Ezekieli 32 – NEN & NIRV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ezekieli 32:1-32

Maombolezo Kwa Ajili Ya Farao

132:1 Eze 31:1; 33:21Katika mwaka wa kumi na mbili, mwezi wa kumi na mbili, siku ya kwanza ya mwezi, neno la Bwana likanijia, kusema: 232:2 2Sam 1:17; 2Nya 35:25; 2Fal 24:1; Nah 2:11-13; Ay 41:31; Eze 29:3; Ay 3:8; Eze 34:18; 2Sam 3:33“Mwanadamu, fanya maombolezo kwa ajili ya Farao mfalme wa Misri na umwambie:

“ ‘Wewe ni kama simba miongoni mwa mataifa,

wewe ni kama joka kubwa baharini,

unayevuruga maji kwa miguu yako

na kuchafua vijito.

332:3 Eze 12:13; Hab 1:15“ ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo:

“ ‘Nikiwa pamoja na wingi mkubwa wa watu

nitautupa wavu wangu juu yako,

nao watakukokota katika wavu wangu.

432:4 Isa 18:6; 1Sam 17:44-46; Eze 39:4-5; 31:12-13Nitakutupa nchi kavu

na kukuvurumisha uwanjani.

Nitawafanya ndege wote wa angani watue juu yako

na wanyama wote wa nchi

watajishibisha nyama yako.

532:5 Eze 31:12Nitatawanya nyama yako juu ya milima

na kujaza mabonde kwa mabaki yako.

632:6 Isa 34:3; Eze 29:5Nitailowanisha nchi kwa damu yako inayotiririka

njia yote hadi milimani,

nayo mabonde yatajazwa na nyama yako.

732:7 Yoe 3:15; Mt 24:29; Ufu 6:12; Isa 34:4; Eze 30:3; Yoe 2:2Nitakapokuzimisha, nitafunika mbingu

na kuzitia nyota zake giza;

nitalifunika jua kwa wingu,

nao mwezi hautatoa nuru yake.

832:8 Za 102:26; Ay 9:7; Yer 4:23; Yoe 2:10Mianga yote itoayo nuru angani

nitaitia giza juu yako;

nitaleta giza juu ya nchi yako,

asema Bwana Mwenyezi.

9Nitaifadhaisha mioyo ya mataifa mengi

nitakapokuangamiza miongoni mwa mataifa,

nikikuleta uhamishoni miongoni mwa nchi

ambazo haujapata kuzijua.

1032:10 Yer 46:10; Eze 26:16; Ufu 18:9-10; Isa 30:32; Eze 27:35; 30:9Nitayafanya mataifa mengi wakustaajabie,

wafalme wao watatetemeka

kwa hofu kwa ajili yako

nitakapotikisa upanga wangu mbele yao.

Siku ya anguko lako

kila mmoja wao atatetemeka

kila dakika kwa ajili ya maisha yake.

1132:11 Isa 19:4; Yer 46:26; Eze 21:19; 46:13; 29:19“ ‘Kwa kuwa hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo:

“ ‘Upanga wa mfalme wa Babeli

utakuja dhidi yako.

1232:12 Eze 28:7; 31:11-12Nitafanya makundi yako ya wajeuri kuanguka

kwa panga za watu mashujaa,

taifa katili kuliko mataifa yote.

Watakivunjavunja kiburi cha Misri,

nayo makundi yake yote

ya wajeuri yatashindwa.

1332:13 Eze 29:8-11Nitaangamiza mifugo yake yote

wanaojilisha kando ya maji mengi,

hayatavurugwa tena kwa mguu wa mwanadamu

wala kwato za mnyama

hazitayachafua tena.

14Kisha nitafanya maji yake yatulie

na kufanya vijito vyake

vitiririke kama mafuta,

asema Bwana Mwenyezi.

1532:15 Kut 7:5; Za 107:33-34; Kut 14:4; 18Nitakapoifanya Misri kuwa ukiwa

na kuiondolea nchi kila kitu

kilichomo ndani yake,

nitakapowapiga wote waishio humo,

ndipo watakapojua kuwa

Mimi ndimi Bwana.’

1632:16 Mwa 50:10; 2Sam 1:17; Eze 26:17; 19:1“Hili ndilo ombolezo watakalomwimbia. Binti za mataifa wataliimba, kwa kuwa Misri na makundi yake yote ya wajeuri wataliimba, asema Bwana Mwenyezi.”

