Ezra 10 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ezra 10:1-44

Toba Ya Watu

110:1 2Nya 20:9; Dan 9:20Wakati Ezra alipokuwa anaomba na kuungama, huku akilia na kujitupa chini mbele ya nyumba ya Mungu, umati mkubwa wa Waisraeli, wanaume, wanawake na watoto walikusanyika kumzunguka. Nao pia wakalia sana. 210:2 Ezr 9:2; Kut 34:13; Neh 13:27; Kum 30:8-10Kisha Shekania mwana wa Yehieli, mmoja wa wazao wa Elamu, akamwambia Ezra, “Tumekosa uaminifu kwa Mungu wetu kwa kuoa wanawake wa kigeni kutoka mataifa yanayotuzunguka. Lakini pamoja na hili, bado liko tumaini kwa ajili ya Israeli. 310:3 2Fal 11:17; 2Nya 34:31; Kut 34:16; Kum 7:2-3; Ezr 9:4; Za 119:53, 120; Isa 66:2Sasa na tufanye agano mbele za Mungu wetu kuwafukuza hawa wanawake wote pamoja na watoto wao, kulingana na maonyo ya bwana wangu pamoja na wale ambao wanaogopa amri za Mungu wetu. Hili na lifanyike sawasawa na hii Sheria. 410:4 1Nya 28:10; Isa 35:3-4Inuka, suala hili lipo mikononi mwako. Sisi tutaungana nawe, uwe na ujasiri ukatende hili.”

510:5 Neh 5:12; 13:25Basi Ezra akainuka na kuwaapisha makuhani viongozi, Walawi na Israeli yote kufanya lile lililokuwa limependekezwa. Nao wakaapa. 610:6 Kum 9:18; Yn 3:7; Za 102:4Ndipo Ezra akaondoka hapo mbele ya nyumba ya Mungu akaenda kwenye chumba cha Yehohanani mwana wa Eliashibu. Wakati alipokuwa hapo, hakula chakula wala hakunywa maji, kwa sababu aliendelea kuomboleza kuhusu kukosa uaminifu kwa watu wa uhamishoni.

7Ndipo lilipotolewa tangazo Yuda yote na Yerusalemu kwa watu wote waliokuwa uhamishoni kukusanyika Yerusalemu. 810:8 Law 27:28; Yos 6:19Yeyote ambaye hangejitokeza kwa muda wa siku tatu angepoteza mali yake yote, kulingana na uamuzi wa maafisa na wazee, naye mtu huyo angefukuzwa kutoka kusanyiko la watu waliokuwa uhamishoni.

910:9 1Sam 12:18; Ezr 1:5Katika muda wa siku tatu, watu wote wa Yuda na Benyamini wakawa wamekusanyika huko Yerusalemu. Kwenye siku ya ishirini ya mwezi wa tisa, watu wote walikuwa wameketi ndani ya uwanja mbele ya nyumba ya Mungu, wakiwa na majonzi mno kwa tukio hilo na kwa sababu ya mvua kubwa. 10Ndipo Kuhani Ezra aliposimama akawaambia, “Mmekosa uaminifu, mmeoa wanawake wa kigeni, mkaongezea hatia ya Israeli. 1110:11 Kum 24:1; Mit 28:13; Mal 2:10-16; Yer 3:13; Isa 1:16-17; Rum 12:2Sasa tubuni kwa Bwana, Mungu wa baba zenu mkafanye mapenzi yake. Jitengeni na mataifa wanaowazunguka na wake zenu wa kigeni.”

1210:12 Yos 6:5Kusanyiko lote likajibu kwa sauti kubwa: “Uko sawa kabisa! Ni lazima tufanye kama unavyosema. 13Lakini hapa pana watu wengi na ni wakati wa mvua, hivyo hatuwezi kusimama nje. Hata hivyo, shauri hili haliwezi kumalizika kwa siku moja au mbili, kwa sababu tumefanya dhambi kubwa katika jambo hili. 1410:14 Kum 16:18; Hes 25:4; 2Nya 30:8; 2Fal 23:26; 2Nya 28:11-13; 29:10; 30:8; Za 78:38; Isa 12:1Maafisa wetu na wafanye kwa niaba ya kusanyiko lote. Kisha kila mmoja katika miji yetu ambaye ameoa mwanamke wa kigeni aje kwa wakati uliopangwa, akiwa pamoja na wazee na waamuzi wa kila mji, hadi hasira kali ya Mungu wetu katika shauri hili itakapoondolewa kwetu.” 1510:15 Neh 11:16Yonathani mwana wa Asaheli na Yazeya mwana wa Tikwa peke yao, wakiungwa mkono na Meshulamu na Shabethai Mlawi, ndio waliopinga jambo hili.

