Ezekieli 3 – NEN & BPH

Kiswahili Contemporary Version (Neno: Bibilia Takatifu)

Ezekieli 3:1-27

13:1 Eze 2:8, 9Naye akaniambia, “Mwanadamu, kula kile kilichoko mbele yako, kula huu ukurasa wa kitabu, kisha uende ukaseme na nyumba ya Israeli.” 23:2 Hes 11:25; Amu 13:25; Neh 9:30Ndipo nikafungua kinywa changu, naye akanilisha ule ukurasa wa kitabu.

33:3 Yer 15:16; Za 19:10; Ufu 10:9-10; Za 19:10Ndipo akaniambia, “Mwanadamu, kula ukurasa huu wa kitabu ninaokupa ujaze tumbo lako.” Kwa hiyo nikaula, ulikuwa mtamu kama asali kinywani mwangu.

4Kisha akaniambia, “Mwanadamu, sasa nenda katika nyumba ya Israeli ukaseme nao maneno yangu. 53:5 Isa 28:11; Yn 1:2Hukutumwa kwa taifa lenye maneno ya kutatiza na lugha ngumu, bali kwa nyumba ya Israeli. 63:6 Yn 3:5-10; Mt 11:21-23Sikukutuma kwa mataifa mengi yenye maneno ya kutatiza na lugha ngumu ambao maneno yao hutayaelewa. Hakika ningekutuma kwa watu hao, wangekusikiliza. 73:7 Isa 48:4; Yn 15:20-23; Yer 7:27; Eze 2:4Lakini nyumba ya Israeli haitakusikiliza kwa kuwa hawako radhi kunisikiliza mimi, kwa kuwa nyumba yote ya Israeli ni wenye vipaji vya nyuso vigumu na mioyo ya ukaidi. 83:8 Yer 1:18; 15:20Tazama nimefanya uso wako mgumu dhidi ya nyuso zao na kipaji cha uso wako kigumu dhidi ya vipaji vya nyuso zao. 93:9 Isa 50:7; 48:4; Mik 3:8; Eze 2:6; 4:6; Yer 5:3Kama vile almasi ilivyo ngumu kuliko gumegume, ndivyo nilivyokifanya kipaji cha uso wako. Usiwaogope wala usiwahofu, ijapokuwa ni nyumba ya kuasi.”

103:10 Ay 22:22Naye akaniambia, “Mwanadamu, sikiliza kwa makini na uyatie moyoni mwako maneno yote nitakayosema nawe. 113:11 Eze 43:5; Mdo 8:39; Eze 8:3Kisha nenda kwa watu wa taifa lako walio uhamishoni, ukaseme nao. Waambie, ‘Hivi ndivyo Bwana Mwenyezi asemavyo,’ kwamba watasikiliza au hawatasikiliza.”

123:12 Eze 3:14; 8:3; 43:5Ndipo Roho akaniinua, nikasikia sauti kubwa nyuma yangu ya ngurumo. (Utukufu wa Bwana na utukuzwe katika mahali pa makao yake!) 133:13 Eze 1:24; 10:5, 16-17; 1:15Ilikuwa ni sauti ya mabawa ya wale viumbe hai yakisuguana moja kwa jingine, sauti kama ya ngurumo. 143:14 1Fal 18:12; Isa 8:11; Eze 37:1Ndipo Roho aliponiinua na kunipeleka mbali. Nikaenda nikiwa na uchungu na hasira moyoni mwangu, nao mkono wa Bwana ukiwa juu yangu. 153:15 Mwa 50:10; Ay 2:13Nikafika kwa wale watu waliokuwa uhamishoni huko Tel-Abibu karibu na Mto Kebari. Nikakaa miongoni mwao kwa muda wa siku saba, nikiwa nimejawa na mshangao.

Onyo Kwa Israeli

163:16 Yer 42:7Mwishoni mwa hizo siku saba neno la Bwana likanijia kusema: 173:17 Isa 52:8; Yer 6:17; Wim 5:7; Eze 11:4; Yer 1:17; Isa 58:1“Mwanadamu, nimekufanya uwe mlinzi wa nyumba ya Israeli, kwa hiyo sikia neno nisemalo, ukawape onyo litokalo kwangu. 183:18 Eze 33:6; Rum 1:16; Mwa 2:17; Yn 8:21Nimwambiapo mtu mwovu, ‘Hakika utakufa,’ na wewe usipomwonya mtu huyo au kumshauri aache njia zake mbaya ili kuokoa maisha yake, huyo mtu mwovu atakufa katika dhambi yake na damu yake nitaidai mkononi mwako. 193:19 2Fal 17:13; 1Tim 4:14-16; Za 7:12; Yer 42:16; Eze 14:14-20; Mdo 18:6Lakini ukimwonya mtu mwovu naye akakataa kuacha uovu wake na njia zake mbaya, atakufa katika dhambi yake, lakini wewe utakuwa umejiokoa nafsi yako.

203:20 2Pet 2:20; Za 125:5; Eze 18:24; Yer 34:16; Isa 8:14; Law 26:37“Tena, mtu mwenye haki akiacha haki yake na kutenda maovu, nami nikaweka kikwazo mbele yake mtu huyo atakufa. Kwa kuwa hukumwonya, atakufa katika dhambi yake. Mambo ya haki aliyotenda, hayatakumbukwa, damu yake nitaidai mkononi mwako. 213:21 Mdo 20:31; Rum 2:7Lakini ukimwonya mwenye haki asitende dhambi na akaacha kutenda dhambi, hakika ataishi kwa sababu alipokea maonyo na utakuwa umejiokoa nafsi yako.”

