Hesabu 17 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Hesabu 17:1-13

Kuchipuka Kwa Fimbo Ya Aroni

1Bwana akamwambia Mose, 217:2 Mwa 32:10; Kut 4:2; Hes 1:4“Sema na Waisraeli, na ujipatie fimbo kumi na mbili kutoka kwao, moja kutoka kwa kila mmoja wa viongozi wa kabila za baba zao. Andika jina la kila mtu kwenye fimbo yake. 317:3 Hes 1:3Kwenye fimbo ya Lawi andika jina la Aroni, kwa maana ni lazima iwepo fimbo moja kwa kila kiongozi kwa ajili ya kila kabila la baba zao. 417:4 Kut 1:3; 16:34; 25:22Ziweke hizo fimbo ndani ya Hema la Kukutania mbele ya Sanduku la Ushuhuda, mahali nikutanapo nawe. 517:5 Hes 16:5; Kut 16:7Fimbo ya mtu nitakayemchagua itachipuka, nami mwenyewe nitayakomesha haya manungʼuniko ya mara kwa mara ya Waisraeli dhidi yako.”

6Hivyo Mose akasema na Waisraeli, nao viongozi wao wakampa fimbo kumi na mbili, fimbo moja kwa ajili ya kila kabila la baba zao, nayo fimbo ya Aroni ikiwa miongoni mwa hizo. 717:7 Kut 38:21; Mdo 7:44Mose akaziweka hizo fimbo mbele za Bwana ndani ya Hema la Ushuhuda.

817:8 Hes 1:50; Eze 17:24; Ebr 9:4Siku iliyofuata Mose aliingia kwenye Hema la Ushuhuda akaona ile fimbo ya Aroni ambayo iliwakilisha jamaa ya Lawi haikuwa tu imechipuka, bali pia ilikuwa imetoa machipukizi, kuchanua maua na kuzaa malozi. 9Ndipo Mose akaleta zile fimbo zote kwa Waisraeli wote kutoka mbele za Bwana. Wakaziangalia, na kila mtu akaichukua fimbo yake mwenyewe.

1017:10 Kut 23:21; Za 66:7; 68:18; Mit 24:21Bwana akamwambia Mose, “Rudisha fimbo ya Aroni mbele ya Sanduku la Ushuhuda, ili ihifadhiwe kama alama kwa waasi. Hili litakomesha manungʼuniko yao dhidi yangu, ili kwamba wasife.” 11Mose akafanya kama Bwana alivyomwamuru.

1217:12 Amu 13:22; Isa 6:5; 15:1Waisraeli wakamwambia Mose, “Tutakufa! Tumepotea, sote tumepotea! 1317:13 Hes 1:51Yeyote akaribiaye Maskani ya Bwana atakufa. Je, sisi sote tutakufa?”

King James Version

Numbers 17:1-13

1And the LORD spake unto Moses, saying, 2Speak unto the children of Israel, and take of every one of them a rod according to the house of their fathers, of all their princes according to the house of their fathers twelve rods: write thou every man’s name upon his rod. 3And thou shalt write Aaron’s name upon the rod of Levi: for one rod shall be for the head of the house of their fathers. 4And thou shalt lay them up in the tabernacle of the congregation before the testimony, where I will meet with you. 5And it shall come to pass, that the man’s rod, whom I shall choose, shall blossom: and I will make to cease from me the murmurings of the children of Israel, whereby they murmur against you.

6¶ And Moses spake unto the children of Israel, and every one of their princes gave him a rod apiece, for each prince one, according to their fathers’ houses, even twelve rods: and the rod of Aaron was among their rods.17.6 a rod…: Heb. a rod for one prince, a rod for one prince 7And Moses laid up the rods before the LORD in the tabernacle of witness.

8And it came to pass, that on the morrow Moses went into the tabernacle of witness; and, behold, the rod of Aaron for the house of Levi was budded, and brought forth buds, and bloomed blossoms, and yielded almonds. 9And Moses brought out all the rods from before the LORD unto all the children of Israel: and they looked, and took every man his rod.

10¶ And the LORD said unto Moses, Bring Aaron’s rod again before the testimony, to be kept for a token against the rebels; and thou shalt quite take away their murmurings from me, that they die not.17.10 rebels: Heb. children of rebellion 11And Moses did so: as the LORD commanded him, so did he. 12And the children of Israel spake unto Moses, saying, Behold, we die, we perish, we all perish. 13Whosoever cometh any thing near unto the tabernacle of the LORD shall die: shall we be consumed with dying?