Ezekieli 37 – NEN & CCB

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ezekieli 37:1-28

Bonde La Mifupa Mikavu

137:1 Eze 8:3; 11:24; Yer 7:32; 40:1; Lk 4:1; Yer 8:2; Mdo 8:39Mkono wa Bwana ulikuwa juu yangu, naye akanitoa nje kwa Roho wa Bwana na kuniweka katikati ya bonde lililokuwa limejaa mifupa tele. 2Akanipitisha pande zote kwenye hiyo mifupa, nami nikaona mifupa mingi sana ndani ya lile bonde, mifupa iliyokuwa imekauka sana. 337:3 1Sam 2:6; 1Kor 15:35; Rum 4:17; Isa 26:19Akaniuliza, “Mwanadamu, mifupa hii yaweza kuishi?”

Nikajibu, “Ee Bwana Mwenyezi, wewe peke yako wajua.”

437:4 Yer 22:29; Rum 10:17Ndipo akaniambia, “Itabirie mifupa hii na uiambie, ‘Enyi mifupa mikavu, sikieni neno la Bwana! 537:5 Mwa 2:7; Ufu 11:11Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo kwa hii mifupa: Nitatia pumzi37:5 Pumzi pia ina maana ya roho kwa Kiebrania. ndani yenu, nanyi mtaishi. 637:6 Kut 6:2; Yoe 2:27; Eze 38:23Nitawawekea mishipa, nami nitaifanya nyama ije juu yenu na kuwafunika kwa ngozi. Nitatia pumzi ndani yenu, nanyi mtakuwa hai. Ndipo mtakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.’ ”

7Basi nikatabiri kama nilivyoamriwa. Wakati nilipokuwa ninatabiri, kukawa na sauti, sauti ya kugongana, nayo mifupa ikasogeleana, mfupa kwa mfupa mwenziwe. 8Nikatazama, mishipa na nyama vikatokea juu ya mifupa na ngozi ikaifunika, lakini hapakuwepo pumzi ndani yake.

937:9 Isa 32:15; Zek 12:10; Eze 39:29; Za 104:30; Yer 49:36; Zek 6:5; Dan 7:2Ndipo aliponiambia, “Utabirie upepo, tabiri, mwanadamu na uuambie, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Njoo kutoka pande nne, ee pumzi, nawe upulizie pumzi ndani ya hawa waliouawa, ili wapate kuishi.’ ” 1037:10 Ufu 11:11; Eze 12:7Hivyo nikatabiri kama alivyoniamuru, nayo pumzi ikawaingia, wakawa hai na wakasimama kwa miguu yao, jeshi kubwa mno.

1137:11 Ay 17:15; Mao 3:54; Isa 49:14Ndipo akaniambia: “Mwanadamu, mifupa hii ni nyumba yote ya Israeli. Nao wanasema, ‘Mifupa yetu imekauka na tumaini letu limetoweka, tumekatiliwa mbali.’ 1237:12 Sef 3:20; Yer 29:14; Amo 9:14; 1Sam 2:9; Kum 32:39; Isa 26:19; Hos 13:14Hivyo watabirie na uwaambie: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Enyi watu wangu, nitayafunua makaburi yenu na kuwatoa ndani yake, nami nitawarudisha tena katika nchi ya Israeli. 1337:13 Kut 6:2; Eze 17:24; Hos 13:14Ndipo ninyi watu wangu, mtakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana, nitakapoyafunua makaburi yenu na kuwatoa humo. 1437:14 Isa 11:2; Yoe 2:28-29; Eze 36:27-28; Yer 43:2; Ufu 11:11Nitatia Roho yangu ndani yenu nanyi mtaishi, nami nitawakalisha katika nchi yenu wenyewe. Ndipo mtakapojua kwamba Mimi Bwana nimenena, nami nitalitenda, asema Bwana!’ ”

Taifa Moja Chini Ya Mfalme Mmoja

15Neno la Bwana likanijia kusema: 1637:16 Hes 17:2; 1Fal 12:20; 2Nya 10:17-19; 15:9“Mwanadamu, chukua fimbo na uandike juu yake, ‘Hii ni kwa ajili ya Yuda na Waisraeli waliofungamana naye.’ Kisha chukua fimbo nyingine, uandike juu yake, ‘Fimbo ya Efraimu, ni kwa ajili ya Yosefu na nyumba yote ya Israeli wanaofungamana naye.’ 1737:17 Isa 11:13; Hos 1:11; Yer 50:4Ziunganishe pamoja kuwa fimbo moja ili kwamba ziwe fimbo moja katika mkono wako.

1837:18 Eze 24:19; 12:9“Watu wako watakapokuuliza, ‘Je, hutatuambia ni nini maana ya jambo hili?’ 1937:19 Zek 10:6Waambie, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Nitaichukua fimbo ya Yosefu, iliyoko mikononi mwa Efraimu na ya makabila ya Israeli yanayofungamana naye na kuiunganisha na fimbo ya Yuda, nikizifanya kuwa fimbo moja, nao watakuwa wamoja katika mkono wangu.’ 2037:20 Eze 12:3Inua mbele ya macho yao zile fimbo ulizoziandika 2137:21 Isa 43:5-6; Mik 4:6; Eze 20:42; 39:27kisha waambie, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Nitawatoa Waisraeli katika mataifa walikokuwa wamekwenda. Nitawakusanya popote walipo na kuwarudisha katika nchi yao wenyewe. 2237:22 Isa 11:13; Yer 3:18; Yn 10:16; Eze 17:22; 34:13-14; Yer 33:24Nitawafanya kuwa taifa moja katika nchi, katika milima ya Israeli. Patakuwa na mfalme mmoja juu yao wote na kamwe hawatagawanyika tena kuwa mataifa mawili au kugawanyika katika falme mbili. 2337:23 Isa 2:18; Nah 2:2; Eze 11:18; Hos 14:8; Zek 13:2-3; Yer 7:24; Eze 43:7Hawatajitia tena unajisi kwa sanamu zao na vinyago vyao visivyo na maana wala kwa makosa yao yoyote, kwa maana nitawaokoa kutoka dhambi zao zote zilizowarudisha nyuma, nami nitawatakasa. Wao watakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wao.