16Basi watu wa uhamishoni wakafanya kama ilivyokuwa imependekezwa. Kuhani Ezra akachagua wanaume waliokuwa viongozi wa jamaa, mmoja kutoka kila mgawanyo wa jamaa, nao wote wakachaguliwa kwa majina. Katika siku ya kwanza ya mwezi wa kumi waliketi kuchunguza mashauri hayo. 17Katika siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza wakawa wamemaliza kushughulikia wanaume wote waliokuwa wameoa wanawake wa kigeni.

Wenye Hatia Ya Kuoa Wake Wa Kigeni

1810:18 Ezr 5:2; Amu 3:6; Zek 6:1Miongoni mwa wazao wa makuhani, wafuatao walikuwa wameoa wanawake wa kigeni:

Kutoka wazao wa Yeshua mwana wa Yosadaki na ndugu zake: Maaseya, Eliezeri, Yaribu na Gedalia. 1910:19 2Fal 10:15; Law 5:15; 6:4-6; 1Nya 29:24; 2Nya 30:8; Gal 2:9; Mit 22:26(Wote walitoa nadhiri kwa kuandika kwa mikono yao kuwafukuza wake zao, kwa hatia yao, kila mmoja akatoa kondoo dume kutoka kundini mwake kama sadaka ya hatia.)

2010:20 1Nya 24:14Kutoka wazao wa Imeri:

Hanani na Zebadia.

2110:21 1Nya 24:8Kutoka wazao wa Harimu:

Maaseya, Eliya, Shemaya, Yehieli na Uzia.

2210:22 1Nya 9:12Kutoka wazao wa Pashuri:

Elioenai, Maaseya, Ishmaeli, Nethaneli, Yozabadi na Elasa.

2310:23 Neh 8:7; 9:4Miongoni mwa Walawi:

Yozabadi, Shimei, Kelaya (ndiye Kelita), Pethahia, Yuda na Eliezeri.

2410:24 Neh 3:1; 12:10Kutoka waimbaji:

Eliashibu.

Kutoka mabawabu:

Shalumu, Telemu na Uri.

2510:25 Ezr 3:2; 8:3; Neh 7:13Miongoni mwa Waisraeli wengine:

Kutoka wazao wa Paroshi:

Ramia, Izia, Malkiya, Miyamini, Eleazari, Malkiya na Benaya.

26Kutoka wazao wa Elamu:

Matania, Zekaria, Yehieli, Abdi, Yeremothi na Eliya.

27Kutoka wazao wa Zatu:

Elioenai, Eliashibu, Matania, Yeremothi, Zabadi na Aziza.

28Kutoka uzao wa Bebai:

Yehohanani, Hanania, Zabai na Athlai.

29Kutoka wazao wa Bani:

Meshulamu, Maluki, Adaya, Yashubu, Sheali na Yeremothi.

30Kutoka wazao wa Pahath-Moabu:

Adna, Kelali, Benaya, Maaseya, Matania, Bezaleli, Binui na Manase.

31Kutoka wazao wa Harimu:

Eliezeri, Ishiya, Malkiya, Shemaya, Shimeoni, 32Benyamini, Maluki, na Shemaria.

33Kutoka wazao wa Hashumu:

Matenai, Matata, Zabadi, Elifeleti, Yeremai, Manase na Shimei.

34Kutoka wazao wa Bani:

Maadai, Amramu, Ueli, 35Benaya, Bedeya, Keluhi, 36Vania, Meremothi, Eliashibu, 37Matania, Matenai na Yaasu.

38Kutoka wazao wa Binui:

Shimei, 39Shelemia, Nathani, Adaya, 40Maknadebai, Shashai, Sharai, 41Azareli, Shelemia, Shemaria, 42Shalumu, Amaria na Yosefu.

4310:43 Ezr 2:29; Hes 32:38Kutoka wazao wa Nebo:

Yeieli, Matithia, Zabadi, Zebina, Yadai, Yoeli na Benaya.

4410:44 Mwa 6:2-5; Kut 23:2; Kum 7:3Hawa wote walikuwa wameoa wanawake wa kigeni, na baadhi yao walikuwa wamezaa nao watoto.

King James Version

Ezra 10:1-44

1Now when Ezra had prayed, and when he had confessed, weeping and casting himself down before the house of God, there assembled unto him out of Israel a very great congregation of men and women and children: for the people wept very sore.10.1 wept…: Heb. wept a great weeping 2And Shechaniah the son of Jehiel, one of the sons of Elam, answered and said unto Ezra, We have trespassed against our God, and have taken strange wives of the people of the land: yet now there is hope in Israel concerning this thing. 3Now therefore let us make a covenant with our God to put away all the wives, and such as are born of them, according to the counsel of my lord, and of those that tremble at the commandment of our God; and let it be done according to the law.10.3 to put…: Heb. to bring forth 4Arise; for this matter belongeth unto thee: we also will be with thee: be of good courage, and do it. 5Then arose Ezra, and made the chief priests, the Levites, and all Israel, to swear that they should do according to this word. And they sware.