17Katika mwaka wa kumi na mbili, mwezi wa kwanza, siku ya kumi na tano ya mwezi, neno la Bwana likanijia kusema: 1832:18 Yer 1:10; Mik 1:8; Eze 26:20; 31:14-16; 32:1“Mwanadamu, omboleza kwa ajili ya makundi ya wajeuri wa Misri na uwatupe kuzimu yeye na binti za mataifa yenye nguvu, waende huko pamoja nao washukao shimoni. 1932:19 Eze 28:10; 31:18Je, ninyi mnamzidi nani kwa uzuri? Shukeni chini! Nanyi mkalazwe pamoja na hao wasiotahiriwa! 2032:20 Za 28:3; Eze 31:17-18Wataanguka miongoni mwa wale waliouawa kwa upanga. Upanga umefutwa, mwache aburutwe mbali pamoja na hao wajeuri wake wote. 2132:21 Isa 14:9; Eze 28:10Kutoka kuzimu viongozi hodari watanena kuhusu Misri pamoja na wale walioungana nao, ‘Wameshuka chini, nao wamelala kimya pamoja na hao wasiotahiriwa, pamoja na wale waliouawa kwa upanga.’

2232:22 Eze 32:24, 26, 29, 30“Ashuru yuko huko pamoja na jeshi lake lote, amezungukwa na makaburi ya watu wake wote waliouawa, wale wote walioanguka kwa upanga. 2332:23 Isa 14:15; Nah 1:14Makaburi yao yako kwenye kina cha chini cha shimo na jeshi lake limelala kulizunguka kaburi lake. Wote waliokuwa wameeneza hofu kuu katika nchi ya walio hai wameuawa, wameanguka kwa upanga.

2432:24 Mwa 10:22; Yer 49:37; Ay 28:13; Eze 26:20“Elamu yuko huko, pamoja na makundi yake yote ya wajeuri wakiwa wamelizunguka kaburi lake. Wote wameuawa, wameanguka kwa upanga. Wote waliokuwa wameeneza hofu katika nchi ya walio hai walishuka kuzimu bila kutahiriwa. Wanaichukua aibu yao pamoja na wale washukao shimoni. 2532:25 Eze 28:10; 28:10Kitanda kimetandikwa kwa ajili yake miongoni mwa waliouawa, pamoja na makundi yake yote ya wajeuri wakiwa wamelizunguka kaburi lake. Wote ni watu wasiotahiriwa, wameuawa kwa upanga. Kwa sababu vitisho vyao vilienea katika nchi ya walio hai, wameichukua aibu yao pamoja na wale washukao shimoni, nao wamewekwa miongoni mwa waliouawa.

2632:26 Mwa 10:2; Eze 27:13“Mesheki na Tubali wako humo, pamoja na makundi yao ya wajeuri wakiwa wameyazunguka makaburi yao. Wote hawakutahiriwa, wameuawa kwa upanga kwa sababu walieneza vitisho vyao katika nchi ya walio hai. 27Je, hawakulala na mashujaa wengine wasiotahiriwa waliouawa, ambao wameshuka kaburini wakiwa na silaha zao za vita, ambao panga zao ziliwekwa chini ya vichwa vyao na uovu wao juu ya mifupa yao? Adhabu kwa ajili ya dhambi zao ilikuwa juu ya mifupa yao, ingawa vitisho vya mashujaa hawa vilikuwa vimeenea hadi kwenye nchi ya walio hai.

28“Wewe pia, ee Farao, utavunjwa nawe utalala miongoni mwa wasiotahiriwa, pamoja na wale waliouawa kwa upanga.

2932:29 Za 137:7; Eze 25:12-14; 35:15; Yer 49:7; Isa 34:5-15“Edomu yuko humo, wafalme wake wote na wakuu wake wote, ambao ijapokuwa wana nguvu, wamelazwa pamoja na wale waliouawa kwa upanga. Wamelala pamoja na wasiotahiriwa, pamoja na wale washukao shimoni.

3032:30 Isa 14:31; Yer 25:26; Mwa 10:15; Eze 38:6; Yer 25:22; Eze 28:10; 28:8“Wakuu wote wa kaskazini na Wasidoni wote wako huko, wameshuka chini pamoja na waliouawa kwa aibu ijapokuwa kuna vitisho vilivyosababishwa na nguvu zao. Wamelala bila kutahiriwa pamoja na wale waliouawa kwa upanga na kuchukua aibu yao pamoja na wale washukao chini shimoni.

3132:31 Eze 14:22; 31:16“Farao, yeye pamoja na jeshi lake lote, atakapowaona atafarijiwa kwa ajili ya makundi yake yote ya wajeuri, wale waliouawa kwa upanga, asema Bwana Mwenyezi. 3232:32 Yer 44:30; Ay 3:14Ingawa nilimfanya Farao aeneze vitisho vyake katika nchi ya walio hai, Farao pamoja na makundi yake yote ya wajeuri watalazwa miongoni mwa wasiotahiriwa, pamoja na wale waliouawa kwa upanga, asema Bwana Mwenyezi.”

New International Reader’s Version

Ezekiel 32:1-32

1It was the 12th year since King Jehoiachin had been brought to Babylon as a prisoner. On the first day of the 12th month, a message from the Lord came to me. The Lord said, 2“Son of man, sing a song of sadness about Pharaoh Hophra, the king of Egypt. Tell him,

“ ‘You are like a lion among the nations.

