Ezekieli 3 – NEN & KJV

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ezekieli 3:1-27

13:1 Eze 2:8, 9Naye akaniambia, “Mwanadamu, kula kile kilichoko mbele yako, kula huu ukurasa wa kitabu, kisha uende ukaseme na nyumba ya Israeli.” 23:2 Hes 11:25; Amu 13:25; Neh 9:30Ndipo nikafungua kinywa changu, naye akanilisha ule ukurasa wa kitabu.

33:3 Yer 15:16; Za 19:10; Ufu 10:9-10; Za 19:10Ndipo akaniambia, “Mwanadamu, kula ukurasa huu wa kitabu ninaokupa ujaze tumbo lako.” Kwa hiyo nikaula, ulikuwa mtamu kama asali kinywani mwangu.

4Kisha akaniambia, “Mwanadamu, sasa nenda katika nyumba ya Israeli ukaseme nao maneno yangu. 53:5 Isa 28:11; Yn 1:2Hukutumwa kwa taifa lenye maneno ya kutatiza na lugha ngumu, bali kwa nyumba ya Israeli. 63:6 Yn 3:5-10; Mt 11:21-23Sikukutuma kwa mataifa mengi yenye maneno ya kutatiza na lugha ngumu ambao maneno yao hutayaelewa. Hakika ningekutuma kwa watu hao, wangekusikiliza. 73:7 Isa 48:4; Yn 15:20-23; Yer 7:27; Eze 2:4Lakini nyumba ya Israeli haitakusikiliza kwa kuwa hawako radhi kunisikiliza mimi, kwa kuwa nyumba yote ya Israeli ni wenye vipaji vya nyuso vigumu na mioyo ya ukaidi. 83:8 Yer 1:18; 15:20Tazama nimefanya uso wako mgumu dhidi ya nyuso zao na kipaji cha uso wako kigumu dhidi ya vipaji vya nyuso zao. 93:9 Isa 50:7; 48:4; Mik 3:8; Eze 2:6; 4:6; Yer 5:3Kama vile almasi ilivyo ngumu kuliko gumegume, ndivyo nilivyokifanya kipaji cha uso wako. Usiwaogope wala usiwahofu, ijapokuwa ni nyumba ya kuasi.”

103:10 Ay 22:22Naye akaniambia, “Mwanadamu, sikiliza kwa makini na uyatie moyoni mwako maneno yote nitakayosema nawe. 113:11 Eze 43:5; Mdo 8:39; Eze 8:3Kisha nenda kwa watu wa taifa lako walio uhamishoni, ukaseme nao. Waambie, ‘Hivi ndivyo Bwana Mwenyezi asemavyo,’ kwamba watasikiliza au hawatasikiliza.”

123:12 Eze 3:14; 8:3; 43:5Ndipo Roho akaniinua, nikasikia sauti kubwa nyuma yangu ya ngurumo. (Utukufu wa Bwana na utukuzwe katika mahali pa makao yake!) 133:13 Eze 1:24; 10:5, 16-17; 1:15Ilikuwa ni sauti ya mabawa ya wale viumbe hai yakisuguana moja kwa jingine, sauti kama ya ngurumo. 143:14 1Fal 18:12; Isa 8:11; Eze 37:1Ndipo Roho aliponiinua na kunipeleka mbali. Nikaenda nikiwa na uchungu na hasira moyoni mwangu, nao mkono wa Bwana ukiwa juu yangu. 153:15 Mwa 50:10; Ay 2:13Nikafika kwa wale watu waliokuwa uhamishoni huko Tel-Abibu karibu na Mto Kebari. Nikakaa miongoni mwao kwa muda wa siku saba, nikiwa nimejawa na mshangao.

Onyo Kwa Israeli

163:16 Yer 42:7Mwishoni mwa hizo siku saba neno la Bwana likanijia kusema: 173:17 Isa 52:8; Yer 6:17; Wim 5:7; Eze 11:4; Yer 1:17; Isa 58:1“Mwanadamu, nimekufanya uwe mlinzi wa nyumba ya Israeli, kwa hiyo sikia neno nisemalo, ukawape onyo litokalo kwangu. 183:18 Eze 33:6; Rum 1:16; Mwa 2:17; Yn 8:21Nimwambiapo mtu mwovu, ‘Hakika utakufa,’ na wewe usipomwonya mtu huyo au kumshauri aache njia zake mbaya ili kuokoa maisha yake, huyo mtu mwovu atakufa katika dhambi yake na damu yake nitaidai mkononi mwako. 193:19 2Fal 17:13; 1Tim 4:14-16; Za 7:12; Yer 42:16; Eze 14:14-20; Mdo 18:6Lakini ukimwonya mtu mwovu naye akakataa kuacha uovu wake na njia zake mbaya, atakufa katika dhambi yake, lakini wewe utakuwa umejiokoa nafsi yako.

203:20 2Pet 2:20; Za 125:5; Eze 18:24; Yer 34:16; Isa 8:14; Law 26:37“Tena, mtu mwenye haki akiacha haki yake na kutenda maovu, nami nikaweka kikwazo mbele yake mtu huyo atakufa. Kwa kuwa hukumwonya, atakufa katika dhambi yake. Mambo ya haki aliyotenda, hayatakumbukwa, damu yake nitaidai mkononi mwako. 213:21 Mdo 20:31; Rum 2:7Lakini ukimwonya mwenye haki asitende dhambi na akaacha kutenda dhambi, hakika ataishi kwa sababu alipokea maonyo na utakuwa umejiokoa nafsi yako.”

