Ezekieli 39 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ezekieli 39:1-29

Majeshi Ya Gogu Yataangamizwa

139:1 Eze 27:13; 38:2; Ufu 20:6“Mwanadamu, tabiri dhidi ya Gogu useme: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ee Gogu mimi ni kinyume nawe, mtawala mkuu wa Roshi, Mesheki na Tubali. 239:2 Eze 32:30; 38:4, 15Nitakugeuza kuelekea ulikotoka na kukuburuta. Nitakuleta kutoka kaskazini ya mbali na kukupeleka wewe dhidi ya milima ya Israeli. 339:3 Amo 2:15; Za 76:3Kisha nitaupiga upinde wako kutoka mkono wako wa kushoto na kuifanya mishale ianguke kutoka mkono wako wa kuume. 439:4 Yer 25:33; Eze 29:5; Mwa 40:19; Isa 34:2-8Utaanguka kwenye milima ya Israeli, wewe pamoja na vikosi vyako vyote na yale mataifa yaliyo pamoja nawe. Nitakutoa uwe chakula cha ndege wa aina zote walao nyama na cha wanyama wa mwituni. 539:5 Eze 32:4Utaanguka katika uwanja, kwa kuwa nimenena, asema Bwana Mwenyezi. 639:6 Ufu 20:9; Yer 25:22; Eze 30:8; Kut 6:7Nitatuma moto juu ya Magogu na kwa wale wanaoishi kwa salama huko pwani, nao watajua kwamba Mimi ndimi Bwana.

739:7 Kut 20:7; Eze 13:19; Isa 12:6; 54:5; Eze 20:9; 36:23; Isa 49:26“ ‘Nitalifanya Jina langu takatifu lijulikane miongoni mwa watu wangu Israeli. Sitaliacha tena Jina langu takatifu litiwe unajisi, nayo mataifa watajua kuwa Mimi Bwana ndimi Aliye Mtakatifu wa Israeli. 839:8 Eze 7:3-8; 38:17Hili jambo linakuja! Hakika litatokea, asema Bwana Mwenyezi. Hii ndiyo siku ile niliyosema habari zake.

939:9 Za 46:9; 76:3“ ‘Ndipo wale wanaoishi katika miji ya Israeli watakapotoka na kutumia hizo silaha kuwashia moto na kuziteketeza, yaani, kigao na ngao, pinde na mishale, rungu za vita na mikuki. Kwa miaka saba watavitumia kama kuni. 1039:10 Isa 33:1; Hab 2:8; Isa 14:2; Kut 3:22Hawatahitaji kukusanya kuni kutoka mashambani wala kukata kuni kutoka kwenye misitu, kwa sababu watatumia silaha kuwa kuni. Nao watawateka mateka wale waliowateka na kuchukua nyara mali za wale waliochukua mali zao nyara, asema Bwana Mwenyezi.

1139:11 Eze 38:2; Isa 34:3“ ‘Siku ile nitampa Gogu mahali pa kuzikia katika Israeli, katika bonde la wale wasafirio upande wa mashariki kuelekea baharini. Jambo hili litazuia njia ya wasafiri kwa sababu Gogu na makundi yake yote ya wajeuri watazikwa huko. Kwa hiyo litaitwa Bonde la Hamon-Gogu.39:11 Hamon-Gogu maana yake Makundi ya wajeuri wa Gogu.

1239:12 Kum 21:23“ ‘Kwa miezi saba nyumba ya Israeli itakuwa ikiwazika ili kuisafisha nchi. 1339:13 Eze 28:22; Za 126:2Watu wote wa nchi watawazika, nayo siku nitakayotukuzwa itakuwa siku ya kumbukumbu kwa ajili yao, asema Bwana Mwenyezi.

1439:14 Eze 39:12“ ‘Watu wataajiriwa mara kwa mara kuisafisha nchi. Baadhi yao watapita nchini kote na zaidi yao hao wengine, watawazika wale waliosalia juu ya uso wa nchi. Mwisho wa hiyo miezi saba wataanza upekuzi wao. 15Wakati wanapopita nchini kote na mmoja wao akaona mfupa wa mwanadamu, ataweka alama kando yake mpaka wachimba kaburi wawe wameuzika katika Bonde la Hamon-Gogu. 1639:16 Eze 39:12(Pia mji uitwao Hamona39:16 Hamona maana yake Kundi (la wajeuri). utakuwa humo.) Hivyo ndivyo watakavyoisafisha nchi.’

