Hesabu 15 – NEN & OL

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Hesabu 15:1-41

Sadaka Za Nyongeza

1Bwana akamwambia Mose, 215:2 Law 23:10“Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Baada ya ninyi kuingia katika nchi ninayowapa kama nyumbani, 315:3 Law 1:2, 9; 23:1-44; Hes 28:13; 7:16; Ezr 1:4; Kum 16:10; Mwa 8:21; Kut 29:18; 2Kor 2:15; Efe 5:2nanyi mkitoa sadaka za kuteketezwa kwa moto, kutoka makundi ya ngʼombe au kondoo, kama harufu nzuri inayompendeza Bwana, ikiwa ni sadaka za kuteketezwa au dhabihu, kwa ajili ya nadhiri maalum ama sadaka ya hiari au sadaka ya sikukuu zenu, 415:4 Law 6:14; Kut 16:36; Law 14:10; Kut 29:40; Isa 66:20ndipo yeye aletaye sadaka yake ataiweka mbele za Bwana sadaka ya nafaka, sehemu ya kumi ya efa15:4 Sehemu ya kumi ya efa ni sawa na kilo moja. ya unga laini uliochanganywa na robo ya hini15:4 Robo ya hini ni sawa na lita moja. ya mafuta. 515:5 Law 3:7; 10:9; Mwa 35:14; Hes 28:7, 14; Gal 3:28; Kol 3:11; Law 24:22Pamoja na kila mwana-kondoo kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa au dhabihu, andaa robo ya hini ya divai kwa sadaka ya kinywaji.

615:6 Law 5:15; 23:13; Hes 28:12; 29:14; Eze 46:14“ ‘Pamoja na kondoo dume andaa sadaka ya nafaka ya sehemu mbili za kumi za efa15:6 Sehemu mbili za kumi za efa ni sawa na kilo 2. za unga laini uliochanganywa na theluthi moja15:6 Theluthi moja ya hini ni sawa na lita moja na nusu. ya hini ya mafuta, 715:7 Law 1:9; 23:13; Hes 28:14; 29:18na theluthi moja ya hini ya divai kama sadaka ya kinywaji. Vitoe kama harufu nzuri inayompendeza Bwana.

815:8 Kut 12:5; Law 1:5; 22:18; 3:6“ ‘Unapoandaa fahali mchanga kama sadaka ya kuteketezwa au dhabihu, kwa ajili ya nadhiri maalum au sadaka ya amani kwa Bwana, 915:9 Law 2:1; 14:10leta pamoja na huyo fahali sadaka ya nafaka ya unga laini sehemu tatu za kumi za efa15:9 Sehemu tatu za kumi za efa ni sawa na kilo 3. uliochanganywa na nusu ya hini15:9 Nusu ya hini ni sawa na lita 2. ya mafuta. 1015:10 Hes 28:14; Law 23:13; 1:9; Amu 2:17; Yer 3:2; 7:24; Hos 4:12; Eze 20:16Pia utaleta nusu ya hini ya divai kama sadaka ya kinywaji. Itakuwa sadaka iliyoteketezwa kwa moto, harufu nzuri inayompendeza Bwana. 11Kila fahali au kondoo dume, kila mwana-kondoo au mbuzi mchanga, atatayarishwa kwa njia hii. 1215:12 Ezr 7:17Fanyeni hivi kwa ajili ya kila mmoja, kwa kadiri ya wingi wa mtakavyoandaa.

1315:13 Law 16:29; 1:9“ ‘Kila mmoja ambaye ni mzawa ni lazima afanye vitu hivi kwa njia hii hapo aletapo sadaka ya kuteketezwa kwa moto kama harufu nzuri inayompendeza Bwana. 1415:14 Law 3:17; 22:18; Hes 10:8; Kut 12:19, 43; 22:21Kwa vizazi vijavyo, wakati wowote mgeni au mtu mwingine yeyote anayeishi miongoni mwenu aletapo sadaka ya kuteketezwa kuwa harufu nzuri ya kumpendeza Bwana, ni lazima afanye sawasawa kabisa na jinsi mnavyofanya ninyi. 1515:15 Hes 9:14Jumuiya itakuwa na sheria hizo hizo kwenu na kwa mgeni aishiye miongoni mwenu; hii ni amri ya kudumu kwa vizazi vijavyo. Ninyi na mgeni mtakuwa sawa mbele za Bwana: 1615:16 Kut 12:49; Law 22:18; Hes 9:14Sheria hizo hizo na masharti hayo hayo hayo, yatawahusu ninyi na mgeni aishiye miongoni mwenu.’ ”

