Ezekieli 45 – NEN & KLB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ezekieli 45:1-25

Mgawanyo Wa Nchi

145:1 Mit 3:9-10; Hes 34:13; Eze 47:21-22; 48:8-9, 29“ ‘Mtakapogawa nchi kuwa urithi, mtaitoa sehemu ya nchi kwa Bwana kuwa eneo takatifu, urefu wake dhiraa 25,000,45:1 Dhiraa 25,000 ni sawa na kilomita 11.25. upana wake dhiraa 20,00045:1 Dhiraa 20,000 ni sawa na kilomita 9. eneo hili lote litakuwa takatifu. 245:2 Eze 42:20Katika hiyo, itakuwepo sehemu mraba ambayo ni mahali patakatifu kila upande dhiraa 500 ikiwa imezungukwa na eneo la wazi lenye upana wa dhiraa hamsini. 345:3 Eze 48:10Katika eneo takatifu, pima sehemu yenye urefu wa dhiraa 25,000 na upana wa dhiraa 10,000.45:3 Dhiraa 10,000 ni sawa na kilomita 4.5. Ndani ya hilo eneo kutakuwa mahali patakatifu, Patakatifu pa Patakatifu. 445:4 Eze 40:46; 48:10-11Itakuwa sehemu takatifu ya nchi kwa ajili ya makuhani, wale wanaohudumu ndani ya mahali patakatifu na ambao hukaribia ili kuhudumu mbele za Bwana. Patakuwa mahali pa nyumba zao pamoja na sehemu kwa ajili ya mahali patakatifu. 545:5 Eze 48:13; 40:17Eneo la urefu wa dhiraa 25,000 na upana wa dhiraa 10,000 litakuwa la Walawi wale wanaotumika hekaluni, kama milki yao kwa ajili ya miji ya kuishi.

645:6 Eze 48:15-18“ ‘Utatoa mji kama mali yao wenye upana wa dhiraa 5,00045:6 Dhiraa 5,000 ni sawa na kilomita 2.25. na urefu wa dhiraa 25,000, karibu na sehemu takatifu, itakuwa mali ya nyumba yote ya Israeli.

745:7 Eze 48:21“ ‘Mkuu anayetawala atakuwa na lile eneo linalopakana na lile eneo lililowekwa wakfu upande huu na upande huu na eneo la mji. Eneo la mji litaenea upande wa magharibi kuanzia upande wa magharibi na upande wa mashariki kuanzia upande wa mashariki, likiendelea kwa urefu kutoka magharibi hadi mpaka wa mashariki sambamba na mojawapo ya sehemu za makabila. 845:8 Hes 26:53; Eze 46:18Nchi hii itakuwa milki yake katika Israeli. Nao wakuu wangu hawataonea tena watu wangu bali watairuhusu nyumba ya Israeli kuimiliki nchi kulingana na makabila yao.

945:9 Yer 22:3; Zek 7:9-10; 8:16; Za 12:5“ ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Yatosha, enyi wakuu wa Israeli! Acheni mbali ukatili wenu na uonevu wenu mkafanye lile lililo haki na sawa. Acheni kuwatoza watu wangu isivyo haki, asema Bwana Mwenyezi. 1045:10 Kum 25:15; Law 19:35; Mit 11:1; Mik 6:10-11; Amo 8:4-6Tumieni mizani sahihi na vipimo sahihi vya efa45:10 Efa ni kipimo cha ujazo cha kupimia vitu vikavu ambacho ni sawa na omeri 10; efa 1 ni sawa na kilo 22. na bathi.45:10 Bathi ni kipimo cha ujazo cha kupimia vitu vya humiminika ambacho ni sawa na 1/10 ya homeri; homeri 1 ni bathi 10 au efa 10. 1145:11 Isa 5:10Efa na bathi viwe sawa, bathi iwe sehemu ya kumi ya homeri na efa iwe sehemu ya kumi ya homeri, homeri itakuwa ndicho kiwango cha kukubalika kwa vyote viwili. 1245:12 Law 27:25; Hes 3:47; Kut 30:13Shekeli moja itakuwa gera ishirini.45:12 Gera 20 ni sawa na shekeli 1. Shekeli ishirini, jumlisha na shekeli ishirini na tano, jumlisha na shekeli kumi na tano zitakuwa mina moja.45:12 Mina 1 hapa ni sawa na shekeli 60; mina ya kawaida ilikuwa sawa na shekeli 50.

