Maji Kutoka Kwenye Mwamba

(Kutoka 17:1-7)

120:1 Hes 13:21; 13:26; 33:36; Kum 1:46; Amu 11:17; Za 29:8; Kut 15:20Katika mwezi wa kwanza jumuiya yote ya Kiisraeli ilifika kwenye Jangwa la Sini, nao wakakaa Kadeshi. Miriamu akafa huko na kuzikwa.

220:2 Kut 15:22; 17:1; Hes 16:19Mahali hapo hapakuwa na maji kwa ajili ya jumuiya hiyo, nao wakakusanyika ili kumpinga Mose na Aroni. 320:3 Mwa 13:7; Kut 17:2; 21:18; 5:21; Hes 14:2; 16:31-35Watu wakagombana na Mose, na kusema, “Laiti tungelikufa wakati ndugu zetu walipoanguka na kufa mbele za Bwana! 420:4 Hes 14:2; Kut 14:11; Hes 14:3; 16:13Kwa nini mmeileta jumuiya ya Bwana kwenye jangwa hili, ili tufe humu, sisi na mifugo yetu? 520:5 Hes 13:23; 16:14; Kut 17:1Kwa nini mmetupandisha kutoka Misri mpaka mahali hapa pa kutisha? Hapa hakuna nafaka wala tini, zabibu au makomamanga. Wala hapa hakuna maji ya kunywa!”

620:6 Kut 40:2; Hes 14:5; 16:19Mose na Aroni wakaondoka pale kwenye kusanyiko mpaka kwenye mlango wa Hema la Kukutania na kuanguka kifudifudi, nao utukufu wa Bwana ukawatokea. 7Bwana akamwambia Mose, 820:8 Kut 4:2; 10:12-13; 17:6; Isa 41:18; 43:20; Yer 31:9“Chukua ile fimbo, na wewe na ndugu yako Aroni mkusanye kusanyiko pamoja. Nena na ule mwamba mbele ya macho yao, nao utatoa maji yake. Utatoa maji kutoka huo mwamba kwa ajili ya jumuiya ili wao na mifugo yao waweze kunywa.”

920:9 Hes 17:2; 17:10Kwa hiyo Mose akaichukua hiyo fimbo kutoka pale ilipokuwa mbele za Bwana kama alivyomwagiza. 1020:10 Za 106:32-33Mose na Aroni wakakusanya kusanyiko pamoja mbele ya huo mwamba, naye Mose akawaambia, “Sikilizeni, enyi waasi. Je, ni lazima tuwatoleeni maji kutoka mwamba huu?” 1120:11 Kut 17:6; Isa 33:21Ndipo Mose akainua mkono wake na kuupiga mwamba mara mbili kwa fimbo yake. Maji yakabubujika, nayo jumuiya na mifugo yao wakanywa.

1220:12 Hes 27:14; Kum 32:51; Isa 5:16; 8:13; Kum 3:27Lakini Bwana akamwambia Mose na Aroni, “Kwa sababu hamkuniamini mimi kiasi cha kuniheshimu kama mtakatifu machoni pa Waisraeli, hamtaiingiza jumuiya hii katika nchi ninayowapa.”

1320:13 Kut 17:7; Law 10:3Haya yalikuwa maji ya Meriba,20:13 Meriba maana yake Kugombana. mahali pale ambapo Waisraeli waligombana na Bwana, naye akajionyesha mwenyewe huko kuwa mtakatifu katikati yao.

Edomu Wakatalia Israeli Kupita

1420:14 Hes 20:1, 16; Mwa 36:16; 25:30; 24:3; Kum 4:39; Yos 2:11; 9:9; Kut 18:8Mose akawatuma wajumbe kutoka Kadeshi kwenda kwa mfalme wa Edomu, akisema:

“Hili ndilo ndugu yako Israeli asemalo: Wewe unafahamu juu ya taabu zote ambazo zimetupata. 1520:15 Mwa 46:6; 15:13; Kut 1:14Baba zetu walishuka Misri, nasi tumeishi huko miaka mingi. Wamisri walitutesa sisi na baba zetu, 1620:16 Mwa 16:11; 21:17; Kut 2:23; 14:19; 12:42; Kum 26:8; Hes 33:37lakini tulipomlilia Bwana, alisikia kilio chetu na akamtuma malaika akatutoa Misri.

“Sasa tupo hapa Kadeshi, mji ulio mpakani mwa nchi yako. 1720:17 Hes 21:22; Kum 2:27; Amu 11:17Tafadhali turuhusu tupite katika nchi yako. Hatutapita katika shamba lolote, wala shamba la mizabibu, au kunywa maji kutoka kwenye kisima chochote. Tutasafiri kufuata njia kuu ya mfalme, na hatutageuka kulia wala kushoto mpaka tuwe tumeshapita nchi yako.”

1820:18 Hes 21:23Lakini mfalme wa Edomu akajibu:

“Hamtapita hapa; kama mkijaribu kupita, tutatoka na kuwashambulia kwa upanga.”

1920:19 Kut 2:23; Kum 2:6, 28Waisraeli wakajibu:

“Sisi tutafuata njia kuu; tena ikiwa sisi au mifugo yetu tutakunywa tone la maji yenu, tutalilipia. Sisi tunataka tu kupita kwa miguu, wala si kitu kingine chochote.”

