Ezra 10 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ezra 10:1-44

Toba Ya Watu

110:1 2Nya 20:9; Dan 9:20Wakati Ezra alipokuwa anaomba na kuungama, huku akilia na kujitupa chini mbele ya nyumba ya Mungu, umati mkubwa wa Waisraeli, wanaume, wanawake na watoto walikusanyika kumzunguka. Nao pia wakalia sana. 210:2 Ezr 9:2; Kut 34:13; Neh 13:27; Kum 30:8-10Kisha Shekania mwana wa Yehieli, mmoja wa wazao wa Elamu, akamwambia Ezra, “Tumekosa uaminifu kwa Mungu wetu kwa kuoa wanawake wa kigeni kutoka mataifa yanayotuzunguka. Lakini pamoja na hili, bado liko tumaini kwa ajili ya Israeli. 310:3 2Fal 11:17; 2Nya 34:31; Kut 34:16; Kum 7:2-3; Ezr 9:4; Za 119:53, 120; Isa 66:2Sasa na tufanye agano mbele za Mungu wetu kuwafukuza hawa wanawake wote pamoja na watoto wao, kulingana na maonyo ya bwana wangu pamoja na wale ambao wanaogopa amri za Mungu wetu. Hili na lifanyike sawasawa na hii Sheria. 410:4 1Nya 28:10; Isa 35:3-4Inuka, suala hili lipo mikononi mwako. Sisi tutaungana nawe, uwe na ujasiri ukatende hili.”

510:5 Neh 5:12; 13:25Basi Ezra akainuka na kuwaapisha makuhani viongozi, Walawi na Israeli yote kufanya lile lililokuwa limependekezwa. Nao wakaapa. 610:6 Kum 9:18; Yn 3:7; Za 102:4Ndipo Ezra akaondoka hapo mbele ya nyumba ya Mungu akaenda kwenye chumba cha Yehohanani mwana wa Eliashibu. Wakati alipokuwa hapo, hakula chakula wala hakunywa maji, kwa sababu aliendelea kuomboleza kuhusu kukosa uaminifu kwa watu wa uhamishoni.

7Ndipo lilipotolewa tangazo Yuda yote na Yerusalemu kwa watu wote waliokuwa uhamishoni kukusanyika Yerusalemu. 810:8 Law 27:28; Yos 6:19Yeyote ambaye hangejitokeza kwa muda wa siku tatu angepoteza mali yake yote, kulingana na uamuzi wa maafisa na wazee, naye mtu huyo angefukuzwa kutoka kusanyiko la watu waliokuwa uhamishoni.

910:9 1Sam 12:18; Ezr 1:5Katika muda wa siku tatu, watu wote wa Yuda na Benyamini wakawa wamekusanyika huko Yerusalemu. Kwenye siku ya ishirini ya mwezi wa tisa, watu wote walikuwa wameketi ndani ya uwanja mbele ya nyumba ya Mungu, wakiwa na majonzi mno kwa tukio hilo na kwa sababu ya mvua kubwa. 10Ndipo Kuhani Ezra aliposimama akawaambia, “Mmekosa uaminifu, mmeoa wanawake wa kigeni, mkaongezea hatia ya Israeli. 1110:11 Kum 24:1; Mit 28:13; Mal 2:10-16; Yer 3:13; Isa 1:16-17; Rum 12:2Sasa tubuni kwa Bwana, Mungu wa baba zenu mkafanye mapenzi yake. Jitengeni na mataifa wanaowazunguka na wake zenu wa kigeni.”

1210:12 Yos 6:5Kusanyiko lote likajibu kwa sauti kubwa: “Uko sawa kabisa! Ni lazima tufanye kama unavyosema. 13Lakini hapa pana watu wengi na ni wakati wa mvua, hivyo hatuwezi kusimama nje. Hata hivyo, shauri hili haliwezi kumalizika kwa siku moja au mbili, kwa sababu tumefanya dhambi kubwa katika jambo hili. 1410:14 Kum 16:18; Hes 25:4; 2Nya 30:8; 2Fal 23:26; 2Nya 28:11-13; 29:10; 30:8; Za 78:38; Isa 12:1Maafisa wetu na wafanye kwa niaba ya kusanyiko lote. Kisha kila mmoja katika miji yetu ambaye ameoa mwanamke wa kigeni aje kwa wakati uliopangwa, akiwa pamoja na wazee na waamuzi wa kila mji, hadi hasira kali ya Mungu wetu katika shauri hili itakapoondolewa kwetu.” 1510:15 Neh 11:16Yonathani mwana wa Asaheli na Yazeya mwana wa Tikwa peke yao, wakiungwa mkono na Meshulamu na Shabethai Mlawi, ndio waliopinga jambo hili.

