Hesabu 17 – NEN & NUB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Hesabu 17:1-13

Kuchipuka Kwa Fimbo Ya Aroni

1Bwana akamwambia Mose, 217:2 Mwa 32:10; Kut 4:2; Hes 1:4“Sema na Waisraeli, na ujipatie fimbo kumi na mbili kutoka kwao, moja kutoka kwa kila mmoja wa viongozi wa kabila za baba zao. Andika jina la kila mtu kwenye fimbo yake. 317:3 Hes 1:3Kwenye fimbo ya Lawi andika jina la Aroni, kwa maana ni lazima iwepo fimbo moja kwa kila kiongozi kwa ajili ya kila kabila la baba zao. 417:4 Kut 1:3; 16:34; 25:22Ziweke hizo fimbo ndani ya Hema la Kukutania mbele ya Sanduku la Ushuhuda, mahali nikutanapo nawe. 517:5 Hes 16:5; Kut 16:7Fimbo ya mtu nitakayemchagua itachipuka, nami mwenyewe nitayakomesha haya manungʼuniko ya mara kwa mara ya Waisraeli dhidi yako.”

6Hivyo Mose akasema na Waisraeli, nao viongozi wao wakampa fimbo kumi na mbili, fimbo moja kwa ajili ya kila kabila la baba zao, nayo fimbo ya Aroni ikiwa miongoni mwa hizo. 717:7 Kut 38:21; Mdo 7:44Mose akaziweka hizo fimbo mbele za Bwana ndani ya Hema la Ushuhuda.

817:8 Hes 1:50; Eze 17:24; Ebr 9:4Siku iliyofuata Mose aliingia kwenye Hema la Ushuhuda akaona ile fimbo ya Aroni ambayo iliwakilisha jamaa ya Lawi haikuwa tu imechipuka, bali pia ilikuwa imetoa machipukizi, kuchanua maua na kuzaa malozi. 9Ndipo Mose akaleta zile fimbo zote kwa Waisraeli wote kutoka mbele za Bwana. Wakaziangalia, na kila mtu akaichukua fimbo yake mwenyewe.

1017:10 Kut 23:21; Za 66:7; 68:18; Mit 24:21Bwana akamwambia Mose, “Rudisha fimbo ya Aroni mbele ya Sanduku la Ushuhuda, ili ihifadhiwe kama alama kwa waasi. Hili litakomesha manungʼuniko yao dhidi yangu, ili kwamba wasife.” 11Mose akafanya kama Bwana alivyomwamuru.

1217:12 Amu 13:22; Isa 6:5; 15:1Waisraeli wakamwambia Mose, “Tutakufa! Tumepotea, sote tumepotea! 1317:13 Hes 1:51Yeyote akaribiaye Maskani ya Bwana atakufa. Je, sisi sote tutakufa?”

Swedish Contemporary Bible

4 Moseboken 17:1-13

Arons stav grönskar

1Herren sa till Mose: 2”Säg åt israeliterna att var och en av stamöverhuvudena ska ge dig en stav, en stav för varje stam, tolv stycken. Skriv namnet på var och en av dess ledare på dessa stavar. 3Skriv Arons namn på Levi stams stav för det ska finnas en stav för varje familjeöverhuvud. 4Lägg sedan alla stavarna i uppenbarelsetältet framför förbundstecknet där jag brukar möta dig framför arken. 5Hans stav som jag har utvalt kommer att grönska. Då slipper jag höra israeliternas ständiga knotande mot er.”

6Mose talade till israeliterna och var och en av de tolv stamledarna, Aron inräknad, bar fram en stav till honom. 7Han lade dem framför Herren i förbundstecknets tält. 8När han kom tillbaka nästa dag, grönskade Arons stav som representerade Levi stam och inte bara grönskade, utan hade knoppar och blommor och bar mogna mandlar. 9Mose bar ut stavarna som låg inför Herren till israeliterna och de såg på dem. Sedan tog var och en sin stav.

10Herren sa till Mose: ”Lägg tillbaka Arons stav vid sidan av arken! Där ska den alltid finnas som en varning för de upproriska. Så gör du slut på deras knotande mot mig och de slipper dö.” 11Mose gjorde i allt som Herren hade sagt.

12Israeliterna sa till Mose: ”Vi dör ju! Vi förgås allihop! 13Var och en som kommer i närheten av Herrens boning dör. Är det verkligen meningen att vi ska gå under allesammans?”