1739:17 Isa 18:6; Ay 15:23; Ufu 19:17; Eze 32:4“Mwanadamu, hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ita kila aina ya ndege na wanyama wote wa mwituni, waambie: ‘Kusanyikeni mje pamoja kutoka pande zote kwa ajili ya dhabihu ninayowaandalia, dhabihu kuu katika milima ya Israeli. Huko mtakula nyama na kunywa damu. 1839:18 Za 22:12; Yer 51:40Mtakula nyama za watu mashujaa na kunywa damu za wakuu wa dunia kana kwamba ni za kondoo dume na kondoo wake, mbuzi na mafahali, wote walionona kutoka Bashani. 1939:19 Law 3:9Katika dhabihu ninayoandaa kwa ajili yenu, mtakula mafuta mpaka mkinai na kunywa damu mpaka mlewe. 2039:20 Yer 12:9; Ufu 19:17-18; Eze 38:4; Isa 56:9Kwenye meza yangu watajishibisha kwa farasi na wapanda farasi, watu mashujaa na askari wa kila aina,’ asema Bwana Mwenyezi.

2139:21 Kut 9:16; Isa 37:20; Eze 38:16“Nitauonyesha utukufu wangu miongoni mwa mataifa, nayo mataifa yote wataiona adhabu nitakayotoa na mkono wangu nitakaouweka juu yao. 22Kuanzia siku ile na kuendelea nyumba ya Israeli itajua kuwa Mimi ndimi Bwana, Mungu wao. 2339:23 Isa 1:15; Kum 31:17; Yer 22:8-9; Isa 59:2; Yer 44:23Na mataifa watajua kuwa nyumba ya Israeli walikwenda utumwani kwa ajili ya dhambi yao, kwa sababu hawakuwa waaminifu kwangu. Hivyo niliwaficha uso wangu na kuwatia mikononi mwa adui zao, nao wote wakaanguka kwa upanga. 2439:24 2Fal 17:23; Dan 9:7; Eze 36:19; 16:53; Yer 4:18Niliwatendea sawasawa na uchafu wao na makosa yao, nami nikawaficha uso wangu.

2539:25 Eze 34:13; Yer 30:18; Isa 27:12-13; Eze 16:53; Yer 33:7“Kwa hiyo hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Sasa nitamrudisha Yakobo kutoka utumwani, nami nitawahurumia watu wote wa Israeli, nami nitakuwa na wivu kwa ajili ya Jina langu takatifu. 2639:26 1Fal 4:25; Yer 32:37; Isa 17:2; Mik 4:4; Dan 9:16; Eze 38:8Wataisahau aibu yao na jinsi walivyoonyesha kutokuwa waaminifu kwangu mimi wakati waliishi salama katika nchi yao, bila kuwa na mtu yeyote wa kuwatia hofu. 2739:27 Eze 37:21; 38:16; 36:23Nitakapokuwa nimewarudisha kutoka mataifa na kuwakusanya kutoka nchi za adui zao, mimi nitajionyesha kuwa mtakatifu kwa kupitia kwao machoni mwa mataifa mengi. 2839:28 Za 147:2; Eze 36:23, 36Ndipo watakapojua kwamba Mimi ndimi Bwana, Mungu wao, ingawa niliwapeleka uhamishoni miongoni mwa mataifa, nitawakusanya tena katika nchi yao wenyewe, bila kumwacha yeyote nyuma. 2939:29 Isa 11:2; Mdo 2:27; Hos 2:20; Yoe 2:28; Kum 31:17; Eze 37:9; 16:42Sitawaficha tena uso wangu, kwa maana nitamimina Roho wangu juu ya nyumba ya Israeli, asema Bwana Mwenyezi.”