16Basi watu wa uhamishoni wakafanya kama ilivyokuwa imependekezwa. Kuhani Ezra akachagua wanaume waliokuwa viongozi wa jamaa, mmoja kutoka kila mgawanyo wa jamaa, nao wote wakachaguliwa kwa majina. Katika siku ya kwanza ya mwezi wa kumi waliketi kuchunguza mashauri hayo. 17Katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza wakawa wamemaliza kushughulikia wanaume wote waliokuwa wameoa wanawake wa kigeni.

Wenye Hatia Ya Kuoa Wake Wa Kigeni

1810:18 Ezr 5:2; Amu 3:6; Zek 6:1Miongoni mwa wazao wa makuhani, wafuatao walikuwa wameoa wanawake wa kigeni:

Kutoka wazao wa Yeshua mwana wa Yosadaki na ndugu zake: Maaseya, Eliezeri, Yaribu na Gedalia. 1910:19 2Fal 10:15; Law 5:15; 6:4-6; 1Nya 29:24; 2Nya 30:8; Gal 2:9; Mit 22:26(Wote walitoa nadhiri kwa kuandika kwa mikono yao kuwafukuza wake zao, kwa hatia yao, kila mmoja akatoa kondoo dume kutoka kundini mwake kama sadaka ya hatia.)

2010:20 1Nya 24:14Kutoka wazao wa Imeri:

Hanani na Zebadia.

2110:21 1Nya 24:8Kutoka wazao wa Harimu:

Maaseya, Eliya, Shemaya, Yehieli na Uzia.

2210:22 1Nya 9:12Kutoka wazao wa Pashuri:

Elioenai, Maaseya, Ishmaeli, Nethaneli, Yozabadi na Elasa.

2310:23 Neh 8:7; 9:4Miongoni mwa Walawi:

Yozabadi, Shimei, Kelaya (ndiye Kelita), Pethahia, Yuda na Eliezeri.

2410:24 Neh 3:1; 12:10Kutoka waimbaji:

Eliashibu.

Kutoka mabawabu:

Shalumu, Telemu na Uri.

2510:25 Ezr 3:2; 8:3; Neh 7:13Miongoni mwa Waisraeli wengine:

Kutoka wazao wa Paroshi:

Ramia, Izia, Malkiya, Miyamini, Eleazari, Malkiya na Benaya.

26Kutoka wazao wa Elamu:

Matania, Zekaria, Yehieli, Abdi, Yeremothi na Eliya.

27Kutoka wazao wa Zatu:

Elioenai, Eliashibu, Matania, Yeremothi, Zabadi na Aziza.

28Kutoka uzao wa Bebai:

Yehohanani, Hanania, Zabai na Athlai.

29Kutoka wazao wa Bani:

Meshulamu, Maluki, Adaya, Yashubu, Sheali na Yeremothi.

30Kutoka wazao wa Pahath-Moabu:

Adna, Kelali, Benaya, Maaseya, Matania, Bezaleli, Binui na Manase.

31Kutoka wazao wa Harimu:

Eliezeri, Ishiya, Malkiya, Shemaya, Shimeoni, 32Benyamini, Maluki, na Shemaria.

33Kutoka wazao wa Hashumu:

Matenai, Matata, Zabadi, Elifeleti, Yeremai, Manase na Shimei.

34Kutoka wazao wa Bani:

Maadai, Amramu, Ueli, 35Benaya, Bedeya, Keluhi, 36Vania, Meremothi, Eliashibu, 37Matania, Matenai na Yaasu.

38Kutoka wazao wa Binui:

Shimei, 39Shelemia, Nathani, Adaya, 40Maknadebai, Shashai, Sharai, 41Azareli, Shelemia, Shemaria, 42Shalumu, Amaria na Yosefu.

4310:43 Ezr 2:29; Hes 32:38Kutoka wazao wa Nebo:

Yeieli, Matithia, Zabadi, Zebina, Yadai, Yoeli na Benaya.

4410:44 Mwa 6:2-5; Kut 23:2; Kum 7:3Hawa wote walikuwa wameoa wanawake wa kigeni, na baadhi yao walikuwa wamezaa nao watoto.

New International Reader’s Version

Ezra 10:1-44

The People Admit They Have Sinned

1Ezra was praying and admitting to God that his people had sinned. He was weeping and throwing himself down in front of the house of God. Then a large crowd of Israelites gathered around him. Men, women and children were there. They too wept bitterly. 2Shekaniah spoke to Ezra. Shekaniah was the son of Jehiel. He belonged to the family line of Elam. Shekaniah said, “We haven’t been faithful to our God. We’ve married women from the nations around us. In spite of that, there is still hope for Israel. 3So let’s make a covenant in front of our God. Let’s promise to send away all these women and their children. That’s what you have advised us to do. Those who respect our God’s commands have given us the same advice. We want to do what the Law says. 4Get up, Ezra. This matter is in your hands. Do what you need to. We will be behind you all the way. Be brave and do it.”

