Ezekieli 46 – NEN & NUB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ezekieli 46:1-24

Sheria Nyingine Mbalimbali

146:1 Eze 40:19; 1Nya 9:18; Isa 66:23“ ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Lango la ukumbi wa ndani linaloelekea upande wa mashariki litakuwa linafungwa kwa siku sita za juma, ila siku ya Sabato na siku ya Mwezi Mwandamo litafunguliwa. 246:2 Eze 44:3; Mt 25:10; Eze 40:39Mkuu anayetawala ataingia kupitia baraza ya njia ya lango la ukumbi na kusimama karibu na nguzo ya lango. Makuhani watatoa sadaka za mkuu anayetawala za kuteketezwa na sadaka za amani. Mkuu anayetawala atasujudu kwenye kizingiti cha njia ya lango, kisha atatoka nje, lakini lango halitafungwa mpaka jioni. 346:3 Za 100:4; Lk 1:10Siku za Sabato na za Mwezi mwandamo watu wote wa nchi wataabudu mbele za Bwana penye lile ingilio la ile njia. 446:4 Hes 28:5, 9, 11, 12; Eze 45:17Sadaka ya kuteketezwa aletazo mkuu anayetawala kwa Bwana siku ya Sabato itakuwa ni wana-kondoo sita na kondoo dume mmoja, wote wasiwe na dosari. 546:5 Eze 45:24; Hes 28:12Sadaka ya nafaka inayotolewa pamoja na huyo kondoo dume itakuwa efa moja na sadaka ya nafaka inayotolewa na hao wana-kondoo itakuwa kiasi apendacho mtu pamoja na hini ya mafuta kwa kila efa. 646:6 Hes 10:10; Law 22:20Siku ya mwezi mwandamo atatoa fahali mchanga, wana-kondoo sita na kondoo dume, wote wasiwe na dosari. 746:7 Eze 45:24Atatoa kuwa sadaka ya nafaka efa moja pamoja na fahali mmoja, efa moja na kondoo dume mmoja na pamoja na wana-kondoo kama atakavyo kutoa, pamoja na hini ya mafuta kwa kila efa. 846:8 Eze 46:2Wakati mkuu anayetawala aingiapo, atapitia kwenye baraza ya njia ya lango, naye atatoka nje kwa njia hiyo hiyo.

946:9 Kut 23:14; 34:20; Kum 16:16“ ‘Wakati watu wa nchi wanapokuja mbele za Bwana katika sikukuu zilizoamriwa, yeyote aingiaye kwa lango la kaskazini kuabudu atatoka nje kwa lango la kusini na yeyote aingiaye kwa lango la kusini atatoka nje kwa lango la kaskazini. Hakuna mtu yeyote atakayerudi kwa kupitia lango lile aliloingilia, lakini kila mmoja atatoka nje kwa lango linalokabili lile aliloingilia. 1046:10 2Sam 6:14-15; Za 42:4Mkuu anayetawala atakuwa miongoni mwao, akiingia nao ndani wanapoingia, naye atatoka nao nje wanapotoka.

1146:11 Eze 46:5“ ‘Kwenye sikukuu na kwenye sikukuu zilizoamriwa, sadaka ya nafaka itakuwa efa moja pamoja na fahali mmoja, efa moja pamoja na kondoo dume mmoja, pamoja na idadi ya wana-kondoo kama mtu apendavyo kutoa, pamoja na hini ya mafuta kwa kila efa. 1246:12 Eze 45:17; Gal 2:20; Yn 10:18; Law 7:16Mkuu anayetawala anapotoa sadaka ya hiari kwa Bwana, ikiwa ni sadaka ya kuteketezwa au sadaka ya amani, lango linaloelekea mashariki litafunguliwa kwa ajili yake. Atatoa sadaka yake ya kuteketezwa au sadaka yake ya amani kama afanyavyo katika siku ya Sabato. Kisha atatoka nje, naye akiisha kutoka nje, lango litafungwa.

