Ezekieli 5 – NEN & CCBT

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ezekieli 5:1-17

Upanga Dhidi Ya Yerusalemu

15:1 Law 21:5; Isa 7:20; Eze 44:20; Hes 6:5; 2Sam 10:14“Mwanadamu, sasa chukua upanga mkali na uutumie kama wembe wa kinyozi ili kunyolea nywele za kichwa chako na ndevu zako. Kisha uchukue mizani ya kupimia ukazigawanye nywele hizo. 25:2 Law 26:33; Yer 39:1-2; Zek 13:8; Yer 21:10; Eze 15:7; Yer 13:24; 9:16Wakati siku zako za kuzingirwa zitakapokwisha, choma theluthi moja ya hizo nywele zako kwa moto ndani ya mji. Chukua theluthi nyingine ya hizo nywele uzipige kwa upanga kuuzunguka mji wote na theluthi nyingine ya mwisho utaitawanya kwa upepo. Kwa kuwa nitawafuatia kwa upanga uliofutwa. 35:3 Yer 40:6; 39:10; 2Fal 25:12; Za 74:11Lakini chukua nywele chache uzifungie ndani ya pindo la vazi lako. 45:4 Eze 10:7; 15:7Tena chukua nywele nyingine chache uzitupe motoni uziteketeze. Moto utaenea kutoka humo na kufika katika nyumba yote ya Israeli.

55:5 Kum 4:6; Mao 1:1; Eze 16:14“Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Huu ndio Yerusalemu ambao nimeuweka katikati ya mataifa ukiwa umezungukwa na nchi pande zote. 65:6 Neh 9:17; Zek 7:11; Rum 1:25; Eze 16:16; 2Fal 17:15; Yer 11:10Lakini katika uovu wake umeasi sheria na amri zangu kuliko mataifa na nchi zinazouzunguka. Umeasi sheria zangu wala haukufuata amri zangu.

75:7 2Fal 21:9; 2Nya 33:9; Yer 2:10-11“Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ninyi mmekuwa wakaidi kuliko mataifa yanayowazunguka na hamkufuata amri zangu wala kuzishika sheria zangu. Wala hamkuweza hata kuzifuata kawaida za mataifa yanayowazunguka.

85:8 Yer 21:5; Zek 14:2; Yer 24:9; Eze 11:9; 15:7“Kwa hiyo, hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo, Mimi mwenyewe, niko kinyume nanyi Yerusalemu, nitawapiga kwa adhabu yangu mbele ya mataifa. 95:9 Dan 9:12; Amo 3:2; Mt 24:21Kwa ajili ya sanamu zenu zote za machukizo, nitawafanyia kile ambacho kamwe sijawafanyia kabla wala kamwe sitawafanyia tena. 105:10 Law 26:29; Mao 2:20; Yer 13:14; Zek 2:6; Za 44:11; Eze 12:14Kwa hiyo katikati yenu baba watakula watoto wao na watoto watakula baba zao. Nitawapiga kwa adhabu, nami nitawatawanya watu wenu walionusurika pande zote za dunia. 115:11 Eze 7:20; 8:6; 2Nya 36:14; Eze 11:18-21; Yer 16:18; Ay 27:22; Hes 14:21; Law 15:2; 15:31; Mao 2:17Kwa hiyo hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, kwa kuwa mmenajisi mahali pangu patakatifu kwa sanamu zenu mbaya sana na desturi zenu za machukizo, mimi mwenyewe nitaondoa fadhili zangu kwenu. 125:12 Ufu 6:8; Za 107:39; Eze 12:14; Zek 13:8; Eze 6:11-12; Yer 21:9; 13:24Theluthi ya watu wako watakufa kwa tauni au kwa njaa humu ndani yako, theluthi nyingine itaanguka kwa upanga nje ya kuta zako, nayo theluthi nyingine nitaitawanya kwenye pande nne kuwafuatia kwa upanga uliofutwa.