5So Ezra got up. He made the leading priests and Levites and all the Israelites make a promise. He made them promise they would do what Shekaniah had suggested. And they made that promise. 6Then Ezra left the house of God. He went to Jehohanan’s room. Jehohanan was the son of Eliashib. While Ezra was there, he didn’t eat any food. He didn’t drink any water. That’s because he was filled with sadness. He mourned because the people weren’t faithful to the Lord’s commands. Those people were the ones who had returned from the land of Babylon.

7Then an announcement was sent all through Judah and Jerusalem. All the people who had returned were told to gather together in Jerusalem. 8They were supposed to come there before three days had passed. If they didn’t, they would lose all their property. They would also be removed from the community of those who had returned. That’s what the officials and elders had decided.

9Before the three days were over, all the men of Judah and Benjamin had gathered together in Jerusalem. It was the 20th day of the ninth month. They were sitting in the open area in front of the house of God. They were very upset by what they knew would happen. And they were upset because it was raining. 10Then Ezra the priest stood up. He said, “You haven’t been faithful to the Lord. You have married women from other lands. So you have added to Israel’s guilt. 11Now honor the Lord, the God of your people. Then do what he wants you to do. Separate yourselves from the nations around you. Send away your wives from other lands.”

12The whole community answered with a loud voice. They said, “You are right! We must do as you say. 13But there are a lot of people here. And it’s the rainy season. So we can’t stand outside. Besides, this matter can’t be taken care of in just a day or two. That’s because we have sinned terribly by what we’ve done. 14Our officials can act for the whole community. Have everyone in our towns who has married a woman from another land come at a certain time. Tell them to come together with the elders and judges of each town. Then our God will no longer be angry with us concerning this whole matter.” 15Only a few men opposed that. They included Jonathan and Jahzeiah. Meshullam and Shabbethai the Levite joined them. Jonathan was the son of Asahel. Jahzeiah was the son of Tikvah.

16So those who had returned did what had been suggested. Ezra the priest chose some family leaders. There was one from each family group. All of them were chosen by name. They sat down to check out each case. They started on the first day of the tenth month. 17By the first day of the first month they were finished. They had handled all the cases of the men who had married women from other lands.

A List of Those Who Had Married Women From Other Lands

18Among the family lines of the priests, here are the men who had married women from other lands.

Maaseiah, Eliezer, Jarib and Gedaliah

came from the family line of Joshua and his brothers. Joshua was the son of Jozadak. 19All of them made a firm promise to send their wives away. Each of these men brought a ram from his flock as a guilt offering.

20Hanani and Zebadiah

came from the family line of Immer.

21Maaseiah and Elijah

came from the family line of Harim. So did Shemaiah, Jehiel and Uzziah.

22Elioenai, Maaseiah and Ishmael

came from the family line of Pashhur. So did Nethanel, Jozabad and Elasah.

23Among the Levites, here are the men who had married women from other lands.

There were Jozabad, Shimei and Kelaiah. There were also Pethahiah, Judah and Eliezer. Kelaiah’s other name was Kelita.

24Eliashib

came from the musicians.

Shallum, Telem and Uri

came from the men who guarded the temple gates.

25Among the other Israelites, here are the men who had married women from other lands.

Ramiah, Izziah, Malkijah and Mijamin

came from the family line of Parosh. So did Eleazar, Malkijah and Benaiah.

26Mattaniah, Zechariah and Jehiel

came from the family line of Elam. So did Abdi, Jeremoth and Elijah.

27Elioenai, Eliashib and Mattaniah

came from the family line of Zattu. So did Jeremoth, Zabad and Aziza.

28Jehohanan, Hananiah, Zabbai and Athlai

came from the family line of Bebai.

29Meshullam, Malluk and Adaiah

came from the family line of Bani. So did Jashub, Sheal and Jeremoth.

30Adna, Kelal, Benaiah and Maaseiah

came from the family line of Pahath-Moab. So did Mattaniah, Bezalel, Binnui and Manasseh.

31Eliezer, Ishijah, Malkijah, Shemaiah and Shimeon

came from the family line of Harim. 32So did Benjamin, Malluk and Shemariah.

33Mattenai, Mattattah, Zabad and Eliphelet

came from the family line of Hashum. So did Jeremai, Manasseh and Shimei.

34Maadai, Amram and Uel

came from the family line of Bani. 35So did Benaiah, Bedeiah, Keluhi, 36Vaniah, Meremoth, Eliashib, 37Mattaniah, Mattenai and Jaasu.

38Shimei

came from the family line of Binnui. 39So did Shelemiah, Nathan, Adaiah, 40Maknadebai, Shashai, Sharai, 41Azarel, Shelemiah, Shemariah, 42Shallum, Amariah and Joseph.

43Jeiel, Mattithiah, Zabad and Zebina

came from the family line of Nebo. So did Jaddai, Joel and Benaiah.

44All these men had married women from other lands. Some of them had even had children by those wives.