Ezekieli 45 – NEN & NVI

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ezekieli 45:1-25

Mgawanyo Wa Nchi

145:1 Mit 3:9-10; Hes 34:13; Eze 47:21-22; 48:8-9, 29“ ‘Mtakapogawa nchi kuwa urithi, mtaitoa sehemu ya nchi kwa Bwana kuwa eneo takatifu, urefu wake dhiraa 25,000,45:1 Dhiraa 25,000 ni sawa na kilomita 11.25. upana wake dhiraa 20,00045:1 Dhiraa 20,000 ni sawa na kilomita 9. eneo hili lote litakuwa takatifu. 245:2 Eze 42:20Katika hiyo, itakuwepo sehemu mraba ambayo ni mahali patakatifu kila upande dhiraa 500 ikiwa imezungukwa na eneo la wazi lenye upana wa dhiraa hamsini. 345:3 Eze 48:10Katika eneo takatifu, pima sehemu yenye urefu wa dhiraa 25,000 na upana wa dhiraa 10,000.45:3 Dhiraa 10,000 ni sawa na kilomita 4.5. Ndani ya hilo eneo kutakuwa mahali patakatifu, Patakatifu pa Patakatifu. 445:4 Eze 40:46; 48:10-11Itakuwa sehemu takatifu ya nchi kwa ajili ya makuhani, wale wanaohudumu ndani ya mahali patakatifu na ambao hukaribia ili kuhudumu mbele za Bwana. Patakuwa mahali pa nyumba zao pamoja na sehemu kwa ajili ya mahali patakatifu. 545:5 Eze 48:13; 40:17Eneo la urefu wa dhiraa 25,000 na upana wa dhiraa 10,000 litakuwa la Walawi wale wanaotumika hekaluni, kama milki yao kwa ajili ya miji ya kuishi.

645:6 Eze 48:15-18“ ‘Utatoa mji kama mali yao wenye upana wa dhiraa 5,00045:6 Dhiraa 5,000 ni sawa na kilomita 2.25. na urefu wa dhiraa 25,000, karibu na sehemu takatifu, itakuwa mali ya nyumba yote ya Israeli.

745:7 Eze 48:21“ ‘Mkuu anayetawala atakuwa na lile eneo linalopakana na lile eneo lililowekwa wakfu upande huu na upande huu na eneo la mji. Eneo la mji litaenea upande wa magharibi kuanzia upande wa magharibi na upande wa mashariki kuanzia upande wa mashariki, likiendelea kwa urefu kutoka magharibi hadi mpaka wa mashariki sambamba na mojawapo ya sehemu za makabila. 845:8 Hes 26:53; Eze 46:18Nchi hii itakuwa milki yake katika Israeli. Nao wakuu wangu hawataonea tena watu wangu bali watairuhusu nyumba ya Israeli kuimiliki nchi kulingana na makabila yao.

945:9 Yer 22:3; Zek 7:9-10; 8:16; Za 12:5“ ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Yatosha, enyi wakuu wa Israeli! Acheni mbali ukatili wenu na uonevu wenu mkafanye lile lililo haki na sawa. Acheni kuwatoza watu wangu isivyo haki, asema Bwana Mwenyezi. 1045:10 Kum 25:15; Law 19:35; Mit 11:1; Mik 6:10-11; Amo 8:4-6Tumieni mizani sahihi na vipimo sahihi vya efa45:10 Efa ni kipimo cha ujazo cha kupimia vitu vikavu ambacho ni sawa na omeri 10; efa 1 ni sawa na kilo 22. na bathi.45:10 Bathi ni kipimo cha ujazo cha kupimia vitu vya humiminika ambacho ni sawa na 1/10 ya homeri; homeri 1 ni bathi 10 au efa 10. 1145:11 Isa 5:10Efa na bathi viwe sawa, bathi iwe sehemu ya kumi ya homeri na efa iwe sehemu ya kumi ya homeri, homeri itakuwa ndicho kiwango cha kukubalika kwa vyote viwili. 1245:12 Law 27:25; Hes 3:47; Kut 30:13Shekeli moja itakuwa gera ishirini.45:12 Gera 20 ni sawa na shekeli 1. Shekeli ishirini, jumlisha na shekeli ishirini na tano, jumlisha na shekeli kumi na tano zitakuwa mina moja.45:12 Mina 1 hapa ni sawa na shekeli 60; mina ya kawaida ilikuwa sawa na shekeli 50.