You are like a monster in the sea.

You move around wildly in your rivers.

You churn the water with your feet.

You make the streams muddy.’ ”

3The Lord and King says,

“I will use a large crowd of people

to throw my net over you.

They will pull you up in it.

4Then I will throw you on the land.

I will toss you into an open field.

I will let all the birds in the sky settle on you.

I will let all the wild animals eat you up.

5I will scatter the parts of your body all over the mountains.

I will fill the valleys with your remains.

6I will soak the land with your blood.

It will flow all the way to the mountains.

The valleys will be filled with the parts of your body.

7When I wipe you out,

I will put a cover over the heavens.

I will darken the stars.

I will cover the sun with a cloud.

The moon will stop shining.

8I will darken all the bright lights

in the sky above you.

I will bring darkness over your land,”

announces the Lord and King.

9“The hearts of many people will be troubled.

That is because I will destroy you among the nations.

You had never known anything about those lands before.

10Many nations will be shocked

when they see what has happened to you.

Their kings will tremble with fear

when they find out about it.

I will get ready to use Nebuchadnezzar

as my sword against them.

On the day you fall from power,

each of the kings will tremble with fear.

Each will be afraid he is the next to die.”

11The Lord and King says,

“I will send against you

the sword of the king of Babylon.

12I will destroy your huge army.

They will be killed by the swords

of Babylon’s mighty soldiers.

The soldiers will not show them any pity.

They will bring Egypt down in all its pride.

Its huge armies will be thrown down.

13I will destroy all its cattle

from the places where they have plenty of water.

Human feet will never stir up the water again.

The hooves of cattle will not make it muddy anymore.

14I will let the waters of Egypt settle.

I will make its streams flow like olive oil,”

announces the Lord and King.

15“I will turn Egypt into an empty land.

I will strip away everything in it.

I will strike down everyone who lives there.

Then they will know that I am the Lord.

16“That is the song of sadness people will sing about Egypt. Women from other nations will sing it. They will weep over Egypt and its huge armies,” announces the Lord and King.

17A message from the Lord came to me. King Jehoiachin had been brought to Babylon as a prisoner. On the 15th day of a month 12 years after that, the message came. The Lord said, 18“Son of man, weep over the huge army of Egypt. Tell the Egyptians they will go down into the earth below. The women singers from the other mighty nations will go down into the grave along with them and others. 19Tell them, ‘Are you any better than others? Since you are not, go down there. Lie down with those who have not been circumcised.’ 20They will fall dead among those who were killed by swords. Nebuchadnezzar is ready to use his sword against them. Let Egypt be dragged off together with its huge armies. 21The mighty leaders who are already in the place of the dead will talk about Egypt. They will also speak about the nations that were going to help it. They will say, ‘They have come down here. They are lying down with those who had not been circumcised. They are here with those who were killed by swords.’

22“Assyria is there with its whole army. Its king is surrounded by the graves of all its people who were killed by swords. 23Their graves are deep down in the pit. Assyria’s army lies around the grave of its king. All those who spread terror while they were alive are now dead. They were killed by swords.

24“Elam is also there. Its huge armies lie around the grave of its king. All those who spread terror while they were alive are now dead. They were killed by swords. They had not been circumcised. They went down into the earth below. Their shame is like the shame of others who go down into the grave. 25A bed is made for Elam’s king among the dead. His huge armies lie around his grave. They had not been circumcised. They were killed by swords. They had spread terror while they were alive. So now their shame is like the shame of others who go down into the grave. They lie down among the dead.

26“Meshek and Tubal are also there. Their huge armies lie around the graves of their kings. None of them had been circumcised. They had spread their terror while they were alive. So they were killed by swords. 27But they do not lie down with the other dead soldiers of long ago. Those soldiers and their weapons had gone down into the place of the dead. Their swords had been placed under their heads. Their shields rest on their bones. The soldiers of Meshek and Tubal do not lie down with them. This is true even though they had also spread terror while they were alive.

28“Pharaoh Hophra, you too will be broken. You will lie down among those who had not been circumcised. You will be there with those who were killed by swords.

29“Edom is also there. So are its kings and all its princes. In spite of their power, they lie down with those who were killed by swords. They lie down with those who had not been circumcised. They are there with others who went down into the grave.

30“All the princes of the north are there too. So are all the people of Sidon. They went down into the grave in dishonor. While they were alive, they used their power to spread terror. They had never been circumcised. But now they lie down there with those who were killed by swords. Their shame is like the shame of others who go down into the grave.

31“Pharaoh and his whole army will see all of them. That will comfort him even though his huge armies were killed by swords.” This is what the Lord and King announces. 32“I let Pharaoh spread terror while he was alive. But now he and his huge armies will be buried with those who had not been circumcised. They will lie down there with those who were killed by swords,” announces the Lord and King.