Hesabu 13 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Hesabu 13:1-33

Kupeleleza Kanaani

(Kumbukumbu 1:19-33)

1Bwana akamwambia Mose, 213:2 Hes 13:16; Kum 1:22; Law 14:34; 24:11; Yos 1:3“Watume baadhi ya watu wakaipeleleze nchi ya Kanaani, ambayo ninawapa Waisraeli. Kutoka kwa kila kabila la baba zao, tuma mmoja wa viongozi wao.”

313:3 Hes 14:6; 24; 34:19; Kum 1:36; Amu 1:12-15Hivyo kwa agizo la Bwana Mose akawatuma kutoka Jangwa la Parani. Wote walikuwa viongozi wa Waisraeli. 4Haya ndiyo majina yao:

kutoka kabila la Reubeni, Shamua mwana wa Zakuri;

5kutoka kabila la Simeoni, Shafati mwana wa Hori;

613:6 Hes 14:6; 24; 34:19; Kum 1:36; Amu 1:12-15; Yos 14:6kutoka kabila la Yuda, Kalebu mwana wa Yefune;

7kutoka kabila la Isakari, Igali mwana wa Yosefu;

813:8 Hes 11:28kutoka kabila la Efraimu, Hoshea mwana wa Nuni;

9kutoka kabila la Benyamini, Palti mwana wa Rafu;

10kutoka kabila la Zabuloni, Gadieli mwana wa Sodi,

11kutoka kabila la Manase (kabila la Yosefu), Gadi mwana wa Susi;

12kutoka kabila la Dani, Amieli mwana wa Gemali;

13kutoka kabila la Asheri, Sethuri mwana wa Mikaeli;

14kutoka kabila la Naftali, Nabi mwana wa Wofsi;

15kutoka kabila la Gadi, Geueli mwana wa Maki.

1613:16 Kum 32:44; Kut 17:9Haya ndiyo majina ya watu ambao Mose aliwatuma kuipeleleza nchi. (Mose akampa Hoshea mwana wa Nuni jina Yoshua.)

1713:17 Yos 14:7; Mwa 12:9; Kum 1:7; Yos 9:1; Mwa 14:10; Kum 1:19; Amu 1:9-10Mose alipowatuma wakaipeleleze Kanaani, alisema, “Pandeni kupitia Negebu, mwende mpaka nchi ya vilima. 18Mwone nchi ni ya namna gani, na kama watu waishio humo wana nguvu au ni wadhaifu, iwapo ni wachache au wengi. 19Wanaishi katika nchi ya namna gani? Je, ni nzuri au mbaya? Wanaishi katika miji ya namna gani? Je, haina kuta au ngome? 2013:20 Kum 1:25; Law 25:5; Kum 8:7, 8; Neh 9:25-35; Eze 20:6; 34:14; Kum 31:6; Yos 1:6, 9; Ebr 13:6Ardhi iko aje? Ina rutuba au la? Je, kuna miti ndani yake au la? Jitahidini kadiri mwezavyo kuleta baadhi ya matunda ya nchi.” (Ulikuwa msimu wa kuiva zabibu za kwanza.)

2113:21 Hes 20:1; 27:14; 33:36; 34:8; Kum 32:51; Yos 15:1; 19:28; 13:5; Amu 1:31; 18:28; 2Sam 10:6; 1Nya 6:75; 13:5; 1Fal 8:65; 2Fal 14:25; 2Nya 7:8; Yer 52:7; Eze 47:16-20; Amo 6:14Hivyo wakapanda na kuipeleleza nchi kutoka Jangwa la Sini hadi Rehobu, kuelekea Lebo-Hamathi. 2213:22 Hes 13:28; Mwa 13:18; 23:19; Yos 15:14; Amu 1:10; Kum 2:10; 9:2; Yos 11:21; 15:13; Za 78:12; Isa 19:11-13; 30:4; Eze 30:14Wakapanda kupitia Negebu hadi wakafika Hebroni, mahali ambapo Ahimani, Sheshai na Talmai, wazao wa Anaki, waliishi. (Hebroni ulikuwa umejengwa miaka saba kabla ya mji wa Soani ulioko Misri.) 2313:23 Mwa 14:13; Kut 28:33; Mwa 3:7; Hes 20:5; Kum 8:8; 2Fal 18:31; Neh 13:15Walipofika katika Bonde la Eshkoli, walivunja tawi lililokuwa na kishada kimoja cha zabibu. Wawili wao wakalichukua lile tawi kwenye mti, pamoja na komamanga na tini. 24Eneo lile likaitwa Bonde la Eshkoli kwa sababu ya kile kishada cha zabibu ambacho Waisraeli walikikata huko. 2513:25 Mwa 7:4; Hes 14:34Mwishoni mwa siku arobaini wakarudi kutoka kuipeleleza nchi.