2437:24 Isa 55:4; Hos 3:5; Amo 9:15; Za 78:70-71; Yer 30:21; 1Sam 13:14“ ‘Mtumishi wangu Daudi atakuwa mfalme juu yao, nao wote watakuwa na mchungaji mmoja. Watafuata sheria zangu na kuzishika amri zangu kwa uangalifu. 2537:25 Ezr 9:12; Amo 9:15; Za 89:3-4; Eze 28:25; Isa 11:1; Eze 34:23-24Wataishi katika nchi niliyompa mtumishi wangu Yakobo, nchi ambamo baba zenu waliishi. Wao na watoto wao na watoto wa watoto wao wataishi humo milele, naye Daudi mtumishi wangu atakuwa mkuu wao milele. 2637:26 Hes 25:12; Isa 55:3; Yer 30:19; Eze 16:62; Mwa 9:16; Kum 29:14Nitafanya nao Agano la amani, litakuwa Agano la milele. Nitawafanya imara na kuongeza idadi yao, nami nitaweka mahali patakatifu pangu miongoni mwao milele. 2737:27 Law 26:11; Yn 1:14; Eze 34:30; 2Kor 6:16; Eze 36:28Maskani yangu yatakuwa pamoja nao, nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu. 2837:28 Kut 31:13; Eze 20:12; Hos 1:10-11; Eze 43:9; Sef 3:15Ndipo mataifa watakapojua kwamba Mimi Bwana ndiye ninayeifanya Israeli kuwa takatifu, wakati mahali patakatifu pangu patakapokuwa miongoni mwao milele.’ ”

Chinese Contemporary Bible (Simplified)

以西结书 37:1-28

枯骨复活

1耶和华的灵降在我身上,把我带到一个山谷,那里遍地都是骸骨。 2祂领我环绕那些骸骨走了一圈,我见到谷中枯干的骸骨相当多。 3祂对我说:“人子啊,这些骸骨能复活吗?”我说:“主耶和华啊,只有你知道。” 4祂又对我说:“你对这些骸骨发预言说,‘枯骨啊,你们要听耶和华说的话! 5主耶和华说,我要使气息进入你们里面,你们就必复活过来。 6我必给你们加上筋,使你们长出肉,再包上皮,将气息放在你们里面,你们就复活了。这样,你们就知道我是耶和华。’”

7于是,我便按耶和华的吩咐向枯骨发预言,我正说预言的时候,忽然有震动的声音,骨头便连在了一起。 8我又发现骨头上有了筋,长了肉,包上了皮,只是还没有气息。 9耶和华对我说:“人子啊,你要向风37:9 ”希伯来文又作“灵”,“气息”。说预言,告诉风,主耶和华这样说,‘风啊,从四方吹来,吹在这些被杀的人身上,使他们复活。’” 10于是,我便按耶和华的吩咐说预言,气息就进入他们里面,他们便复活了,并且站立起来,成为一支大军。

11耶和华对我说:“人子啊,这些骸骨就是所有的以色列人,他们说,‘我们骨头枯干,希望幻灭,彻底完了。’ 12你要说预言,告诉他们,‘主耶和华说,我的子民啊,我要打开你们的坟墓,领你们出来,我要领你们返回以色列13我的子民啊,当我这样做的时候,你们就知道我是耶和华。 14我要把我的灵放在你们里面,叫你们复活,安居在自己的土地上,那时你们就知道我耶和华言出必行。这是耶和华说的。’”

15耶和华对我说: 16“人子啊,你拿一根杖来,写上‘犹大和他的以色列同伴’,然后再拿另一根杖,写上‘约瑟,即以法莲,与他的以色列同伴’。 17然后把这两根杖连成一根,拿在手中。 18当你的同胞问你这是什么意思时, 19你就告诉他们,主耶和华这样说,‘我要把约瑟和他的以色列同伴的杖,就是以法莲手中的杖,与犹大的杖在我手中连成一根。’ 20你要拿着这两根写着字的杖让他们看, 21告诉他们,主耶和华这样说,‘我要把以色列的百姓从他们分散的各国招聚起来,领他们回归故土。 22我要使他们在以色列的土地和群山上成为一国,只有一位王统治他们,不再分为两个国家。 23他们不会再因祭拜偶像、行可憎之事而玷污自己,我要从他们犯罪的地方把他们救出来,洗净他们的罪。他们要做我的子民,我要做他们的上帝。

24“‘我的仆人大卫要做王治理他们,成为他们唯一的牧人。他们必恪守我的典章,谨遵我的律例。 25他们要安居在我赐给我仆人雅各的土地上,就是你们祖先居住的地方。他们世世代代都要居住在那里,我仆人大卫要永远做他们的王。 26我要与他们订立永存的平安之约,使他们安居,人丁兴旺。我的圣所要永远设立在他们当中。 27我要住在他们中间。我要做他们的上帝,他们要做我的子民。 28各国的人看见我的圣所永远设立在他们当中,便会知道是我耶和华使以色列圣洁了。’”