Hesabu 19 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Hesabu 19:1-22

Maji Ya Utakaso

1Bwana akamwambia Mose na Aroni: 219:2 Mwa 15:9; Ebr 9:13; Law 22:19-25; Kum 21:3; 1Sam 6:7“Hivi ndivyo sheria ambayo Bwana ameagiza itakavyo: Waambie Waisraeli wakuletee mtamba mwekundu asiye na dosari wala waa, na ambaye hajapata kufungwa nira. 319:3 Hes 3:4; Kut 29:14Mpeni kuhani Eleazari huyo mtamba; naye atatolewa nje ya kambi na kuchinjwa mbele yake huyo kuhani. 419:4 Law 4:17Kisha kuhani Eleazari atachukua baadhi ya damu yake kwenye kidole chake na kuinyunyiza mara saba kuelekea upande wa mbele ya Hema la Kukutania. 519:5 Kut 29:14Wakati angali akitazama, mtamba huyo atateketezwa: ngozi yake, nyama yake, damu na sehemu zake za ndani. 619:6 Za 51:7; Law 14:4Kuhani atachukua kuni za mti wa mwerezi, hisopo na sufu nyekundu, na kuvitupa kwenye huyo mtamba anayeungua. 719:7 Law 11:25; 14:8Baada ya hayo, kuhani lazima afue nguo zake, na aoge mwili wake kwa maji. Kisha anaweza kurudi kambini, lakini atakuwa najisi kwa kawaida ya ibada mpaka jioni. 8Mtu amchomaye huyo mtamba lazima naye pia afue nguo zake na kuoga kwa maji, naye pia atakuwa najisi mpaka jioni.

919:9 Ebr 9:13; Kut 29:31; Law 4:12; Hes 8:1; Mwa 35:2“Mtu ambaye ni safi atakusanya majivu ya mtamba huyo na kuyaweka mahali ambapo ni safi nje ya kambi kwa taratibu za kiibada. Yatahifadhiwa na jumuiya ya Kiisraeli kwa matumizi katika maji ya utakaso; ni kwa ajili ya kutakasa kutoka dhambini. 1019:10 Law 15:10; 14:46; 3:17; 22:18Mtu akusanyaye majivu ya huyo mtamba ni lazima pia afue nguo zake, kadhalika naye pia atakuwa najisi hadi jioni. Hili litakuwa agizo la kudumu kwa Waisraeli na kwa wageni wanaoishi miongoni mwao.

1119:11 Law 21:1; 8:33; Hes 31:19“Mtu yeyote agusaye maiti ya mtu yeyote atakuwa najisi kwa siku saba. 1219:12 Hes 31:19; 2Nya 26:21Ni lazima ajitakase mwenyewe kwa maji katika siku ya tatu na siku ya saba, ndipo atakuwa safi. Lakini kama hatajitakasa mwenyewe katika siku ya tatu na ya saba, hatakuwa safi. 1319:13 Law 21:11; 15:31; 2Nya 36:14; Za 79:1; Law 22:3; 7:20; Hag 2:13Mtu yeyote agusaye maiti ya mtu yeyote na kushindwa kujitakasa mwenyewe hunajisi Maskani ya Bwana. Mtu huyo ni lazima akatiliwe mbali na Israeli. Kwa sababu hajanyunyiziwa maji ya utakaso, yeye ni najisi; unajisi wake unabaki juu yake.

14“Hii ndiyo sheria itumikayo wakati mtu amekufa ndani ya hema: Yeyote aingiaye ndani ya hema hilo na yeyote aliye ndani yake watakuwa najisi kwa muda wa siku saba, 1519:15 Law 6:28nacho kila chombo kisicho na kifuniko juu yake kitakuwa najisi.

1619:16 Hes 31:19; 1Fal 13:2; 2Fal 23:14; Eze 6:5; 2Fal 23:6; Mt 23:27; Law 5:3“Mtu yeyote aliyeko nje mahali pa wazi agusaye mtu aliyeuawa kwa upanga au mtu aliyekufa kwa kifo cha kawaida, au mtu yeyote agusaye mfupa wa mtu aliyekufa au kaburi, atakuwa najisi kwa siku saba.