Taarifa Juu Ya Upelelezi

2613:26 Mwa 14:6-7; Hes 32:8; Kum 1:25Wakarudi kwa Mose, Aroni na jumuiya yote ya Waisraeli huko Kadeshi kwenye Jangwa la Parani. Hapo ndipo walipotoa habari kwao na kwa kusanyiko lote na kuwaonyesha matunda ya hiyo nchi. 2713:27 Kut 3:8; Kum 1:25; Yer 2:7Wakampa Mose taarifa hii: “Tuliingia katika nchi uliyotutuma, nayo inatiririka maziwa na asali! Hili hapa tunda lake. 2813:28 Kum 1:28; Yos 14:12Lakini watu wanaoishi huko ni wenye nguvu, na miji yao ina ngome na ni mikubwa sana. Huko tuliona hata wazao wa Anaki. 2913:29 Mwa 10:16, 18; 13:10; 14:7; 10:15; Kum 7:1; 20:17; 1Fal 9:20; 10:29; 2Fal 6:7; Kut 3:8; Hes 22:1; 32:5; Amu 3:28; Za 42:6Waamaleki wanaishi Negebu; Wahiti, Wayebusi na Waamori wanaishi katika nchi ya vilima; nao Wakanaani wanaishi karibu na bahari na kando ya Yordani.”

3013:30 Yos 14:7; Za 60:12; 119:10; Isa 11:10; Rum 8:31; Flp 4:13; Ebr 11:33, 34Kisha Kalebu akawanyamazisha watu mbele ya Mose na kusema, “Imetupasa kupanda na kuimiliki nchi, kwa maana hakika tunaweza kufanya hivyo.”

3113:31 Kum 9:1; Yos 14:8Lakini watu waliokuwa wamepanda pamoja naye wakasema, “Hatuwezi kuwashambulia wale watu; wana nguvu kutuliko sisi.” 3213:32 Hes 14:36-37; Eze 36:13-14; Kum 1:28; Amo 2:9Wakaeneza taarifa mbaya miongoni mwa Waisraeli kuhusu nchi waliyoipeleleza. Wakasema, “Nchi tuliyoipeleleza hula watu waishio ndani yake. Watu wote tuliowaona huko ni majitu. 3313:33 Mwa 6:4; Kum 1:28; Yos 11:22; 14:12; Mhu 12:5; Isa 40:22Tuliwaona Wanefili huko (wazao wa Anaki wanatokana na Wanefili.) Tulijiona kama panzi machoni petu wenyewe, nao ndivyo walivyotuona.”

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

民数记 13:1-33

打探迦南

1耶和华对摩西说: 2“你要派十二位首领,每个支派一位,去打探我要赐给以色列人的迦南。” 3摩西就按耶和华的吩咐,从巴兰旷野派出了十二位首领。 4他们的名字如下:吕便支派撒刻的儿子沙姆亚5西缅支派何利的儿子沙法6犹大支派耶孚尼的儿子迦勒7以萨迦支派约色的儿子以迦8以法莲支派的儿子何西阿9便雅悯支派拉孚的儿子帕提10西布伦支派梭底的儿子迦叠11约瑟的子孙、玛拿西支派稣西的儿子迦底12支派基玛利的儿子亚米利13亚设支派米迦勒的儿子西帖14拿弗他利支派缚西的儿子拿比15迦得支派玛基的儿子臼利16以上是摩西派去打探迦南的人,他称的儿子何西阿约书亚

17摩西派他们去打探迦南,并嘱咐说:“你们先去南地,然后再进山区, 18打探那地方,看看那里的居民是强是弱,是多是少; 19那地方是好是坏,人们住的是坚固的城池还是不设防的营地; 20土地是肥沃还是贫瘠,有没有树木。尽量带些当地的果子回来。”当时是葡萄初熟的季节。

21于是,他们从旷野一直打探到哈马口附近的利合22他们经南地到达希伯仑希伯仑城比埃及锁安城还要早建七年,那里住着亚衲人的子孙亚希幔示筛挞买23他们来到以实各谷,在那里砍下一根葡萄枝,上面有一串葡萄,由两个人用杠子抬着,又采了一些石榴和无花果。 24因为他们在那里砍了一串葡萄,所以就称那地方为以实各13:24 以实各”意思是“一串”。谷。

25过了四十天,他们打探完毕,返回营地。 26他们来到巴兰旷野的加低斯摩西亚伦以色列全体会众汇报,把当地的果子给大家看。 27他们对摩西说:“我们照你的指示打探了那地方,果然是奶蜜之乡,这些都是那里的果子。 28但那里的居民很强悍,城邑又大又坚固。我们在那里还见到亚衲人的子孙。 29亚玛力人住在南地,人、耶布斯人和亚摩利人住在山区,迦南人住在海边和约旦河沿岸。” 30迦勒让站在摩西面前的民众安静,然后说:“我们立刻去占领那地方吧!我们必能取胜。” 31跟他一起去打探的人却说:“我们不能去攻打那些人,他们比我们强大。” 32他们还危言耸听,说:“我们去打探的地方是吞吃居民之地,我们看见的人个个身材高大。 33我们在那里看见了亚衲人的子孙,他们是巨人的后裔,我们跟他们相比就像蚱蜢,他们看我们也像蚱蜢。”