Ezekieli 38 – NEN & NIV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ezekieli 38:1-23

Unabii Dhidi Ya Gogu

1Neno la Bwana likanijia kusema: 238:2 Mwa 10:2; Eze 27:13; Ufu 20:8; Eze 39:11“Mwanadamu, kaza uso wako dhidi ya Gogu, katika nchi ya Magogu, mkuu wa Roshi, Mesheki na Tubali, tabiri dhidi yake 338:3 Eze 39:1na useme: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Ee Gogu, mimi ni kinyume nawe, mtawala mkuu wa Roshi, Mesheki na Tubali. 438:4 2Fal 19:28; Isa 43:17; Dan 11:40; Eze 23:12; 29:4; 39:2Nitakugeuza kuelekea ulikotoka na kukutia ndoana kwenye mataya yako na kukutoa nje wewe pamoja na jeshi lako lote, yaani, farasi wako, wapanda farasi wako waliojiandaa tayari kwa vita, pamoja na kundi kubwa la wajeuri wakiwa na ngao na vigao, wote wakipunga panga zao. 538:5 Eze 27:10-14; Mwa 10:6Uajemi, Kushi38:5 Kushi ni Ethiopia. na Putu watakuwa pamoja nao, wote wakiwa na ngao na kofia za chuma, 638:6 Mwa 10:2-3; Eze 32:30pia Gomeri pamoja na vikosi vyake vyote, na Beth-Togarma kutoka kaskazini ya mbali pamoja na vikosi vyake vyote, mataifa mengi wakiwa pamoja nawe.

738:7 Isa 8:9; 8:10; Yer 46:3, 4, 14; 51:12“ ‘Jiandae, uwe tayari, wewe na makundi yako yote ya wajeuri yaliyokusanyika pamoja nawe, nawe waamrishe. 838:8 Isa 11:11; 24:22; Kum 4:30; Yer 23:6; Yoe 3:1; Eze 28:26Baada ya siku nyingi utaitwa vitani. Katika miaka ijayo, utaivamia nchi ile ambayo imepona kutoka vita, ambayo watu wake walikusanywa kutoka mataifa mengi kuja katika milima ya Israeli, ambayo kwa muda mrefu ilikuwa imeachwa ukiwa. Wameletwa kutoka mataifa na sasa wote wanaishi katika hali ya salama. 938:9 Isa 25:4; 28:2; Yer 4:13; Yoe 2:2; Ufu 20:8Wewe na vikosi vyako vyote na mataifa mengi yaliyo pamoja nawe mtapanda juu, mtawazoa kama tufani na kuifunika nchi kama wingu.

1038:10 Yer 17:10; Za 36:4; Mik 2:1“ ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Katika siku ile mawazo yataingia moyoni mwako nawe utapanga mipango mibaya. 1138:11 Yer 49:31; Zek 2:4; Amu 18:7-27; Mwa 34:25Utasema, “Nitapigana vita na nchi ambayo vijiji vyake havina maboma. Nitawashambulia watu wanaoishi kwa amani na wasiotarajia vita: wote wanaishi bila maboma na bila malango na makomeo. 12Nitateka mateka na kuchukua nyara mali za wale waliorudi kuishi katika mahame na wale watu waliokusanywa kutoka kwa mataifa, ambao sasa wana mifugo na mali nyingi, wanaoishi katikati ya nchi.” 1338:13 Mwa 10:7; Eze 27:22; Isa 33:23; Yer 15:13; Mwa 25:3; Isa 10:6Sheba na Dedani pamoja na wafanyabiashara wa Tarshishi na vijiji vyake vyote watakuambia, “Je, umekuja kuteka mateka? Je, umekusanya makundi yako ya wajeuri ili kuchukua nyara mali, kutwaa fedha na dhahabu, kutunyangʼanya mifugo na mali na kuteka nyara nyingi zaidi?” ’

1438:14 Law 25:18; Yer 16:15; Zek 2:5“Kwa hiyo, mwanadamu, tabiri na umwambie Gogu: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Katika siku ile, watu wangu Israeli watakapokuwa wanaishi salama, Je, wewe mwenyewe hutalijua hilo? 1538:15 Eze 39:2; Ufu 20:8; Eze 32:30Utakuja kutoka kwako huko kaskazini ya mbali, ukiwa pamoja na mataifa mengi, wote wakiwa wamepanda farasi, kundi kubwa, jeshi kuu. 1638:16 Eze 38:9; 38:8; Kut 14:4; Eze 36:23; 39:21Utakuja dhidi ya watu wangu Israeli kama wingu lifunikavyo nchi. Siku zijazo, ee Gogu, nitakuleta wewe dhidi ya nchi yangu, ili kwamba mataifa wapate kunijua Mimi nitakapojionyesha mtakatifu kwa kukupitia wewe mbele ya macho yao.