17Bwana akamwambia Mose, 1815:18 Law 23:10“Sema na Waisraeli na uwaambie: ‘Mtakapoingia katika nchi ninayowapeleka 1915:19 Yos 5:11; 12; Hes 18:8nanyi mkala chakula cha nchi hiyo, toeni sehemu ya chakula hicho kama sadaka kwa Bwana. 2015:20 Law 23:14; Hes 18:2; Mwa 50:10; Kut 23:19; Neh 10:37; Mit 3:9; Law 2:14Toeni andazi kutoka kwa malimbuko ya chakula chenu kitokacho katika ardhi, na mkitoe kama sadaka kutoka sakafu ya kupuria nafaka. 2115:21 Law 23:14; Eze 44:30; Rum 11:16Kwa vizazi vyote vijavyo hamna budi kutoa sadaka hii kwa Bwana kutoka kwa malimbuko ya unga wenu.

Sadaka Kwa Ajili Ya Dhambi Isiyo Ya Makusudi

2215:22 Law 4:2; 1Yn 2:1“ ‘Basi kama pasipo kukusudia umeshindwa kushika mojawapo katika amri hizi ambazo Bwana alimpa Mose, 23amri yoyote ya Bwana kwenu kupitia Mose, tangu siku ile Bwana alipowapa na inaendelea hadi vizazi vyote vijavyo; 2415:24 Law 5:15; 4:14; 23:13; 4:3; Hes 6:15; Law 4:13, 23; Hes 28:15; Ezr 6:17; 8:35ikiwa hili limefanyika pasipo kukusudia bila jumuiya kuwa na habari nalo, basi jumuiya yote itatoa fahali mchanga kuwa sadaka ya kuteketezwa ikiwa harufu nzuri inayompendeza Bwana, pamoja na sadaka ya nafaka na ya kinywaji zilizoamriwa kwayo, na mbuzi dume kwa ajili ya sadaka ya dhambi. 2515:25 Law 4:3, 20; Rum 3:25; Ebr 2:17; Rum 5; 11; Dan 9:24; Ebr 10:10-12Kuhani atafanya upatanisho kwa ajili ya jumuiya yote ya Kiisraeli, nao watasamehewa, kwa kuwa haikuwa makusudi nao wamemletea Bwana sadaka iliyoteketezwa kwa moto na sadaka ya dhambi kwa ajili ya kosa lao. 26Jumuiya yote ya Kiisraeli pamoja na wageni waishio miongoni mwao watasamehewa, kwa sababu watu wote walihusika katika kosa lile lisilokusudiwa.

2715:27 Law 4:3, 27; Hes 6:14; Za 19:13; Lk 12:48“ ‘Lakini kama mtu mmoja peke yake akitenda dhambi pasipo kukusudia, ni lazima alete mbuzi mke wa mwaka mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi. 2815:28 Hes 8:12; 28:22; Law 4:20Kuhani atafanya upatanisho mbele za Bwana kwa ajili ya yule aliyekosa kwa kufanya dhambi pasipo kukusudia, upatanisho utakapofanywa kwa ajili yake, atasamehewa. 2915:29 Kut 12:49Sheria hiyo moja itamhusu kila mmoja ambaye ametenda dhambi pasipo kukusudia, awe Mwisraeli mzawa ama mgeni.

