Hesabu 10 – NEN & HTB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Hesabu 10:1-36

Tarumbeta Za Fedha

1Bwana akamwambia Mose: 210:2 Hes 31:6; Neh 4:18; 12:35; Za 47:5; 98:6; 105:3; Yer 4:5; 19; 6:1; Hos 5:8; 8:1; Yoe 2:1“Tengeneza tarumbeta mbili za fedha ya kufua, uzitumie kwa kuita jumuiya pamoja na wakati wa kuvunja makambi ili kuondoka. 3Tarumbeta zote mbili zikipigwa, jumuiya yote itakusanyika mbele yako katika ingilio la Hema la Kukutania. 410:4 Kut 18:21; Hes 7:2Kama tarumbeta moja tu ikipigwa, viongozi, yaani wakuu wa koo za Israeli, ndio watakaokusanyika mbele yako. 5Wakati mlio wa kujulisha hatari ukipigwa, makabila yaliyo na makambi upande wa mashariki yataondoka. 6Ukisikika mlio wa pili wa jinsi hiyo, walioko kwenye makambi ya kusini wataondoka. Mlio huo wa kujulisha hatari utakuwa ishara ya kuondoka. 710:7 Yer 4:5; 6:1; Eze 33:3; Yoe 2:1; 1Kor 14:8Ili kukusanya kusanyiko, piga tarumbeta zote, lakini siyo kwa mlio wa kujulisha hatari.

810:8 Mwa 9:12; Hes 15:14; 35:29; Yos 6:4; 2Nya 13:12“Wana wa Aroni, makuhani, ndio watakaopiga hizo tarumbeta. Hili litakuwa agizo la kudumu kwa ajili yenu na kwa vizazi vijavyo. 910:9 Kut 3:9; Amu 2:18; 6:9; 1Sam 10:18; 2Fal 13:4; Za 106:42; Law 23:24; 2Nya 13:12; Mwa 8:1Wakati mtakapopigana vita katika nchi yenu wenyewe dhidi ya adui anayewaonea, piga tarumbeta kwa mlio wa kujulisha hatari. Ndipo utakumbukwa na Bwana Mungu wenu na kuokolewa kutoka kwa adui zenu. 1010:10 Hes 28:11; 1Sam 20:5, 24; 2Fal 4:23; 2Nya 8:13; Za 81:3; Isa 1:13; Eze 45:17; 46:6; Amo 8:5; Law 23:24; 1:3; 3:1; 11:44; Hes 6:14Pia nyakati za furaha yenu, yaani sikukuu zenu zilizoamriwa na sikukuu za Mwezi Mwandamo, mtapiga tarumbeta juu ya sadaka zenu za kuteketezwa na sadaka zenu za amani, nazo zitakuwa ukumbusho kwa ajili yenu mbele za Mungu wenu. Mimi ndimi Bwana, Mungu wenu.”

Waisraeli Waondoka Sinai

1110:11 Kut 38:21; 40:17; Hes 9:17Katika siku ya ishirini ya mwezi wa pili wa mwaka wa pili, wingu liliinuka kutoka juu ya maskani ya Ushuhuda. 1210:12 Mwa 14:6; Kum 1:1; 33:2; Kut 40:36; Hes 12:16; Hab 3:3Ndipo Waisraeli wakaondoka kutoka Jangwa la Sinai wakasafiri kutoka sehemu moja hadi nyingine mpaka wingu lilipotua katika Jangwa la Parani. 1310:13 Kum 1:6; Hes 2:34Waliondoka kwa mara ya kwanza kwa agizo la Bwana kupitia kwa Mose.

1410:14 Hes 1:52; 2:3-9; 1:7Vikosi vya kambi ya Yuda vilitangulia kwanza chini ya alama yao. Nashoni mwana wa Aminadabu alikuwa kiongozi wao. 1510:15 Law 24:11; Hes 1:8Nethaneli mwana wa Suari alikuwa kiongozi wa kabila la Isakari, 1610:16 Hes 2:7; 1:9naye Eliabu mwana wa Heloni alikuwa kiongozi wa kabila la Zabuloni. 1710:17 Hes 4:21-32Ndipo Maskani iliposhushwa, nao wana wa Gershoni na wana wa Merari ambao waliibeba wakaondoka.