1719:17 Hes 8:7“Kwa mtu aliye najisi, weka majivu ya sadaka ya utakaso wa dhambi ndani ya chombo, umimine maji safi juu yao. 1819:18 Kut 12:22; Law 4:17Kisha mtu aliye safi kwa kawaida za kiibada atachukua hisopo, achovye ndani ya maji, na kunyunyizia hema na vifaa vyote pamoja na watu ambao walikuwamo. Pia ni lazima amnyunyizie mtu yeyote ambaye amegusa mfupa wa mtu aliyekufa, au kaburi, au mtu ambaye ameuawa, au mtu ambaye amekufa kifo cha kawaida. 1919:19 Law 16:14-15; Hes 31:19; Eze 36:25; Ebr 10:22; Mwa 35:2Mtu ambaye ni safi ndiye atakayemnyunyizia yeyote ambaye ni najisi siku ya tatu na siku ya saba, na katika siku ya saba atamtakasa mtu huyo. Mtu ambaye ametakaswa lazima afue nguo zake na kuoga kwa maji, na jioni ile atakuwa safi. 2019:20 Za 14:7; Law 15:31; 14:8Lakini ikiwa mtu ambaye ni najisi hakujitakasa mwenyewe, ni lazima akatiliwe mbali na jumuiya, kwa sababu ameinajisi Maskani ya Bwana. Maji ya utakaso hayajanyunyizwa juu yake, naye ni najisi. 2119:21 Kut 27:21Hii ni sheria ya kudumu kwao.

“Mtu yeyote ambaye ananyunyiza yale maji ya utakaso lazima pia afue nguo zake, na yeyote ambaye hugusa maji ya utakaso atakuwa najisi mpaka jioni. 2219:22 Law 5:2; 15:4-12Kitu chochote anachogusa mtu aliye najisi kitakuwa najisi, na yeyote akigusaye huwa najisi mpaka jioni.”

New International Reader’s Version

Numbers 19:1-22

The Special Water That Makes People “Clean”

1The Lord spoke to Moses and Aaron. He said, 2“Here is what the law I have commanded requires. Tell the Israelites to bring you a young red cow. It must not have any flaws at all. It must never have pulled a load. 3Give it to Eleazar the priest. It must be taken outside the camp and killed in front of him. 4Then Eleazar the priest must put some of its blood on his finger. He must sprinkle the blood toward the front of the tent of meeting. He must do it seven times. 5While he watches, the young cow must be burned. Its hide, meat, blood and guts must be burned. 6The priest must get some cedar wood, branches of a hyssop plant, and bright red wool. He must throw them on the young cow as it burns. 7After that, the priest must wash his clothes. He must also take a bath. Then he can come into the camp. But he will be ‘unclean’ until evening. 8The man who burns the young cow must wash his clothes. He must also take a bath. He too will be ‘unclean’ until evening.

9“A man who is ‘clean’ will gather up the ashes of the young cow. He must put them in a place that is ‘clean.’ The place must be outside the camp. The ashes must be kept by the community of Israel. They will be added to the special water. The water will be used to make people pure from their sin. 10The man who gathers up the ashes of the young cow must wash his clothes. He too will be ‘unclean’ until evening. This law is for the Israelites. It is also for the outsiders living among them. The law will last for all time to come.

11“Anyone who touches a dead person’s body will be ‘unclean’ for seven days. 12They must make themselves pure and ‘clean’ with the special water. They must do it on the third day. They must also do it on the seventh day. Then they will be ‘clean.’ But suppose they do not make themselves pure and ‘clean’ on the third and seventh days. Then they will not be ‘clean.’ 13Anyone who touches a dead person’s body and does not make themselves pure and ‘clean’ makes my holy tent ‘unclean.’ They must be separated from Israel. The special water has not been sprinkled on them. So they are ‘unclean.’ And they remain ‘unclean.’

14“Here is the law that applies when a person dies in a tent. Anyone who enters the tent will be ‘unclean’ for seven days. Anyone in the tent will also be ‘unclean’ for seven days. 15And anything in it that is open and has no lid will be ‘unclean.’

16“Suppose someone is out in the country. And suppose they touch someone who has been killed by a sword. Or they touch someone who has died a natural death. Or they touch a human bone or a grave. Then anyone who touches any of those things will be ‘unclean’ for seven days.

17“Here is what I want you to do for someone who is ‘unclean.’ Put some ashes from the burned young cow into a jar. Pour fresh water on the ashes. 18Then a man who is ‘clean’ must dip branches of a hyssop plant in the water. He must sprinkle the tent with it. Everything that belongs to the tent must be sprinkled with it. The people in the tent must also be sprinkled. Anyone who has touched a human bone or a grave must be sprinkled. So must anyone who has touched someone who has been killed. And so must anyone who has touched someone who has died a natural death. 19The man who is ‘clean’ must sprinkle those who are ‘unclean.’ That must be done on the third and seventh days. On the seventh day those who are ‘unclean’ must be made pure and ‘clean.’ Those being made ‘clean’ must wash their clothes. They must take a bath. Then that evening they will be ‘clean.’ 20But what if those who are ‘unclean’ do not make themselves pure and ‘clean?’ Then they must be separated from the community. They have made my holy tent ‘unclean.’ The special water has not been sprinkled on them. They are ‘unclean.’ 21This law will apply to all those people for all time to come.

“The man who sprinkles the special water must also wash his clothes. Anyone who touches the water will be ‘unclean’ until evening. 22Anything that an ‘unclean’ person touches becomes ‘unclean.’ And anyone who touches it becomes ‘unclean’ until evening.”