3015:30 Hes 14:40-44; Kum 1:43; 17:13; Za 19:13; 2Fal 19:6, 20; Isa 37:6, 23; Eze 20:27; Mwa 17:14; Ay 31:22“ ‘Lakini yeyote ambaye amefanya dhambi kwa dharau awe mzawa au mgeni, anamkufuru Bwana, naye mtu huyo ni lazima akatiliwe mbali na watu wake. 3115:31 Hes 11:14; Mit 13:13; Za 119:126; 1Sam 15:23-26; 2Sam 11:27; 12:9; Eze 18:20Kwa sababu amelidharau neno la Bwana na kuvunja amri zake, mtu huyo ni lazima akatiliwe mbali; hatia yake inabaki juu yake.’ ”

Mvunja Sabato Auawe

3215:32 Hes 12:16; Kut 31:14-15; 35:2-3Waisraeli walipokuwa jangwani, mtu mmoja alikutwa akikusanya kuni siku ya Sabato. 33Wale waliomkuta akikusanya kuni wakamleta kwa Mose, Aroni na kusanyiko lote, 3415:34 Hes 9:8; Law 24:12nao wakamweka kifungoni, kwa sababu haikufahamika kwa wazi kwamba afanyiwe nini. 3515:35 Kut 31:14-15; Law 20:2; Lk 4:29; Mdo 7:58Ndipo Bwana akamwambia Mose, “Huyo mtu ni lazima afe. Kusanyiko lote lazima limpige mawe nje ya kambi.” 3615:36 Law 20:2; Kut 31:14; Yer 17:21Hivyo kusanyiko likamtoa nje ya kambi na kumpiga mawe hadi akafa, kama Bwana alivyomwamuru Mose.

Vifundo Kwenye Mavazi

37Bwana akamwambia Mose, 3815:38 Law 3:17; Hes 10:8; Kum 22:12; Mt 23:5“Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Kwa vizazi vyote vijavyo jifanyieni vifundo katika pindo za mavazi yenu vikiwa na uzi wa buluu kwenye kila kifundo. 3915:39 Kum 4:23; 6:12; Za 73:27; 78:37; 106:39; Law 17:7Mtakuwa mkivitazama vifundo hivyo ili mpate kukumbuka amri zote za Bwana, ili mpate kuzitii msije mkajitia uzinzi wenyewe kwa kuzifuata tamaa za mioyo yenu na za macho yenu. 4015:40 Mwa 26:5; Kum 11:13; Za 103:18; 119:56; Law 11:44; Rum 12:1; Kol 1:22; 1Pet 1:15Ndipo mtakumbuka kuzitii amri zangu zote nanyi mtawekwa wakfu kwa Mungu wenu. 4115:41 Mwa 17:7; Kut 20:2Mimi Ndimi Bwana Mungu wenu, niliyewatoa Misri niwe Mungu wenu. Mimi Ndimi Bwana Mungu wenu.’ ”

O Livro

Números 15:1-41

Ofertas suplementares

1O Senhor disse a Moisés 2que desse as seguintes instruções ao povo de Israel: “Quando os vossos filhos viverem finalmente na terra que vou dar-lhes, 3e quiserem agradar ao Senhor, oferecendo-lhe um holocausto ou qualquer outra oferta pelo fogo, se os seus sacrifícios forem um animal, tomá-lo-ão dos seus rebanhos de ovelhas e de carneiros ou das suas manadas de gado. Cada sacrifício, seja um sacrifício vulgar ou o cumprimento de um voto, uma oferta voluntária ou um sacrifício especial na ocasião das solenidades anuais, 4será acompanhado de uma oferta de cereais. Se uma ovelha for sacrificada, usem 2,2 litros de farinha fina misturada com um litro de azeite, 5acompanhada de um litro de vinho como oferta.

6Se o sacrifício for um carneiro, usem 4,4 litros de farinha fina misturada com 1,3 litros de azeite, 7e 1,3 litros de vinho como oferta. Isto será um sacrifício de cheiro agradável ao Senhor.

8-9Se o sacrifício ou holocausto, for um novilho, então a oferta de cereais a acompanhá-lo deverá consistir em 6,6 litros de farinha fina misturada com 1,9 litros de azeite, 10mais 1,9 litros de vinho como oferta. Isto será oferecido pelo fogo como cheiro agradável ao Senhor.

