Habakuki 1 – NEN & NVI-PT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Habakuki 1:1-17

11:1 Nah 1:1Neno alilopokea nabii Habakuki.

Lalamiko La Habakuki

21:2 Za 13:1-2; 22:1-2; 6:3; 27:7; Yer 14:9Ee Bwana, hata lini nitakuomba msaada,

lakini wewe husikilizi?

Au kukulilia, “Udhalimu!”

Lakini hutaki kuokoa?

31:3 Ay 9:23; Yer 20:8; Za 55:9Kwa nini unanifanya nitazame dhuluma?

Kwa nini unavumilia makosa?

Uharibifu na udhalimu viko mbele yangu;

kuna mabishano na mapambano kwa wingi.

41:4 Ay 12:6; Za 12:8; 58:2Kwa hiyo sheria imepotoshwa,

nayo haki haipo kabisa.

Waovu wanawazunguka wenye haki,

kwa hiyo haki imepotoshwa.

Jibu La Bwana

5“Yatazame mataifa,

uangalie na ushangae kabisa.

Kwa sababu katika siku zako nitafanya kitu

ambacho hungeamini,

hata kama ungeambiwa.

6Nitawainua Wakaldayo,

watu hao wakatili na wenye haraka,

ambao hupita dunia yote

kuteka mahali pa kuishi pasipo pao wenyewe.

7Ni watu wanoogopwa na wanaotisha;

wenyewe ndio sheria yao,

na huinua heshima yao wenyewe.

8Farasi wao ni wepesi kuliko chui,

na wakali kuliko mbwa mwitu wakati wa machweo.

Askari wapanda farasi wao huenda mbio;

waendesha farasi wao wanatoka mbali.

Wanaruka kasi kama tai ili kurarua;

91:9 Hab 2:5wote wanakuja tayari kwa fujo.

Makundi yao ya wajeuri yanasonga mbele

kama upepo wa jangwani,

na kukusanya wafungwa

kama mchanga.

101:10 2Nya 36:6; Yer 33:4Wanawabeza wafalme,

na kuwadhihaki watawala.

Wanaicheka miji yote iliyozungushiwa maboma;

wanafanya malundo ya udongo na kuiteka hiyo miji.

111:11 Yer 4:11-12; Dan 4:30Kisha wanapita kasi kama upepo na kusonga mbele:

watu wenye hatia, ambao nguvu zao ndio mungu wao.”

Lalamiko La Pili La Habakuki

121:12 Mwa 21:33; Isa 31:1; 37:23; Kut 33:22; Isa 10:6; Mwa 49:24; Za 118:17Ee Bwana, je, wewe sio wa tangu milele?

Mungu wangu, Uliye Mtakatifu wangu, hatutakufa.

Ee Bwana, umewachagua wao ili watekeleze hukumu;

Ee Mwamba, umewaamuru watuadhibu.

131:13 Za 18:26; Mao 3:34-36; Za 25:3; Ay 21:7Macho yako ni safi mno hata yasiweze kuutazama uovu,

wala huwezi kuvumilia makosa.

Kwa nini basi unawavumilia wadanganyifu?

Kwa nini unakuwa kimya wakati waovu

wanawameza wale wenye haki

kuliko wao wenyewe?

14Umewafanya watu kama samaki baharini,

kama viumbe wa bahari wasio na mtawala.

151:15 Yer 5:26; Isa 19:8; Ay 18:8; Yer 16:16Adui mwovu anawavuta wote kwa ndoana,

anawakamata katika wavu wake,

anawakusanya katika juya lake;

kwa hiyo anashangilia na anafurahi.

161:16 Yer 44:8Kwa hiyo anatoa kafara kwa wavu wake,

na kuchoma uvumba kwa juya lake,

kwa kuwa kwa wavu wake anaishi kwa starehe,

na anafurahia chakula kizuri.

171:17 Isa 14:6; 19:8Je, aendelee kuwatoa walio katika wavu wake,

akiangamiza mataifa bila huruma?

Nova Versão Internacional

Habacuque 1:1-17

1Advertência revelada ao profeta Habacuque.

A Primeira Queixa de Habacuque

2Até quando, Senhor, clamarei por socorro,

sem que tu ouças?

Até quando gritarei a ti: “Violência!”

sem que tragas salvação?

3Por que me fazes ver a injustiça,

e contemplar a maldade?

A destruição e a violência estão diante de mim;

há luta e conflito por todo lado.

4Por isso a lei se enfraquece,

e a justiça nunca prevalece.

Os ímpios prejudicam os justos,

e assim a justiça é pervertida.

A Resposta do Senhor

5“Olhem as nações e contemplem-nas,

fiquem atônitos e pasmem;

pois nos seus dias farei algo em que não creriam

se a vocês fosse contado.

6Estou trazendo os babilônios1.6 Hebraico: caldeus.,

nação cruel e impetuosa,

que marcha por toda a extensão da terra

para apoderar-se de moradias que não lhe pertencem.

7É uma nação apavorante e temível,

que cria a sua própria justiça

e promove a sua própria honra.

8Seus cavalos são mais velozes que os leopardos,

mais ferozes1.8 Ou ligeiros que os lobos no crepúsculo.

Sua cavalaria vem de longe.

Seus cavalos vêm a galope;

vêm voando como ave de rapina que mergulha para devorar;

9todos vêm prontos para a violência.

Suas hordas avançam como o vento do deserto,

e fazem tantos prisioneiros como a areia da praia.

10Menosprezam os reis e zombam dos governantes.

Riem de todas as cidades fortificadas,

pois constroem rampas de terra

e por elas as conquistam.

11Depois passam como o vento e prosseguem;

homens carregados de culpa

que têm por deus a sua própria força.”

A Segunda Queixa de Habacuque

12Senhor, tu não és desde a eternidade?

Meu Deus, meu Santo, tu não morrerás1.12 O Texto Massorético diz nós não morreremos..

Senhor, tu designaste essa nação para executar juízo;

ó Rocha, determinaste que ela aplicasse castigo.

13Teus olhos são tão puros

que não suportam ver o mal;

não podes tolerar a maldade.

Então, por que toleras os perversos?

Por que ficas calado enquanto os ímpios devoram

os que são mais justos que eles?

14Tornaste os homens como peixes do mar,

como animais1.14 Ou peixes, criaturas do mar, que não são governados por ninguém.

15O inimigo puxa todos com anzóis;

apanha-os em sua rede e nela os arrasta;

então alegra-se e exulta.

16E por essa razão ele oferece sacrifício à sua rede

e queima incenso em sua honra;

pois, graças à sua rede,

vive em grande conforto e desfruta iguarias.

17Mas continuará ele esvaziando a sua rede,

destruindo sem misericórdia as nações?