Sadaka Na Siku Takatifu

(Kutoka 12:1-20; Walawi 23:33-43)

13“ ‘Hili ndilo toleo maalum mtakalotoa: moja ya sita ya efa kutoka kila homeri ya ngano na moja ya sita ya efa kutoka kila homeri ya shayiri. 14Sehemu ya mafuta iliyoamriwa, yaliyopimwa kwa bathi, ni sehemu ya kumi ya bathi kutoka kila kori moja45:14 Kori 1 ni sawa na bathi 10 au homeri 1. (ambayo ina bathi kumi au homeri moja.) 1545:15 Law 1:4; 6:30; Rum 5:10; Efe 2:16; Kol 1:21; Tit 2:14Pia kondoo mmoja atachukuliwa kutoka kwenye kila kundi la kondoo mia mbili kutoka kwenye malisho yaliyonyeshewa vizuri ya Israeli. Hivi vitatumika kwa ajili ya sadaka ya nafaka, sadaka ya kuteketezwa na sadaka za amani ili kufanya upatanisho kwa ajili ya watu, asema Bwana Mwenyezi. 16Watu wote wa nchi wataungana pamoja na mkuu anayetawala Israeli ili kutoa hii sadaka maalum. 1745:17 Yn 6:51; Gal 3:13; Isa 66:23; 1Fal 8:62; 2Nya 31:3; Hes 10:10; Eze 46:4-12Huu utakuwa ndio wajibu wa mkuu anayetawala kutoa sadaka ya kuteketezwa, sadaka ya nafaka na sadaka ya kinywaji kwenye sikukuu, Mwezi Mwandamo na Sabato, kwenye sikukuu zote zilizoamriwa za nyumba ya Israeli. Atatoa sadaka za dhambi, sadaka za nafaka, sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani ili kufanya upatanisho kwa ajili ya nyumba ya Israeli.

1845:18 Kut 12:2; Law 22:20; Ebr 9:14; Law 16:33“ ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Katika mwezi wa kwanza, siku ya kwanza ya huo mwezi utamchukua fahali mchanga asiye na dosari na kutakasa mahali patakatifu. 1945:19 Eze 43:17; Law 16:18-19; Eze 43:20Kuhani itampasa achukue sehemu ya hiyo damu ya sadaka ya dhambi na kuipaka kwenye miimo ya Hekalu, kwenye pembe nne za juu za ukingo wa hayo madhabahu na juu ya miimo ya lango la ukumbi wa ndani. 2045:20 Law 4; 27Itakupasa kufanya vivyo hivyo katika siku ya saba ya mwezi huo kwa ajili ya mtu yeyote ambaye hutenda dhambi bila kukusudia au bila kujua, hivyo utafanya upatanisho kwa ajili ya Hekalu.

2145:21 Kut 12:11; Law 23:5-6; Hes 9:2-3“ ‘Katika mwezi wa kwanza siku ya kumi na nne utaadhimisha Pasaka. Sikukuu itaendelea kwa siku saba, wakati huo wa hizo siku saba mtakula mikate isiyotiwa chachu. 2245:22 Law 4:14; 1Pet 2:24Katika siku hiyo mkuu anayetawala atatoa fahali kuwa sadaka ya dhambi kwa ajili yake mwenyewe na kwa ajili ya watu wote wa nchi. 2345:23 Hes 28:15, 25; 22:40; Ay 42:8Kila siku wakati wa hizo siku saba za sikukuu atatoa mafahali saba na kondoo dume saba wasio na dosari kuwa sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana na beberu kwa ajili ya sadaka ya dhambi. 2445:24 Hes 28:12-13; Eze 46:5-7Pia atatoa sadaka ya nafaka efa moja kwa kila fahali na efa moja kwa kila kondoo dume, pamoja na hini moja45:24 Hini ni kipimo cha kupimia vitu vya humiminika chenye ujazo wa 1/6 ya bathi, na ni sawa na lita 4. ya mafuta kwa kila efa.

2545:25 Kum 16:13; Law 23:34-43; Hes 29:12-38“ ‘Wakati wa hizo siku saba za sikukuu, ambayo huanza katika mwezi wa saba kwenye siku ya kumi na tano, mkuu anayetawala atatoa mahitaji yale yale kwa ajili ya sadaka za dhambi, sadaka za kuteketezwa, sadaka za nafaka na mafuta.

Nueva Versión Internacional

Ezequiel 45:1-25

División de la tierra

1»”Cuando por sorteo se repartan la tierra como herencia, deberán reservar una porción de terreno, la cual será consagrada al Señor. Esta porción santa será de veinticinco mil codos de largo por veinte mil codos45:1 veinte mil codos (LXX); diez mil codos (TM). de ancho. Todo este territorio será santo. 2De allí se adjudicará para el santuario un terreno cuadrado de quinientos codos por lado. Además, alrededor de ese terreno se reservará un espacio libre de cincuenta codos de ancho. 3En esa sección reservada apartarás una parcela de veinticinco mil codos de largo por diez mil codos de ancho, donde estará el santuario, el Lugar Santísimo. 4Esta será la porción santa de tierra para los sacerdotes que ministran en el santuario y que se acercan para ministrar delante del Señor. Allí construirán sus casas y el santuario del Señor. 5Además, a los levitas que sirven en el Templo se les adjudicará un espacio de veinticinco mil codos de largo por diez mil codos de ancho, para que tengan ciudades donde vivir.45:5 ciudades donde vivir (LXX); veinte habitaciones (TM).

