Ezekieli 35 – NEN & BPH

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ezekieli 35:1-15

Unabii Dhidi Ya Edomu

1Neno la Bwana likanijia kusema: 235:2 Mwa 14:6; Kum 2:5; Yer 49:7-8; Amo 1:11“Mwanadamu, elekeza uso wako juu ya mlima Seiri, utabiri dhidi yake 335:3 Yer 6:12; Eze 34:10; 25:12-14; Oba 1:10na useme: ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Mimi ni kinyume nawe, ee mlima Seiri, nami nitanyoosha mkono wangu dhidi yako na kukufanya ukiwa na usiyekaliwa na watu wala kulimika. 435:4 Yer 49:10; 44:2Nitaifanya miji yako kuwa magofu nawe utakuwa ukiwa. Ndipo utakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.

535:5 Za 137:7; Eze 21:29; Za 63:10; Oba 1:13“ ‘Kwa sababu ulificha moyoni uadui wa siku nyingi nawe ukawatoa Waisraeli wauawe kwa upanga wakati wa maafa yao, wakati adhabu yake ilipofikia kilele chake, 635:6 Isa 63:2-6; 34:3kwa hiyo hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, nitakutia katika umwagaji damu nao utakufuatia. Kwa kuwa hakuchukia kumwaga damu, kumwaga damu kutakufuatia. 735:7 Yer 46:19; 49:17Nitaufanya Mlima Seiri ukiwa na usiokaliwa na watu wala kulimika na kuukatilia mbali na wote wanaokuja na wanaokwenda. 835:8 Eze 31:12Nitaijaza milima yenu kwa watu wake waliouawa, wale waliouawa kwa upanga wataanguka juu ya vilima vyako na katika mabonde yako na katika makorongo yako yote. 935:9 Isa 34:5-6; Yer 49:13-17; Oba 1:10Nitakufanya ukiwa milele, watu hawataishi katika miji yako. Ndipo utakapojua kuwa Mimi ndimi Bwana.

1035:10 Za 83:12; Eze 36:2-5“ ‘Kwa sababu umesema, “Mataifa haya mawili na nchi hizi zitakuwa zetu nasi tutazimiliki,” ingawa hata mimi Bwana nilikuwa huko, 1135:11 Eze 25:14; Oba 1:15; Mt 7:2; Isa 26:9; Za 9:16kwa hiyo hakika kama niishivyo, asema Bwana Mwenyezi, nitakutenda kwa kadiri ya hasira na wivu uliouonyesha katika chuki yako juu yao nami nitafanya nijulikane miongoni mwao wakati nitakapokuhukumu. 1235:12 Yer 50:7; Za 9:16Ndipo utakapojua kuwa Mimi Bwana nimesikia mambo yote ya dharau uliyosema dhidi ya milima ya Israeli. Ulisema, “Wamefanyika ukiwa na kutiwa mikononi mwetu tuwararue.” 1335:13 Dan 11:36; Yer 49:16Ulijigamba dhidi yangu na kusema maneno dhidi yangu bila kujizuia, nami nikayasikia. 1435:14 Yer 51:48Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: Wakati dunia yote inashangilia nitakufanya ukiwa. 1535:15 Mit 17:5; Eze 36:5; Oba 1:12; Mao 4:4-21; Yer 50:11-13; Isa 34:5-6; Eze 32:29Kwa sababu ulishangilia wakati urithi wa nyumba ya Israeli ulipofanyika ukiwa, hivyo ndivyo nitakavyokutendea. Utakuwa ukiwa, ee mlima Seiri, wewe na Edomu yote. Kisha ndipo watajua kuwa Mimi ndimi Bwana.’ ”

Bibelen på hverdagsdansk

Ezekiels Bog 35:1-15

Dom over Edom

1Herren sagde til mig: 2„Du menneske, ret blikket mod Seirs bjerg og profetér imod Edoms folk:

3Jeg er imod jer, Seirs stolte bjerge. Jeg løfter min hånd for at straffe jer og gøre jeres land til en ødemark. 4Jeg jævner jeres byer med jorden og lægger hele landet øde, så I kan forstå, at jeg er Herren.

5I har altid hadet mit folk, Israel. I overfaldt dem og sablede dem ned, dengang jeg var nødt til at straffe dem. 6Så sandt jeg lever, siger Herren: I elsker at se blod, og I skal få blod at se, for nu kommer turen til jer. 7Jeg gør Seirs bjerge til ødemark og udrydder folket, som færdes der. 8Jeg sørger for, at bjergsider, dale og vandløb bliver fyldt med lig. 9Landet bliver en ødemark for evigt, og ingen skal bo i byerne igen. Da skal I indse, at jeg er Herren.

10I rykkede ud mod Israel og Juda for at erobre dem, selvom I vidste, at jeg var deres Gud. 11Så sandt jeg lever, vil jeg straffe jer på grund af jeres vrede, had og jalousi, og I skal erkende, at det er mig, Herren, som griber ind og dømmer jer. 12Da skal I indse, at jeg hørte hvert eneste hånende ord, I udtalte imod Israels bjerge, da I mente, at de lå øde hen, og at I derfor havde ret til at besætte dem. 13I hånede mig med de mange ord, I udtalte imod mig. Men jeg hørte det alt sammen.

14Gud Herren siger: Hele verden vil fryde sig over jeres undergang. 15I frydede jer over Israels sørgelige skæbne. Nu er det min tur til at fryde mig over jeres, for I vil blive udryddet, alle I folk i Seirs bjerge og i hele Edom. Da skal I indse, at jeg er Herren.