Sadaka Na Siku Takatifu

(Kutoka 12:1-20; Walawi 23:33-43)

13“ ‘Hili ndilo toleo maalum mtakalotoa: moja ya sita ya efa kutoka kila homeri ya ngano na moja ya sita ya efa kutoka kila homeri ya shayiri. 14Sehemu ya mafuta iliyoamriwa, yaliyopimwa kwa bathi, ni sehemu ya kumi ya bathi kutoka kila kori moja45:14 Kori 1 ni sawa na bathi 10 au homeri 1. (ambayo ina bathi kumi au homeri moja.) 1545:15 Law 1:4; 6:30; Rum 5:10; Efe 2:16; Kol 1:21; Tit 2:14Pia kondoo mmoja atachukuliwa kutoka kwenye kila kundi la kondoo mia mbili kutoka kwenye malisho yaliyonyeshewa vizuri ya Israeli. Hivi vitatumika kwa ajili ya sadaka ya nafaka, sadaka ya kuteketezwa na sadaka za amani ili kufanya upatanisho kwa ajili ya watu, asema Bwana Mwenyezi. 16Watu wote wa nchi wataungana pamoja na mkuu anayetawala Israeli ili kutoa hii sadaka maalum. 1745:17 Yn 6:51; Gal 3:13; Isa 66:23; 1Fal 8:62; 2Nya 31:3; Hes 10:10; Eze 46:4-12Huu utakuwa ndio wajibu wa mkuu anayetawala kutoa sadaka ya kuteketezwa, sadaka ya nafaka na sadaka ya kinywaji kwenye sikukuu, Mwezi Mwandamo na Sabato, kwenye sikukuu zote zilizoamriwa za nyumba ya Israeli. Atatoa sadaka za dhambi, sadaka za nafaka, sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani ili kufanya upatanisho kwa ajili ya nyumba ya Israeli.

1845:18 Kut 12:2; Law 22:20; Ebr 9:14; Law 16:33“ ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Katika mwezi wa kwanza, siku ya kwanza ya huo mwezi utamchukua fahali mchanga asiye na dosari na kutakasa mahali patakatifu. 1945:19 Eze 43:17; Law 16:18-19; Eze 43:20Kuhani itampasa achukue sehemu ya hiyo damu ya sadaka ya dhambi na kuipaka kwenye miimo ya Hekalu, kwenye pembe nne za juu za ukingo wa hayo madhabahu na juu ya miimo ya lango la ukumbi wa ndani. 2045:20 Law 4; 27Itakupasa kufanya vivyo hivyo katika siku ya saba ya mwezi huo kwa ajili ya mtu yeyote ambaye hutenda dhambi bila kukusudia au bila kujua, hivyo utafanya upatanisho kwa ajili ya Hekalu.

2145:21 Kut 12:11; Law 23:5-6; Hes 9:2-3“ ‘Katika mwezi wa kwanza siku ya kumi na nne utaadhimisha Pasaka. Sikukuu itaendelea kwa siku saba, wakati huo wa hizo siku saba mtakula mikate isiyotiwa chachu. 2245:22 Law 4:14; 1Pet 2:24Katika siku hiyo mkuu anayetawala atatoa fahali kuwa sadaka ya dhambi kwa ajili yake mwenyewe na kwa ajili ya watu wote wa nchi. 2345:23 Hes 28:15, 25; 22:40; Ay 42:8Kila siku wakati wa hizo siku saba za sikukuu atatoa mafahali saba na kondoo dume saba wasio na dosari kuwa sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana na beberu kwa ajili ya sadaka ya dhambi. 2445:24 Hes 28:12-13; Eze 46:5-7Pia atatoa sadaka ya nafaka efa moja kwa kila fahali na efa moja kwa kila kondoo dume, pamoja na hini moja45:24 Hini ni kipimo cha kupimia vitu vya humiminika chenye ujazo wa 1/6 ya bathi, na ni sawa na lita 4. ya mafuta kwa kila efa.

2545:25 Kum 16:13; Law 23:34-43; Hes 29:12-38“ ‘Wakati wa hizo siku saba za sikukuu, ambayo huanza katika mwezi wa saba kwenye siku ya kumi na tano, mkuu anayetawala atatoa mahitaji yale yale kwa ajili ya sadaka za dhambi, sadaka za kuteketezwa, sadaka za nafaka na mafuta.

Korean Living Bible

에스겔 45:1-25

거룩하게 구별한 땅

1“너희가 땅을 분배할 때에는 한 구역을 거룩하게 구별하여 나 여호와 에게 바쳐라. 그 땅은 길이가 13.1킬로미터이며 폭이 45:1 또는 10,000규빗, 곧 5.3킬로미터10.5킬로미터이다. 그 구역 전체가 거룩한 땅이 될 것이다.

2그 중에서도 성소에 속할 땅은 가로 세로 262.5미터의 정사각형 땅이며 그 땅 26.3미터 폭의 사방 둘레는 빈터가 되게 하라.

3그 구별한 땅 중에서 길이 13.1킬로미터와 폭 5.3킬로미터를 측량하여 그 구역 내에 성전을 세워라.