20Watu wa Edomu wakajibu tena:

“Hamwezi kupita hapa.”

Ndipo watu wa Edomu wakatoka dhidi ya Waisraeli, jeshi kubwa lenye nguvu. 2120:21 Hes 21:23; 21:4; Kum 2:8; Amu 11:18Kwa kuwa Waedomu waliwakatalia Waisraeli kupita katika nchi yao, Israeli wakageuka, wakawaacha.

Kifo Cha Aroni

2220:22 Kum 1:46; Hes 33:37; 34:7; Kum 32:50Jumuiya yote ya Kiisraeli ikaondoka kutoka Kadeshi, wakafika kwenye Mlima Hori. 23Kwenye Mlima Hori, karibu na mpaka wa Edomu, Bwana akamwambia Mose na Aroni, 2420:24 Mwa 25; 8; Kut 17:7“Aroni atakusanywa pamoja na watu wake. Hataingia katika nchi ninayowapa Waisraeli, kwa sababu ninyi wawili mliasi dhidi ya agizo langu kwenye maji ya Meriba. 2520:25 Hes 33:38Watwae Aroni na Eleazari mwanawe, na uwapandishe juu katika Mlima wa Hori. 2620:26 Kut 28:1-4; 40:13; Law 16:4; Hes 27:13; 31:2Mvue Aroni mavazi yake, na umvike Eleazari mwanawe, kwa maana Aroni atakusanywa pamoja na watu wake; atakufa huko.”

2720:27 Hes 33:38Mose akafanya kama Bwana alivyomwagiza: Wakapanda Mlima Hori mbele ya macho ya jumuiya yote ya Kiisraeli. 2820:28 Kut 29:29; Hes 33:38; Kum 10:6; 32:50; Mwa 27:41; Law 10:6; Kum 34:8Mose akamvua Aroni mavazi yake na kumvika mwanawe Eleazari mavazi hayo. Naye Aroni akafia pale juu ya mlima. Kisha Mose na Eleazari wakateremka kutoka mlimani. 29Jumuiya yote ilipofahamu kwamba Aroni amekufa, jamaa yote ya Kiisraeli wakamwomboleza kwa siku thelathini.

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

民數記 20:1-29

磐石出水

1一月,以色列全體會眾抵達曠野,在加低斯安營。米利暗離世,葬在那裡。 2會眾沒有水喝,就聚集起來反對摩西亞倫3他們埋怨說:「還不如當初跟我們的弟兄一起死在耶和華面前! 4你們為什麼領耶和華的會眾到這曠野來,要叫我們和牲畜都死在這裡嗎? 5你們為什麼把我們領出埃及,帶到這不毛之地?這裡沒有五穀、無花果樹、葡萄樹和石榴樹,甚至沒有水喝。」 6摩西亞倫離開會眾到會幕門口,俯伏在地。耶和華的榮光向他們顯現。 7耶和華對摩西說: 8「你拿著杖和你哥哥亞倫招聚會眾,當著他們的面吩咐磐石流出水來,水就會從磐石流出,供會眾和牲畜喝。」 9摩西遵命而行,從耶和華面前取了杖, 10然後和亞倫把會眾招聚到磐石前,說:「你們這些叛逆之徒聽著,非要我們叫磐石給你們流出水來嗎?」 11接著,摩西舉起手中的杖擊打磐石兩下,水便噴湧而出,會眾和牲畜都喝了。

12耶和華對摩西亞倫說:「你們對我沒有足夠的信心,沒有當著以色列人的面尊我為聖,所以你們不得帶領會眾進入我將要賜給他們的土地。」 13這地方叫米利巴泉,因為以色列人在那裡埋怨耶和華,耶和華就向他們彰顯了祂的聖潔。

以東王不借路

14摩西加低斯派使者去見以東王,說:「你的弟兄以色列人說,你知道我們遭遇的種種困難。 15我們祖先到埃及寄居多年,我們世代受埃及人虐待。 16但我們呼求耶和華,祂就垂聽了我們的聲音,差遣天使把我們領出埃及。現在我們來到你邊境的加低斯城, 17求你容我們借道貴國。我們不會踏入田地和葡萄園,也不會喝井裡的水,只走大路,不會偏離,直到走出貴國。」 18以東王卻說:「你們不可從我這裡經過,否則我必兵戎相見。」 19以色列人說:「我們只走大路,倘若我們和牲畜喝了你的水,我們會付錢。我們別無他求,只求步行穿過貴國。」 20以東王仍然不准,還率領大軍嚴陣以待。 21由於無法從以東穿過,以色列人只好繞道。

亞倫離世

22以色列全體會眾從加低斯出發,來到何珥山。 23耶和華在位於以東邊界的何珥山對摩西亞倫說: 24亞倫要去他祖先那裡了,他不能進入我賜給以色列人的土地,因為你們在米利巴泉違背了我的命令。 25摩西啊,你要帶亞倫和他兒子以利亞撒何珥山, 26亞倫的聖衣脫下來給他兒子以利亞撒穿上,因為亞倫將死在那裡。」 27摩西遵命而行。他們三人就當著全體會眾的面上了何珥山。 28摩西亞倫的聖衣脫下,給以利亞撒穿上。隨後亞倫在山頂離世。摩西以利亞撒便下了山。 29以色列全體會眾得知亞倫離世,就為他哀悼了三十天。