1346:13 Kut 29:28; Hes 28:3; Za 5:3“ ‘Kila siku utamtoa mwana-kondoo wa mwaka mmoja asiyekuwa na dosari kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana, utaitoa kila siku asubuhi. 1446:14 Dan 8:11; Hes 15:6Pia kila siku asubuhi pamoja na hiyo sadaka utatoa sadaka ya nafaka, ikiwa na sehemu ya sita ya efa pamoja na theluthi moja ya hini46:14 Theluthi moja ya hini ni sawa na lita 1.3. ya mafuta ya kuchanganya na ule unga. Utoaji wa sadaka hii ya nafaka kwa Bwana ni amri ya daima. 1546:15 Kut 29:38-42; Hes 28:5-6Kwa hiyo mwana-kondoo na sadaka ya nafaka na mafuta vitatolewa kila siku asubuhi kwa ajili ya sadaka ya daima ya kuteketezwa.

1646:16 2Nya 21:3“ ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ikiwa mkuu atawalaye atatoa zawadi kutoka kwenye urithi wake na kumpa mmoja wa wanawe, hiyo zawadi itakuwa pia kwa wazao wake, itakuwa mali yao kwa urithi. 1746:17 Law 25:9-10; Isa 61:2Hata hivyo, kama atatoa zawadi kutoka urithi wake na kumpa mmoja wa watumishi wake, mtumishi anaweza kuiweka mpaka mwaka wa uhuru, kisha itarudishwa kwa mkuu anayetawala. Urithi wake ni wa wanawe peke yao, ni mali yao. 1846:18 Law 25:23; Mik 2:1-2; Za 78:72; Isa 8:14; Eze 45:8Mkuu anayetawala hana ruhusa kuchukua urithi wowote wa watu na kuwaondoa kwenye mali zao. Mkuu atawalaye atawapa wanawe urithi wao, kutoka kwenye mali zake mwenyewe, ili kwamba pasiwe na mtu wangu yeyote atakayetengwa na urithi wake.’ ”

1946:19 Eze 42:4-9Kisha mtu yule akanileta kwa kupitia kwenye ingilio lililokuwa kando ya lango mpaka kwenye vyumba vitakatifu vinavyoelekea kaskazini, ambavyo ni vya makuhani, naye akanionyesha mahali fulani upande wa mwisho wa magharibi. 2046:20 Law 6:27; Zek 14:20; Law 2:4-7Akaniambia, “Mahali hapa ndipo makuhani watakapotokosea sadaka ya hatia na sadaka ya dhambi na kuoka sadaka ya nafaka, kuepuka kuzileta katika ukumbi wa nje na kushirikisha utakatifu kwa watu.”

21Baada ya hapo akanileta kwenye ukumbi wa nje na kunizungusha kwenye pembe zake nne, nami nikaona katika kila pembe ya huo ukumbi kulikuwa na ukumbi mwingine. 22Katika pembe nne za huo ukumbi wa nje kulikuwa na kumbi nyingine, zenye urefu wa dhiraa arobaini na upana wake dhiraa thelathini, ambapo hizo kumbi kwenye hizo pembe nne zilikuwa na vipimo vilivyo sawa. 23Mzunguko wa ndani wa hizo kumbi nne ulikuwa na ukingo wa jiwe, zikiwa na sehemu zilizojengwa kwa ajili ya moto kuzunguka chini ya huo ukingo. 2446:24 Eze 46:20; Rum 12:1; 15:16; Ebr 13:16Akaniambia, “Hizi ndizo sehemu za kupikia ambazo wale wanaohudumu kwenye Hekalu watatokosea dhabihu za watu.”