1810:18 Hes 2:16; 2:10-16; 1:5Vikosi vya kambi ya Reubeni vilifuata, chini ya alama yao. Elisuri mwana wa Shedeuri alikuwa kiongozi wao. 19Shelumieli mwana wa Surishadai aliongoza kikosi cha kabila la Simeoni, 2010:20 Hes 1:14naye Eliasafu mwana wa Deueli aliongoza kikosi cha kabila la Gadi. 2110:21 Hes 2:17; 4:20Kisha Wakohathi wakaondoka, wakichukua vitu vitakatifu. Maskani ilikuwa isimamishwe kabla wao hawajafika.

2210:22 Hes 2:24; 1:10Vikosi vya kambi ya Efraimu vilifuata, chini ya alama yao. Elishama mwana wa Amihudi alikuwa kiongozi wao. 23Gamalieli mwana wa Pedasuri aliongoza kikosi cha kabila la Manase, 2410:24 Hes 1:11naye Abidani mwana wa Gideoni alikuwa kiongozi wa kikosi cha kabila la Benyamini.

2510:25 Hes 2:31; 1:12; Yos 6:9Mwishowe, kama kikosi cha nyuma cha ulinzi wa vikosi vyote, vikosi vya kambi ya Dani viliondoka chini ya alama yao. Ahiezeri mwana wa Amishadai alikuwa kiongozi wao. 26Pagieli mwana wa Okrani aliongoza kikosi cha kabila la Asheri, 27naye Ahira mwana wa Enani aliongoza kikosi cha kabila la Naftali. 2810:28 Za 80:1; Wim 6:10Huu ndio ulikuwa utaratibu wa kuondoka wa vikosi vya Waisraeli walipokuwa wanaondoka.

2910:29 Amu 4:11; Kut 2:18; 3:1; Mwa 12:7; 15:14Basi Mose akamwambia Hobabu mwana wa Reueli, Mmidiani, mkwewe Mose, “Tunaondoka kwenda mahali ambapo Bwana amesema ‘Nitawapa ninyi mahali hapo.’ Twende pamoja nasi tutakutendea mema, kwa maana Bwana ameahidi mambo mema kwa Israeli.”

3010:30 Mt 21:29; Kut 18:27Akajibu, “Hapana, sitakwenda; nitarudi kwenye nchi yangu mwenyewe na watu wangu mwenyewe.”

3110:31 Ay 29:15Lakini Mose akasema, “Tafadhali usituache. Wewe unajua mahali ambapo yatupasa kupiga kambi jangwani, nawe unaweza kuwa macho yetu. 3210:32 Kut 12:48; Kum 10:18; Za 22:27-31; 67:5-7Ikiwa utafuatana nasi, tutashirikiana nawe mema yoyote tutakayopewa na Bwana.”

3310:33 Kum 1:33; 10:8; 31:9; Yos 3:3; Amu 20:27; 2Sam 15:24; Yer 31:2Hivyo waliondoka kutoka mlima wa Bwana, nao wakasafiri kwa siku tatu. Sanduku la Agano la Bwana liliwatangulia kwa zile siku tatu ili kuwatafutia mahali pa kupumzika. 3410:34 Hes 9:15-23; Kut 13:21; Neh 9:12, 19Wingu la Bwana lilikuwa juu yao wakati wa mchana walipoondoka kambini.

3510:35 2Nya 6:41; Za 17:13; 44:26; 94:2; 132:8; Amu 5:31; 2Sam 2:1; Za 68:1; 92:9; Kum 5:9; 7:10; Isa 17:12-14; 59:18Wakati wowote Sanduku lilipoondoka, Mose alisema,

“Ee Bwana, inuka!

Watesi wako na watawanyike;

adui zako na wakimbie mbele zako.”

3610:36 Isa 52:8; 63:17; Mwa 15:5; 26:4; Kum 1:10; 10:22; Neh 9:23Wakati wowote Sanduku liliposimama, alisema,

“Ee Bwana, rudi,

kwa maelfu ya Waisraeli wasiohesabika.”