11-14Estas são as instruções quanto ao que deve acompanhar cada animal de sacrifício, boi, carneiro, cordeiro ou cabra. Estas instruções aplicam-se tanto aos israelitas como aos estrangeiros que vivam no vosso meio e que queiram agradar ao Senhor com sacrifícios passados pelo fogo. 15-16Porque a lei e os mandamentos são para todos, naturais e estrangeiros, e isto deverá ser assim por todas as gerações futuras. São todos iguais perante o Senhor. Sim, uma só lei para todos!”

17O Senhor disse ainda a Moisés nesta mesma ocasião: 18“Dá ordens ao povo de Israel de que, quando chegarem à terra que lhes vou dar, 19-20deverão apresentar ao Senhor uma amostra de cada nova colheita anual, fazendo um bolo de farinha dos primeiros grãos da colheita do ano. Este bolo deverá ser oferecido com um movimento baloiçante perante o altar, com o gesto de oferta ao Senhor. 21É uma oferta anual feita da vossa eira, e deverá ser respeitada por todas as gerações futuras.

Sacrifícios por culpa involuntária

22Se por engano, vocês ou os vossos descendentes, falharem no cumprimento dos regulamentos que o Senhor vos tem dado durante estes anos através de Moisés, 23-24então, quando se derem conta do seu erro, deverão oferecer um novilho por holocausto. Será de cheiro agradável ao Senhor e deverá ser oferecido com a usual oferta de cereais e de vinho, e ainda com um bode como oferta pelo pecado. 25O sacerdote fará expiação por todo o povo de Israel e serão perdoados; visto que foi um engano e procuraram corrigi-lo, oferecendo um sacrifício pelo fogo perante o Senhor e um sacrifício pelo pecado. 26Todo o povo será perdoado, incluindo os estrangeiros que vivem no vosso meio, pois toda a população foi igualmente envolvida no mesmo erro e esquecimento.

27Se se tratar de um só indivíduo que errou, então deverá sacrificar uma cabra de um ano como oferta pelo pecado; 28o sacerdote fará expiação por ele perante o Senhor e será perdoado. 29Esta mesma lei se aplica também aos estrangeiros que vivem entre vocês.

30Mas se acontecer que alguém deliberadamente desobedeça a um mandamento, seja natural ou estrangeiro, isso é uma blasfémia ao Senhor e deverá ser expulso de entre o seu povo. 31Porque desrespeitou a palavra do Senhor e deliberadamente transgrediu o seu mandamento, deverá ser expulso do seu povo; será responsável pela sua culpa.”

Desrespeito à lei do sábado leva à morte

32Um dia, enquanto o povo de Israel estava no deserto, um deles foi achado a apanhar lenha num dia de sábado. 33Foi preso e trazido à presença de Moisés, de Aarão e de todo o povo. 34Puseram-no sob guarda, pois não estava ainda declarado o que se deveria fazer.

35Então o Senhor disse a Moisés: “O homem deve morrer; todo o povo o apedrejará fora do acampamento, até que morra.”

36Eles assim fizeram; levaram-no para fora do acampamento e mataram-no como o Senhor ordenara.

As borlas nas roupas

37Disse o Senhor a Moisés: 38“Diz ao povo de Israel que faça franjas para as bainhas das suas roupas, isto deverá tornar-se um regulamento permanente por todas as gerações vindouras, e que prenda essas franjas à roupa com cordões azuis. 39A finalidade deste regulamento é, sempre que repararem nas franjas, lembrar-vos dos meus mandamentos e que devem obedecer às minhas leis, em vez de seguirem os desejos de andarem nos vossos próprios caminhos. 40Isso lembrar-vos-á de obedecerem a todos os meus mandamentos e de serem santos para o vosso Deus. 41Porque eu sou o Senhor, o vosso Deus, que vos trouxe da terra do Egito. Sim, eu sou o Senhor, vosso Deus.”