Ezekieli 7 – NEN & NIVUK

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ezekieli 7:1-27

Mwisho Umewadia

1Neno la Bwana likanijia kusema: 27:2 Amo 8:2-10; Ufu 20:8; Mao 4:18“Mwanadamu, hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo kwa nchi ya Israeli: Mwisho! Mwisho umekuja juu ya pembe nne za nchi. 37:3 Eze 18:30; Mwa 6:13Sasa mwisho umekuja juu yenu nami nitamwaga hasira yangu dhidi yenu. Nitawahukumu sawasawa na matendo yenu na kuwalipiza kwa ajili ya desturi zenu zote za kuchukiza. 47:4 Yer 13:14; Eze 5:11; 23:49Sitawaonea huruma wala sitawarehemu, hakika nitalipiza kwa ajili ya matendo yenu na desturi zenu za machukizo miongoni mwenu. Ndipo mtakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.

57:5 2Fal 21:12“Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Maafa! Maafa ambayo hayajasikiwa yanakuja. 67:6 Eze 39:8Mwisho umewadia! Mwisho umewadia! Umejiinua wenyewe dhidi yenu. Umewadia! 77:7 Sef 1:14; Mal 3:2; 1Pet 4:17; Ay 18:20; Isa 2:12; Amo 5:18-20; Eze 12:23Maangamizi yamekuja juu yenu, ninyi mnaoishi katika nchi. Wakati umewadia, siku imekaribia, kuna hofu kuu ya ghafula, wala si furaha, juu ya milima. 87:8 Hos 5:10; Nah 1:6; Eze 36:19; 14:19; 20:8, 21; 9:8; Isa 42:25Ninakaribia kumwaga ghadhabu yangu juu yenu na kumaliza hasira yangu dhidi yenu, nitawahukumu sawasawa na matendo yenu na kuwalipiza kwa ajili ya desturi zenu zote za machukizo. 97:9 Yer 21:9; Isa 9:13; Eze 5:11; 22:31; Za 39:10Sitawaonea huruma wala sitawarehemu; nitawalipiza sawasawa na matendo yenu na desturi zenu za machukizo miongoni mwenu. Ndipo mtajua kuwa Mimi ndimi Bwana ambaye huwapiga kwa mapigo.

107:10 Za 89:32; Isa 10:5“Siku imefika! Imewadia! Maangamizi yamezuka ghafula, fimbo imechanua majivuno yamechipua! 117:11 Yer 16:6; Sef 1:18; Isa 58:4; Za 55:9Jeuri imeinuka kuwa fimbo ya kuadhibu uovu, hakuna hata mmoja wa hao watu atakayeachwa, hata mmoja wa kundi lile, hakuna utajiri, hakuna chenye thamani. 127:12 Isa 5:13-14; Eze 30:3; Isa 24:2Wakati umewadia, siku imefika. Mnunuzi na asifurahi wala muuzaji asihuzunike, kwa maana ghadhabu iko juu ya kundi lote. 137:13 Law 25:24-25Muuzaji hatajipatia tena ardhi aliyoiuza wakati wote wawili wangali hai, kwa kuwa maono kuhusu kundi lote hayatatanguka. Kwa sababu ya dhambi zao, hakuna hata mmoja atakayeokoa maisha yake. 147:14 Ay 39:24; Yer 25:38Wajapopiga tarumbeta na kuweka kila kitu tayari, hakuna hata mmoja atakayekwenda vitani, kwa maana ghadhabu yangu iko juu ya kundi lote.

157:15 Kum 32:25; Yer 14:18; Mao 1:20; Eze 5:12; 33:27“Nje ni upanga, ndani ni tauni na njaa, wale walioko shambani watakufa kwa upanga, nao wale waliomo mjini njaa na tauni vitawala. 167:16 Mwa 8:8; Isa 59:11; 10:20; Ezr 9:15; Yer 9:19; 41:16; 42:17Wale wote watakaopona na kutoroka watakuwa milimani, wakiomboleza kama hua wa mabondeni, kila mmoja kwa sababu ya dhambi zake. 177:17 2Fal 19:26; Isa 13:7; Dan 6:5; Yer 43:7; Eze 21:7; 22:14Kila mkono utalegea na kila goti litakuwa dhaifu kama maji. 187:18 Isa 15:2-3; Amo 8:10; Za 55:5; Yer 6:26; 4:8; 49:3; 48:37Watavaa nguo ya gunia na kufunikwa na hofu. Nyuso zao zitafunikwa na aibu na nywele za vichwa vyao zitanyolewa. 197:19 Isa 42:25; Sef 1:18; Hos 4:5; Eze 3:20; Mit 11:4; Yoe 1:15; Eze 13:5; 14:3Watatupa fedha yao barabarani, nayo dhahabu yao itakuwa najisi. Fedha yao na dhahabu yao havitaweza kuwaokoa katika siku hiyo ya ghadhabu ya Bwana. Hawatashibisha njaa yao au kujaza matumbo yao kwa hiyo fedha wala dhahabu, kwa sababu imewaponza wajikwae dhambini. 207:20 Eze 5:11; 16:17; Yer 7:30; 10:3; Isa 2:20Walijivunia vito vyao vizuri na kuvitumia kufanya sanamu za machukizo na vinyago vya upotovu. Kwa hiyo nitavifanya vitu hivyo kuwa najisi kwao. 217:21 2Fal 24:13; Hes 14:3Nitavitia vyote mikononi mwa wageni kuwa nyara na kuwa vitu vilivyotekwa mikononi mwa watu waovu wa dunia, nao watavinajisi. 227:22 Yer 2:27; 19:13; Eze 39:23-24; Za 74:7-8Nitageuza uso wangu mbali nao, nao waovu wa dunia watapanajisi mahali pangu pa thamani, wanyangʼanyi watapaingia na kupanajisi.

