Habakuki 2 – NEN & NIV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Habakuki 2:1-20

12:1 Isa 21:8; Za 48:13; 85:8; Eze 3:17; Za 73:16, 17; 5:3Nitasimama katika zamu yangu,

na kujiweka mwenyewe juu ya maboma;

nitatazama nione atakaloniambia,

na ni jibu gani nitakalotoa kuhusu lalamiko hili.

Jibu La Bwana

22:2 Isa 8:1; 30:8; Kum 27:8; Rum 4:24; 15:4; Yer 36:2; Eze 24:2; Ufu 1:19Kisha Bwana akajibu:

“Andika ufunuo huu,

na ukaufanye wazi juu ya vibao,

ili mpiga mbiu akimbie nao.

32:3 Dan 10:14; 11:27; 8:17; Za 27:14; Eze 12:25Kwa kuwa ufunuo huu unasubiri wakati uliokubalika;

unazungumzia mambo ya mwisho,

na kamwe hautakosea.

Iwapo utakawia, wewe usubiri;

kwa hakika utakuja na hautachelewa.

42:4 Eze 18:9; Yn 3:36; 2Kor 5:7; Rum 1:17; Gal 3:11; Ebr 10:37-38“Tazama, amejaa majivuno;

anavyovitamani si vya unyofu:

lakini mwenye haki ataishi kwa imani yake:

52:5 Mit 20:1; Isa 2:11; Mit 27:20; 30:15-16; Hab 1:9hakika mvinyo humsaliti;

ni mwenye kiburi na hana amani.

Kwa sababu ni mlafi kama kuzimu

na kama kifo kamwe hatosheki;

anajikusanyia mataifa yote

na kuchukua watu wote mateka.

62:6 Isa 14:4; Amo 2:8“Je, watu wote hawatamsuta kwa dhihaka na kumbeza, wakisema,

“ ‘Ole wake yeye akusanyaye bidhaa zilizoibwa

na kujifanyia utajiri kwa kutoza kwa nguvu!

Ataendelea hivi kwa muda gani?’

72:7 Mit 29:1Je, wadai wako hawatainuka ghafula?

Je, hawataamka na kukufanya utetemeke?

Kisha utakuwa mhanga kwao.

82:8 Zek 1:122:8 Isa 33:1; Yer 50:17-18; Oba 1:15; Zek 2:8-9; Eze 39:10Kwa kuwa umeteka nyara mataifa mengi,

watu waliobaki watakuteka nyara wewe.

Kwa kuwa umemwaga damu ya mtu;

umeharibu nchi na miji, na kila mmoja ndani yake.

92:9 Yer 22:13; 51:13; Ay 39:27; Isa 10:14“Ole wake yeye ajengaye milki yake kwa mapato ya udhalimu,

awekaye kiota chake juu,

ili kukimbia makucha ya uharibifu!

102:10 Yer 26:19; Nah 3:6Umefanya shauri la maangamizi ya watu wengi,

ukiaibisha nyumba yako mwenyewe, na kupotewa na maisha yako.

112:11 Yos 24:27; Zek 5:4; Lk 19:40Mawe ya kuta yatapiga kelele,

na mihimili ya kazi ya mbao itarudisha mwangwi wake.

122:12 Eze 22:2; Mik 3:10“Ole wake yeye ajengaye mji kwa kumwaga

damu na kuusimamisha mji kwa uhalifu!

132:13 Isa 50:11; 47:13Je, Bwana Mwenye Nguvu Zote hakuonyesha

kwamba kazi ya wanadamu ni mafuta tu kwa ajili ya moto,

na kwamba mataifa

yanajichosha bure?

142:14 Kut 16:7; Hes 14:21; Isa 11:9Kwa kuwa dunia itajazwa na maarifa ya utukufu wa Bwana,

kama maji yaifunikavyo bahari.

152:15 Mit 23:20“Ole wake yeye awapaye jirani zake kileo,

akiimimina kutoka kwenye kiriba

cha mvinyo mpaka wamelewa,

ili apate kutazama miili yao iliyo uchi.

162:16 Eze 23:32-34; Hos 4:7; Law 10:9; Mao 4:21; Za 16:5; Isa 51:22Utajazwa na aibu badala ya utukufu.

Sasa ni zamu yako! Kunywa na ujifunue!