135:13 2Nya 12:7; Ay 20:23; Isa 1:24; Mao 4:11; Eze 21:17; 24:13; Hos 10:10“Ndipo hasira yangu itakapokoma na ghadhabu yangu dhidi yao itatulia, nami nitakuwa nimelipiza kisasi. Baada ya kuimaliza ghadhabu yangu juu yao, watajua kuwa mimi Bwana nimenena katika wivu wangu.

145:14 Mik 3:12; Isa 64:11; Neh 2:17; Za 74:3-10; Eze 22:4; Dan 9:16“Nitakuangamiza na kukufanya kitu cha kudharauliwa miongoni mwa mataifa yanayokuzunguka, machoni pa watu wote wapitao karibu nawe. 155:15 Kum 28:20; 1Fal 9:7; Yer 23:40; Eze 25:17; Mao 2:15; Isa 43:28; Yer 22:8-9Utakuwa kitu cha kudharauliwa na cha aibu, cha dhihaka, ovyo na kitu cha kutisha kwa mataifa yanayokuzunguka, nitakapokupiga kwa adhabu yangu katika hasira na ghadhabu yangu kwa kukukemea kwa ukali. Mimi Bwana nimesema. 165:16 Law 26:26; Kum 32:24; Eze 14:21Nitakapokupiga kwa mishale yangu ya kufisha na yenye kuharibu ya njaa, nitaipiga ili kukuangamiza. Nitaleta njaa zaidi na zaidi juu yako na kukomesha upatikanaji wa chakula kwako. 175:17 Eze 38:23; Law 26:25; Eze 28:22Nitapeleka njaa na wanyama wa mwituni dhidi yenu, navyo vitawaacha bila watoto. Tauni na umwagaji wa damu utapita katikati yenu, nami nitaleta upanga juu yenu. Mimi Bwana nimenena haya.”

Chinese Contemporary Bible (Traditional)

以西結書 5:1-17

1「人子啊,去拿一把快刀當作剃頭刀,剃掉你的頭髮和鬍鬚,然後用天平把鬚髮平均分成三份。 2圍城期滿後,你要把三分之一的鬚髮焚燒在城中,三分之一在城的四周用刀砍斷,三分之一要揚在風中吹散,因為我要拔刀追殺他們。 3你要從鬚髮中取出幾縷用衣服包上, 4再從中取出幾根丟在火裡焚燒,必有火從這裡燃起,蔓延到整個以色列。」

5主耶和華說:「這就是耶路撒冷!我把她安置在萬邦的中央,使列國環繞著她。 6但她違背我的典章,作惡甚於列邦,觸犯我的律例甚於她周圍的列國。他們拒絕我的典章,不遵守我的律例。」 7所以主耶和華說:「你們比周圍的國家更混亂不堪,你們沒有遵行我的律例,不謹守我的典章,連周圍的國家都不如。」 8因此主耶和華這樣說:「看啊,我要對付你們,我必在列國面前審判你們。 9因為你們一切的惡行,我必向你們施行空前絕後的懲罰。 10在你們中間,父親要吃自己的兒子,兒子要吃自己的父親。我必懲罰你們,把你們餘下的人分散到各地各方。」 11主耶和華說:「因為你們用一切可憎的偶像和惡行玷污我的聖所,我憑我的永恆起誓,我必毫不留情地剷除你們。 12你們三分之一的人要死於饑荒瘟疫,三分之一的人要死於刀下,我必把其餘的三分之一分散到各地各方,並拔刀追殺他們。 13這樣,我對你們的怒氣才會發完,我才會息怒。我把烈怒傾倒在你們身上的時候,你們就會知道我耶和華的話是出於痛恨不貞。 14我必使你們的家園在周圍的列國中,在路人眼前成為荒涼之地,使你們飽受羞辱。 15當我在氣憤和烈怒中嚴厲地審判你們時,你們在各國必受羞辱和嘲諷,成為警戒,下場可怕。這是我耶和華說的。 16我要向你們射出饑荒的毒箭,破壞和毀滅你們,並且使饑荒越來越嚴重,斷絕你們的糧源。 17我必讓饑荒和猛獸來侵害你們,奪走你們的兒女,使你們飽受瘟疫、暴行和刀劍之災,這是我耶和華說的。」