6»”Y como territorio para la ciudad se asignará, junto a la sección reservada para el santuario, un espacio de cinco mil codos de ancho por veinticinco mil codos de largo. Este terreno pertenecerá a todo el pueblo de Israel.

7»”Al príncipe se le asignará una porción de tierra a ambos lados de la sección reservada para el santuario y de la sección reservada para la ciudad. Por el lado oeste se extenderá hacia el oeste y hacia el este por el lado oriental. Su longitud de este a oeste será igual a la de los terrenos asignados a una de las tribus. 8Esta tierra será su posesión en Israel; así mis príncipes no volverán a oprimir a mi pueblo, sino que dejarán que las tribus de Israel ocupen la tierra.

9»”Así dice el Señor y Dios: ¡Basta ya, príncipes de Israel! ¡Abandonen la violencia y la explotación! ¡Practiquen el derecho y la justicia! ¡Dejen de extorsionar a mi pueblo!, afirma el Señor y Dios. 10¡Usen balanzas justas; el peso y la medida del efa45:10 Es decir, aprox. 16 kg. y el bato45:10 Es decir, aprox. 22 l. deberán ser exactos! 11El efa y el bato serán de una misma medida. Cada uno será equivalente a una décima parte de un jómer,45:11 Un jómer era una medida para áridos con un equivalente aproximado de 220 l o 160 kg. el cual servirá de patrón para ambas medidas. 12En cuanto a las medidas de peso: un siclo45:12 Es decir, aprox. 11.5 g. será igual a veinte guerás45:12 Un guerá era equivalente aprox. a 0.57 g. y una mina45:12 Es decir, 60 siclos; la mina común contenía 50 siclos. Sesenta siclos era aprox. 690 g. será igual a sesenta siclos.

13»”Esta es la ofrenda especial que presentarán: por cada jómer de trigo, la sexta parte de un efa;45:13 Es decir, aprox. 2.7 kg de trigo. por cada jómer de cebada, la sexta parte de un efa.45:13 Es decir, aprox. 2.3 kg de cebada. 14La medida para el aceite es la siguiente: por cada coro de aceite, la décima parte de un bato.45:14 Es decir, aprox. 2.2 l. El coro equivale tanto a diez batos como a un jómer, pues diez batos equivalen a un jómer.

15»”En cuanto a las ovejas, se tomará una de cada doscientas de los rebaños que pastan en las mejores praderas de Israel. Estas se usarán para las ofrendas de cereales, el holocausto y el sacrificio de comunión, a fin de obtener perdón por los pecados de ellos, afirma el Señor. 16Todo el pueblo de la tierra estará obligado a contribuir para esta ofrenda especial del príncipe de Israel. 17Será deber del príncipe proveer los holocaustos, las ofrendas de cereales y las ofrendas líquidas en las fiestas, las lunas nuevas, los sábados y en todas las fiestas señaladas en el pueblo de Israel. Deberá también proveer las ofrendas por el pecado, las ofrendas de cereales, los holocaustos y las ofrendas de comunión para obtener perdón por los pecados de Israel.

18»”Así dice el Señor y Dios: El día primero del mes primero tomarás un novillo sin defecto y lo ofrecerás como sacrificio para purificar de pecado el santuario. 19El sacerdote tomará de la sangre de la ofrenda por el pecado y la pondrá sobre los postes de la puerta del Templo, en las cuatro esquinas del zócalo superior del altar y en los postes de la puerta del atrio interior. 20Lo mismo harás el día siete del mes con todo el que haya pecado sin intención o por ignorancia. Así el Templo quedará purificado.

21»”El día catorce del mes primero deberás celebrar la fiesta de la Pascua. Durante siete días comerás pan sin levadura. 22Ese día el príncipe deberá ofrecer un novillo como sacrificio por su pecado y el de todo el pueblo. 23Y cada día, durante los siete días de la fiesta, el príncipe deberá ofrecer en holocausto al Señor siete novillos y siete carneros sin defecto. Además, cada día ofrecerá un macho cabrío como sacrificio por el pecado. 24También ofrecerá, como ofrenda de grano, un efa de cereal por cada novillo, un efa por cada carnero y un hin45:24 Es decir, aprox. 3.8 l. de aceite por cada efa.

25»”Durante los siete días de la fiesta, que comienza el día quince del mes séptimo, el príncipe deberá proveer lo mismo para el sacrificio por el pecado, el holocausto y las ofrendas de cereales y de aceite.