17“ ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Je, wewe si yule niliyenena juu yako katika siku za zamani kwa kupitia kwa watumishi wangu manabii wa Israeli? Wakati ule walitabiri kwa miaka mingi kwamba ningekuleta upigane nao. 18Hili ndilo litakalotokea katika siku ile: Gogu atakaposhambulia nchi ya Israeli, hasira yangu kali itaamka, asema Bwana Mwenyezi. 1938:19 Za 18:7; Hag 2:6, 21; Isa 29:23; Yoe 3:11; Law 10:3Katika wivu wangu na ghadhabu yangu kali ninasema kuwa wakati ule patakuwepo tetemeko kuu katika nchi ya Israeli. 2038:20 Za 76:8; Yer 4:24; Kut 15:14; Isa 42:15; Ay 14:18; Hos 4:3Samaki wa baharini, ndege wa angani, wanyama wa kondeni, kila kiumbe kitambaacho ardhini, na watu wote walio juu ya uso wa nchi watatetemeka mbele zangu. Milima itapinduka, majabali yatapasuka na kila ukuta utaanguka chini. 2138:21 Isa 66:16; Kut 9:18; Ufu 16:21; Yer 25:31; Amu 7:22; 1Sam 14:20; Hag 2:22Nitaita upanga vita dhidi ya Gogu juu ya milima yangu yote, asema Bwana Mwenyezi. Upanga wa kila mtu utakuwa dhidi ya ndugu yake. 2238:22 Yer 25:31; Eze 36:5; 14:19; Kut 9:18; Za 18:12; Ufu 16:21Nitatekeleza hukumu juu yake kwa tauni na kwa umwagaji wa damu. Nitaifanya mvua ya mafuriko kunyesha, mvua ya mawe na moto wa kiberiti juu yake na juu ya vikosi vyake na juu ya mataifa mengi walio pamoja naye. 2338:23 Eze 20:42; 36:23; 37:6Nami hivyo ndivyo nitakavyoonyesha ukuu wangu na utakatifu wangu, nami nitajijulisha mbele ya macho ya mataifa mengi. Ndipo watakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.’

New International Version

Ezekiel 38:1-23

The Lord’s Great Victory Over the Nations

1The word of the Lord came to me: 2“Son of man, set your face against Gog, of the land of Magog, the chief prince of38:2 Or the prince of Rosh, Meshek and Tubal; prophesy against him 3and say: ‘This is what the Sovereign Lord says: I am against you, Gog, chief prince of38:3 Or Gog, prince of Rosh, Meshek and Tubal. 4I will turn you around, put hooks in your jaws and bring you out with your whole army—your horses, your horsemen fully armed, and a great horde with large and small shields, all of them brandishing their swords. 5Persia, Cush38:5 That is, the upper Nile region and Put will be with them, all with shields and helmets, 6also Gomer with all its troops, and Beth Togarmah from the far north with all its troops—the many nations with you.

7“ ‘Get ready; be prepared, you and all the hordes gathered about you, and take command of them. 8After many days you will be called to arms. In future years you will invade a land that has recovered from war, whose people were gathered from many nations to the mountains of Israel, which had long been desolate. They had been brought out from the nations, and now all of them live in safety. 9You and all your troops and the many nations with you will go up, advancing like a storm; you will be like a cloud covering the land.

10“ ‘This is what the Sovereign Lord says: On that day thoughts will come into your mind and you will devise an evil scheme. 11You will say, “I will invade a land of unwalled villages; I will attack a peaceful and unsuspecting people—all of them living without walls and without gates and bars. 12I will plunder and loot and turn my hand against the resettled ruins and the people gathered from the nations, rich in livestock and goods, living at the center of the land.38:12 The Hebrew for this phrase means the navel of the earth.13Sheba and Dedan and the merchants of Tarshish and all her villages38:13 Or her strong lions will say to you, “Have you come to plunder? Have you gathered your hordes to loot, to carry off silver and gold, to take away livestock and goods and to seize much plunder?” ’

14“Therefore, son of man, prophesy and say to Gog: ‘This is what the Sovereign Lord says: In that day, when my people Israel are living in safety, will you not take notice of it? 15You will come from your place in the far north, you and many nations with you, all of them riding on horses, a great horde, a mighty army. 16You will advance against my people Israel like a cloud that covers the land. In days to come, Gog, I will bring you against my land, so that the nations may know me when I am proved holy through you before their eyes.

17“ ‘This is what the Sovereign Lord says: You are the one I spoke of in former days by my servants the prophets of Israel. At that time they prophesied for years that I would bring you against them. 18This is what will happen in that day: When Gog attacks the land of Israel, my hot anger will be aroused, declares the Sovereign Lord. 19In my zeal and fiery wrath I declare that at that time there shall be a great earthquake in the land of Israel. 20The fish in the sea, the birds in the sky, the beasts of the field, every creature that moves along the ground, and all the people on the face of the earth will tremble at my presence. The mountains will be overturned, the cliffs will crumble and every wall will fall to the ground. 21I will summon a sword against Gog on all my mountains, declares the Sovereign Lord. Every man’s sword will be against his brother. 22I will execute judgment on him with plague and bloodshed; I will pour down torrents of rain, hailstones and burning sulfur on him and on his troops and on the many nations with him. 23And so I will show my greatness and my holiness, and I will make myself known in the sight of many nations. Then they will know that I am the Lord.’