223:22 Eze 8:4; Mdo 9:6Mkono wa Bwana ulikuwa juu yangu huko, naye akaniambia, “Simama uende mpaka sehemu tambarare, nami nitasema nawe huko.” 233:23 Mwa 17:3; Eze 1:28Kwa hiyo niliinuka nikaenda mpaka mahali pa tambarare. Utukufu wa Bwana ulikuwa umesimama huko, kama utukufu ule niliouona kando ya Mto Kebari, nami nikaanguka kifudifudi.

243:24 Eze 2:2; Yer 15:17Ndipo Roho akaja ndani yangu akanisimamisha kwa miguu yangu. Akasema nami akaniambia: “Nenda ukajifungie ndani ya nyumba yako. 253:25 Eze 4:8Nawe, ee mwanadamu, watakufunga kwa kamba, watakufunga ili usiweze kutoka na kuwaendea watu. 263:26 Eze 33:22; Hos 4:4; Eze 24:27; Za 22:15; Eze 2:5Nitaufanya ulimi wako ushikamane kwenye kaa la kinywa chako, ili uwe kimya usiweze kuwakemea, wajapokuwa ni nyumba ya kuasi. 273:27 Eze 24:27; 29:21; Ufu 22:11; Eze 12:3; 33:22Lakini nitakaposema nawe, nitafungua kinywa chako nawe utawaambia, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo.’ Yeyote atakayesikiliza na asikilize, na yeyote atakayekataa na akatae; kwa kuwa wao ni nyumba ya kuasi.

Bibelen på hverdagsdansk

Ezekiels Bog 3:1-27

1„Spis nu den her bogrulle,” sagde han, „og forkynd derefter mit ord for Israels folk.” 2Så åbnede jeg munden, og han puttede bogrullen i munden på mig, 3idet han tilføjede: „Spis hele bogrullen. Lad den fuldstændigt fylde dit indre.” Så spiste jeg den, og den smagte sødt som honning.

4„Jeg sender dig til Israels folk med et budskab fra mig,” fortsatte han. 5„Jeg sender dig ikke til et fremmed folk, hvis sprog du ikke forstår. 6Hvis jeg gjorde det, ville de i det mindste lytte til dig. 7I stedet sender jeg dig til Israels folk, og de vil ikke lytte mere til dig, end de lytter til mig, for de er stivnakkede og egenrådige i bund og grund. 8Men se, jeg gør dig hård og ubøjelig som dem, så du kan holde stand imod dem. 9Jeg gør dig hårdhudet og stærk som en klippe, så du ikke bliver såret af deres vrede blikke. Husk på, at det er et oprørsk folk. 10Hør godt efter alt, hvad jeg siger til dig, og lad budskabet blive en del af dig selv. 11Gå derefter rundt til folket, der bor i eksil, og forkynd dem mit ord, uanset om de hører efter eller ej.”

12Så løftede Ånden mig op og førte mig bort. Bag mig hørte jeg en buldrende røst, som lovpriste Herrens herlighed, 13og jeg hørte lyden af de levende væseners vinger, der rørte ved hinanden, og en voldsom rumlen fra hjulene, der fulgtes med dem.

14Efter at Ånden havde løftet mig op og ført mig bort, vandrede jeg om med forpint sjæl og oprørt indre, og Herrens kraft var stadig over mig. 15Så kom jeg til judæerne, som boede i Tel-Abib ved Kebarfloden. Der satte jeg mig tavs ned og stirrede lamslået frem for mig i syv dage.

Ezekiel kaldes til at være en vagtpost for folket

16Da de syv dage var gået, sagde Herren til mig:

17„Jeg har udvalgt dig til at holde udkig og stå vagt for Israels folk. Når du får et budskab fra mig, skal du straks give advarslen videre. 18Hvis jeg siger om nogle, at de skal dø som straf for deres ondskab, så skal du advare dem, så de har en chance for at ændre deres liv og undgå straffen. Hvis du ikke advarer dem, og de derfor ikke ændrer deres liv, så skal de dø for deres ondskab, men du skal også dø, for jeg vil holde dig ansvarlig for deres død. 19Hvis du derimod advarer dem, og de bliver ved med at synde uden at omvende sig, så skal de dø for deres ondskab, men du redder livet.

20Hvis retskafne mennesker bliver onde, og jeg derfor må straffe dem, så er det deres egen ondskab, der er skyld i deres død. Alle deres tidligere gode gerninger kan ikke redde dem. Og hvis du undlader at advare dem, bliver du også straffet. 21Men advarer du dem, så de holder op med deres ondskab, redder du både dig selv og dem.”

22Da mærkede jeg Herrens kraft over mig igen, og han sagde til mig: „Rejs dig og gå ud i dalen. Der vil jeg tale til dig.” 23Så rejste jeg mig og gik derud, og jeg så Herrens herlighed, som jeg tidligere havde set ved Kebarfloden, og jeg kastede mig ned med ansigtet mod jorden.

24Åndens kraft kom over mig og rejste mig op. „Gå hjem og luk dig inde i dit hus,” sagde han. 25„Der vil du blive bundet, så du ikke kan gå uden for din dør. 26Og jeg vil lade din tunge klæbe til ganen, så du ikke af dig selv kan anklage mit oprørske folk. 27Men når du får et budskab fra mig, vil jeg løse din tunge og lade dig tale, så du kan advare dem. ‚Hør hvad Gud Herren siger til jer!’ skal du sige. Nogle vil lytte til dig, men andre nægter at høre efter, for det er et oprørsk folk.”