Kikombe kutoka kwenye mkono wa kuume wa Bwana kinakujia,

na aibu itafunika utukufu wako.

172:17 Yer 50:33; 51:35; 50:15Ukatili ulioifanyia Lebanoni utakufunika,

na uharibifu uliowafanyia wanyama utakutisha.

Kwa sababu umemwaga damu ya mtu;

umeharibu nchi na miji na kila mmoja aliyeko ndani yake.

182:18 1Sam 12:21; Amu 10:14; Isa 40:19; Yer 5:21; 14:22; 10:14; 1Kor 12:2“Sanamu ina thamani gani,

kwani mwanadamu ndiye alichonga?

Ama kinyago kinachofundisha uongo?

Kwa kuwa yeye aliyekitengeneza

hutegemea kazi ya mikono yake mwenyewe;

hutengeneza sanamu zisizoweza kuzungumza.

192:19 1Fal 18:27; Yer 10:4; Hos 4:12; Dan 5:4, 23Ole wake yeye auambiaye mti, ‘Uwe hai!’

Ama asemaye na jiwe lisilo na uhai, ‘Amka!’

Je, linaweza kuongoza?

Limefunikwa kwa dhahabu na fedha;

hakuna pumzi ndani yake.

202:20 Za 11:4; Isa 41:1Lakini Bwana yuko katika Hekalu lake takatifu;

dunia yote na inyamaze mbele yake.”

New International Version

Habakkuk 2:1-20

1I will stand at my watch

and station myself on the ramparts;

I will look to see what he will say to me,

and what answer I am to give to this complaint.2:1 Or and what to answer when I am rebuked

The Lord’s Answer

2Then the Lord replied:

“Write down the revelation

and make it plain on tablets

so that a herald2:2 Or so that whoever reads it may run with it.

3For the revelation awaits an appointed time;

it speaks of the end

and will not prove false.

Though it linger, wait for it;

it2:3 Or Though he linger, wait for him; / he will certainly come

and will not delay.

4“See, the enemy is puffed up;

his desires are not upright—

but the righteous person will live by his faithfulness2:4 Or faith

5indeed, wine betrays him;

he is arrogant and never at rest.

Because he is as greedy as the grave

and like death is never satisfied,

he gathers to himself all the nations

and takes captive all the peoples.

6“Will not all of them taunt him with ridicule and scorn, saying,

“ ‘Woe to him who piles up stolen goods

and makes himself wealthy by extortion!

How long must this go on?’

7Will not your creditors suddenly arise?

Will they not wake up and make you tremble?

Then you will become their prey.

8Because you have plundered many nations,

the peoples who are left will plunder you.

For you have shed human blood;

you have destroyed lands and cities and everyone in them.

9“Woe to him who builds his house by unjust gain,

setting his nest on high

to escape the clutches of ruin!

10You have plotted the ruin of many peoples,

shaming your own house and forfeiting your life.

11The stones of the wall will cry out,

and the beams of the woodwork will echo it.

12“Woe to him who builds a city with bloodshed

and establishes a town by injustice!

13Has not the Lord Almighty determined

that the people’s labor is only fuel for the fire,

that the nations exhaust themselves for nothing?

14For the earth will be filled with the knowledge of the glory of the Lord

as the waters cover the sea.

15“Woe to him who gives drink to his neighbors,

pouring it from the wineskin till they are drunk,

so that he can gaze on their naked bodies!

16You will be filled with shame instead of glory.

Now it is your turn! Drink and let your nakedness be exposed2:16 Masoretic Text; Dead Sea Scrolls, Aquila, Vulgate and Syriac (see also Septuagint) and stagger!

The cup from the Lord’s right hand is coming around to you,

and disgrace will cover your glory.

17The violence you have done to Lebanon will overwhelm you,

and your destruction of animals will terrify you.

For you have shed human blood;

you have destroyed lands and cities and everyone in them.

18“Of what value is an idol carved by a craftsman?

Or an image that teaches lies?

For the one who makes it trusts in his own creation;

he makes idols that cannot speak.

19Woe to him who says to wood, ‘Come to life!’

Or to lifeless stone, ‘Wake up!’

Can it give guidance?

It is covered with gold and silver;

there is no breath in it.”

20The Lord is in his holy temple;

let all the earth be silent before him.