223:22 Eze 8:4; Mdo 9:6Mkono wa Bwana ulikuwa juu yangu huko, naye akaniambia, “Simama uende mpaka sehemu tambarare, nami nitasema nawe huko.” 233:23 Mwa 17:3; Eze 1:28Kwa hiyo niliinuka nikaenda mpaka mahali pa tambarare. Utukufu wa Bwana ulikuwa umesimama huko, kama utukufu ule niliouona kando ya Mto Kebari, nami nikaanguka kifudifudi.

243:24 Eze 2:2; Yer 15:17Ndipo Roho akaja ndani yangu akanisimamisha kwa miguu yangu. Akasema nami akaniambia: “Nenda ukajifungie ndani ya nyumba yako. 253:25 Eze 4:8Nawe, ee mwanadamu, watakufunga kwa kamba, watakufunga ili usiweze kutoka na kuwaendea watu. 263:26 Eze 33:22; Hos 4:4; Eze 24:27; Za 22:15; Eze 2:5Nitaufanya ulimi wako ushikamane kwenye kaa la kinywa chako, ili uwe kimya usiweze kuwakemea, wajapokuwa ni nyumba ya kuasi. 273:27 Eze 24:27; 29:21; Ufu 22:11; Eze 12:3; 33:22Lakini nitakaposema nawe, nitafungua kinywa chako nawe utawaambia, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo.’ Yeyote atakayesikiliza na asikilize, na yeyote atakayekataa na akatae; kwa kuwa wao ni nyumba ya kuasi.

King James Version

Ezekiel 3:1-27

1Moreover he said unto me, Son of man, eat that thou findest; eat this roll, and go speak unto the house of Israel. 2So I opened my mouth, and he caused me to eat that roll. 3And he said unto me, Son of man, cause thy belly to eat, and fill thy bowels with this roll that I give thee. Then did I eat it; and it was in my mouth as honey for sweetness.

4¶ And he said unto me, Son of man, go, get thee unto the house of Israel, and speak with my words unto them. 5For thou art not sent to a people of a strange speech and of an hard language, but to the house of Israel;3.5 of a…: Heb. deep of lip, and heavy of tongue 6Not to many people of a strange speech and of an hard language, whose words thou canst not understand. Surely, had I sent thee to them, they would have hearkened unto thee.3.6 of a…: Heb. deep of lip, and heavy of language3.6 Surely…: or, If I had sent thee, etc. would they not have hearkened unto thee? 7But the house of Israel will not hearken unto thee; for they will not hearken unto me: for all the house of Israel are impudent and hardhearted.3.7 impudent…: Heb. stiff of forehead, and hard of heart 8Behold, I have made thy face strong against their faces, and thy forehead strong against their foreheads. 9As an adamant harder than flint have I made thy forehead: fear them not, neither be dismayed at their looks, though they be a rebellious house. 10Moreover he said unto me, Son of man, all my words that I shall speak unto thee receive in thine heart, and hear with thine ears. 11And go, get thee to them of the captivity, unto the children of thy people, and speak unto them, and tell them, Thus saith the Lord GOD; whether they will hear, or whether they will forbear. 12Then the spirit took me up, and I heard behind me a voice of a great rushing, saying, Blessed be the glory of the LORD from his place. 13I heard also the noise of the wings of the living creatures that touched one another, and the noise of the wheels over against them, and a noise of a great rushing.3.13 touched: Heb. kissed 14So the spirit lifted me up, and took me away, and I went in bitterness, in the heat of my spirit; but the hand of the LORD was strong upon me.3.14 in bitterness: Heb. bitter3.14 heat: Heb. hot anger

15¶ Then I came to them of the captivity at Tel-abib, that dwelt by the river of Chebar, and I sat where they sat, and remained there astonished among them seven days.

16And it came to pass at the end of seven days, that the word of the LORD came unto me, saying, 17Son of man, I have made thee a watchman unto the house of Israel: therefore hear the word at my mouth, and give them warning from me. 18When I say unto the wicked, Thou shalt surely die; and thou givest him not warning, nor speakest to warn the wicked from his wicked way, to save his life; the same wicked man shall die in his iniquity; but his blood will I require at thine hand. 19Yet if thou warn the wicked, and he turn not from his wickedness, nor from his wicked way, he shall die in his iniquity; but thou hast delivered thy soul. 20Again, When a righteous man doth turn from his righteousness, and commit iniquity, and I lay a stumblingblock before him, he shall die: because thou hast not given him warning, he shall die in his sin, and his righteousness which he hath done shall not be remembered; but his blood will I require at thine hand.3.20 righteousness which: Heb. righteousnesses 21Nevertheless if thou warn the righteous man, that the righteous sin not, and he doth not sin, he shall surely live, because he is warned; also thou hast delivered thy soul.

22¶ And the hand of the LORD was there upon me; and he said unto me, Arise, go forth into the plain, and I will there talk with thee. 23Then I arose, and went forth into the plain: and, behold, the glory of the LORD stood there, as the glory which I saw by the river of Chebar: and I fell on my face. 24Then the spirit entered into me, and set me upon my feet, and spake with me, and said unto me, Go, shut thyself within thine house. 25But thou, O son of man, behold, they shall put bands upon thee, and shall bind thee with them, and thou shalt not go out among them: 26And I will make thy tongue cleave to the roof of thy mouth, that thou shalt be dumb, and shalt not be to them a reprover: for they are a rebellious house.3.26 a reprover: Heb. a man reproving 27But when I speak with thee, I will open thy mouth, and thou shalt say unto them, Thus saith the Lord GOD; He that heareth, let him hear; and he that forbeareth, let him forbear: for they are a rebellious house.