New International Reader’s Version

Ezekiel 39:1-29

1“Son of man, prophesy against Gog. Tell him, ‘The Lord and King says, “Gog, I am against you. You are the chief prince of Meshek and Tubal. 2But I will turn you around. I will drag you along. I will bring you from the far north. I will send you against the mountains of Israel. 3Then I will knock your bow out of your left hand. I will make your arrows drop from your right hand. 4You will fall dead on the mountains of Israel. You and all your troops will die there. So will the nations that join you. I will feed you to all kinds of birds that eat dead bodies. So they and the wild animals will eat you up. 5You will fall dead in the open fields. I have spoken,” announces the Lord and King. 6“I will send fire on the land of Magog. It will burn up the people who live in safety on the coast. So they will know that I am the Lord.

7“ ‘ “I will make my holy name known among my people Israel. I will no longer let them treat my name as if it were not holy. Then the nations will know that I am the Holy One in Israel. I am the Lord. 8The day I will judge you is coming. You can be sure of it,” announces the Lord and King. “It is the day I have spoken about.

9“ ‘ “At that time those who live in the towns of Israel will go out and light a fire. They will use it to burn up the weapons. That includes small and large shields. It also includes bows and arrows, war clubs and spears. It will take seven years to burn all of them up. 10People will not gather wood from the fields. They will not cut down the forests. Instead, they will burn the weapons. And they will rob those who robbed them. They will steal from those who stole from them,” announces the Lord and King.

11“ ‘ “Gog, at that time I will bury you in a grave in Israel. It will be in the valley where people travel east of the Dead Sea. It will block the path of travelers. That’s because you and your huge armies will be buried there. So it will be called the Valley of Gog’s Armies.

12“ ‘ “It will take seven months for the Israelites to bury the bodies. They will do this to make the land ‘clean’ again. 13All the people in the land will bury them. The day that I show how glorious I am will be a time to remember.” This is what the Lord and King announces. 14“People will keep being hired to make the land ‘clean’ again. They will go all through it. They and others will bury any bodies lying on the ground.

“ ‘ “After the seven months they will search even more carefully. 15As they go through the land here is what they’ll do. When anyone sees a bone, they will put a marker beside it. Then those who dig the graves will take the bone to the Valley of Gog’s Armies. There they will bury it. 16That is how they will make the land ‘clean’ again.” ’ ” Also a town called Gog’s Armies is near there.

17The Lord and King said to me, “Son of man, speak to every kind of bird. Call out to all the wild animals. Tell them, ‘Gather together. Come from everywhere. Gather around the sacrifice I am preparing for you. It is the great sacrifice on the mountains of Israel. There you will eat human bodies and drink human blood. 18You will eat the bodies of mighty men. You will drink the blood of the princes of the earth. You will eat their bodies and drink their blood. You will do this as if they were rams and lambs, goats and bulls. You will enjoy it as if you were eating the fattest animals from Bashan. 19So I am preparing a sacrifice for you. You will eat fat until you are completely full. You will drink blood until you are drunk. 20At my table you will eat horses, riders, mighty men and soldiers until you are full,’ announces the Lord and King.

21“ ‘I will show all the nations my glory. They will see how I punish them when I use my power against them. 22From that time on, the people of Israel will know that I am the Lord their God. 23The nations will know that the people of Israel were taken away as prisoners because they sinned against me. They were not faithful to me. So I turned my face away from them. I handed them over to their enemies. All of them were killed by swords. 24I punished them because they were “unclean.” They did many things that were wrong. So I turned my face away from them.’ ”

25The Lord and King says, “I will now cause the people of Jacob to recover from my judgment. I will show my tender love for all the people of Israel. I will make sure that my name is kept holy. 26My people will forget the shameful things they have done. They will not remember all the ways they were unfaithful to me. They used to live in safety in their land. At that time no one made them afraid. 27So I will bring them back from the nations. I will gather them from the countries of their enemies. And I will use them to prove to many nations how holy I am. 28Then they will know that I am the Lord their God. I let the nations take my people away as prisoners. But now I will bring them back to their own land. I will not leave anyone behind. 29I will no longer turn my face away from the people of Israel. I will pour out my Spirit on them,” announces the Lord and King.