4그 땅은 거룩한 곳으로 성소에서 나를 섬기는 제사장들이 사용할 것이며 제사장들의 집과 성전을 짓는 터가 될 것이다.

5그리고 그 나머지 땅인 길이 13.1킬로미터와 폭 5.3킬로미터의 땅은 성전에서 섬기는 레위 사람들의 소유로 주어 그들이 사는 부락이 되게 하라.

6“그리고 거룩하게 구별한 땅과 인접한 폭 2.6킬로미터와 길이 13.1킬로미터의 땅은 이스라엘 백성이 누구든지 살 수 있는 성의 기지로 삼아라.

7“거룩하게 구별된 땅과 성의 기지 양쪽 옆으로 인접해 있는 땅은 왕이 차지할 땅이다. 그것은 서쪽으로 서쪽 국경까지 뻗고 동쪽으로는 동쪽 국경까지 뻗어 그 길이가 이스라엘 한 지파에게 분배된 땅의 길이와 같다.

8이 땅이 왕의 소유가 되면 내 왕들이 다시는 내 백성을 억압하지 않을 것이다. 그리고 나머지 땅은 이스라엘 백성에게 지파대로 나누어 주도록 하라.

9“나 여호와가 말한다. 이스라엘의 통치자들아, 너희가 오랫동안 범죄하였다. 너희는 횡포와 탄압을 중단하고 공정하고 옳은 일을 하며 내 백성을 착취하는 일을 버려라. 이것은 나 주 여호와의 말이다.

10“너희는 45:10 또는 ‘공평한 저울과 공평한 에바와 공평한 밧을 쓸지니’정확한 저울과 되를 사용하라.

11마른 것을 되는 에바와 액체를 되는 밧의 용량을 동일하게 하고 그 기준은 호멜로 하라. 한 호멜은 10에바이며 10밧이다.

12그리고 한 세겔은 20게라이고 20세겔과 25세겔과 15세겔을 모두 합한 60세겔이 한 미나이다.”

예물과 명절에 대한 규정

13“너희가 바쳐야 할 예물의 기준은 이렇다. 밀과 보리는 너희 수확의 60분의 을 바치고

14기름은 너희 수확에서 밧으로 되어 100분의 을 바쳐라. 10밧이 한 호멜이며 한 고르이다.

15그리고 이스라엘의 모든 목장에서 양 200마리에 한 마리씩 바쳐라. 이 모든 예물은 백성의 죄가 용서받을 수 있도록 곡식으로 드리는 소제와 불로 태워 바치는 번제와 화해를 위한 화목제물로 사용되어야 할 것이다. 이것은 나 주 여호와의 말이다.

16이 땅에 사는 모든 백성은 이 예물을 이스라엘 왕에게 드려야 하며

17명절과 매월 초하루와 안식일과 이스라엘의 모든 지정된 명절에 번제와 소제와 술을 따르는 전제를 준비하는 것은 왕이 해야 할 일이다. 왕은 또 이스라엘 백성의 죄를 씻기 위해 속죄제와 소제와 번제와 화목제를 준비해야 한다.

18“나 여호와가 말한다. 정월 초하룻날에 너희는 흠 없는 수송아지 한 마리를 가져다가 성소를 정결하게 하라.

19제사장은 속죄제물의 피를 가져다가 성전의 문설주와 제단 밑받침 네 모퉁이와 안뜰로 들어가는 출입문 기둥에 발라야 한다.

20너희는 또 무심결에 범죄하거나 무지해서 범죄한 자를 위해 그 달 7일에도 그렇게 하여 45:20 또는 ‘전을 속죄할지니라’성전을 거룩하게 하라.

21“1월 14일에는 7일 동안 계속되는 유월절을 지키고 이 기간 동안은 누룩 넣지 않은 빵을 먹어라.

22이 명절 45:22 또는 ‘그 날에’첫날에 왕은 자기와 모든 백성을 위해 죄를 씻는 속죄제물로 송아지 한 마리를 준비할 것이며

23그는 또 그 명절 7일 동안에 매일 흠 없는 것으로 수송아지 일곱 마리와 숫양 일곱 마리를 나 여호와에게 바칠 번제물로 준비하고 속죄제물로 매일 숫염소 한 마리를 준비해야 한다.

24또 곡식으로 드리는 소제로는 수송아지 한 마리와 숫양 한 마리에 대해서 각각 밀가루 45:24 히 ‘한 에바’22리터씩 준비하고 밀가루 22리터에 대해서는 기름 45:24 히 ‘한 힌’약 4리터씩 준비해야 한다.

25“7월 15일부터 시작되는 명절 7일 동안에도 왕은 매일 똑같은 것을 준비하여 속죄제와 번제와 소제와 기름을 드릴 수 있도록 하라.”