237:23 2Fal 21:16; Isa 1:15; Za 10:8; Eze 11:6; 22:9; Mwa 6:11“Andaa minyororo, kwa sababu nchi imejaa umwagaji wa damu na mji umejaa udhalimu. 247:24 Mao 2:7; Eze 24:21; 28:7; 2Nya 7:20Nitaleta taifa ovu kuliko yote ili kumiliki nyumba zao, nitakomesha kiburi cha wenye nguvu na mahali pao patakatifu patatiwa unajisi. 257:25 Yer 6:14; 8:11; Eze 13:10-16Hofu ya ghafula itakapokuja, watatafuta amani, lakini haitakuwepo. 267:26 Kum 29:21; 31:17; Yer 4:20; 18:18; Amo 8:11; Mik 3:6; Mal 2:7-9; Isa 47:11; 3:11; Eze 18:20; Za 109:19Maafa juu ya maafa yatakuja, tetesi ya mabaya juu ya tetesi ya mabaya. Watajitahidi kupata maono kutoka kwa nabii, mafundisho ya sheria toka kwa kuhani yatapotea, vivyo hivyo shauri kutoka kwa wazee. 27Mfalme ataomboleza, mwana wa mfalme atavikwa kukata tamaa, nayo mikono ya watu wa nchi itatetemeka. Nitawashughulikia sawasawa na matendo yao na kwa kanuni zao wenyewe nitawahukumu. Ndipo watajua kwamba Mimi ndimi Bwana.”

New International Version – UK

Ezekiel 7:1-27

The end has come

1The word of the Lord came to me: 2‘Son of man, this is what the Sovereign Lord says to the land of Israel:

‘ “The end! The end has come

upon the four corners of the land!

3The end is now upon you,

and I will unleash my anger against you.

I will judge you according to your conduct

and repay you for all your detestable practices.

4I will not look on you with pity;

I will not spare you.

I will surely repay you for your conduct

and for the detestable practices among you.

‘ “Then you will know that I am the Lord.”

5‘This is what the Sovereign Lord says:

‘ “Disaster! Unheard-of7:5 Most Hebrew manuscripts; some Hebrew manuscripts and Syriac Disaster after disaster!

See, it comes!

6The end has come!

The end has come!

It has roused itself against you.

See, it comes!

7Doom has come upon you,

upon you who dwell in the land.

The time has come! The day is near!

There is panic, not joy, on the mountains.

8I am about to pour out my wrath on you

and spend my anger against you.

I will judge you according to your conduct

and repay you for all your detestable practices.

9I will not look on you with pity;

I will not spare you.

I will repay you for your conduct

and for the detestable practices among you.

‘ “Then you will know that it is I the Lord who strikes you.

10‘ “See, the day!

See, it comes!

Doom has burst forth,

the rod has budded,

arrogance has blossomed!

11Violence has arisen,7:11 Or The violent one has become

a rod to punish the wicked.

None of the people will be left,

none of that crowd –

none of their wealth,

nothing of value.

12The time has come!

The day has arrived!

Let not the buyer rejoice

nor the seller grieve,

for my wrath is on the whole crowd.

13The seller will not recover

the property that was sold –

as long as both buyer and seller live.

For the vision concerning the whole crowd

will not be reversed.

Because of their sins, not one of them

will preserve their life.

14‘ “They have blown the trumpet,

they have made all things ready,

but no-one will go into battle,

for my wrath is on the whole crowd.

15Outside is the sword;

inside are plague and famine.

Those in the country

will die by the sword;

those in the city

will be devoured by famine and plague.

16The fugitives who escape

will flee to the mountains.

Like doves of the valleys,

they will all moan,

each for their own sins.

17Every hand will go limp;

every leg will be wet with urine.

18They will put on sackcloth

and be clothed with terror.

Every face will be covered with shame,

and every head will be shaved.

19‘ “They will throw their silver into the streets,

and their gold will be treated as a thing unclean.

Their silver and gold

will not be able to deliver them

in the day of the Lord’s wrath.

It will not satisfy their hunger

or fill their stomachs,

for it has caused them to stumble into sin.

20They took pride in their beautiful jewellery

and used it to make their detestable idols.

They made it into vile images;

therefore I will make it a thing unclean for them.

21I will give their wealth as plunder to foreigners

and as loot to the wicked of the earth,

who will defile it.

22I will turn my face away from the people,

and robbers will desecrate the place I treasure.

They will enter it

and will defile it.

23‘ “Prepare chains!

For the land is full of bloodshed,

and the city is full of violence.

24I will bring the most wicked of nations

to take possession of their houses.

I will put an end to the pride of the mighty,

and their sanctuaries will be desecrated.

25When terror comes,

they will seek peace in vain.

26Calamity upon calamity will come,

and rumour upon rumour.

They will go searching for a vision from the prophet,

priestly instruction in the law will cease,

the counsel of the elders will come to an end.

27The king will mourn,

the prince will be clothed with despair,

and the hands of the people of the land will tremble.

I will deal with them according to their conduct,

and by their own standards I will judge them.

‘ “Then they will know that I am the Lord.” ’