Hagai 1 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Hagai 1:1-15

Wito Wa Kuijenga Nyumba Ya Bwana

11:1 Ezr 4:24; 5:1-3; 2:2; 3:2; 1Nya 3:19; 6:15; Mt 1:12-13Katika mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Dario wa Uajemi, katika siku ya kwanza ya mwezi wa sita, neno la Bwana lilikuja kupitia kwa nabii Hagai kwenda kwa Zerubabeli mwana wa Shealtieli, mtawala wa Yuda na kwa Yoshua1:1 Yoshua kwa Kiebrania ni Yeshua, maana yake ni Yehova ni wokovu. mwana wa kuhani mkuu Yehosadaki:

21:2 Isa 13:4; 29:13Hivi ndivyo asemavyo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Hawa watu husema, ‘Wakati haujawadia wa kujenga nyumba ya Bwana.’ ”

31:3 Ezr 5:1Kisha neno la Bwana likaja kupitia kwa nabii Hagai: 41:4 2Sam 7:2; Yer 33:12“Je, ni wakati wenu ninyi wa kuishi katika nyumba zenu zilizojengwa vizuri, wakati hii nyumba ikibaki, gofu?”

51:5 Mao 3:40; Hag 2:15-18Sasa hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Zitafakarini vyema njia zenu. 61:6 Law 26:20; Isa 5:10; 9:20; 55:2; Amo 4:8; Hag 2:16; Zek 8:10Mmepanda vingi, lakini mmevuna haba. Mnakula lakini hamshibi, mnakunywa, lakini hamtosheki. Mnavaa nguo, lakini hamsikii joto. Mnapata mishahara, lakini inatoweka kama imewekwa kwenye mfuko uliotobokatoboka.”

7Hili ndilo asemalo Bwana Mwenye Nguvu Zote: “Zitafakarini vyema njia zenu. 81:8 Ay 22:3; Yer 13:11; 1Nya 14:1; Za 132:13-14; Kut 29:43Pandeni milimani mkalete miti na kujenga nyumba, ili nipate kuifurahia, na nitukuzwe,” asema Bwana. 91:9 Kum 28:38; Isa 5:10; Neh 13:11; Za 103:16; Eze 22:21“Mlitarajia mengi, kumbe, yametokea kidogo. Ulichokileta nyumbani nilikipeperusha. Kwa nini?” asema Bwana Mwenye Nguvu Zote. “Ni kwa sababu ya nyumba yangu, inayobaki katika hali ya magofu, wakati kila mmoja wenu anajishughulisha na nyumba yake mwenyewe. 101:10 Kum 28:24; Mwa 27:28; 1Fal 17:1; 2Nya 6:26; Yer 3:3; Law 26:19; Yoe 1:18-19Kwa hiyo, kwa sababu yenu mbingu zimezuia umande wake na ardhi mavuno yake. 111:11 Kum 11:26; 28:22; Rut 1:1; 1Fal 17:1; Hag 2:17; Isa 5:6; 7:25; Hes 18:12Niliita ukame mashambani na milimani, kwenye nafaka, mvinyo mpya, mafuta pamoja na chochote kinachozalishwa na ardhi, juu ya watu na ngʼombe, pamoja na kazi za mikono yenu.”

121:12 Isa 1:9; 50:10; 55:11; Mt 28:20; Kum 31:12; Hag 2:2; Ezr 5:2; Mhu 12:13; Ay 36:11Kisha Zerubabeli mwana wa Shealtieli, Yoshua kuhani mkuu mwana wa Yehosadaki, pamoja na mabaki yote ya watu wakaitii sauti ya Bwana Mungu wao pamoja na ujumbe wa nabii Hagai, kwa sababu alikuwa ametumwa na Bwana Mungu wao. Watu walimwogopa Bwana.

131:13 Hes 14:9; 27:21; 2Nya 15:2; 36:15; Mwa 26:3; Rum 8:31; Isa 41:10; Mt 28:20Kisha Hagai, mjumbe wa Bwana, akawapa watu ujumbe huu wa Bwana: “Mimi niko pamoja nanyi,” asema Bwana. 141:14 Ezr 5:2; Za 110:3; 2Nya 36:22; Hag 2:21; 1Nya 6:15; 1Kor 15:58Kwa hiyo Bwana akachochea roho ya Zerubabeli mwana wa Shealtieli, mtawala wa Yuda, na roho ya kuhani mkuu Yoshua mwana wa Yehosadaki, pamoja na roho za mabaki yote ya watu. Walikuja wakaanza kufanya kazi katika nyumba ya Bwana Mwenye Nguvu Zote, Mungu wao, 151:15 Hag 2:10, 20; Ezr 4:24katika siku ya ishirini na nne mwezi wa sita, katika mwaka wa pili wa utawala wa Mfalme Dario.

King James Version

Haggai 1:1-15

1In the second year of Darius the king, in the sixth month, in the first day of the month, came the word of the LORD by Haggai the prophet unto Zerubbabel the son of Shealtiel, governor of Judah, and to Joshua the son of Josedech, the high priest, saying, 1.1 by: Heb. by the hand of1.1 governor: or, captain 2Thus speaketh the LORD of hosts, saying, This people say, The time is not come, the time that the LORD’s house should be built. 3Then came the word of the LORD by Haggai the prophet, saying, 4Is it time for you, O ye, to dwell in your cieled houses, and this house lie waste? 5Now therefore thus saith the LORD of hosts; Consider your ways.1.5 Consider…: Heb. Set your heart on your ways 6Ye have sown much, and bring in little; ye eat, but ye have not enough; ye drink, but ye are not filled with drink; ye clothe you, but there is none warm; and he that earneth wages earneth wages to put it into a bag with holes.1.6 with holes: Heb. pierced through

7¶ Thus saith the LORD of hosts; Consider your ways.1.7 Consider…: Heb. Set your heart on your ways 8Go up to the mountain, and bring wood, and build the house; and I will take pleasure in it, and I will be glorified, saith the LORD. 9Ye looked for much, and, lo, it came to little; and when ye brought it home, I did blow upon it. Why? saith the LORD of hosts. Because of mine house that is waste, and ye run every man unto his own house.1.9 blow…: or, blow it away 10Therefore the heaven over you is stayed from dew, and the earth is stayed from her fruit. 11And I called for a drought upon the land, and upon the mountains, and upon the corn, and upon the new wine, and upon the oil, and upon that which the ground bringeth forth, and upon men, and upon cattle, and upon all the labour of the hands.

12¶ Then Zerubbabel the son of Shealtiel, and Joshua the son of Josedech, the high priest, with all the remnant of the people, obeyed the voice of the LORD their God, and the words of Haggai the prophet, as the LORD their God had sent him, and the people did fear before the LORD. 13Then spake Haggai the LORD’s messenger in the LORD’s message unto the people, saying, I am with you, saith the LORD. 14And the LORD stirred up the spirit of Zerubbabel the son of Shealtiel, governor of Judah, and the spirit of Joshua the son of Josedech, the high priest, and the spirit of all the remnant of the people; and they came and did work in the house of the LORD of hosts, their God, 15In the four and twentieth day of the sixth month, in the second year of Darius the king.