Swedish Contemporary Bible

Hesekiel 46:1-24

Särskilda offer i templet

1Så säger Herren, Herren: Den inre förgårdens östra port ska vara stängd under de sex arbetsdagarna men öppen på sabbaten och nymånadsfesten. 2Fursten ska komma in utifrån genom portens förhus och ställa sig vid dörrposten. Prästerna ska offra hans brännoffer och gemenskapsoffer. Han ska tillbe vid portens tröskel och sedan gå ut. Porten får inte stängas förrän på kvällen. 3Folket i landet ska tillbe Herren vid ingången till denna port på sabbaterna och nymånadsfesterna.

4Det brännoffer som fursten bär fram till Herren på sabbatsdagen ska bestå av sex felfria lamm och en felfri bagge. 5Matoffret som han bär fram ska vara en efa mjöl för baggen och ett mått som han själv bestämmer för lammen, samt en hin olja för varje efa.46:5-7,11,14 För måtten se not till 45:10-14 och 45:24.

6På nymånadsfesten ska han offra en felfri ungtjur, sex lamm och en bagge, alla felfria. 7Som matoffer ska han offra en efa för tjuren, en efa för baggen och för lammen vad han själv bestämmer, samt en hin olja för varje efa.

8När fursten kommer ska han gå in genom portens förhus och ut igen samma väg. 9Men när folket i landet kommer inför Herren vid högtiderna, ska den som har gått in genom norra porten för att tillbe gå ut genom södra porten. Den som har gått in genom södra porten ska gå ut genom den norra. Ingen får gå tillbaka ut genom samma port som han kom in, utan man måste alltid gå ut genom den motsatta porten. 10Fursten ska vara med dem, komma in med dem och gå ut med dem.

11Vid högtider och fester ska matoffret vara en efa mjöl för tjuren, en efa för baggen och så mycket för lammen som han själv bestämmer, samt en hin olja för varje efa. 12När fursten vill bära fram ett frivilligt offer till Herren, ett brännoffer eller ett gemenskapsoffer, ska den östra porten öppnas för honom, så att han kan bära fram sitt brännoffer och gemenskapsoffer precis som på sabbaten. Sedan ska han gå ut igen, och porten ska stängas efter honom.

13Du ska dagligen ge ett årsgammalt felfritt lamm som brännoffer till Herren. Varje morgon ska du offra ett sådant. 14Du ska också som matoffer varje morgon ge en sjättedels efa mjöl och en tredjedels hin olja att fukta mjölet med. Denna förordning för Herrens matoffer ska gälla som en bestående stadga för alltid. 15Lammet, matoffret och oljan ska bäras fram varje morgon som ett regelbundet brännoffer.

16Så säger Herren, Herren: Om fursten ger någon av sina söner en del av sin egendom som gåva, ska den tillhöra hans söner. Det ska vara deras egendom som de ärvt. 17Men om han ger en del av sin egendom som gåva till någon av sina tjänare, får denne behålla den fram till friåret. Då återgår den till fursten. Det är bara hans söner som får behålla hans egendom. 18Fursten får inte heller ta något av folkets arvedel eller tvinga bort dem från deras egendom. Han ska ge sina söner av sin egendom, för att ingen bland mitt folk ska behöva skiljas från sin egendom.’ ”

19Sedan förde han mig genom ingången vid sidan om porten till prästernas heliga rum som låg mot norr. Längst bort vid västra ändan syntes en plats. 20Han sa till mig: ”Det här är platsen där prästerna kokar skuldoffret och syndoffret och bakar matoffret, för att slippa bära dem till den yttre förgården och därmed helga folket.”

21Därefter förde han mig ut till den yttre förgården och runt till dess fyra hörn. I varje hörn syntes en gård. 22I den yttre förgårdens fyra hörn fanns det slutna gårdar, 20 meter långa och 15 meter breda, alla gårdarna i de fyra hörnen var lika stora. 23Utmed insidan av de fyra gårdarna fanns på alla sidor en mur, och nertill i muren runt omkring hade man byggt eldstäder för kokning. 24Han sa till mig: ”I dessa kök kokar tempeltjänarna folkets slaktoffer.”