6¶ Then Ezra rose up from before the house of God, and went into the chamber of Johanan the son of Eliashib: and when he came thither, he did eat no bread, nor drink water: for he mourned because of the transgression of them that had been carried away. 7And they made proclamation throughout Judah and Jerusalem unto all the children of the captivity, that they should gather themselves together unto Jerusalem; 8And that whosoever would not come within three days, according to the counsel of the princes and the elders, all his substance should be forfeited, and himself separated from the congregation of those that had been carried away.10.8 forfeited: Heb. devoted

9¶ Then all the men of Judah and Benjamin gathered themselves together unto Jerusalem within three days. It was the ninth month, on the twentieth day of the month; and all the people sat in the street of the house of God, trembling because of this matter, and for the great rain.10.9 the great…: Heb. the showers 10And Ezra the priest stood up, and said unto them, Ye have transgressed, and have taken strange wives, to increase the trespass of Israel.10.10 have taken: Heb. have caused to dwell, or, have brought back 11Now therefore make confession unto the LORD God of your fathers, and do his pleasure: and separate yourselves from the people of the land, and from the strange wives. 12Then all the congregation answered and said with a loud voice, As thou hast said, so must we do. 13But the people are many, and it is a time of much rain, and we are not able to stand without, neither is this a work of one day or two: for we are many that have transgressed in this thing.10.13 we are many…: or, we have greatly offended in this thing 14Let now our rulers of all the congregation stand, and let all them which have taken strange wives in our cities come at appointed times, and with them the elders of every city, and the judges thereof, until the fierce wrath of our God for this matter be turned from us.10.14 for this…: or, till this matter be dispatched

15¶ Only Jonathan the son of Asahel and Jahaziah the son of Tikvah were employed about this matter: and Meshullam and Shabbethai the Levite helped them.10.15 were…: Heb. stood 16And the children of the captivity did so. And Ezra the priest, with certain chief of the fathers, after the house of their fathers, and all of them by their names, were separated, and sat down in the first day of the tenth month to examine the matter. 17And they made an end with all the men that had taken strange wives by the first day of the first month.

18¶ And among the sons of the priests there were found that had taken strange wives: namely, of the sons of Jeshua the son of Jozadak, and his brethren; Maaseiah, and Eliezer, and Jarib, and Gedaliah. 19And they gave their hands that they would put away their wives; and being guilty, they offered a ram of the flock for their trespass. 20And of the sons of Immer; Hanani, and Zebadiah. 21And of the sons of Harim; Maaseiah, and Elijah, and Shemaiah, and Jehiel, and Uzziah. 22And of the sons of Pashur; Elioenai, Maaseiah, Ishmael, Nethaneel, Jozabad, and Elasah. 23Also of the Levites; Jozabad, and Shimei, and Kelaiah, (the same is Kelita,) Pethahiah, Judah, and Eliezer. 24Of the singers also; Eliashib: and of the porters; Shallum, and Telem, and Uri. 25Moreover of Israel: of the sons of Parosh; Ramiah, and Jeziah, and Malchiah, and Miamin, and Eleazar, and Malchijah, and Benaiah. 26And of the sons of Elam; Mattaniah, Zechariah, and Jehiel, and Abdi, and Jeremoth, and Eliah. 27And of the sons of Zattu; Elioenai, Eliashib, Mattaniah, and Jeremoth, and Zabad, and Aziza. 28Of the sons also of Bebai; Jehohanan, Hananiah, Zabbai, and Athlai. 29And of the sons of Bani; Meshullam, Malluch, and Adaiah, Jashub, and Sheal, and Ramoth. 30And of the sons of Pahath-moab; Adna, and Chelal, Benaiah, Maaseiah, Mattaniah, Bezaleel, and Binnui, and Manasseh. 31And of the sons of Harim; Eliezer, Ishijah, Malchiah, Shemaiah, Shimeon, 32Benjamin, Malluch, and Shemariah. 33Of the sons of Hashum; Mattenai, Mattathah, Zabad, Eliphelet, Jeremai, Manasseh, and Shimei. 34Of the sons of Bani; Maadai, Amram, and Uel, 35Benaiah, Bedeiah, Chelluh, 36Vaniah, Meremoth, Eliashib, 37Mattaniah, Mattenai, and Jaasau, 38And Bani, and Binnui, Shimei, 39And Shelemiah, and Nathan, and Adaiah, 40Machnadebai, Shashai, Sharai,10.40 Machnadebai: or, Mabnadebai, according to some copies 41Azareel, and Shelemiah, Shemariah, 42Shallum, Amariah, and Joseph. 43Of the sons of Nebo; Jeiel, Mattithiah, Zabad, Zebina, Jadau, and Joel, Benaiah. 44All these had taken strange wives: and some of them had wives by whom they had children.