Het Boek

Numeri 10:1-36

Op weg met God

1-2 Nu zei de Here tegen Mozes: ‘Maak twee trompetten van gedreven zilver. Die moeten worden gebruikt om het sein “verzamelen” en “opbreken” te blazen. 3Als op twee trompetten wordt geblazen, is dat het teken dat het hele volk zich moet verzamelen bij de ingang van de tabernakel. 4Als één trompet wordt geblazen, moeten alleen de stamhoofden zich bij u verzamelen. 5-7Er zullen verschillende trompetsignalen nodig zijn om onderscheid te maken tussen het sein “verzamelen” en “opbreken en verder trekken”. Als het vertreksignaal wordt geblazen, moeten de stammen die aan de oostkant van de tabernakel hun kamp hebben, het eerst vertrekken. Bij het volgende signaal vertrekken de stammen aan de zuidkant. 8Alleen de priesters mogen de trompet blazen. Dit is een vaste instelling die van generatie op generatie moet worden nageleefd. 9Wanneer u aankomt in het beloofde land en oorlog voert tegen uw vijanden, zal de Here u horen en u te hulp komen als u in nood alarm blaast op de trompetten. 10Gebruik de trompetten ook in tijden van blijdschap: tijdens de jaarlijkse feesten en aan het begin van elke maand om uw vreugde over de brandoffers en vredeoffers te laten blijken. God zal dan steeds weer denken aan zijn verbond met u. Want Ik ben de Here, uw God.’

11De wolk steeg op boven de tabernakel op de twintigste dag van de tweede maand van het tweede jaar na Israëls uittocht uit Egypte. 12De Israëlieten verlieten de Sinaï-woestijn en volgden de wolk naar de woestijn Paran. 13Dit was hun eerste reis sinds de Here aan Mozes de reisopdrachten had gegeven.

14Aan het hoofd van de stoet liep de stam Juda, gegroepeerd achter de stambanier, onder leiding van Nachson, de zoon van Amminadab. 15Daarachter kwamen de stam van Issachar, onder leiding van Netanel, de zoon van Suar, 16en de stam van Zebulon, geleid door Eliab, de zoon van Chelon. 17De tabernakel was afgebroken en de Gersonieten en Merarieten waren de volgende groep in de stoet. Zij droegen de tabernakel op hun schouders. 18Daarachter kwam de banier van Ruben, waar Elisur, de zoon van Sedeür zijn mensen leidde. 19De volgende stammen waren die van Simeon, onder leiding van Selumiël, de zoon van Surisaddai, 20en die van Gad, onder leiding van Eljasaf, de zoon van Deüel. 21Achter deze twee stammen liepen de Kehatieten, die de voorwerpen uit het Heilige droegen. Wanneer zij op de nieuwe kampplaats aankwamen, hadden de anderen de tabernakel al opgezet. 22Achter deze Levieten kwamen de stam van Efraïm, onder leiding van Elisama, de zoon van Ammihud, 23de stam van Manasse, onder leiding van Gamliël, de zoon van Pedasur, 24en die van Benjamin, onder leiding van Abidan, de zoon van Gidoni. 25De achterhoede van de stoet bestond uit de stam van Dan, onder leiding van Achiëzer, de zoon van Ammisaddai, 26de stam van Aser, onder leiding van Pagiël, de zoon van Ochran, 27en ten slotte de stam van Naftali, onder leiding van Achira, de zoon van Enan. 28Dat was de volgorde waarin de stammen reisden.

29Op een dag zei Mozes tegen zijn zwager Chobab, de zoon van zijn schoonvader Jetro: ‘Wij zijn nu eindelijk echt op weg naar het beloofde land. Ga toch met ons mee, er zal goed voor je gezorgd worden. Want de Here heeft Israël veel goeds beloofd.’ 30Maar zijn zwager antwoordde: ‘Nee, ik wil terug naar mijn eigen land en mijn familie.’ 31‘Blijf toch bij ons,’ drong Mozes aan, ‘want jij kent de weg in de woestijn en je zou ons goed kunnen helpen. 32Als je meegaat, kun je ook genieten van al het goede dat de Here ons gaat geven.’

33Nadat de Israëlieten bij de berg Sinaï waren opgebroken, trokken zij drie dagreizen verder. De ark ging voorop om de volgende stopplaats aan te wijzen. 34Het was dag toen zij vertrokken en de wolk ging voor hen uit toen zij zich in beweging zetten. 35Wanneer de ark werd opgenomen en verder gedragen, riep Mozes luid: ‘Sta op, Here, en sla uw vijanden uiteen, laten zij voor U op de vlucht slaan!’ 36En wanneer de ark werd neergezet, zei hij: ‘Keer terug, Here, en zegen de stammen van Israël.’